< Josué 13 >
1 Or Josué était vieux et avancé en âge. Yahvé lui dit: « Tu es vieux et avancé en âge, et il te reste encore beaucoup de terres à posséder.
Sasa Yoshua alikuwa mzee wakati Yahweh alipomwambia, “Umekuwa mzee, lakini bado kuna nchi kubwa ya kuteka.
2 « Voici le pays qui subsiste encore: toutes les régions des Philistins et tous les Gueschuriens,
Nchi iliyosalia ndio hii: mikoa yote ya Wafilisti, na mikoa ile ya Wageshuri,
3 depuis le Schichhor, qui est en face de l'Égypte, jusqu'à la frontière d'Ékron au nord, qui est comptée comme Cananéenne, les cinq seigneurs des Philistins, les Gazites, les Asdodites, les Ashkelonites, les Gittites et les Ékronites, et aussi les Avvim,
(tangu Shihori, iliyoko mashariki mwa Misri, na upande wa kaskazini kuelekea mpaka wa Ekroni, inayofikiriwa kuwa ni mali ya Wakanaani; wafalme watano wa Wafilisti, wale wafalme wa Gaza, Ashidodi, Ashikeloni, Gathi na Ekroni - miliki ya Waavi.
4 au sud; tout le pays des Cananéens, et Meara qui appartient aux Sidoniens, jusqu'à Aphek, jusqu'à la frontière des Amorrhéens;
Katika upande wa kusini, kulisalia nchi yote ya Wakanaani, na Meara ambayo ni miliki ya Wasidoni, hadi Afeki, hata mpaka wa Waamori;
5 le pays des Gébalites, et tout le Liban, vers le soleil levant, depuis Baal Gad au pied de la montagne de l'Hermon jusqu'à l'entrée de Hamath;
nchi ya Wagebali, Lebanoni kuelekea upande wa mapambazuko ya jua, kutoka Baali- Gadi chini ya Mlima Hermoni mpaka Lebo Hamathi.
6 tous les habitants de la montagne, depuis le Liban jusqu'à Misrephoth Maïm, tous les Sidoniens. Je les chasserai de devant les enfants d'Israël. Tu le donneras en héritage à Israël, comme je te l'ai ordonné.
Pia, wenyeji wote wa nchi ya milima kutoka Lebanoni hadi Misrefothi - Maimu, pamoja na watu wa Sidoni. Nitawafukuza mbele ya jeshi la Israeli. Uwe na uhakika wa kuwapa Waisraeli nchi kama urithi, kama nilivyokuagiza.
7 Maintenant, partagez donc ce pays en héritage entre les neuf tribus et la demi-tribu de Manassé. »
Igawanye nchi hii kama urithi kwa makabila tisa na kwa nusu ya kabila la Manase.
8 Les Rubénites et les Gadites reçurent avec lui l'héritage que Moïse leur avait donné, au-delà du Jourdain, à l'orient, comme Moïse, serviteur de Yahvé, le leur avait donné:
Pamoja na nusu nyingine ya kabila la Manase, Wareubeni na Wagadi wamekwisha kupokea urithi wao ambao Musa aliwapa katika upande wa mashariki wa Yordani,
9 depuis Aroër, qui est sur le bord du torrent de l'Arnon, et la ville qui est au milieu du torrent, et toute la plaine de Medeba jusqu'à Dibon;
kutoka Aroeri, iliyo katika ukingo wa bonde la mto Arnoni (kujumuisha na mji ambao uko katikati ya bonde), kwa nyanda zote za Medeba hadi Diboni;
10 et toutes les villes de Sihon, roi des Amoréens, qui régnait à Hesbon, jusqu'à la frontière des enfants d'Ammon;
miji yote ya Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alitawala katika Heshiboni, hata mpaka wa Waamori,
11 Galaad, le territoire des Gueschuriens et des Maacathiens, toute la montagne de l'Hermon, tout Basan jusqu'à Salca,
Gileadi na mkoa wa Wageshuri na Maakathi, mlima wote wa Hermoni, Bashani yote mpaka Saleka;
12 tout le royaume d'Og en Basan, qui régnait à Aschtaroth et à Édréi, le reste des Rephaïm, car Moïse les attaqua et les chassa.
ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyetawala katika Ashitarothi na Edrei - hawa ni wale waliosalia katika Refaimu - ambao Musa aliwapiga na kuwafukuzia mbali.
13 Cependant, les enfants d'Israël ne chassèrent pas les Gueshuriens et les Maacathiens; mais Gueshur et Maacath vivent en Israël jusqu'à ce jour.
