< Juges 7 >
1 Et Jerubbaal, qui est Gédéon, et tout le peuple qui était avec lui, se levèrent de bonne heure et campèrent près de la source de Harod. Le camp de Madian était au nord, près de la colline de Moreh, dans la vallée.
Ndipo Yerub-Baali (yaani Gideoni) na lile jeshi lililokuwa pamoja naye, wakaondoka asubuhi na mapema na kupiga kambi kando ya chemchemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa kaskazini yao katika bonde karibu na kilima cha More.
2 Yahvé dit à Gédéon: « Le peuple qui est avec toi est trop nombreux pour que je livre les Madianites entre leurs mains, de peur qu'Israël ne se vante de moi en disant: « Ma propre main m'a sauvé ».
Bwana akamwambia Gideoni, “Jeshi lililo pamoja nawe ni kubwa sana kwa mimi kuwatia Wamidiani mikononi mwao. Ili kwamba Israeli asije akajisifu juu yangu akisema, ‘Mkono wangu ndio ulioniokoa,
3 Maintenant, proclame aux oreilles du peuple: « Que celui qui a peur et qui tremble s'en retourne et s'éloigne de la montagne de Galaad ». Ainsi, vingt-deux mille personnes du peuple s'en retournèrent, et dix mille restèrent.
kwa hiyo sasa tangaza jeshi lote likiwa linasikia, kwamba: Yeyote anayeogopa na kutetemeka, yeye na arudi nyumbani, aondoke katika Mlima Gileadi.’” Hivyo watu 22,000 walirudi, wakabaki 10,000.
4 Yahvé dit à Gédéon: « Il y a encore trop de monde. Fais-les descendre jusqu'à l'eau, et là, je les mettrai à l'épreuve pour toi. Ceux à qui je dirai: « Ceci ira avec vous » iront avec vous, et ceux à qui je dirai: « Ceci n'ira pas avec vous » n'iront pas. »
Lakini Bwana akamwambia Gideoni, “Idadi ya jeshi bado ni kubwa. Wapeleke chini katika maji nami nitawajaribu huko kwa ajili yako. Kama nikikuambia, ‘Huyu atakwenda pamoja nawe,’ yeye atakwenda; lakini kama nikisema, ‘Huyu hatakwenda pamoja nawe,’ yeye hatakwenda.”
5 Il fit donc descendre le peuple vers l'eau, et Yahvé dit à Gédéon: « Si quelqu'un lèche l'eau avec sa langue, comme un chien, tu le mettras à part, et si quelqu'un s'agenouille pour boire, tu le mettras à part. »
Hivyo Gideoni akalileta lile jeshi chini kwenye maji naye Bwana akamwambia Gideoni, “Watenge upande mmoja wale wote wanywao maji kwa ulimi, kama vile mbwa anywavyo, wale wote wapigao magoti ili kunywa wakipeleka mikono yao vinywani mwao, waweke upande mwingine.”
6 Le nombre de ceux qui laperont l'eau, en portant la main à la bouche, sera de trois cents hommes; mais tout le reste du peuple se prosternera à genoux pour boire l'eau.
Idadi ya wale waliokunywa kwa kuramba ramba walikuwa 300, lakini wengine wote katika jeshi walipiga magoti ili kunywa.
7 Yahvé dit à Gédéon: « Je te sauverai par les trois cents hommes qui ont lapé, et je livrerai les Madianites entre tes mains. Laisse partir tout le reste du peuple, chacun à sa place. »
Bwana akamwambia Gideoni, “Kwa hao watu 300 walioramba maji nitawaokoa ninyi, nami nitawatia Wamidiani mkononi mwako. Waache hao watu wengine wote warudi kila mmoja nyumbani mwake.”
8 Et le peuple prit en main de la nourriture et ses trompettes; et il envoya tous les autres hommes d'Israël dans leurs tentes, mais il garda les trois cents hommes; et le camp de Madian était au-dessous de lui dans la vallée.
