< Juges 20 >
1 Alors tous les enfants d'Israël sortirent, et l'assemblée se rassembla comme un seul homme, depuis Dan jusqu'à Beer Schéba, avec le pays de Galaad, vers l'Éternel à Mitspa.
Ndipo Waisraeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na wa kutoka nchi ya Gileadi wakatoka kama mtu mmoja wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
2 Les chefs de tout le peuple, de toutes les tribus d'Israël, se présentèrent à l'assemblée du peuple de Dieu, quatre cent mille hommes de pied tirant l'épée.
Viongozi wote wa kabila za Israeli wakakaa kwenye nafasi zao katika kusanyiko la watu wa Mungu, askari 400,000 waendao kwa miguu wenye panga.
3 (Les enfants de Benjamin apprirent que les enfants d'Israël étaient montés à Mitspa.) Les enfants d'Israël dirent: « Dis-nous, comment cette méchanceté est-elle arrivée? »
(Wabenyamini wakasikia kuwa Waisraeli wamepanda kwenda Mispa.) Ndipo Waisraeli wakasema, “Tuelezeni jinsi jambo hili ovu lilivyotendeka.”
4 Le Lévite, mari de la femme assassinée, répondit: « Je suis venu à Guibea, qui appartient à Benjamin, moi et ma concubine, pour passer la nuit.
Hivyo yule Mlawi, mume wa yule mwanamke aliyeuawa, akasema, “Mimi na suria wangu tulifika Gibea ya Benyamini ili tulale huko.
5 Les hommes de Guibea se sont soulevés contre moi et ont encerclé la maison pendant la nuit. Ils voulaient me tuer, ils ont violé ma concubine, et elle est morte.
Wakati wa usiku watu wa Gibea wakanijia na kuizingira nyumba, wakitaka kuniua. Wakambaka suria wangu mpaka akafa.
6 J'ai pris ma concubine, je l'ai coupée en morceaux, et je l'ai envoyée dans tout le pays de l'héritage d'Israël, car on s'est livré à la débauche et à la folie en Israël.
Ndipo nikamchukua suria wangu, nikamkatakata vipande vipande na kuvipeleka katika nchi yote ya urithi wa Israeli, kwa kuwa wametenda uasherati mkubwa na jambo la aibu katika Israeli.
7 Voici, vous, enfants d'Israël, vous tous, donnez ici vos avis et vos conseils. »
Sasa, ninyi Waisraeli wote, semeni na mtoe uamuzi wenu.”
8 Tout le peuple se leva comme un seul homme, et dit: Aucun de nous n'ira à sa tente, et aucun de nous ne se tournera vers sa maison.
Watu wote wakainuka wakasema, kama mtu mmoja, “Hakuna hata mmoja wetu atakayekwenda nyumbani. Wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
9 Voici maintenant ce que nous ferons à Guibea: nous monterons contre elle par le sort;
Sasa hili ndilo tutakaloitendea Gibea: Tutaikabili jinsi kura itakavyotuongoza.
10 et nous prendrons dix hommes sur cent dans toutes les tribus d'Israël, cent sur mille, et mille sur dix mille, pour procurer de la nourriture au peuple, afin qu'il fasse, en arrivant à Guibea de Benjamin, toutes les folies que les hommes de Guibea ont commises en Israël. »
Tutatoa watu kumi katika kila 100 kutoka kwenye kabila zote za Israeli, watu 100 katika watu 1,000 na watu 1,000 katika 10,000, ili waende wakalete mahitaji kwa ajili ya jeshi. Basi wakati jeshi litakapofika Gibea ya Benyamini, watawatendea yale wanayostahili, kwa ajili ya uovu huu wa aibu waliotenda katika Israeli.”
11 Et tous les hommes d'Israël se rassemblèrent contre la ville, unis comme un seul homme.
Hivyo wanaume wote wa Israeli wakakutanika pamoja na kujiunga kama mtu mmoja dhidi ya huo mji.
12 Les tribus d'Israël envoyèrent des hommes dans toute la tribu de Benjamin, en disant: « Quelle est cette méchanceté qui est arrivée parmi vous?
Makabila ya Israeli yakatuma watu kwenda katika kabila la Benyamini lote na kuwaambia, “Ni uovu gani huu wa kutisha uliotendeka katikati yenu?
