< Juges 3 >

1 Voici les nations que l'Éternel laissa pour mettre Israël à l'épreuve par elles, tous ceux qui n'avaient pas connu toutes les guerres de Canaan,
Sasa Bwana aliyaacha mataifa haya yaijaribu Israeli, yaani kila mtu katika Israeli ambaye hakushiriki vita yoyote huko Kanaani.
2 afin que les générations des enfants d'Israël le sachent, pour leur apprendre la guerre, du moins à ceux qui ne l'avaient pas connue auparavant:
(Alifanya hivyo ili kuwafundisha vita kizazi kipya cha Waisraeli ambao hawakujua kabla).
3 les cinq princes des Philistins, tous les Cananéens, les Sidoniens et les Héviens qui habitaient la montagne du Liban, depuis la montagne de Baal Hermon jusqu'à l'entrée de Hamath.
Haya ndio mataifa: wafalme watano kutoka kwa Wafilisti, Wakanaani wote, Wasidoni, na Wahivi waliokaa milima ya Lebanoni, kutoka Mlima Baali Hermoni hadi Hamathi.
4 On les laissa pour éprouver Israël par eux, afin de savoir s'ils écouteraient les commandements de l'Éternel, qu'il avait prescrits à leurs pères par Moïse.
Mataifa haya yaliachwa kama njia ambayo Bwana angeijaribu Israeli, kuthibitisha kama watazitii amri alizowapa babu zao kupitia Musa.
5 Les enfants d'Israël habitaient parmi les Cananéens, les Hittites, les Amorites, les Perizzites, les Hivvites et les Jébusites.
Basi wana wa Israeli wakakaa kati ya Wakanaani, na Wahiti, na Waamori, na Waperizi, na Wahivi, na Wayebusi.
6 Ils prirent leurs filles pour femmes, donnèrent leurs propres filles à leurs fils et servirent leurs dieux.
Waliwachukua binti zao kuwa wake zao, nao wakawapa wana wao binti zao, nao wakaitumikia miungu yao.
7 Les enfants d'Israël firent ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, ils oublièrent l'Éternel, leur Dieu, et servirent les Baals et les Ashéroths.
Wana wa Israeli walifanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wakamsahau Bwana, Mungu wao. Waliabudu Baali na Asherah.
8 La colère de l'Éternel s'enflamma contre Israël, et il les vendit entre les mains de Cushan Rishathaim, roi de Mésopotamie; les enfants d'Israël furent au service de Cushan Rishathaim pendant huit ans.
Basi, hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawauza mkononi mwa Kushan-rishathaimu mfalme wa Aram Naharaimu. Watu wa Israeli walitumikia Kushan Rishathaimu kwa miaka nane.
9 Lorsque les enfants d'Israël crièrent à l'Éternel, l'Éternel suscita aux enfants d'Israël un sauveur qui les sauva, Othniel, fils de Kenaz, frère cadet de Caleb.
Watu wa Israeli walipomwomba Bwana, Bwana akamuinua mtu atakayewasaidia wana wa Israeli, na mtu atakayewaokoa: Othnieli mwana wa Kenazi (ndugu mdogo wa Kalebu).
10 L'Esprit de Yahvé descendit sur lui, et il jugea Israël. Il partit en guerre, et Yahvé livra entre ses mains Cushan Rishathaim, roi de Mésopotamie. Sa main l'emporta sur Cushan Rishathaim.
Roho wa Bwana akamtia nguvu, naye akahukumu Israeli na akatoka kwenda vitani. Bwana akampa kuishinda Kush-rishataimu mfalme wa Aramu. Mkono wa Othnieli alishinda Kushan Rishathaimu.
11 Le pays fut en repos pendant quarante ans, puis Othniel, fils de Kenaz, mourut.
Nchi ilikuwa na amani kwa miaka arobaini. Ndipo Otinieli mwana wa Kenazi akafa.
12 Les enfants d'Israël firent encore ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, et l'Éternel fortifia Églon, roi de Moab, contre Israël, parce qu'ils avaient fait ce qui est mal aux yeux de l'Éternel.
Baada ya hayo, Waisraeli wakafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana; Bwana akampa Egloni mfalme wa Moabu nguvu, kuwashinda Waisraeli.
13 Il rassembla à lui les fils d'Ammon et d'Amalek, et il alla frapper Israël, et ils possédèrent la ville des palmiers.
Eglon alijiunga na wana wa Amoni na Waamaleki wakaenda na kuwashinda Israeli, na walichukua mji wa Mitende.
14 Les enfants d'Israël servirent Églon, roi de Moab, pendant dix-huit ans.
Watu wa Israeli walimtumikia Eglon mfalme wa Moabu kwa miaka kumi na nane.
15 Mais lorsque les enfants d'Israël crièrent à Yahvé, Yahvé leur suscita un sauveur: Ehud, fils de Gera, le Benjamite, un gaucher. Les enfants d'Israël envoyèrent par lui un tribut à Eglon, roi de Moab.
Wana wa Israeli walipomwomba Bwana, Bwana akamwinua mtu aliyewasaidia, Ehudi mwana wa Gera, Mbenjamini, mtu shoto. Wana wa Israeli wakamtuma kwa Egloni, mfalme wa Moabu, kwa malipo yao ya kodi.
16 Ehud se fabriqua une épée à deux tranchants, longue d'une coudée, qu'il porta sous ses vêtements, sur sa cuisse droite.
Ehudi akajifanyia upanga uliokuwa na makali kuwili, urefu wa dhiraa moja; aliufunga chini ya nguo zake juu ya mguu wake wa kulia.
