< Lévitique 22 >
1 Yahvé parla à Moïse, et dit:
Yahweh akazungumza na Musa, kusema,
2 « Dis à Aaron et à ses fils de se séparer des choses saintes des enfants d'Israël, qu'ils me consacrent, et de ne pas profaner mon saint nom. Je suis Yahvé.
“Ongea na Aroni na wanawe, waambie wajiepushe na vitu vitakatifu vya watu wa Israeli wanavyovitenga kwangu. Wasilinajisi jina langu. Mimi ndimi Yahweh.
3 « Dis-leur: « Si quelqu'un de tous vos descendants, de génération en génération, s'approche des choses saintes que les enfants d'Israël consacrent à Yahvé, en ayant sur lui son impureté, cette personne sera retranchée de devant moi. Je suis Yahvé.
Waambie, 'Ikiwa mmoja wa wazao wenu katika vizazi vyenu vyote anakaribia vitu vitakatiifu vile ambavyo watu wa Israeli wamevitenga kwa Yahweh, wakati akiwa najisi, sharti mtu huyo akatiliwe mbali atoke mbele zangu. Mimi ndimi Yahweh.
4 "'Quiconque, parmi les descendants d'Aaron, est lépreux ou a des pertes, ne mangera pas des choses saintes jusqu'à ce qu'il soit pur. Celui qui touchera une chose souillée par un mort, ou un homme qui a une émission séminale,
Hatakuwapo yeyote wa uzao wa Aroni aliye na ungonjwa wa ngozi wa kuambukiza, au maambukizi yatirirkayo kutoka mwilini mwake, atakayekula sehemu yoyote ya dhabihu inatolewayo kwa Yahweh mpaka atakapotakasika. Yeyote agusaye kitu chochote kilichonajisi kwa njia ya kugusa maiti, au kwa kumgusa mtu yeyote aliyetokwa na shahawa,
5 ou celui qui touchera un reptile par lequel il peut être souillé, ou un homme de qui il peut être souillé, quelle que soit sa souillure -
au yeyote agusaye mnyama atakayemtia unajisi, au mtu yeyote atakayemfanya najisi, kwa hiyo unajisi wowote unaweza kuwa—
6 celui qui aura touché l'une de ces choses sera souillé jusqu'au soir, et ne mangera pas des choses saintes, à moins qu'il ne se lave le corps dans l'eau.
kuhani yeyote agusaye kitu chochote kisichosafi atakuwa najisi hata jioni. Hatakula chochote cha vitu vitakatifu, isipokuwa ameuosha mwili wake katika maji.
7 Au coucher du soleil, il sera pur; ensuite, il mangera des choses saintes, car c'est son pain.
Jua linapotua, ndipo atakuwa safi. Baada ya machweo anaweza kula kutoka katika vitu vitakatifu, kwasababu hivyo ni vyakuala vyake.
8 Il ne mangera pas de ce qui meurt de lui-même ou qui est déchiré par les animaux, car il s'en souillerait. Je suis Yahvé.
Asile mzoga wowote uliookotwa au mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori, ambaye kwake atajitia unajisi. Mimi ndimi Yahweh.
9 "'Ils suivront donc mon commandement, de peur de porter un péché à cause de lui et de mourir en lui, s'ils le profanent. C'est moi, Yahvé, qui les sanctifie.
Ni lazima makuhani wafuate maagizo yangu, ama sivyo watakuwa na hatia ya dhambi na wangeweza kufa kwa kunitia unajisi. Mimi ndimi Yahweh ninayewafanya wao watakatifu.
10 "'Aucun étranger ne mangera de la chose sainte: un étranger qui habite avec les prêtres, ou un mercenaire, ne mangera pas de la chose sainte.
Hakuna mtu kutoka nje ya familia ya kuahani, wakiwemo wageni wa kuhani au watumwa wake wa kuajiliwa, atakayeweza kula kitu chochote kilicho kitakatifu.
11 Mais si un prêtre achète un esclave, acquis par son argent, il en mangera; et ceux qui sont nés dans sa maison mangeront de son pain.