13 Maintenant, livrez les hommes, les méchants qui sont à Guibea, afin que nous les fassions mourir et que nous fassions disparaître le mal d'Israël. » Mais Benjamin ne voulut pas écouter la voix de ses frères, les enfants d'Israël.
Basi watoeni hao watu waovu kabisa walioko Gibea, ili tupate kuwaua na kuondoa uovu katika Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakuwasikia ndugu zao, Waisraeli.
14 Les fils de Benjamin se rassemblèrent des villes jusqu'à Guibea, pour aller combattre les enfants d'Israël.
Wakatoka katika miji yao, wakakutanika Gibea ili kupigana na Waisraeli.
15 Ce jour-là, on compta parmi les enfants de Benjamin, sur les villes, vingt-six mille hommes tirant l'épée, sans compter les habitants de Guibea, qui étaient au nombre de sept cents hommes d'élite.
Siku ile Wabenyamini wakakusanya watu 26,000 kutoka miji yao, waliojifunga panga, mbali na hao 700 waliochaguliwa miongoni mwa hao waliokaa Gibea.
16 Parmi tous ces soldats, il y avait sept cents hommes d'élite qui étaient gauchers. Chacun d'eux pouvait lancer une pierre à un cheveu sans la manquer.
Miongoni mwa hao askari wote kulikuwa na watu 700 bora waliochaguliwa watumiao mkono wa kushoto, kila mmoja wao aliweza kutupa jiwe kwa kombeo na kulenga unywele mmoja bila kukosa.
17 Les hommes d'Israël, outre Benjamin, comptèrent quatre cent mille hommes tirant l'épée. Tous ces hommes étaient des hommes de guerre.
Nao watu wa Israeli, mbali na hao wa Benyamini, wakakusanya watu waume 400,000, wenye kutumia panga, wote hao walikuwa mashujaa.
18 Les enfants d'Israël se levèrent, montèrent à Béthel, et demandèrent conseil à Dieu. Ils demandèrent: « Qui montera le premier pour nous dans la bataille contre les enfants de Benjamin? » Yahvé a dit: « Juda d'abord. »
Waisraeli wakapanda Betheli na kumuuliza Mungu, “Ni nani miongoni mwetu atakayetangulia mbele yetu ili kupigana na Wabenyamini?” Bwana akawajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia.”
19 Les enfants d'Israël se levèrent le matin et campèrent devant Guibea.
Asubuhi yake Waisraeli wakaamka na kupiga kambi karibu na Gibea.
20 Les hommes d'Israël sortirent pour combattre Benjamin, et les hommes d'Israël se rangèrent en bataille contre eux à Guibea.
Waisraeli wakatoka kupigana na Wabenyamini, nao Waisraeli wakajiweka kwenye nafasi zao katika vita dhidi yao huko Gibea.
21 Les enfants de Benjamin sortirent de Guibea et, ce jour-là, ils détruisirent par terre vingt-deux mille hommes des Israélites.
Wabenyamini wakatoka Gibea na kuwaua watu 22,000 wa Israeli siku ile.
22 Le peuple, les hommes d'Israël, s'encouragèrent et se rangèrent en bataille à l'endroit où ils s'étaient rangés le premier jour.
Lakini Waisraeli wakatiana moyo kila mmoja na mwenzake, nao wakajiweka kwenye nafasi zao katika vile vita mara ya pili mahali pale walipokuwa wamejiweka mara ya kwanza.
23 Les enfants d'Israël montèrent et pleurèrent devant l'Éternel jusqu'au soir, et ils demandèrent à l'Éternel: « M'approcherai-je encore pour combattre les enfants de Benjamin, mon frère? » Yahvé a dit: « Monte contre lui. »
Waisraeli wakapanda mbele za Bwana na kulia mbele zake mpaka jioni, nao wakamuuliza Bwana wakisema, “Je, tupande tena kupigana vita na Wabenyamini, ndugu zetu?” Bwana akajibu, “Pandeni mkapigane nao.”
24 Les enfants d'Israël s'approchèrent des enfants de Benjamin le second jour.
Ndipo Waisraeli wakawakaribia Wabenyamini siku ya pili.
25 Benjamin sortit contre eux de Guibea, le second jour, et il détruisit encore par terre dix-huit mille hommes des enfants d'Israël. Tous tirèrent l'épée.
Wakati huu, Wabenyamini walipotoka Gibea ili kupigana nao, wakawaua watu Waisraeli 18,000, wote wakiwa wamejifunga panga.