17 Il offrit le tribut à Églon, roi de Moab. Or Églon était un homme très gras.
Akampa Egloni Mfalme wa Moabu malipo ya kodi. (Egloni alikuwa mtu mnene sana.)
18 Quand Ehud eut fini d'offrir le tribut, il renvoya les gens qui portaient le tribut.
Baada ya Ehudi kulipa malipo ya kodi, aliondoka na wale waliokuwa wameibeba.
19 Mais lui-même s'éloigna des idoles de pierre qui se trouvaient près de Gilgal et dit: « J'ai un message secret pour toi, ô roi. » Le roi dit: « Tais-toi! » Tous ceux qui se tenaient près de lui le quittèrent.
Hata hivyo Ehudi mwenyewe, alipofikia mahali ambapo sanamu za kuchonga zilitengenezwa karibu na Gilgali, akageuka na kurudi, akasema, 'Nina ujumbe wa siri kwako, mfalme wangu.' Eglon akasema, 'Nyamazeni kimya!' Kwa hiyo wote waliomtumikia wakatoka kwenye chumba.
20 Ehud vint le trouver, et il était assis seul dans la chambre haute et fraîche. Ehud dit: « J'ai un message de Dieu pour toi. » Il se leva de son siège.
Ehudi akaja kwake. Mfalme alikuwa amekaa peke yake, peke yake katika chumba cha juu cha baridi. Ehudi akasema, 'Nina ujumbe kutoka kwa Mungu kwa ajili yeko.' Mfalme akasimama kutoka katika kiti chake.
21 Ehud étendit sa main gauche, prit l'épée de sa cuisse droite et se la planta dans le corps.
Ehudi akanyoosha mkono wake wa kushoto na akachukua upanga kutoka mguu wake wa kulia, na akautia ndani ya mwili wa mfalme.
22 La poignée entra aussi après la lame; et la graisse se referma sur la lame, car il n'avait pas retiré l'épée de son corps; et elle sortit par derrière.
Na kipini cha upanga kikaingia ndani yake baada ya upanga, nao ukatokea nyuma yake, na mafuta yakashikamana juu ya upanga, kwa kuwa Ehudi hakuutoa upanga nje ya mwili wake.
23 Ehud sortit sur le portique, ferma sur lui les portes de la chambre haute et les verrouilla.
Kisha Ehudi akatoka kwenye ukumbi na akafunga milango ya chumba cha juu nyuma yake na akawafungia.
24 Après qu'il fut parti, ses serviteurs vinrent et virent que les portes de la chambre haute étaient fermées. Ils dirent: « Il est sûrement en train de se couvrir les pieds dans la chambre haute. »
Baada ya Ehudi kuondoka, watumishi wa mfalme wakaja; wakaona milango ya chumba cha juu imefungwa, kwa hiyo wakafikiri, 'Hakika atakuwa anajitoa mwenyewe katika hali ya baridi ya chumba cha juu.'
25 Ils attendirent jusqu'à ce qu'ils aient honte; et voici qu'il n'ouvrait pas les portes de la chambre haute. Ils prirent donc la clé et les ouvrirent, et voici que leur seigneur était tombé mort sur le sol.
Walizidi kuwa na wasiwasi hata walipoanza kuhisi kuwa walikuwa wakipuuza wajibu wao wakati mfalme bado hakufungua milango ya chumba cha juu. Kwa hiyo walichukua ufunguo wakawafungua, tazama bwana wao, ameanguka chini, amekufa.
26 Ehud s'échappa pendant qu'ils attendaient, passa au-delà des idoles de pierre et se sauva à Seirah.
Wakati watumishi wakisubiri, wakijiuliza nini wanapaswa kufanya, Ehudi alikimbia na kupita mahali ambako kulikuwa na sanamu za kuchonga, na hivyo akakimbia kwenda Seira.
27 Lorsqu'il fut arrivé, il sonna de la trompette dans la montagne d'Ephraïm; les enfants d'Israël descendirent avec lui de la montagne, et il les conduisit.
Alipofika, alipiga tarumbeta katika nchi ya mlima wa Efraimu. Kisha wana wa Israeli wakashuka pamoja naye kutoka milimani, naye akawaongoza.
28 Il leur dit: « Suivez-moi, car Yahvé a livré entre vos mains les Moabites, vos ennemis. » Ils le suivirent et prirent les gués du Jourdain contre les Moabites, et ne permirent à aucun homme de passer.
Akawaambia, Nifuate, kwa kuwa Bwana atawashinda adui zenu, Wamoabu. Wakamfuata, wakakamata vivuko vya Bonde la Yordani, toka kwa Wamoabi, wala hawakuruhusu mtu yeyote kuvuka mto.
29 Ils frappèrent en ce temps-là environ dix mille hommes de Moab, tous les hommes forts et tous les hommes valeureux. Aucun homme n'échappa.
Wakati huo waliwaua watu elfu kumi wa Moabu, na wote walikuwa watu wenye nguvu na wenye uwezo. Hakuna aliyekimbia.
30 Moab fut donc soumis en ce jour sous la main d'Israël. Et le pays fut en repos pendant quatre-vingts ans.
Kwa hiyo siku hiyo Moabu ilishindwa na nguvu ya Israeli. Na nchi ilikuwa na amani kwa miaka thelathini.
31 Après lui, Shamgar, fils d'Anath, frappa six cents hommes des Philistins avec un aiguillon à bœuf. Il sauva aussi Israël.
Baada ya Ehudi, mwamuzi aliyefuata alikuwa Shamgari mwana wa Anathi ambaye aliwaua Wafilisti 600 kwa konzo la ng'ombe. Pia aliwaokoa Israeli kutoka kwenye hatari.

< Juges 3 >