< Juges 6 >
1 Les enfants d'Israël firent ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, et l'Éternel les livra entre les mains de Madian pendant sept ans.
Waisraeli wakafanya tena yaliyo maovu mbele za Bwana, naye kwa miaka saba Bwana akawatia mikononi mwa Wamidiani.
2 La main de Madian l'emporta sur Israël, et les enfants d'Israël se firent, à cause de Madian, des repaires dans les montagnes, des cavernes et des forteresses.
Mkono wa Midiani ukawa na nguvu dhidi ya Israeli na kwa ajili ya Wamidiani, Waisraeli wakajitengenezea mahali pa kujificha milimani, kwenye mapango na ngome.
3 Lorsqu'Israël eut semé, les Madianites, les Amalécites et les fils de l'Orient montèrent contre eux.
Kila wakati Waisraeli walipopanda mazao mashambani, Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki walivamia nchi yao.
4 Ils campèrent contre eux et détruisirent les produits de la terre, jusqu'à ce que tu arrives à Gaza. Ils ne laissèrent en Israël aucune subsistance, ni brebis, ni bœuf, ni âne.
Wakapiga kambi katika mashamba yao na kuharibu mazao ya nchi yote hadi kufikia Gaza, wala hawakuacha kiumbe chochote kilicho hai kwa Waisraeli, iwe kondoo au ngʼombe au punda.
5 Car ils sont montés avec leur bétail et leurs tentes. Ils sont entrés comme des sauterelles pour la multitude. Ils étaient innombrables, eux et leurs chameaux, et ils sont entrés dans le pays pour le détruire.
Walipanda na mifugo yao na mahema yao, mfano wa makundi ya nzige. Ilikuwa haiwezekani kuwahesabu watu na ngamia zao; wakavamia nchi ili kuiharibu.
6 Israël fut très humilié à cause de Madian, et les enfants d'Israël crièrent à l'Éternel.
Waisraeli wakafanywa kuwa maskini sana na Wamidiani, hata Israeli wakamlilia Bwana kuomba msaada.
7 Lorsque les enfants d'Israël crièrent à Yahvé à cause de Madian,
Waisraeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Wamidiani,
8 Yahvé envoya un prophète aux enfants d'Israël, qui leur dit: « Yahvé, le Dieu d'Israël, dit: Je vous ai fait monter d'Égypte et je vous ai fait sortir de la maison de servitude.
Bwana akawapelekea nabii, ambaye aliwaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Niliwapandisha mtoke Misri, toka nchi ya utumwa.
9 Je vous ai délivrés de la main des Égyptiens et de la main de tous ceux qui vous opprimaient, je les ai chassés devant vous et je vous ai donné leur pays.
Nikawanyakua kutoka mikononi mwa Wamisri na kutoka mikononi mwa watesi wenu wote. Nikawafukuza watoke mbele yenu nami nikawapa ninyi nchi yao.
10 Je t'ai dit: « Je suis Yahvé, ton Dieu. Tu ne craindras pas les dieux des Amoréens, dans le pays desquels tu habites. » Mais vous n'avez pas écouté ma voix.'"
Nikawaambia, ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; msiiabudu miungu ya Waamori, ambayo mnakaa katika nchi yao!’ Lakini ninyi hamkuitii sauti yangu.”
11 L'ange de Yahvé vint s'asseoir sous le chêne qui était à Ophra, et qui appartenait à Joas, l'Abiézerite. Son fils Gédéon battait le blé dans le pressoir, pour le cacher aux Madianites.
Malaika wa Bwana akaja akaketi chini ya mti wa mwaloni huko Ofra, ambao ulikuwa mali ya Yoashi, Mwabiezeri, ambako Gideoni mwanawe alikuwa akipepeta ngano penye shinikizo la kukamulia zabibu, ili kuificha Wamidiani wasiione.
12 L'ange de Yahvé lui apparut et lui dit: « Yahvé est avec toi, vaillant homme! »
Malaika wa Bwana alipomtokea Gideoni, akamwambia, “Bwana yu pamoja nawe, Ewe shujaa mwenye nguvu.”
13 Gédéon lui dit: « Oh, mon seigneur, si Yahvé est avec nous, pourquoi donc tout cela nous est-il arrivé? Où sont passées toutes les merveilles dont nos pères nous ont parlé, en disant: « Yahvé ne nous a-t-il pas fait monter d'Égypte? Mais maintenant, Yahvé nous a rejetés et nous a livrés entre les mains de Madian. »
Gideoni akajibu, “Ee Bwana wangu, kama Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametutokea? Yako wapi basi yale matendo yake makuu baba zetu waliyotusimulia juu yake waliposema, ‘Je, Bwana hakutupandisha kutoka Misri?’ Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia katika mkono wa Midiani.”
14 L'Éternel le regarda et dit: « Va avec ta force, et sauve Israël de la main de Madian. Ne t'ai-je pas envoyé? »
Bwana akamgeukia na kusema “Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli kutoka mikononi mwa Wamidiani. Je, si mimi ninayekutuma wewe?”
