< Jude 1 >
1 Jude, serviteur de Jésus-Christ et frère de Jacques, à ceux qui sont appelés, sanctifiés par Dieu le Père et gardés pour Jésus-Christ:
Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo.
2 Que la miséricorde, la paix et la charité vous soient multipliées!
Nawatakieni huruma, amani na upendo kwa wingi.
3 Bien-aimés, alors que j'étais très désireux de vous écrire au sujet de notre salut commun, j'ai été contraint de vous écrire pour vous exhorter à lutter avec ardeur pour la foi qui a été une fois pour toutes livrée aux saints.
Ndugu wapenzi, wakati nimo katika jitihada ya kuwaandikieni juu ya ule wokovu tunaoshiriki sote, nimeona lazima ya kuwaandikieni na kuwahimizeni mwendelee kupigana kwa ajili ya imani ambayo Mungu amewajalia watu wake mara moja tu kwa wakati wote.
4 Car il y a des hommes qui se sont glissés en secret dans l'Église, ceux-là mêmes qui ont été annoncés depuis longtemps pour cette condamnation, des hommes impies, qui transforment la grâce de notre Dieu en indécence, et qui renient notre seul Maître, Dieu et Seigneur, Jésus-Christ.
Maana watu wasiomcha Mungu wamepata kujiingiza kwa siri miongoni mwetu, watu ambao, kwa faida ya maisha yao mabaya, wanaupotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu na kumkana Yesu Kristo aliye peke yake kiongozi na Bwana wetu. Maandiko Matakatifu yalikwisha bashiri tangu awali hukumu inayowangojea watu hao.
5 Je veux maintenant vous rappeler, bien que vous le sachiez déjà, que le Seigneur, après avoir sauvé un peuple du pays d'Égypte, a ensuite détruit ceux qui n'ont pas cru.
Nataka kuwakumbusheni mambo fulani ambayo mmekwisha yajua: kumbukeni jinsi Bwana alivyowaokoa watu wa Israeli na kuwatoa katika nchi ya Misri, lakini baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
6 Les anges qui n'ont pas gardé leur premier domaine, mais qui ont déserté leur propre demeure, il les a gardés dans des liens éternels, sous les ténèbres, pour le jugement du grand jour. (aïdios )
Na, malaika ambao hawakuridhika na cheo chao, wakayaacha makao yao ya asili, Mungu amewafunga gizani kwa minyororo ya milele wahukumiwe Siku ile kuu. (aïdios )
7 De même que Sodome et Gomorrhe et les villes voisines, qui, comme elles, se sont livrées à l'impudicité et ont recherché la chair étrangère, sont montrées en exemple, subissant le châtiment du feu éternel. (aiōnios )
Kumbukeni pia Sodoma na Gomora, na miji ya kandokando yake; wenyeji wake walifanya kama wale malaika; walifanya uzinzi na mambo yaliyo kinyume cha maumbile, wakapewa hukumu ya moto wa milele, iwe onyo kwa watu wote. (aiōnios )
8 Mais de la même manière, ceux-ci aussi, dans leur rêve, souillent la chair, méprisent l'autorité et calomnient les êtres célestes.
Hivyo ndivyo pia walivyo watu hawa. ndoto zao huwaongoza katika kuichafua miili yao wenyewe, kuyadharau mamlaka ya Mungu na kuvitukana viumbe vitukufu vya huko juu.
9 Mais Michel, l'archange, lorsqu'il était aux prises avec le diable et qu'il discutait du corps de Moïse, n'osait pas porter contre lui une condamnation injurieuse, mais disait: « Que le Seigneur te reprenne! »
Hata Mikaeli, malaika mkuu, hakufanya hivyo. Katika ule ubishi kati yake na Ibilisi waliobishana juu ya mwili wa Mose, Mikaeli hakuthubutu kumhukumu Ibilisi kwa matusi; ila alisema: “Bwana mwenyewe na akukaripie.”
10 Mais ceux-là disent du mal des choses qu'ils ne connaissent pas. Ils sont détruits dans ces choses qu'ils comprennent naturellement, comme les créatures sans raison.
Lakini watu hawa hutukana chochote wasichokielewa; mambo yaleyale wanayoyajua kwa silika kama vile wanyama wanayoyajua ndiyo yanayowaangamiza.
11 Malheur à eux! Car ils ont suivi la voie de Caïn, ils se sont égarés dans l'erreur de Balaam, et ils ont péri dans la rébellion de Koré.
Ole wao! Watu hao wamefuata mwenendo uleule wa Kaini. Kwa ajili ya fedha, wamejiingiza katika mkosi uleule wa Baalamu. Wameasi kama Kora alivyoasi na wameangamizwa kama yeye alivyoangamizwa.
