< Josué 20 >

1 Yahvé parla à Josué, et dit:
Baada ya hayo, Yahweh akamwambia Yoshua,
2 Parle aux enfants d'Israël, et dis: « Attribuez les villes de refuge dont je vous ai parlé par Moïse,
“Waambia watu wa Israeli, na kusema, 'Chagueni miji ya makimbilio ambayo niliwaambia kupitia kwa Musa.
3 afin que le meurtrier qui tue quelqu'un par accident ou involontairement puisse s'y réfugier. Elles seront pour vous un refuge contre le vengeur du sang.
Fanyeni hivi ili mtu akiua mtu bila kukusudia aweze kwenda huko. Miji hii itakuwa ni sehemu ya kukimbilia kutoka kwa mtu yeyote yule anayetaka kulipiza kisasi kwa damu ya mtu aliyeuliwa.
4 Il s'enfuira dans l'une de ces villes, se tiendra à l'entrée de la porte de la ville et exposera son cas aux oreilles des anciens de cette ville. Ils le prendront avec eux dans la ville et lui donneront une place, afin qu'il vive au milieu d'eux.
Atakimbilia kwa mji mmoja miongoni mwa miji hiyo na atasimama mlangoni mwa lango la mji, na ataeleza kesi yake kwa wazee wa mji ule. Kisha watamwingiza ndani ya mji na watampatia sehemu yake ya kuishi miongoni mwao.
5 Si le vengeur du sang le poursuit, on ne livrera pas entre ses mains le meurtrier de l'homme, parce qu'il a frappé son prochain sans le vouloir et sans le haïr auparavant.
Na kama mtu akija akataka kulipiza kisasi kwa damu ya mtu yule ambaye aliuliwa, ndipo watu wa mji hawatatakiwa kumtoa kwa wenye mamlaka mtu huyo aliyeua. Hawaruhusiwi kufanya hivyo kwasababu alimwua jirani bila kukusudia na hakuwa na chuki naye hapo awali.
6 Il demeurera dans cette ville jusqu'à ce qu'il se présente devant l'assemblée pour être jugé, jusqu'à la mort du grand prêtre qui aura lieu en ces jours-là. Alors l'homme qui a tué son prochain s'en retournera et reviendra dans sa ville et dans sa maison, dans la ville qu'il a fuie.'"
Ni lazima akae katika mji ule mpaka pale atakapokuwa amesimama mbele ya kusanyiko kwa ajili ya kuhukumiwa, hadi pale atakapokufa mtu yule anayetumika katika nafasi ya kuhani mkuu katka siku hizo. Na kisha mtu yule aliyeua bila kukusudia aweza kurudi nyumbani kwake, katika mji ule ulikotoka.
7 Ils mirent à part Kedesh en Galilée, dans la montagne de Nephtali, Sichem dans la montagne d'Ephraïm, et Kiriath Arba (appelée aussi Hébron) dans la montagne de Juda.
Kwahiyo, Waisraeli wakaichaguia Kedeshi iliyoko Galilaya katika nchi ya milima ya Nafutali, Shekemu katika nchi ya milima ya Efraimu, na Kiriathi Arba (ambayo ndio Herbroni) katika nchi ya milima ya Yuda.
8 Au-delà du Jourdain, à Jéricho, vers l'est, ils attribuèrent Bezer dans le désert, dans la plaine, à la tribu de Ruben, Ramoth en Galaad, à la tribu de Gad, et Golan en Basan, à la tribu de Manassé.
Katika ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko, walichagua mji wa Bezeri huko nyikani katika nyanda za kabila la Rubeni; na Ramothi Gileadi kutoka kabila la Gadi; na Golani katika Bashani, kutoka katika kabila la Manase.
9 Ces villes étaient destinées à tous les enfants d'Israël et à l'étranger qui vit au milieu d'eux, afin que quiconque tuerait quelqu'un involontairement puisse s'y réfugier et ne pas mourir de la main du vengeur du sang, jusqu'à ce qu'il soit jugé devant l'assemblée.
Hii ni miji iliyochaguliwa kwa ajili ya watu wote wa Israeli na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwao, ili kwamba mtu yeyote amwuaye mtu bila kukusudia aweza kukimbilia huko kwa ajili ya kupata usalama. Mtu huyu hatakufa kwa mkono wa mtu yule anayetake kulipiza kisasi cha damu iliyomwagwa, mpaka hapo kwanza mtuhumiwa atakaposimama mbele ya kusanyiko la watu.

< Josué 20 >