< Juges 1 >

1 Après la mort de Josué, les enfants d'Israël demandèrent à Yahvé: « Qui montera pour nous le premier contre les Cananéens, pour les combattre? »
Baada ya kifo cha Yoshua, wana wa Israeli walimuuliza Yahweh wakisema, “Ni nani atawashambulia kwanza Wakanaani kwa ajili yetu, ili kupigana nao?
2 Yahvé dit: « Juda montera. Voici, j'ai livré le pays entre ses mains. »
Yahweh akasema, “Yuda atawashambulia. Tazama, nimewapa kumiliki nchi hii.
3 Juda dit à Siméon, son frère: « Monte avec moi dans mon lot, afin que nous combattions les Cananéens; et moi aussi, je monterai avec toi dans ton lot. » Siméon alla donc avec lui.
Watu wa Yuda wakawaambia wana wa Simeoni, ndugu zao, “Njoo pamoja nasi katika eneo letu ambalo tumepewa ili kwa pamoja tupigane na Wakanaani. Na sisi pia tutakwenda nanyi katika eneo mlilopewa.” Basi kabila la Simeoni wakaenda pamoja nao.
4 Juda monta, et Yahvé livra entre leurs mains les Cananéens et les Phéréziens. Ils frappèrent dix mille hommes à Bézek.
Watu wa Yuda wakashinda, na Bwana akawapa ushindi juu ya Wakanaani na Waperizi. Wakawaua watu elfu kumi huko Bezeki.
5 Ils trouvèrent Adoni-Bézek à Bézek, et ils lui livrèrent bataille. Ils battirent les Cananéens et les Phéréziens.
Wakamkuta Adoni Bezeki huko Bezeki, nao wakapigana naye na kuwashinda Wakanaani na Waperizi.
6 Mais Adoni-Bézek s'enfuit. Ils le poursuivirent, l'attrapèrent, et lui coupèrent les pouces et les gros orteils.
Lakini Adoni Bezeki akamkimbilia, wakamfuata na kumshika, nao wakavikata vidole gumba na vidole vyake vikubwa.
7 Adoni-Bézek dit: « Soixante-dix rois, qui ont eu les pouces et les gros orteils coupés, ont fait les poubelles sous ma table. Ce que j'ai fait, Dieu me l'a fait. » On le conduisit à Jérusalem, où il mourut.
Adoni Bezek akasema, “Wafalme sabini, ambao na vidole gumba vyako na vidole vikubwa vilivyokatwa, walikusanya chakula chao chini ya meza yangu. Kama nilivyofanya, hata hivyo Mungu amefanya kwangu.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
8 Les fils de Juda combattirent contre Jérusalem, la prirent, la frappèrent du tranchant de l'épée et mirent le feu à la ville.
Watu wa Yuda wakapigana dhidi ya jiji la Yerusalemu na kulichukua. Walishambulia kwa makali ya upanga na wakauwasha mji kwa moto.
9 Après cela, les fils de Juda descendirent pour combattre les Cananéens qui habitaient dans la montagne, dans le midi et dans la plaine.
Baada ya hayo, watu wa Yuda walikwenda kupigana na Wakanaani waliokaa mlimani, Negebu, na magharibi mwa milima.
10 Juda marcha contre les Cananéens qui habitaient à Hébron. (Le nom d'Hébron était auparavant Kiriath Arba.) Ils frappèrent Sheshai, Ahiman et Talmai.
Yuda akaenda dhidi ya Wakanaani waliokaa Hebroni (jina la Hebroni hapo awali ilikuwa Kiriath-arba), nao wakamshinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
11 De là, il alla contre les habitants de Debir. (Le nom de Debir était auparavant Kiriath Sepher.)
Kutoka huko watu wa Yuda walipigana na wenyeji wa Debiri (jina la Debiri hapo awali ilikuwa Kiriath-seferi).
12 Caleb dit: « Je donnerai ma fille Acsa pour femme à l'homme qui frappera Kiriath Sepher et la prendra. »
Kalebu akasema, Yeyote atakayeivamia Kiriath-seferi na kuichukua, nitampa Aksa, binti yangu, awe mkewe.