Hivyo Gideoni akawaacha wale Waisraeli wengine kila mmoja aende kwenye hema yake. Akabakia na wale 300, ambao walichukua vyakula na tarumbeta za wale wenzao. Basi kambi ya Wamidiani ilikuwa chini yake bondeni.
9 Cette même nuit, Yahvé lui dit: « Lève-toi, descends dans le camp, car je l'ai livré entre tes mains.
Usiku ule ule Bwana akamwambia Gideoni, “Ondoka, ushuke kambini, kwa kuwa nimeitia mkononi mwako.
10 Mais si tu as peur de descendre, descends au camp avec Purah, ton serviteur.
Lakini kama unaogopa kushambulia, shuka kambini pamoja na mtumishi wako Pura,
11 Tu entendras ce qu'ils diront, et tes mains seront fortifiées pour descendre au camp. » Et il descendit avec Purah, son serviteur, jusqu'à l'extrémité des hommes armés qui étaient dans le camp.
nawe sikiliza wanayosema. Hatimaye, utatiwa moyo kushambulia kambi.” Basi yeye na Pura mtumishi wake wakashuka na kufikia walinzi wa mbele wenye silaha waliokuwa mle kambini.
12 Les Madianites et les Amalécites, et tous les fils de l'Orient, étaient couchés dans la vallée comme des sauterelles, en grand nombre; et leurs chameaux étaient innombrables, comme le sable qui est au bord de la mer, en grand nombre.
Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine yote ya mashariki walikaa bondeni, nao walikuwa mfano wa nzige kwa wingi wao. Ngamia zao hazikuhesabika, wingi wao ulikuwa kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.
13 Lorsque Gédéon arriva, voici qu'un homme racontait un rêve à son compagnon. Il dit: « Voici, j'ai eu un songe; et voici, un gâteau de pain d'orge est tombé dans le camp de Madian, est venu jusqu'à la tente, l'a frappée de telle sorte qu'elle est tombée, et l'a retournée, de sorte que la tente est restée à plat. »
Gideoni alifika wakati huo huo kukiwa na mtu mmoja aliyekuwa anamweleza mwenzake ndoto yake, akisema, “Niliota ndoto: Tazama mkate wa shayiri ulioviringana ulianguka katika kambi moja ya Wamidiani, ukaipiga na ikaanguka nao ukaipindua juu chini na hema ikaporomoka chini.”
14 Son compagnon répondit: « Ce n'est autre que l'épée de Gédéon, fils de Joas, homme d'Israël. Dieu a livré Madian entre ses mains, avec toute son armée. »
Rafiki yake akamjibu, “Habari hii si kitu kingine zaidi ya upanga wa Gideoni mwana wa Yoashi, Mwisraeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi lote mkononi mwake.”
15 Lorsque Gédéon entendit le récit du rêve et son interprétation, il se prosterna. Puis il revint dans le camp d'Israël et dit: « Levez-vous, car Yahvé a livré entre vos mains l'armée de Madian! »
Gideoni alipoisikia hiyo ndoto na tafsiri yake, akamwabudu Mungu. Akarudi kwenye kambi ya Israeli na kusema, “Inukeni! Bwana amelitia jeshi la Wamidiani mikononi mwenu.”
16 Il divisa les trois cents hommes en trois compagnies, et il mit entre les mains de chacun d'eux des trompettes et des cruches vides, avec des torches dans les cruches.
Akawagawa wale watu 300 katika makundi matatu, akawakabidhi tarumbeta mikononi mwao wote na mitungi isiyokuwa na maji yenye mienge ndani yake.
17 Il leur dit: « Observez-moi, et faites de même. Voici, quand j'arriverai à l'extrémité du camp, vous ferez ce que je fais.
Akawaambia, “Nitazameni, fanyeni kama nitakavyofanya, nitakapofika mwisho wa kambi mfanye kama nitakavyofanya.
18 Quand je sonnerai de la trompette, moi et tous ceux qui sont avec moi, vous sonnerez aussi des trompettes de tous les côtés de tout le camp, et vous crierez: « Pour l'Éternel et pour Gédéon ».