26 Alors tous les enfants d'Israël et tout le peuple montèrent et vinrent à Béthel; ils pleurèrent, s'assirent là devant l'Éternel, et jeûnèrent ce jour-là jusqu'au soir; puis ils offrirent devant l'Éternel des holocaustes et des sacrifices de prospérité.
Ndipo Waisraeli, watu wote, wakapanda Betheli, huko wakakaa mbele za Bwana wakilia. Wakafunga siku ile mpaka jioni na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani kwa Bwana.
27 Les enfants d'Israël demandèrent à l'Éternel (car l'arche de l'alliance de Dieu était là en ce temps-là,
Nao Waisraeli wakauliza kwa Bwana. (Katika siku hizo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa huko
28 et Phinées, fils d'Éléazar, fils d'Aaron, se tenait devant elle en ce temps-là): « Irai-je encore combattre les enfants de Benjamin, mon frère, ou bien cesserai-je? » Yahvé dit: « Monte, car demain je le livrerai entre tes mains. »
na Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Aroni, alikuwa anahudumu mbele za hilo Sanduku.) Wakauliza, “Je, tupande kwenda vitani kupigana tena na Wabenyamini ndugu zetu, au la?” Bwana akajibu, “Nendeni, kwa kuwa kesho nitawatia mikononi mwenu.”
29 Israël dressa des embuscades tout autour de Guibea.
Basi Waisraeli wakaweka waviziao kuizunguka Gibea.
30 Le troisième jour, les enfants d'Israël montèrent contre les enfants de Benjamin, et ils se rangèrent en bataille contre Guibea, comme les autres fois.
Kisha Waisraeli wakapanda kupigana na Wabenyamini katika siku ya tatu na kujiweka kwenye nafasi zao dhidi ya Gibea kama walivyokuwa wamefanya hapo kwanza.
31 Les Benjamites sortirent à l'encontre du peuple, et s'éloignèrent de la ville; ils se mirent à frapper et à tuer du peuple, comme les autres fois, sur les routes, dont l'une monte à Béthel et l'autre à Guibea, dans les champs, environ trente hommes d'Israël.
Wabenyamini wakatoka ili kukabiliana nao, Waisraeli wakawavuta Wabenyamini watoke katika mji. Wakaanza kupigana na kuua watu wapatao thelathini wa Israeli, kama walivyofanya nyakati nyingine, katika njia kuu, moja iendayo Betheli na nyingine Gibea.
32 Les fils de Benjamin dirent: « Ils sont frappés devant nous, comme au début. » Mais les enfants d'Israël dirent: « Fuyons, et attirons-les loin de la ville sur les routes. »
Wabenyamini wakafikiri, “Wanapigwa mbele yetu kama hapo kwanza.” Waisraeli wakasema, “Sisi na turudi nyuma ili tuwavute wauache mji waende kuelekea barabarani.”
33 Tous les hommes d'Israël se levèrent de leur place et se rangèrent en bataille devant Baal Tamar. Et les embusqueurs d'Israël sortirent de leur place, même de Maareh Guéba.
Watu wote wa Israeli wakaondoka kwenye sehemu zao na kujipanga huko Baal-Tamari, nao wale waviziaji wa Waisraeli, wakatoka hapo walipokuwa kwenye uwanda wa magharibi ya Gibea.
34 Dix mille hommes d'élite de tout Israël s'avancèrent contre Guibea, et le combat fut rude; mais ils ne savaient pas que le désastre était proche d'eux.
Ndipo watu 10,000 bora waliochaguliwa katika Israeli wote, wakaja kuishambulia Gibea. Vita vilikuwa vikali sana, hata Wabenyamini hawakutambua kuwa maangamizi yalikuwa karibu nao kwa kiasi hicho.
35 L'Éternel frappa Benjamin devant Israël, et les enfants d'Israël détruisirent ce jour-là vingt-cinq mille cent hommes de Benjamin. Tous tirèrent l'épée.
Bwana akawashinda Wabenyamini mbele ya Waisraeli na siku ile Waisraeli wakawaua Wabenyamini watu waume 25,100, wote wakiwa wenye kujifunga silaha za vita.
36 Les fils de Benjamin virent qu'ils étaient frappés, car les hommes d'Israël avaient cédé à Benjamin parce qu'ils avaient confiance dans les embusqueurs qu'ils avaient placés contre Gibéa.