Lakini kama huyo kuhani amenunua mtumwa kwa fedha yake mwenyewe, mtumwa huyo anaweza kula kutoka katika vitu vilivyotengwa kwa Yahweh. Na watu wa familia ya kuhani na watumwa waliozaliwa nyumbani mwake, pia wanaweza kula pamoja naye kutoka katika vitu hivyo.
12 Si la fille d'un prêtre est mariée à un étranger, elle ne mangera pas de l'offrande par élévation des choses saintes.
Ikiwa binti wa kuhani ameolewa na mtu asiye kuhani, hataweza kula chochote cha mchango wa matoleo matakatifu.
13 Mais si la fille d'un prêtre est veuve ou divorcée, qu'elle n'a pas d'enfant et qu'elle est retournée dans la maison de son père comme dans sa jeunesse, elle pourra manger le pain de son père, mais aucun étranger n'en mangera.
Lakini ikiwa huyo binti wa kuhani ni mjane au ametalikiwa, na ikiwa hana mtoto, na anarudi kuishi knyumbani kwa baba yake kama alivyokuwa wakati wa ujana wake, anaweza kula kutoka katika chakula cha baba yake. Lakini hakuna yeyote asiye wa familia ya kikuhani anatakayeruhusiwa kula kutoka katika chakula cha kuhani.
14 "'Si un homme mange involontairement une chose sainte, il y ajoutera le cinquième de sa valeur, et il donnera la chose sainte au prêtre.
Kama mtu anakula chakula kitakatifu bila ya kukijua, naye atamlipa kuahani kwa ajili ya hicho; itampasa kuongeza moja ya tano juu yake na kukirejesha kwa kuhani.
15 Les prêtres ne profaneront pas les choses saintes des enfants d'Israël, qu'ils offrent à l'Éternel,
Haiwapasi watu wa Israeli kutoheshimu vitu vitakatifu ambavyo vimeinuliwa juu na kuletwa kwa Yahweh,
16 et ne leur feront pas porter l'iniquité qui les rend coupables lorsqu'ils mangent leurs choses saintes, car je suis l'Éternel qui les sanctifie.'"
kisha wakajisababishia wenyewe kuchukua dhambi amabyo ingewafanya kuwa na hatia ya kula chakula kitakatifu, kwa kuwa mimi ndimi Yahweh awafanyaye wao watakatifu.”
17 Yahvé parla à Moïse, et dit:
Yahweh akazungumza na Musa, akasema,
18 Parle à Aaron, à ses fils et à tous les enfants d'Israël, et tu leur diras: « Si quelqu'un de la maison d'Israël ou des étrangers en Israël présente une offrande, qu'il s'agisse d'un de leurs vœux ou d'une de leurs offrandes volontaires, qu'ils offrent à Yahvé en holocauste:
“Sema na Aroni na wanawe, na kwa watu wa Israeli wote. Waambie, Mwisraeli yeyote, au Mgeni anayeishi katika Israeli, waletapo dhabihu—iwe ni kutimiza kiapo, au iwe ni sadaka ya hiari, au wanaleta kwa Yahweh sadaka ya kuteketezwa kwa moto,
19 Afin que tu sois agréé, tu offriras un mâle sans défaut, parmi les taureaux, les moutons ou les chèvres.
ikiwa wanataka ikubalike, ni lazima watowe mnyama dume asiye na dosari, kutoka kwenye kundi la ng'ombe, kondoo au mbuzi
20 Mais tu n'offriras pas ce qui a un défaut, car cela ne sera pas agréé pour toi.
Lakini hamtatoa chochote kilicho na dosari. Sitakipokea kwa niaba yenu.
21 Celui qui offrira à Yahvé un sacrifice d'actions de grâces pour l'accomplissement d'un vœu, ou pour une offrande volontaire du gros ou du menu bétail, sera parfait pour être accepté. Il n'aura aucun défaut.
Yeyote atoae dhabihu ya sadaka ya ushirika kutoka katika kundi la ng'ombe au la kondoo kwa Yahweh ili kutimiza kiapo, au kama sadaka ya hiari, ili ikubalike, ni lazima isiwe na kilema. Ni lazima pasiweko na kasoro katika mnyama.
