< Lévitique 8 >
1 Yahvé parla à Moïse, et dit:
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
2 « Prends avec lui Aaron et ses fils, les vêtements, l'huile d'onction, le taureau expiatoire, les deux béliers et la corbeille de pains sans levain,
“Walete Aroni na wanawe pamoja naye, mavazi na mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili, na kikapu cha mkate usio na hamira.
3 et rassemble toute l'assemblée à l'entrée de la tente de la Rencontre. »
Ita kusanyiko lote kwenye ingilio la hema la kukutania.”
4 Moïse fit ce que Yahvé lui avait ordonné; et l'assemblée se rassembla à l'entrée de la tente de la Rencontre.
Kwa hiyo Musa akafanya kama Yahweh alivyomwamru, nalo kusanyiko lilikuja pamoja mbele ya ingilio la hema la kukutania. Kisha Musa akaliambia kusanyiko,
5 Moïse dit à l'assemblée: « Voici ce que l'Éternel a ordonné de faire. »
“Hivi ndivyo alivyotuamru Yahweh tutende.”
6 Moïse fit venir Aaron et ses fils, et les lava avec de l'eau.
Musa akamleta Aroni na wanawe na kuwaosha kwa maji.
7 Il lui mit la tunique, lui attacha la ceinture, le revêtit de la robe, lui mit l'éphod, et il attacha sur lui la bande de l'éphod, habilement tissée, et la lui fixa avec elle.
Akamvika Aroni kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini na kumfunga ukumbuu kiunoni mwake, akamvika joho la nje lenye mikono mirefu na kumvika kile kizibao chenye vipande viwili tumboni na mgongoni na kukifunga kuzunguka kiunoni mwake kwa mshipi uliosokotwa kwa ustadi na kukikaza mwilini mwake.
8 Il plaça sur lui le pectoral. Il mit l'urim et le thummim dans le pectoral.
Kisha Musa akaweka kifuko kifuani mwa Aroni, na ndani ya kifuko hicho akaweka Urimu na Thumimu.
9 Il mit le turban sur sa tête. Il plaça la plaque d'or, la couronne sacrée, sur le devant du turban, comme l'avait ordonné l'Éternel à Moïse.
Na kisha akamfunga kiremba kichwani, na juu ya kiremba kwa mbele, akaweka bamba la dhahabu; liwe taji takatifu, kama Yahweh alivyomwamru yeye.
10 Moïse prit l'huile d'onction, oignit le tabernacle et tout ce qui s'y trouvait, et les sanctifia.
Musa akayatwaa hayo mafuta ya upako, akalipaka lile hema la kukutania na kila kitu kilichokuwamo ndani yake na kuvitenga kwa ajili ya Yahweh.
11 Il en fit sept fois l'aspersion sur l'autel, et il oignit l'autel et tous ses ustensiles, ainsi que le bassin et sa base, pour les sanctifier.
Akayanyunyiza hayo mafuta juu ya madhabahu mara saba, na kisha akaipaka mafuta hiyo madhabahu na vyombo vyake vyote, na sinia la kunawia na kitako chake ili kuvitenga wa ajili ya Yahweh.
12 Il versa de l'huile d'onction sur la tête d'Aaron et l'oignit, afin de le sanctifier.
Akamimina sehemu ya mafuta ya upako juu ya kichwa cha Aroni na kisha akampaka mafuta ili kumtenga.
13 Moïse fit venir les fils d'Aaron, les revêtit de tuniques, leur attacha des ceintures et leur mit des bandeaux, comme Yahvé l'avait ordonné à Moïse.
Musa akawaleta wana wa Aroni na kuwavika kila mmoja kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini. Kila mmoja wao akamfunga kwa ukumbuu kiunoni mwake na kuwafunga vitambaa vya kitani kichwani pao, kama vile Yahweh alivyokuwa amemru Musa.
14 Il amena le taureau du sacrifice pour le péché, et Aaron et ses fils posèrent leurs mains sur la tête du taureau du sacrifice pour le péché.