13 Othniel, fils de Kenaz, frère cadet de Caleb, la prit, et il lui donna pour femme sa fille Acsa.
Otinieli, mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu, akaiteka Debiri, naye Kalebu akampa Aksa, binti yake, awe mkewe.
14 Quand elle arriva, elle lui demanda de demander un champ à son père. Elle descendit de son âne; et Caleb lui dit: « Que veux-tu? »
Ndipo Aksa alifika kwa Othnieli, naye akamsihi amuombe baba yake ampe shamba. Alipokuwa akishuka katika punda wake, Kalebu akamwuliza, “Nikufanyie nini?”
15 Elle lui dit: « Donne-moi une bénédiction; puisque tu m'as établie dans le pays du Midi, donne-moi aussi des sources d'eau. » Et Caleb lui donna les sources supérieures et les sources inférieures.
Akamwambia, Nibariki. Kwa kuwa umenipa nchi ya Negebu, nipe pia chemchemi za maji. Kwa hiyo Kalebu akampa chemchemi za juu na chemchemi za chini.
16 Les fils du Kénite, beau-frère de Moïse, montèrent de la ville des palmiers avec les fils de Juda dans le désert de Juda, qui est au sud d'Arad, et ils allèrent habiter avec le peuple.
Kizazi cha Mkeeni shemeji yake na Musa, walikwenda kutoka mji wa Mitende pamoja na watu wa Yuda, mpaka jangwa la Yuda, ambalo liko Negevu, kuishi na watu wa Yuda karibu na Arad.
17 Juda partit avec Siméon, son frère, et ils frappèrent les Cananéens qui habitaient Zéphath, et la détruisirent par interdit. Le nom de la ville fut appelé Horma.
Nao watu wa Yuda wakaenda pamoja na wana wa Simeoni ndugu zao, wakawaangamiza Wakanaani waliokaa Zefathi, wakaiharibu kabisa. Mji uliitwa Horma.
18 Juda prit aussi Gaza et son territoire, Ashkelon et son territoire, et Ekron et son territoire.
Watu wa Yuda pia waliiteka Gaza na nchi iliyoizunguka, Ashkeloni na nchi iliyoizunguka, na Ekron na nchi iliyoizunguka.
19 L'Éternel fut avec Juda, et il chassa les habitants de la montagne, car il ne put chasser les habitants de la vallée, parce qu'ils avaient des chars de fer.
Yahweh alikuwa pamoja na watu wa Yuda na wakaimiliki nchi ya milima, lakini hawakuweza kuwatoa wenyeji wa kwenye bonde kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
20 On donna Hébron à Caleb, comme Moïse l'avait dit, et il en chassa les trois fils d'Anak.
Hebroni alipewa Kalebu (kama Musa alivyosema), naye akawafukuza kutoka huko wana watatu wa Anaki.
21 Les fils de Benjamin ne chassèrent pas les Jébusiens qui habitaient Jérusalem, mais les Jébusiens habitent avec les fils de Benjamin à Jérusalem jusqu'à ce jour.
Lakini wana wa Benyamini hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa Yerusalemu. Basi Wayebusi wakakaa na watu wa Benyamini huko Yerusalemu hata leo.
22 La maison de Joseph monta aussi contre Béthel, et l'Éternel fut avec eux.
Nyumba ya Yusufu ilijiandaa kuishambulia Betheli, na Yahweh alikuwa pamoja nao.
23 La maison de Joseph envoya espionner Béthel.
Walipeleka watu kuipeleleza Betheli (jiji lililoitwa Luzu).
24 Les observateurs virent un homme sortir de la ville et ils lui dirent: « Montre-nous l'entrée de la ville, et nous te traiterons avec bienveillance. »
Wapelelezi waliona mtu akitoka nje ya jiji, wakamwambia, “Tafadhali tuonyeshe jinsi ya kuingia ndani ya jiji, na tutakutendea mema.”
25 Il leur montra l'entrée de la ville, et ils frappèrent la ville du tranchant de l'épée; mais ils laissèrent partir l'homme et toute sa famille.
Aliwaonyesha njia ya kuingia kwenye mji. Waliuteka mji kwa makali ya upanga, lakini wakamuacha mtu huyo na ndugu zake wote waondoke.
26 L'homme alla dans le pays des Hittites, bâtit une ville et l'appela Luz, nom qu'elle porte encore aujourd'hui.
Na mtu huyo akaenda nchi ya Wahiti, akajenga mji, akauita Luzu, ambalo jina lake hata leo.