22 Tu n'offriras pas à l'Éternel un aveugle, un blessé, un mutilé, une verrue, un suppurant ou un ulcère, et tu n'en feras pas un sacrifice par le feu sur l'autel de l'Éternel.
Msitoe kabisa wanyama waliovipofu, waliojeruhiwa, wala walio na kilema, wenye upele, vidonda vitokavyo usaha, wala wenye vigaga. Msiwatoe hawa kuwa dhabihu ya kuteketezwa kwa moto iliyotolewa kwa Yahweh juu ya madhabahu.
23 Soit un taureau ou un agneau qui a une difformité ou un défaut de ses parties, que vous pourrez offrir en offrande volontaire; mais pour un vœu, il ne sera pas accepté.
Unaweza kumleta makisai au mwana-kondoo mlemavu au aliyedumaa kuwa sadaka ya hiari, lakini sadaka kama hiyo kwa ajili kutimiza kiapo, haitapokelewa.
24 Vous n'offrirez pas à Yahvé ce qui a les testicules meurtris, écrasés, cassés ou coupés. Vous ne ferez pas cela dans votre pays.
Usitoe kwa Yahweh mnyama yeyote aliyetiwa jeraha, kupondwa, au kukatwa korodani zake.
25 Vous n'offrirez rien de tout cela comme pain de votre Dieu, de la main d'un étranger, car il y a en eux de la corruption. Il y a en eux un défaut. Ils ne seront pas acceptés pour vous. »"
Usifanye haya katika nchi yako. Usilete mkate wa Mungu wako kutoka mkononi mwa mgeni. Hao wanyama wenye vilema na dosari ndani yao, hawatapokelewa kabisa kwa ajili yako.
26 Yahvé parla à Moïse et dit:
Yahweh akamwambia Musa na akasema,
27 « Lorsqu'un taureau, un mouton ou une chèvre naîtra, il restera sept jours avec sa mère. A partir du huitième jour, il sera accepté pour l'offrande d'un sacrifice consumé par le feu à Yahvé.
“Wakati ndama, mwana—kondo au mwana—mbuzi azaliwapo, sharti abaki na mama yake kwa muda wa siku saba. Ndipo kuanzia siku ya nane na kuendelea, anaweza kupokelewa kuwa dhabihu iliyofanywa kwa moto kwa Yahweh.
28 Qu'il s'agisse d'une vache ou d'une brebis, vous ne l'égorgerez pas avec son petit en un seul jour.
Usimchinje ng'ombe jike pamoja na ndama wake au mbuzi jike pamoja na kitoto chake kwa siku moja.
29 « Lorsque tu offriras un sacrifice d'action de grâces à Yahvé, tu le sacrifieras pour être agréé.
Utoapo sadaka ya shukrani kwa Yahweh utaitoa kwa njia iliyokubalika.
30 Il sera mangé le jour même; tu n'en laisseras rien jusqu'au matin. Je suis Yahvé.
Ni lazima iliwe siku iyo hiyo inayotolewa. Hutakiwi kubakiza chochote hata asubuhi. Mimi ndimi Yahweh.
31 « C'est pourquoi vous garderez mes commandements et vous les mettrez en pratique. Je suis Yahvé.
Kwa hiyo imewapasa kuzishika amri zangu na kuzifuata. Mimi ndimi Yahweh.
32 Vous ne profanerez pas mon saint nom, mais je serai sanctifié au milieu des enfants d'Israël. Je suis Yahvé, qui vous rend saints,
Msiliabishe jina langu takatifu. Ni lazima nitambuliwe kuwa ni mtakatifu na watu wa Israeli. Mimi ndimi Yahweh niwafanyaye ninyi watakatifu,
33 qui vous a fait sortir du pays d'Égypte, pour être votre Dieu. Je suis Yahvé. »
ambaye amewaleta kutoka katika nchi ya Misri ili niwe Mungu wenu: Mimi ndimi Yahweh.”