Musa akamleta huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha fahali ambaye wamemelete kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
15 Il l'égorgea; Moïse prit le sang et le mit avec son doigt autour des cornes de l'autel; il purifia l'autel, versa le sang au pied de l'autel et le sanctifia pour en faire l'expiation.
Musa akamchinja, na kisha akachukua sehemu ya damu yake kwa kidole chake na kuiweka juu ya mpembe za madhabahu, akaitakasa hiyo madhabahu, na kuitenga kwa Mungu, ambapo kwa kufanya hivyo, aliisababisha madhabahu kuwa sehemu ya kufaa kwa kufanyia upatanisho.
16 Il prit toute la graisse qui était sur les entrailles, la couverture du foie, les deux rognons et leur graisse, et Moïse les brûla sur l'autel.
Akachukua mafuta yote yaliyokuwa sehemu za ndani, kile kiwambo cha ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake, Musa akaichoma hiyo nyama yote juu ya madhabahu.
17 Mais le taureau, sa peau, sa viande et ses excréments, il les brûla au feu en dehors du camp, comme Yahvé l'avait ordonné à Moïse.
Lakini yule fahali, ngozi yake, nyama yake na kinyesi chake, akavichoma nje ya kambi, kama vile Yehweh alivyokuwa amemwamru yeye.
18 Il présenta le bélier de l'holocauste. Aaron et ses fils posèrent leurs mains sur la tête du bélier.
Musa akamleta yule konndoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo kondoo.
19 Il l'égorgea et Moïse fit aspersion du sang tout autour de l'autel.
Musa akamchinja kondoo na kuinyunyizia damu yake kila upande wa madhabahu.
20 Il coupa le bélier en morceaux, et Moïse brûla la tête, les morceaux et la graisse.
Naye akamkatakata kondoo vipande vipande na akakiteketeza kichwa chake pamoja na vile vipande na mafuta.
21 Il lava à l'eau les entrailles et les jambes, et Moïse brûla le bélier tout entier sur l'autel. C'était un holocauste pour un parfum agréable. C'était un sacrifice consumé par le feu à Yahvé, comme Yahvé l'avait ordonné à Moïse.
Akaziosha kwa maji zile sehemu za ndani pamoja na miguu na akamteketeza kandoo mzima juu ya madhabahu. Ilikuwa ni dhabihu ya kuteketezwa na ilitoa harufu ya kupendeza, sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamru Musa.
22 Il présenta l'autre bélier, le bélier de consécration. Aaron et ses fils posèrent leurs mains sur la tête du bélier.
Kisha Musa akamleta yule kondoo dume mwingine, kondoo wa kuwekwa wakfu, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo.
23 Il l'égorgea; Moïse prit un peu de son sang et en mit sur le bout de l'oreille droite d'Aaron, sur le pouce de sa main droite et sur le gros orteil de son pied droit.
Aroni akamchinja, naye Musa akachukua sehemu ya damu na kuiweka kwenye ncha ya sikio la Aroni la kulia, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye kidole kikumbwa cha mguu wake wa kulia.
24 Il fit venir les fils d'Aaron; Moïse mit un peu de sang sur le bout de leur oreille droite, sur le pouce de leur main droite et sur le gros orteil de leur pied droit; Moïse fit asperger le sang tout autour de l'autel.
Akawaleta wana wa Aroni, naye akaweka sehemu ya damu ya kondoo yule kwenye ncha ya sikio lao la kulia, kwenye dole gumba lao cha mkono wa kulia na kwenye kidole chao kikubwa cha mguu wa kulia. Kisha Musa akainyunyiza damu ya huyo kila upande wa madhabahu
25 Il prit la graisse, la queue, toute la graisse qui était sur les entrailles, la couverture du foie, les deux rognons et leur graisse, et la cuisse droite;
Naye akayatwaa yale mafuta, mafuta ya mkiani, mafuta liyolikuwa sehemu za ndani, na mafuta yafunikayo ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake na paja la kulia.
26 et dans la corbeille de pains sans levain qui était devant l'Éternel, il prit un gâteau sans levain, un gâteau de pain huilé et une galette, et les plaça sur la graisse et sur la cuisse droite.