Hivyo Wabenyamini wakaona kuwa wamepigwa. Basi Waisraeli walikuwa wameondoka mbele ya Wabenyamini, kwa sababu Waisraeli waliwategemea hao waviziaji waliokuwa wamewaweka dhidi ya Gibea.
37 Les embusqueurs se hâtèrent et se précipitèrent sur Gibéa; ils se répandirent et frappèrent toute la ville du tranchant de l'épée.
Wale waviziaji wakafanya haraka kuingia Gibea, wakasambaa na kuwaua watu wote wa mji kwa upanga.
38 Or le signe fixé entre les hommes d'Israël et les embusqueurs était de faire monter de la ville un grand nuage de fumée.
Waisraeli walikuwa wamepatana na hao waviziaji kuwa wangefanya lipande wingu kubwa la moshi kutoka huo mji,
39 Les hommes d'Israël se retournèrent dans la bataille, et Benjamin commença à frapper et à tuer environ trente personnes parmi les hommes d'Israël, car ils disaient: « Certainement ils ont été frappés devant nous, comme dans la première bataille. »
ndipo watu wa Waisraeli wangegeuka kupigana. Watu wa Benyamini walikuwa wameanza kuwapiga na kuua watu wa Israeli (wapatao thelathini), hivyo wakafikiri, “Hakika tutawapiga, kama tulivyowashinda katika vita hapo kwanza.”
40 Mais lorsque la nuée commença à s'élever de la ville en une colonne de fumée, les Benjamites regardèrent derrière eux, et voici que toute la ville montait en fumée vers le ciel.
Lakini wakati lile wingu la moshi lilipoanza kupanda kutoka ule mji, Wabenyamini wakageuka na kuona moshi wa mji mzima unapaa juu angani.
41 Les hommes d'Israël se retournèrent, et les hommes de Benjamin furent consternés, car ils virent que le désastre les atteignait.
Ndipo watu wa Israeli wakawageukia, nao Wabenyamini wakatiwa hofu, kwa kuwa walitambua kwamba maafa yamewajia.
42 Ils tournèrent le dos devant les hommes d'Israël pour prendre le chemin du désert, mais la bataille les suivit de près, et ceux qui sortirent des villes les détruisirent au milieu d'elles.
Basi wakakimbia mbele ya Waisraeli kuelekea nyikani, lakini hawakuweza kukwepa vile vita. Nao watu wa Israeli waliotoka katika ile miji wakawaua huko.
43 Ils entourèrent les Benjamites, les poursuivirent et les foulèrent aux pieds sur leur lieu de repos, jusqu'aux environs de Guibea, vers le lever du soleil.
Wakawazingira Wabenyamini pande zote, wakawafuatia na kuwapata hapo walipopumzika katika viunga vya Gibea upande wa mashariki.
44 Dix-huit mille hommes de Benjamin tombèrent; tous étaient des hommes valeureux.
Wakaanguka Wabenyamini 18,000 ambao wote ni mashujaa.
45 Ils se retournèrent et s'enfuirent vers le désert, au rocher de Rimmon. Ils en glanèrent cinq mille dans les chemins, les poursuivirent jusqu'à Gidom, et en battirent deux mille.
Walipogeuka na kukimbia kuelekea nyikani hata kufikia mwamba wa Rimoni, Waisraeli wakawaua watu 5,000 wakiwa njiani. Wakawafuata kwa kasi mpaka Gidomu huko wakawaua watu wengine 2,000.
46 Ainsi, tous ceux de Benjamin qui tombèrent ce jour-là furent vingt-cinq mille hommes qui tirèrent l'épée. Tous ceux-là étaient des hommes valeureux.
Siku ile wakawaua Wabenyamini 25,000 waliokuwa mashujaa wa vita.
47 Mais six cents hommes se détournèrent et s'enfuirent vers le désert, au rocher de Rimmon, et ils restèrent quatre mois au rocher de Rimmon.
Lakini watu 600 wakakimbia kuelekea nyikani katika mwamba wa Rimoni, na kukaa huko muda wa miezi minne.
48 Les hommes d'Israël se retournèrent contre les fils de Benjamin et les frappèrent du tranchant de l'épée, y compris toute la ville, le bétail et tout ce qu'ils trouvèrent. Ils incendièrent aussi toutes les villes qu'ils trouvèrent.
Waisraeli wakarudi na kuua watu wote wa Benyamini, pamoja na wanyama na kila walichokikuta. Pia kila mji waliouona waliuchoma moto.