< Lévitique 6 >

1 Yahvé parla à Moïse, et dit:
Bwana akamwambia Mose:
2 « Si quelqu'un pèche et commet une infidélité à l'égard de Yahvé, s'il traite faussement son prochain dans une affaire de dépôt, de marchandage ou de vol, s'il a opprimé son prochain,
“Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
3 s'il a retrouvé ce qui était perdu et a menti à son sujet, et a juré de mentir - dans l'une quelconque de ces choses, un homme pèche par ses actions -
au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
4 alors, s'il a péché et s'il est coupable, il restituera ce qu'il a pris par vol, ou ce qu'il a obtenu par oppression, ou le dépôt qui lui a été confié, ou la chose perdue qu'il a trouvée,
wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
5 ou toute chose sur laquelle il a juré faussement: il le restituera intégralement, et y ajoutera un cinquième de plus. Il la rendra à celui à qui elle appartient, le jour où il sera déclaré coupable.
au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
6 Il apportera son sacrifice de culpabilité à l'Éternel: un bélier sans défaut du troupeau, selon votre estimation, en sacrifice de culpabilité, au prêtre.
Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
7 Le prêtre fera pour lui l'expiation devant Yahvé, et il lui sera pardonné tout ce qu'il aura fait pour se rendre coupable. »
Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
8 Yahvé parla à Moïse, et dit:
Bwana akamwambia Mose:
9 « Donne cet ordre à Aaron et à ses fils: Voici la loi de l'holocauste: l'holocauste restera sur le foyer de l'autel toute la nuit jusqu'au matin, et le feu de l'autel restera allumé sur lui.
“Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
10 Le prêtre revêtira son vêtement de lin, et il mettra sur son corps son pantalon de lin; il enlèvera la cendre de l'endroit où le feu a consumé l'holocauste sur l'autel, et il la mettra à côté de l'autel.
Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
11 Il ôtera ses vêtements, en mettra d'autres, et portera les cendres hors du camp, dans un lieu pur.
Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
12 Le feu restera allumé sur l'autel, il ne s'éteindra pas, et le prêtre y brûlera du bois chaque matin. Il y déposera l'holocauste en ordre, et il y brûlera la graisse des sacrifices de prospérité.
Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
13 Le feu brûlera continuellement sur l'autel; il ne s'éteindra pas.
Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
14 "'Voici la loi de l'offrande de gâteau: les fils d'Aaron l'offriront devant l'Éternel, devant l'autel.
“‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
15 Il prendra là une poignée de la fleur de farine de l'offrande, de son huile et de tout l'encens qui est sur l'offrande, et il la brûlera sur l'autel, en guise d'odeur agréable, comme sa portion commémorative, devant l'Éternel.
Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
16 Ce qui en restera, Aaron et ses fils le mangeront. On le mangera sans levure, dans un lieu saint. Ils le mangeront dans le parvis de la tente d'assignation.
Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
17 Il ne sera pas cuit au four avec de la levure. Je le leur ai donné comme part de mes offrandes consumées par le feu. Il est très saint, comme le sacrifice pour le péché et le sacrifice de culpabilité.
Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
18 Tout mâle parmi les enfants d'Aaron en mangera, c'est la part qui lui reviendra de génération en génération, parmi les offrandes consumées par le feu de l'Éternel. Quiconque les touchera sera saint. »"
Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
19 L'Éternel parla à Moïse, et dit:
Tena Bwana akamwambia Mose,
20 Voici l'offrande qu'Aaron et ses fils présenteront à l'Éternel le jour où il sera oint: un dixième d'épha de fleur de farine, en offrande perpétuelle, une moitié le matin et une moitié le soir.
“Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
21 On la fera cuire à l'huile dans une poêle. Lorsqu'elle sera trempée, tu l'apporteras. Tu offriras l'offrande de repas en morceaux cuits, comme une odeur agréable à Yahvé.
Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
22 Le prêtre oint qui sera à sa place, parmi ses fils, l'offrira. C'est une loi perpétuelle: elle sera entièrement consumée devant l'Éternel.
Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
23 Toute offrande de repas d'un prêtre sera entièrement brûlée. On ne la mangera pas. »
Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
24 Yahvé parla à Moïse et dit:
Bwana akamwambia Mose,
25 Parle à Aaron et à ses fils, et dis: « Voici la loi du sacrifice pour le péché: dans le lieu où l'on égorge l'holocauste, on égorgera le sacrifice pour le péché devant Yahvé. Elle est très sainte.
“Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
26 Le prêtre qui l'offrira pour le péché la mangera. Il la mangera dans un lieu saint, dans le parvis de la tente d'assignation.
Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
27 Tout ce qui touchera sa chair sera saint. Si un vêtement est aspergé de son sang, vous laverez celui sur lequel il a été aspergé dans un lieu saint.
Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
28 Mais le vase de terre dans lequel on l'aura fait bouillir sera brisé; et si on l'a fait bouillir dans un vase de bronze, on le récurera et on le rincera à l'eau.
Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
29 Tout mâle parmi les prêtres en mangera. C'est une chose très sainte.
Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
30 On ne mangera pas le sacrifice pour le péché dont on a apporté une partie du sang dans la tente d'assignation pour faire l'expiation dans le lieu saint. Il sera brûlé au feu.
Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.

< Lévitique 6 >