15 Il lui dit: « Seigneur, comment sauverai-je Israël? Voici, ma famille est la plus pauvre de Manassé, et je suis le plus petit dans la maison de mon père. »
Gideoni akauliza, “Ee Bwana wangu, nitawezaje kuwaokoa Israeli? Ukoo wangu ndio dhaifu kuliko zote katika Manase, nami ndiye mdogo wa wote katika jamaa yangu.”
16 Yahvé lui dit: « Je serai avec toi, et tu frapperas les Madianites comme un seul homme. »
Bwana akamjibu, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kana kwamba walikuwa ni mtu mmoja.”
17 Il lui dit: « Si maintenant j'ai trouvé grâce à tes yeux, montre-moi un signe que c'est toi qui me parles.
Gideoni akajibu, “Kama basi nimepata kibali machoni pako, nipe ishara kuonyesha kweli kwamba ni wewe unayesema nami.
18 Ne t'en va pas, je te prie, jusqu'à ce que je vienne à toi, que j'apporte mon cadeau et que je le dépose devant toi. » Il a dit: « Je vais attendre que tu reviennes. »
Tafadhali ninakuomba usiondoke hapa mpaka nitakaporudi na kukuletea sadaka yangu na kuiweka mbele yako.” Naye Bwana akamwambia, “Nitangoja mpaka utakaporudi.”
19 Gédéon entra et prépara un chevreau et des gâteaux sans levain d'un épha de farine. Il mit la viande dans un panier et il mit le bouillon dans un pot; il l'apporta sous le chêne et le présenta.
Gideoni akaingia ndani ya nyumba yake na kuandaa mwana-mbuzi pamoja na kuoka mikate isiyotiwa chachu kutokana na efa moja ya unga. Akaweka nyama kwenye kikapu na mchuzi kwenye chungu, akamletea huyo malaika hapo nje chini ya mti wa mwaloni na kumpa.
20 L'ange de Dieu lui dit: « Prends la viande et les gâteaux sans levain, pose-les sur ce rocher, et verse le bouillon. » Il fit ainsi.
Malaika wa Mungu akamwambia, “Itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu, uviweke juu ya mwamba huu na umimine huo mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo.
21 Et l'ange de Yahvé étendit l'extrémité du bâton qu'il avait à la main, et toucha la viande et les gâteaux sans levain; et le feu monta du rocher et consuma la viande et les gâteaux sans levain. Puis l'ange de Yahvé s'en alla hors de sa vue.
Malaika wa Bwana akainyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake, ncha yake ikagusa ile nyama na ile mikate isiyotiwa chachu, nao moto ukatoka kwenye mwamba ukateketeza ile nyama na ile mikate. Malaika wa Bwana akatoweka kutoka machoni pake.
22 Gédéon vit que c'était l'ange de Yahvé; et Gédéon dit: « Hélas, Seigneur Yahvé! Car j'ai vu l'ange de Yahvé face à face! »
Gideoni alipotambua kuwa ni malaika wa Bwana, akapiga kelele kwa mshangao, akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenyezi! Kwa kuwa nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”
23 Yahvé lui dit: « Que la paix soit avec toi! N'aie pas peur. Tu ne mourras pas. »
Lakini Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope. Hutakufa.”
24 Et Gédéon y construisit un autel à Yahvé et l'appela « Yahvé est paix ». Aujourd'hui encore, il se trouve à Ophra, chez les Abiézrites.
Hivyo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu mahali pale na kupaita, Yehova-Shalom. Mpaka leo ingalipo imesimama huko Ofra ya Waabiezeri.
25 Cette même nuit, Yahvé lui dit: « Prends le taureau de ton père, le second taureau âgé de sept ans, et jette l'autel de Baal que ton père a, et coupe l'ashère qui est à côté.
Usiku ule ule Bwana akamwambia, “Mchukue ngʼombe dume wa baba yako, yaani, yule wa pili mwenye miaka saba, na ubomoe madhabahu ya Baali aliyo nayo baba yako, na ukaikate Ashera iliyo karibu nayo.
26 Puis tu construiras un autel à Yahvé, ton Dieu, sur le sommet de cette forteresse, de façon ordonnée, et tu prendras le second taureau, et tu offriras un holocauste avec le bois de l'ashère que tu abattras. »
Kisha mjengee Bwana Mungu wako, madhabahu halisi, kwa taratibu zake, juu ya huu mwamba. Kwa kutumia kuni za hiyo nguzo ya Ashera uliyoikatakata, mtoe sadaka huyo dume wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa.”
27 Alors Gédéon prit dix hommes parmi ses serviteurs et fit ce que Yahvé lui avait dit. Comme il craignait la maison de son père et les hommes de la ville, il ne put le faire de jour, mais il le fit de nuit.
Basi Gideoni akawachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa kuwa aliwaogopa jamaa yake na watu wa mji, akafanya haya usiku badala ya mchana.
