< Luc 16 >
1 Il dit aussi à ses disciples: « Il y avait un homme riche qui avait un gérant. On lui reprocha que cet homme gaspillait ses biens.
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Palikuwa na tajiri mmoja na msimamizi wake. Ilisemekana kwamba huyo msimamizi alikuwa anatumia vibaya mali ya tajiri yake.
2 Il l'appela et lui dit: « Qu'est-ce que j'entends dire de toi? Rends compte de ta gestion, car tu ne peux plus être gérant.
Hivyo huyo tajiri akamwita na kumuuliza, ‘Ni mambo gani haya ninayoyasikia kukuhusu? Toa taarifa ya usimamizi wako, kwa sababu huwezi kuendelea kuwa msimamizi.’
3 « Le gérant se dit en lui-même: « Que vais-je faire, puisque mon seigneur m'enlève le poste de gérant? Je n'ai pas la force de creuser. J'ai honte de mendier.
“Yule msimamizi akawaza moyoni mwake, ‘Nitafanya nini sasa? Bwana wangu ananiondoa katika kazi yangu. Sina nguvu za kulima, nami ninaona aibu kuombaomba.
4 Je sais ce que je ferai, afin que, lorsque je serai relevé de mes fonctions, on me reçoive dans sa maison.
Najua nitakalofanya ili nikiachishwa kazi yangu hapa, watu wanikaribishe nyumbani kwao.’
5 Appelant chacun des débiteurs de son maître, il dit au premier: « Combien dois-tu à mon maître? »
“Kwa hiyo akawaita wadeni wote wa bwana wake, mmoja mmoja. Akamuuliza wa kwanza, ‘Deni lako kwa bwana wangu ni kiasi gani?’
6 Il répondit: « Cent batos d'huile ». Il lui dit: « Prends ton billet, assieds-toi vite et écris cinquante ».
“Akajibu, ‘Galoni 800za mafuta ya mizeituni.’ “Msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati ya deni lako, ibadilishe upesi, uandike galoni 400.’
7 Il dit ensuite à un autre: « Combien dois-tu? Il répondit: « Cent cors de blé ». Il lui dit: « Prends ta note, et écris quatre-vingts.
“Kisha akamuuliza wa pili, ‘Wewe deni lako ni kiasi gani?’ “Akajibu, ‘Vipimo 1,000vya ngano.’ “Yule msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati yako, andika vipimo 800!’
8 « Son seigneur a félicité le gérant malhonnête parce qu'il avait agi avec sagesse, car les enfants de ce monde sont, dans leur propre génération, plus sages que les enfants de la lumière. (aiōn )
“Yule bwana akamsifu yule msimamizi dhalimu kwa jinsi alivyotumia ujanja. Kwa maana watu wa dunia hii wana ujanja zaidi wanapojishughulisha na mambo ya dunia kuliko watu wa nuru. (aiōn )
9 Je vous le dis, faites-vous des amis au moyen de mammon inique, afin que, lorsque vous échouerez, ils vous reçoivent dans les tentes éternelles. (aiōnios )
Nawaambia, tumieni mali ya kidunia kujipatia marafiki, ili itakapokwisha, mkaribishwe katika makao ya milele. (aiōnios )
10 Celui qui est fidèle en peu de chose l'est aussi en beaucoup. Celui qui est malhonnête pour peu de choses est aussi malhonnête pour beaucoup.
“Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, pia ni mwaminifu hata katika mambo makubwa, naye mtu ambaye si mwaminifu katika mambo madogo pia si mwaminifu katika mambo makubwa.
11 Si donc vous n'avez pas été fidèles dans les richesses injustes, qui vous confiera les véritables richesses?
Ikiwa hamkuwa waaminifu katika mali ya kidunia, ni nani atakayewaaminia mali ya kweli?
12 Si tu n'as pas été fidèle dans ce qui appartient à autrui, qui te donnera ce qui t'appartient en propre?
Nanyi kama hamkuwa waaminifu na mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
13 Aucun serviteur ne peut servir deux maîtres, car ou bien il haïra l'un et aimera l'autre, ou bien il s'attachera à l'un et méprisera l'autre. Vous ne pouvez pas servir Dieu et Mammon. »
“Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.”
14 Les pharisiens, qui aimaient l'argent, entendirent aussi toutes ces choses, et ils se moquèrent de lui.
Mafarisayo, waliokuwa wapenda fedha, waliyasikia hayo yote na wakamcheka kwa dharau.
15 Il leur dit: « Vous êtes ceux qui se justifient aux yeux des hommes, mais Dieu connaît vos cœurs. Car ce qui est élevé parmi les hommes est une abomination aux yeux de Dieu.
Yesu akawaambia, “Ninyi mnajionyesha kuwa wenye haki mbele za wanadamu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana vile vitu ambavyo wanadamu wanavithamini sana, kwa Mungu ni machukizo.