Wakati mimi na wale walio pamoja nami wote, tutakapopiga tarumbeta zetu, ninyi nanyi pigeni tarumbeta pande zote za kambi na mpige kelele, mseme, ‘Upanga wa Bwana na wa Gideoni.’”
19 Et Gédéon et les cent hommes qui étaient avec lui arrivèrent à l'extrémité du camp, au commencement de la veille du milieu, quand on venait de commencer la veille. Ils sonnèrent des trompettes et brisèrent les cruches qu'ils avaient à la main.
Gideoni na wale watu 100 waliokuwa pamoja naye wakafika mwisho wa kambi usiku mwanzoni mwa zamu ya kati, mara tu walipokuwa wamebadili zamu. Wakapiga zile tarumbeta zao na kuvunja ile mitungi iliyokuwa mikononi mwao.
20 Les trois corps d'armée sonnèrent des trompettes, brisèrent les cruches, tinrent dans leur main gauche les torches et dans leur main droite les trompettes avec lesquelles ils sonnaient, et ils crièrent: « L'épée de Yahvé et de Gédéon ».
Yale makundi matatu yakapiga tarumbeta na kuvunja mitungi. Wakashika mienge kwa mikono yao ya kushoto na katika mikono yao ya kuume tarumbeta ili kuzipiga, wakapaza sauti zao, “Upanga wa Bwana na wa Gideoni!”
21 Ils se tinrent chacun à sa place autour du camp, et toute l'armée accourut; ils crièrent et les mirent en fuite.
Wakasimama kila mtu mahali pake kuizunguka kambi pande zote, Wamidiani wote wakakimbia, huku wakipiga kelele.
22 On sonna des trois cents trompettes, et l'Éternel mit l'épée de chacun contre son compagnon et contre toute l'armée; et l'armée s'enfuit jusqu'à Beth Shittah, vers Zérach, jusqu'à la frontière d'Abel Meholah, vers Tabbath.
Walipozipiga zile tarumbeta 300, Bwana akafanya watu katika kambi yote kugeuziana upanga kila mmoja na mwenziwe. Jeshi likakimbia mpaka Beth-Shita kuelekea Serera hadi mpakani mwa Abel-Mehola karibu na Tabathi.
23 Les hommes d'Israël se rassemblèrent de Nephtali, d'Aser et de tout Manassé, et ils poursuivirent Madian.
Watu wa Israeli wakaitwa kutoka Naftali, Asheri na Manase, wakawafuatia Wamidiani.
24 Gédéon envoya des messagers dans toute la montagne d'Éphraïm, en disant: « Descendez contre Madian, et prenez les eaux devant eux jusqu'à Beth Bara, jusqu'au Jourdain. » Tous les hommes d'Ephraïm se rassemblèrent donc et prirent les eaux jusqu'à Beth Bara, le Jourdain.
Gideoni akatuma wajumbe katika nchi yote ya vilima vya Efraimu akisema, “Teremkeni dhidi ya Wamidiani na mkazuie vivuko vya maji mbele yao hadi Beth-Bara na pia Yordani.” Hivyo watu wote wa Efraimu wakakutanika pamoja na kuzingira mto wa Yordani hadi Beth-Bara.
25 Ils prirent les deux princes de Madian, Oreb et Zeeb. Ils tuèrent Oreb au rocher d'Oreb, et ils tuèrent Zeeb au pressoir de Zeeb, pendant qu'ils poursuivaient Madian. Puis ils apportèrent les têtes d'Oreb et de Zeeb à Gédéon, de l'autre côté du Jourdain.
Wakawakamata wakuu wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu. Wakamuulia Orebu pale penye mwamba wa Orebu, na Zeebu wakamuulia penye shinikizo la kukamulia divai la Zeebu. Wakawafuatia Wamidiani na kuleta vichwa vya Orebu na Zeebu kwa Gideoni, huko ngʼambo ya Yordani.