28 Les gens de la ville se levèrent de bon matin, et voici, l'autel de Baal était démoli, l'idole d'Astarté qui était près de lui était coupée, et le second taureau était offert sur l'autel qui avait été bâti.
Watu wa mji walipoamka asubuhi, tazama madhabahu ya Baali imebomolewa na nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwakatwa na yule ngʼombe wa pili ametolewa sadaka juu ya madhabahu yaliyojengwa upya!
29 Ils se dirent les uns aux autres: « Qui a fait cela? » Quand ils se sont renseignés et ont demandé, ils ont dit: « Gédéon, fils de Joash, a fait cette chose. »
Wakaulizana, “Ni nani aliyetenda mambo haya?” Walipochunguza kwa makini, wakaambiwa, “Ni Gideoni mwana wa Yoashi, ndiye alitenda hivi.”
30 Alors les gens de la ville dirent à Joas: « Fais sortir ton fils, et qu'il meure, parce qu'il a démoli l'autel de Baal et qu'il a abattu l'ashère qui était près de lui. »
Watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mlete mwanao hapa. Ni lazima afe, kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali na kukatakata nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo.”
31 Joas dit à tous ceux qui s'opposaient à lui: « Allez-vous lutter pour Baal? Ou le sauverez-vous? Que celui qui le défendra soit mis à mort dès demain matin! Si c'est un dieu, qu'il se défende lui-même, car on a démoli son autel! »
Lakini Yoashi akauambia ule umati uliokuwa umezunguka ukiwa kinyume naye, “Je, ninyi mtamtetea Baali? Mnajaribu kumwokoa? Yeyote mwenye kumpigania atauawa kufikia kesho asubuhi! Kama Baali ni mungu kweli, anaweza kujitetea mwenyewe wakati mtu anapobomoa madhabahu yake.”
32 C'est pourquoi, ce jour-là, il lui donna le nom de Jerub-Baal, en disant: « Que Baal conteste contre lui, car il a démoli son autel. »
Basi siku ile wakamwita Gideoni “Yerub-Baali,” yaani, “Baali na ashindane naye,” kwa sababu alibomoa madhabahu yake.
33 Et tous les Madianites et les Amalécites et les fils de l'Orient se rassemblèrent; et ils passèrent et campèrent dans la vallée de Jizréel.
Basi Wamidiani wote, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki wakaunganisha majeshi yao, wakavuka ngʼambo ya Yordani na kupiga kambi katika Bonde la Yezreeli.
34 Mais l'Esprit de Yahvé vint sur Gédéon, et il sonna de la trompette; et Abiezer se rassembla pour le suivre.
Ndipo Roho wa Bwana akamjia Gideoni, akapiga tarumbeta, akiwaita Waabiezeri ili wamfuate.
35 Il envoya des messagers dans tout Manassé, et eux aussi se rassemblèrent pour le suivre. Il envoya des messagers à Aser, à Zabulon et à Nephtali, et ils montèrent à leur rencontre.
Akatuma wajumbe waende katika Manase yote, akiwataka wachukue silaha na pia katika Asheri, Zabuloni na Naftali, nao wakakwea ili kukutana nao.
36 Gédéon dit à Dieu: « Si tu veux sauver Israël par ma main, comme tu l'as dit,
Gideoni akamwambia Mungu, “Kama utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi:
37 voici, je mettrai une toison de laine sur l'aire de battage. S'il y a de la rosée sur la toison seulement, et qu'il y ait du sec sur tout le sol, alors je saurai que tu sauveras Israël par ma main, comme tu l'as dit. »
tazama, nitaweka ngozi ya kondoo kwenye kiwanja cha kupuria nafaka, na kama utakuwepo umande juu ya ngozi tu, nayo ardhi yote ikiwa kavu, ndipo nitakapojua kuwa utaokoa Israeli kwa mkono wangu, kama ulivyosema.”
38 Il en fut ainsi, car il se leva de bonne heure le lendemain, pressa la toison et en tira la rosée, une coupe pleine d'eau.
Hivyo ndivyo ilivyotokea. Gideoni akaamka asubuhi na mapema kesho yake, akaikamua ile ngozi, umande ukatoka, maji ya kujaa bakuli.
39 Gédéon dit à Dieu: « Que ta colère ne s'enflamme pas contre moi, et je ne parlerai que cette fois-ci. Laisse-moi, je t'en prie, faire l'épreuve de la toison pour cette fois seulement. Qu'il n'y ait de sec que sur la toison, et sur toute la terre, qu'il y ait de la rosée. »
Kisha Gideoni akamwambia Bwana, “Usinikasirikie. Ninaomba nifanye ombi moja lingine. Niruhusu nifanye jaribio jingine moja kwa ngozi hii. Wakati huu uifanye ngozi hii kavu na ardhi yote ifunikwe na umande.”
40 Dieu fit ainsi cette nuit-là, car il faisait sec sur la toison seulement, et il y avait de la rosée sur toute la terre.
Usiku ule Mungu akafanya hivyo. Ngozi ile ilikuwa kavu, nayo ardhi yote ikafunikwa na umande.