27 Manassé ne chassa pas les habitants de Beth Shean et de ses villes, ni de Taanach et de ses villes, ni les habitants de Dor et de ses villes, ni les habitants d'Ibleam et de ses villes, ni les habitants de Megiddo et de ses villes; mais les Cananéens demeurèrent dans ce pays.
Watu wa Manase hawakuwafukuza watu waliokuwa katika miji ya Bethsheani na vijiji vyake, au Taanaki na vijiji vyake, au wale waliokaa Dori na vijiji vyake, wala wale waliokaa Ibleamu na vijiji vyake, wala walioshi Megido na vijiji vyake, kwa sababu Wakanaani walikuwa wameamua kuishi katika nchi hiyo.
28 Lorsqu'Israël fut devenu fort, il mit les Cananéens au travail forcé et ne les chassa pas complètement.
Israeli ipokuwa na nguvu, waliwalazimisha Wakanaani wawatumikie kwa kazi ngumu, lakini hawakuwafukuza kabisa.
29 Ephraïm ne chassa pas les Cananéens qui habitaient à Guézer, mais les Cananéens habitèrent à Guézer au milieu d'eux.
Efraimu hakuwafukuza Wakanaani waliokaa Gezeri; kwa hiyo Wakanaani wakakaa kati yao.
30 Zabulon ne chassa pas les habitants de Kitron ni ceux de Nahalol, mais les Cananéens habitèrent parmi eux et furent soumis au travail forcé.
Zebuloni hakuwafukuza watu wa Kitroni, wala watu waliokuwa Nahaloli; na Wakanaani wakaendelea kuishi pamoja nao; lakini Zabuloni akawalazimisha Wakanaani wawatumikie kwa kazi ngumu.
31 Asher ne chassa pas les habitants d'Acco, ni ceux de Sidon, ni ceux d'Ahlab, ni ceux d'Achzib, ni ceux d'Helba, ni ceux d'Aphik, ni ceux de Rehob;
Asheri hakuwafukuza watu wanaoishi Aka, au watu wanaoishi Sidoni, au wale wanaoishi Alabu, Akzib, Helba, Afeka, au Rehobu.
32 mais les Asher habitèrent parmi les Cananéens, habitants du pays, car ils ne les chassèrent pas.
Kwa hiyo kabila ya Asheri iliishi kati ya Wakanaani (waliokaa katika nchi hiyo), kwa sababu hawakuwafukuza.
33 Nephtali ne chassa pas les habitants de Beth Shemesh ni ceux de Beth Anath, mais il habita au milieu des Cananéens, habitants du pays. Néanmoins, les habitants de Beth Shemesh et de Beth Anath furent soumis au travail forcé.
Na kabila la Naftali halikuwafukuza watu waliokuwa wakiishi Bethshemeshi, wala waliokuwa wakiishi Bethanathi. Kwa hiyo kabila la Naftali liliishi kati ya Wakanaani (watu waliokuwa wakiishi katika nchi hiyo). Hata hivyo, wenyeji wa Bethshemeshi na Bethanathi walilazimishwa kufanya kazi ngumu kwa Naphthali.
34 Les Amorrhéens forcèrent les enfants de Dan à aller dans la montagne, car ils ne leur permirent pas de descendre dans la vallée;
Waamori waliwalazimisha kabila la Dani kuishi katika nchi ya kilima, hawakuwaruhusu kuja bondeni.
35 mais les Amorrhéens habitèrent au mont Hérès, à Aijalon et à Shaalbim. Mais la main de la maison de Joseph l'emporta, de sorte qu'ils furent soumis au travail forcé.
Basi Waamori waliishi katika mlima wa Heresi, huko Aiyaloni, na Shaalbimu, lakini nguvu za kijeshi za nyumba ya Yusufu ziliwashinda, nao wakalazimishwa kuwatumikia kwa kazi ngumu.
36 La frontière des Amoréens s'étendait depuis la montée d'Akrabbim, depuis le rocher et vers le haut.
Mpaka wa Waamori ulikuwa kutoka kilima cha Akrabimu huko Sela hadi nchi ya vilima.

< Juges 1 >