< Josué 23 >

1 Après de nombreux jours, lorsque Yahvé eut donné du repos à Israël contre ses ennemis de tous les côtés, et que Josué fut vieux et avancé en âge,
Na baada ya siku nyingi, kipindi ambacho Yahweh alikuwa ameipa Israeli pumziko kutoka maadui zao waliowazunguka,
2 Josué convoqua tout Israël, ses anciens et ses chefs, ses juges et ses officiers, et leur dit: « Je suis vieux et avancé en âge.
Joshua alikuwa mzee sana. Yoshua aliwaita Waisraeli wote, na wazee wao, na viongozi, na waamuzi, na kwa maafisa, na kisha akawaambia, “Mimi nimezeeka sana.
3 Vous avez vu tout ce que Yahvé votre Dieu a fait à toutes ces nations à cause de vous, car c'est Yahvé votre Dieu qui a combattu pour vous.
Mmeshaona kila kitu ambacho Yahweh Mungu wenu ameshafanya kwa mataifa haya yote kwa ajili yenu, kwa kuwa ni Yahweh Mungu wenu ambaye amewapigania ninyi.
4 Voici, je vous ai donné en héritage pour vos tribus ces nations qui restent, depuis le Jourdain, avec toutes les nations que j'ai retranchées, jusqu'à la grande mer, vers le coucher du soleil.
Tazama! Nimeshawakabidhi kwenu mataifa yaliyosalia ili kuyateka kwa ajili ya kupata urithi ya makabila yenu, sambasamba na mataifa yote ambayo tayari nimeshayaangamiza, tangu Yordani hadi Bahari kuu katika upande wa magharibi.
5 Yahvé, ton Dieu, les chassera devant toi et les fera disparaître de ta vue. Tu posséderas leur pays, comme Yahvé ton Dieu te l'a dit.
Yahweh Mungu wenu atayaondoa. Atayafukuzia mbali kutoka kwenu. Ataiteka nchi yao, nanyi mtaimiliki nchi yao, kama vile Yahweh Mungu wenu alivyowaahidi ninyi.
6 « C'est pourquoi, gardez et mettez en pratique avec beaucoup de courage tout ce qui est écrit dans le livre de la loi de Moïse, sans vous en détourner ni à droite ni à gauche;
Hivyo, iweni jasiri, ili kwamba mtunze na kuyafanya yale yote yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa, msikengeuke upande wa kulia wala upande wa kushoto,
7 sans venir parmi ces nations, celles qui restent au milieu de vous, sans mentionner le nom de leurs dieux, sans faire jurer par eux, sans les servir et sans vous prosterner devant eux;
basi msichanganyikane na mataifa haya ambayo yamesalia miongoni mwenu, wala msiyataje majina ya miungu yao, wala msiape kwayo, wala msiiabudu, wala msiipigie magoti.
8 mais attachez-vous à Yahvé, votre Dieu, comme vous l'avez fait jusqu'à ce jour.
Badala yake, mnatakiwa kumshika sana Yahweh Mungu wenu kama vile mlivyofanya siku hii ya leo.
9 « Car Yahvé a chassé devant toi des nations grandes et fortes. Mais toi, aucun homme ne s'est dressé devant toi jusqu'à ce jour.
Kwa kuwa Yahweh ameyafukuzia mbali mbele yenu mataifa makubwa yenye nguvu. Hakuna hata mmoja aliyeweza kusimama mbele yenu hata siku hii ya leo.
10 Un seul d'entre vous en poursuivra mille, car c'est Yahvé, ton Dieu, qui combat pour toi, comme il te l'a dit.
Mtu yeyote mmoja wa kwenu atawafanya watu elfu wakimbie mbali, kwa kuwa Yahweh Mungu wenu, ndiye anayepigania ninyi, kama vile alivyowaahidi.
11 Prenez donc garde à vous, afin d'aimer Yahvé votre Dieu.
Zingatieni kwa uangalifu ili mmpende Yahweh Mungu wenu.
12 « Mais si tu retournes en arrière, si tu t'attaches au reste de ces nations, à celles qui restent au milieu de toi, si tu te maries avec elles, si tu entres chez elles et si elles entrent chez toi,
Lakini kama mkiegeuka na kushikamana na watu walioalia wa mataifa haya waliobaki miongoni mwenu, au kuoana nao, au kama mkishirikiana pamoja nao, na wao pamoja nanyi,
13 sache que l'Éternel, ton Dieu, ne chassera plus ces nations loin de toi, mais qu'elles seront pour toi un piège et une embûche, un fléau dans tes flancs et des épines dans tes yeux, jusqu'à ce que tu périsses de ce bon pays que l'Éternel, ton Dieu, t'a donné.
jueni kwa hakika kwamba Yahweh Mungu wenu hatayafukuzia mbali mataifa haya yatoke kati yenu. Badala yake, watakuwa kitanzi na mtego kwenu, viboko migongoni mwenu na miiba machoni mwenu, mpaka pale mtakapoangamia katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
14 « Voici qu'aujourd'hui je prends le chemin de toute la terre. Vous savez dans tous vos cœurs et dans toutes vos âmes que rien n'a manqué de toutes les bonnes choses dont Yahvé votre Dieu a parlé à votre sujet. Tout vous est arrivé. Pas une seule chose n'a manqué.
Na sasa ninaenda katika njia ya dunia yote, na mnajua kwa moyo na roho zenu zote kwamba hakuna hata neno moja ambalo halijatimia kati ya mambo yote mazuri ambayo Yahweh Mungu wenu aliyaahidi juu yenu. Vitu hivi vyote vimetokea kwa ajili yenu. Hakuna hata moja lililoshindikana.
15 Mais, de même que toutes les bonnes choses dont vous a parlé l'Éternel, votre Dieu, vous sont arrivées, de même l'Éternel fera venir sur vous toutes les mauvaises choses, jusqu'à ce qu'il vous ait fait disparaître de ce bon pays que l'Éternel, votre Dieu, vous a donné,
Lakini kama kila neno ambalo Yahweh Mungu wenu alilowaahidi limekwisha kutimia, hivyo Yahweh atawaletea juu yenu mabaya yote mpaka pale atakapokuwa amewaangamiza katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
16 lorsque vous désobéirez à l'alliance de l'Éternel, votre Dieu, qu'il vous a prescrite, et que vous irez servir d'autres dieux et vous prosterner devant eux. Alors la colère de Yahvé s'enflammera contre vous, et vous périrez rapidement du bon pays qu'il vous a donné. »
Atafanya hivi kama mtalivunja agano la Yahweh Mungu wenu, ambalo aliwaagizeni kulitunza. Kama mtaenda na kuiabudu miungu mingine na kuiinamia, ndipo hasira ya Yahweh itawaka kinyume nanyi, na ninyi mtaangamia upesi katika nchi nzuri ambayo amekwisha kuwapeni ninyi.”

< Josué 23 >