12 Ce sont des écueils cachés dans vos festins d'amour, quand ils festoient avec vous, des bergers qui sans crainte se nourrissent eux-mêmes; des nuages sans eau, emportés par les vents; des arbres d'automne sans fruit, deux fois morts, arrachés par les racines;
Kwa makelele yao yasiyo na adabu, watu hao ni kama madoa machafu katika mikutano yenu ya karamu ya Bwana. Hujipendelea wao wenyewe tu, na wako kama mawingu yanayopeperushwa huko na huko na upepo bila ya kuleta mvua. Wao ni kama miti isiyozaa matunda hata wakati wa majira yake, wamekufa kabisa.
13 des vagues sauvages de la mer, écumant leur propre honte; des étoiles errantes, pour lesquelles l'obscurité des ténèbres a été réservée à jamais. (aiōn )
Watu hao ni kama mawimbi makali ya bahari, na matendo yao ya aibu yanaonekana dhahiri kama vile mapovu ya mawimbi. Wao ni kama nyota zinazotangatanga, ambao Mungu amewawekea mahali pao milele katika giza kuu. (aiōn )
14 C'est à leur sujet qu'Hénoch, le septième depuis Adam, a prophétisé, en disant: « Voici, le Seigneur est venu avec dix mille de ses saints,
Henoki, ambaye ni babu wa saba tangu Adamu, alibashiri hivi juu ya watu hawa: “Sikilizeni! Bwana atakuja pamoja na maelfu ya malaika wake watakatifu
15 pour exercer un jugement sur tous, et pour condamner tous les impies pour toutes les œuvres d'impiété qu'ils ont commises d'une manière impie, et pour toutes les paroles dures que les pécheurs impies ont proférées contre lui. » 16 Ce sont des murmures et des plaintes, et ce sont des gens qui se plaignent.
kutoa hukumu juu ya binadamu wote, kuwahukumu wote kwa ajili ya matendo yao yote maovu waliyotenda na kwa ajili ya maneno yote mabaya ambayo watu waovu walimkashifu nayo.”
16 Ce sont des murmureurs et des râleurs, qui marchent selon leurs convoitises, et leur bouche profère des paroles orgueilleuses, en faisant preuve de respect pour les personnes, afin d'obtenir des avantages.
Watu hawa wananung'unika daima na kuwalaumu watu wengine. Hufuata tamaa zao mbaya, hujigamba na kuwasifu watu wengine mno kusudi wafaulu katika mipango yao.
17 Mais vous, bien-aimés, souvenez-vous des paroles qui ont été dites auparavant par les apôtres de notre Seigneur Jésus-Christ.
Lakini ninyi wapenzi wangu, kumbukeni yale mliyoambiwa hapo awali ni mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo.
18 Ils vous ont dit: « Au dernier temps, il y aura des moqueurs, marchant selon leurs propres désirs impies. »
Waliwaambieni: “Siku za mwisho zitakapofika, watatokea watu watakaowadhihaki ninyi, watu wafuatao tamaa zao mbaya.”
19 Ce sont ceux qui provoquent des divisions, qui sont sensuels et qui n'ont pas l'Esprit.
Hao ndio watu wanaosababisha mafarakano, watu wanaotawaliwa na tamaa zao za kidunia, watu wasio na Roho wa Mungu.
20 Mais vous, bien-aimés, édifiez-vous sur votre très sainte foi, en priant dans l'Esprit Saint.
Lakini ninyi, wapenzi wangu, endeleeni kujijenga kikamilifu katika imani yenu takatifu. Salini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu,
21 Restez dans l'amour de Dieu, attendant la miséricorde de notre Seigneur Jésus-Christ pour la vie éternelle. (aiōnios )
na kubaki katika upendo wa Mungu, mkiwa mnamngojea Bwana wetu Yesu Kristo awapeni uzima wa milele kwa huruma yake. (aiōnios )
22 Les uns ont compassion, en faisant une distinction,
Muwe na huruma kwa watu walio na mashaka;
23 et les autres sauvent, en les arrachant du feu avec crainte, en détestant même les vêtements souillés par la chair.
waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni; na kwa wengine muwe na huruma pamoja na hofu, lakini chukieni hata mavazi yao ambayo yamechafuliwa na tamaa zao mbaya.
24 Or, à celui qui peut les préserver de la chute et vous présenter sans défaut devant la présence de sa gloire dans une grande joie,
Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta ninyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake,
25 à Dieu notre Sauveur, qui seul est sage, soient gloire et majesté, domination et puissance, maintenant et pour toujours. Amen. (aiōn )
kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina. (aiōn )