16 « La loi et les prophètes ont été jusqu'à Jean. Dès lors, la Bonne Nouvelle du Royaume de Dieu est prêchée, et chacun y entre de force.
“Sheria na Manabii vilihubiriwa mpaka kuja kwa Yohana Mbatizaji. Tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu zinahubiriwa, na kila mmoja hujiingiza kwa nguvu.
17 Mais il est plus facile que le ciel et la terre passent que de faire tomber un petit trait de plume de la loi.
Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita kuliko hata herufi moja kuondoka katika Sheria.
18 « Quiconque répudie sa femme et en épouse une autre commet un adultère. Celui qui épouse une femme divorcée commet un adultère.
“Mtu yeyote amwachaye mkewe na kumwoa mwanamke mwingine anazini, naye mwanaume amwoaye mwanamke aliyetalikiwa anazini.
19 Il y avait là un homme riche, vêtu de pourpre et de fin lin, et vivant chaque jour dans le luxe.
“Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, ambaye aliishi kwa anasa kila siku.
20 Un mendiant, nommé Lazare, fut conduit à sa porte, couvert d'ulcères,
Hapo penye mlango wake aliishi maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima.
21 et désireux de se nourrir des miettes qui tombaient de la table du riche. Et même les chiens venaient lécher ses plaies.
Huyo Lazaro alitamani kujishibisha kwa makombo yaliyoanguka kutoka mezani kwa yule tajiri. Hata mbwa walikuwa wakija na kuramba vidonda vyake.
22 Le mendiant mourut, et il fut emporté par les anges dans le sein d'Abraham. Le riche aussi mourut et fut enseveli.
“Wakati ukafika yule maskini akafa, nao malaika wakamchukua akae pamoja na Abrahamu. Yule tajiri naye akafa na akazikwa.
23 Dans le séjour des morts, il leva les yeux, étant en proie aux tourments, et il vit au loin Abraham, et Lazare dans son sein. (Hadēs )
Kule kuzimu alipokuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Abrahamu kwa mbali, naye Lazaro alikuwa karibu yake. (Hadēs )
24 Il s'écria: « Père Abraham, aie pitié de moi, et envoie Lazare, afin qu'il trempe le bout de son doigt dans l'eau et me rafraîchisse la langue. Car je suis en proie à l'angoisse dans cette flamme.
Hivyo yule tajiri akamwita, ‘Baba Abrahamu, nihurumie na umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake ndani ya maji aupoze ulimi wangu, kwa sababu nina maumivu makuu kwenye moto huu.’
25 « Mais Abraham dit: 'Mon fils, souviens-toi que toi, de ton vivant, tu as reçu tes bonnes choses, et Lazare, de la même manière, de mauvaises choses. Mais voici qu'il est maintenant réconforté et toi, tu es dans l'angoisse.
“Lakini Abrahamu akamjibu, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba wakati wa uhai wako ulipata mambo mazuri, lakini Lazaro alipata mambo mabaya. Lakini sasa anafarijiwa hapa na wewe uko katika maumivu makuu.
26 En plus de tout cela, entre nous et vous, un grand fossé est fixé, de sorte que ceux qui veulent passer d'ici à vous ne le peuvent pas, et que personne ne peut passer de là à nous.''
Zaidi ya hayo, kati yetu na ninyi huko kumewekwa shimo kubwa, ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko wasiweze, wala mtu yeyote asiweze kuvuka kutoka huko kuja kwetu.’
27 Il dit: « Je te demande donc, père, de l'envoyer dans la maison de mon père -
“Akasema, ‘Basi, nakuomba, umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu,
28 car j'ai cinq frères - afin qu'il leur rende témoignage et qu'ils n'aillent pas eux aussi dans ce lieu de tourments ».
maana ninao ndugu watano. Awaonye, ili wasije nao wakafika mahali hapa pa mateso.’
29 « Mais Abraham lui dit: « Ils ont Moïse et les prophètes. Qu'ils les écoutent.
“Abrahamu akamjibu, ‘Ndugu zako wana Maandiko ya Mose na Manabii, wawasikilize hao.’
30 « Il répondit: 'Non, père Abraham, mais si quelqu'un leur vient d'entre les morts, ils se repentiront'.
“Yule tajiri akasema, ‘Hapana, baba Abrahamu, lakini mtu kutoka kwa wafu akiwaendea, watatubu.’
31 « Il lui dit: 'S'ils n'écoutent pas Moïse et les prophètes, ils ne seront pas non plus convaincus si quelqu'un ressuscite d'entre les morts.'"
“Abrahamu akamwambia, ‘Kama wasipowasikiliza Mose na Manabii, hawataweza kushawishika hata kama mtu akifufuka kutoka kwa wafu.’”