Akachukua mkate mmoja kutoka kwenye kikapu cha mikate isiyo na hamira ambayoo ilikuwa mbele za Yahweh, akatwaa mkate moja usio na hamira, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na mkate mwemba wa kaki na akaiweka juu ya mafuta na juu ya paja la kulia la kondoo.
27 Il mit tout cela dans les mains d'Aaron et dans les mains de ses fils, et il les agita comme une offrande par agitation devant l'Éternel.
Akaiweka yote mikoni mwa Aroni na katika mikono ya wanawe na kuitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa
28 Moïse les prit de leurs mains et les brûla sur l'autel, sur l'holocauste. Elles constituaient une offrande de consécration pour un parfum agréable. C'était une offrande faite par le feu à Yahvé.
Kisha Musa akaichukua mikate hiyo kutoka mikononi mwao na kuiteketeza juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Zilikuwa ni sadaka ya kuwekwa wakfu na ilitoa harufu ya kupendeza. Ilikuwa sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto.
29 Moïse prit la poitrine et l'agita comme une offrande par agitation devant Yahvé. C'était la part de Moïse du bélier de consécration, comme Yahvé l'avait ordonné à Moïse.
Musa akakichukua kidari na kukitikisa kuwa sadaka ya kutikiswa kwa Yahweh. Ilikuwa ni mgao wa Musa wa kondoo wa kuwekewa mikono kwa makuhani, Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru yeye.
30 Moïse prit de l'huile d'onction et du sang qui était sur l'autel; il en fit l'aspersion sur Aaron, sur ses vêtements, sur ses fils et sur les vêtements de ses fils avec lui, et il sanctifia Aaron, ses vêtements, ses fils et les vêtements de ses fils avec lui.
Musa akatwaa sehemu ya mafuta ya upako na damu iliyokuwa juu ya madhabahu; naye akayanyunyiza haya juu ya nguo za Aroni, juu ya nguo zake mwenyewe na juu ya nguo za wana wa Aruni waliokua pamoja naye. Kwa njia hii alimtenga Aroni na nguo zake, na wanawe na nguo zao kwa ajili ya Yahweh.
31 Moïse dit à Aaron et à ses fils: « Faites bouillir la viande à l'entrée de la tente de la Rencontre, et là, mangez-la, ainsi que le pain qui est dans la corbeille de consécration, comme je l'ai ordonné, en disant: « Aaron et ses fils la mangeront ».
Kwa hiyo Musa akawambia Aruni na wanawe, “Ipikeni nyama mbele ya ingilio la hema la kukutania, na hapo mtaila pamoja na mkate ulio kwenye kikapu cha kuwekwa wakfu, kama ilivyoamriwa, kusema, 'Aroni na wanawe wataila.'
32 Ce qui restera de la viande et du pain, vous le brûlerez au feu.
Masalio yoyote ya nyama na mikate utayateketeza kwa moto.
33 Tu ne sortiras pas de l'entrée de la Tente d'assignation pendant sept jours, jusqu'à ce que les jours de ta consécration soient accomplis, car il te consacrera sept jours.
Na hamtatoka kwenye ingilio la hema la kukutania kwa muda wa siku saba, hata zitakapotimia siku za kuwekwa mikono kwenu. Kwa kuwa kwa muda wa siku saba, Yahweh atawaweka wakfu.
34 Ce qui a été fait aujourd'hui, Yahvé a ordonné de le faire, afin de faire l'expiation pour vous.
Kilichotendeka siku hii— Yahweh ndiye amekiamru kitendekeke ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
35 Tu resteras jour et nuit à l'entrée de la Tente de la Rencontre, pendant sept jours, et tu observeras l'ordre de l'Éternel, afin que tu ne meures pas; car c'est ainsi qu'on me l'ordonne. »
Mtakaa kwenye ingilio la hema la kukutania mchana na usiku siku saba, nanyi ishikeni amri ya Yahweh ili msije mkafa, kwa sababu hivi ndivyo ilivyoamriwa.
36 Aaron et ses fils firent tout ce que l'Éternel avait ordonné par Moïse.
Kwa hiyo Aroni na wanawe wakafanya mambo yote ambayo Yahweh alikuwa amewaamru kwa kinywa cha Musa.