< Josué 5 >
1 Lorsque tous les rois des Amoréens, qui étaient de l'autre côté du Jourdain, à l'ouest, et tous les rois des Cananéens, qui étaient près de la mer, apprirent comment Yahvé avait mis à sec les eaux du Jourdain, depuis devant les enfants d'Israël jusqu'à ce que nous ayons traversé, leur cœur se fondit, et il n'y eut plus d'esprit en eux, à cause des enfants d'Israël.
Basi wafalme wote wa Waamori magharibi ya Yordani na wafalme wote wa Kanaani waliokuwa kwenye pwani waliposikia jinsi Bwana alivyoukausha Mto Yordani mbele ya Waisraeli hata tulipokwisha kuvuka, mioyo yao ikayeyuka kwa hofu, wala hawakuwa na ujasiri kuwakabili Waisraeli.
2 En ce temps-là, Yahvé dit à Josué: « Fais des couteaux de silex, et circoncis de nouveau les fils d'Israël pour la seconde fois. »
Wakati huo Bwana akamwambia Yoshua, “Tengeneza visu vya mawe magumu sana na uwatahiri Waisraeli tena.”
3 Josué se fit des couteaux de silex, et il circoncit les fils d'Israël à la colline des prépuces.
Kwa hiyo Yoshua akatengeneza visu vya mawe magumu sana na kutahiri Waisraeli huko Gibeath-Haaralothi.
4 Voici pourquoi Josué les circoncit: tout le peuple sorti d'Égypte, les mâles, tous les hommes de guerre, moururent dans le désert, en chemin, après leur sortie d'Égypte.
Hii ndiyo sababu ya Yoshua kufanya hivyo: Wanaume wote waliotoka Misri, wote wenye umri wa kwenda vitani, walikufa jangwani wakiwa njiani baada ya kuondoka Misri.
5 Car tous ceux qui étaient sortis d'Égypte étaient circoncis, mais tous ceux qui étaient nés dans le désert, sur le chemin de la sortie d'Égypte, n'avaient pas été circoncis.
Watu wote waliotoka Misri walikuwa wametahiriwa, lakini watu wote waliozaliwa jangwani wakiwa safarini toka Misri walikuwa hawajatahiriwa.
6 Les enfants d'Israël marchèrent quarante ans dans le désert, jusqu'à ce que toute la nation, même les hommes de guerre qui étaient sortis d'Égypte, aient été consumés, parce qu'ils n'avaient pas écouté la voix de Yahvé. Yahvé leur jura de ne pas leur laisser voir le pays que Yahvé avait juré à leurs pères de nous donner, un pays où coulent le lait et le miel.
Waisraeli walitembea jangwani miaka arobaini mpaka wanaume wote wale waliokuwa na umri wa kwenda vitani wakati waliondoka Misri walipokwisha kufa, kwa kuwa hawakumtii Bwana. Kwa maana Bwana alikuwa amewaapia kuwa wasingeweza kuona nchi ambayo alikuwa amewaahidi baba zao katika kuapa kutupatia, nchi inayotiririka maziwa na asali.
7 Leurs enfants, qu'il suscita à leur place, furent circoncis par Josué, car ils étaient incirconcis, faute d'avoir été circoncis en chemin.
Kwa hiyo akawainua wana wao baada yao na hawa ndio hao ambao Yoshua aliwatahiri. Walikuwa hawajatahiriwa bado kwa sababu walikuwa safarini.
8 Lorsqu'ils eurent fini de circoncire toute la nation, ils restèrent à leur place dans le camp jusqu'à ce qu'ils soient guéris.
Baada ya taifa lote kutahiriwa, waliendelea kukaa kambini mpaka walipokuwa wamepona.
9 Yahvé dit à Josué: « Aujourd'hui, je roule loin de toi l'opprobre de l'Égypte. » C'est pourquoi le nom de ce lieu a été appelé Gilgal jusqu'à ce jour.
Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nimeiondoa aibu ya Wamisri kutoka kwenu.” Basi mahali pale pakaitwa Gilgali hadi leo.
10 Les enfants d'Israël campèrent à Guilgal. Ils célébrèrent la Pâque le quatorzième jour du mois, le soir, dans les plaines de Jéricho.
Jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi, wakiwa kambini huko Gilgali katika tambarare za Yeriko, Waisraeli wakaadhimisha Pasaka.
11 Ils mangèrent des gâteaux sans levain et des grains desséchés provenant des produits du pays le lendemain de la Pâque, le même jour.
Siku iliyofuata Pasaka, katika siku ile ile, wakala mazao ya nchi, mikate isiyotiwa chachu na nafaka za kukaanga.
12 La manne cessa le jour suivant, après qu'ils eurent mangé des produits du pays. Les enfants d'Israël n'eurent plus de manne, mais ils mangèrent des fruits du pays de Canaan cette année-là.
Mana ilikoma siku iliyofuata baada ya Waisraeli kula chakula kilichotoka katika nchi; hapakuwa na mana tena kwa ajili ya Waisraeli, ila mwaka huo walikula mazao ya nchi ya Kanaani.
13 Lorsque Josué fut près de Jéricho, il leva les yeux et regarda, et voici qu'un homme se tenait devant lui, son épée tirée à la main. Josué alla vers lui et lui dit: « Es-tu pour nous, ou pour nos ennemis? ».
Basi wakati Yoshua alipokuwa karibu na Yeriko, akainua macho, akaona mtu aliyesimama mbele yake, akiwa na upanga mkononi uliofutwa kwenye ala. Yoshua akamwendea na kumuuliza, “Je, wewe uko upande wetu au upande wa adui zetu?”
14 Il répondit: « Non, mais je suis venu maintenant comme commandant de l'armée de l'Éternel. » Josué tomba la face contre terre, se prosterna et lui demanda: « Que dit mon seigneur à son serviteur? »
Akajibu, “La, siko upande wowote, lakini mimi nimekuja nikiwa jemadari wa jeshi la Bwana.” Yoshua akaanguka kifudifudi hadi chini, akasujudu, akamuuliza, “Je, Bwana, una ujumbe gani kwa mtumishi wako?”
15 Le prince de l'armée de Yahvé dit à Josué: « Enlève tes sandales, car le lieu sur lequel tu te tiens est saint. « Josué fit ainsi.
Jemadari wa jeshi la Bwana akajibu, “Vua viatu vyako, kwa maana mahali hapa unaposimama ni patakatifu.” Naye Yoshua akafanya hivyo.