Lakini watu wa Israeli hawakuwafukuza Wageshuri wala Wamakathi. Badala yake, Wageshuri na Wamakathi wanaishi miongoni mwa Waisraeli hadi leo.
14 Seulement, il ne donna aucun héritage à la tribu de Lévi. Les offrandes de Yahvé, le Dieu d'Israël, faites par le feu, sont son héritage, comme il le lui a dit.
Kabila la Lawi pekee halikupewa urithi na Musa. Urithi wao ni sadaka za Yahweh, Mungu wa Israeli, zilizotolewa kwa moto, kama Mungu alivyomwagiza Musa.
15 Moïse donna à la tribu des fils de Ruben, selon leurs familles.
Musa aliwapa urithi kabila la Rubeni, ukoo kwa ukoo.
16 Leur territoire s'étendait depuis Aroër, qui est sur le bord du torrent de l'Arnon, et la ville qui est au milieu du torrent, et toute la plaine près de Medeba;
Miliki yao ilikuwa kutoka Aroeri, juu ya ukingo wa bonde la Mto Arnoni, na mji ulio katikati ya bonde, na nyanda zote za Medeba.
17 Hesbon et toutes ses villes qui sont dans la plaine; Dibon, Bamoth Baal, Beth Baal Meon,
Wareubeni walipata pia Heshiboni, na miji yake yote zilizo katika uwanda, Diboni, na Bamathi Baali, na Bethi Baalimeoni,
18 Jahaz, Kedemoth, Mephaath,
na Yahazi, na Kedemothi, na Mefaathi,
19 Kiriathaïm, Sibma, Zereth Schahar sur la montagne de la vallée,
na Kiriathaimu, na Sibuma, na Zerethishahari juu ya kilima cha bonde.
20 Beth Peor, les pentes du Pisga, Beth Jeshimoth,
Wareubeni walipata pia Bethi Peori, miteremko ya Pisiga, Bethi Yeshimothi,
21 toutes les villes de la plaine, et tout le royaume de Sihon, roi des Amoréens, qui régnait à Hesbon, et que Moïse frappa avec les chefs de Madian, Evi, Rékem, Tsur, Hur et Réba, princes de Sihon, qui habitaient le pays.
miji yote ya uwanda, na ufalme wote wa Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa ametawala katika Heshiboni, ambaye Musa alikuwa amemshinda pamoja na viongozi wa Midiani, Evi, Rekemu, Zuri, Huri na Reba, wana wa mfalme wa Sihoni, ambao walikuwa wameishi katika nchi.
22 Les enfants d'Israël tuèrent aussi par l'épée Balaam, fils de Beor, le devin, parmi le reste de leurs morts.
Pia, watu wa Israeli walimwua kwa upanga Baalam mwana wa Beori, ambaye alifanya mambo ya uaguzi, miongoni mwa wale waliowaua.
23 La limite des fils de Ruben était la rive du Jourdain. Tel fut l'héritage des fils de Ruben, selon leurs familles, les villes et leurs villages.
Mpaka wa kabila la Rubeni ni Mto Yordani; huu ndio mpaka wao. Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Rubeni, uliotolewa kwa kila ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
24 Moïse donna à la tribu de Gad, aux fils de Gad, selon leurs familles.
Hiki ndicho Musa alilipa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
25 Leur limite était Jaezer, toutes les villes de Galaad et la moitié du pays des enfants d'Ammon, jusqu'à Arœr, près de Rabba;
Himaya yao ilikuwa Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Waamoni, hadi Aroeri, iliyo mashariki mwa Raba,
26 depuis Hesbon, jusqu'à Ramath Mitspé, et Bétonim; depuis Mahanaïm, jusqu'à la frontière de Debir;
kutoka Heshiboni hadi Ramathi - Mizipe na Betonimu, kutoka Mahanaimu mpaka himaya ya Debiri.
27 et dans la vallée, Beth Haram, Beth Nimrah, Succoth et Zaphon, le reste du royaume de Sihon, roi de Hesbon, la rive du Jourdain, jusqu'à l'extrémité de la mer de Chinnereth, au-delà du Jourdain, à l'est.
Katika bonde, Musa aliwapa Bethi -Haramu, Bethi - Nimra, Sukothi, na Zafoni, ufalme uliobakia wa Sihoni mfalme wa Heshiboni, pamoja na Yordani kama mpaka, katika sehemu za chini za mwisho wa Bahari ya Kinerethi, upande wa mashariki ng'ambo ya Yordani.
28 Tel est l'héritage des fils de Gad, selon leurs familles, les villes et leurs villages.
Huu ni urithi wa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
29 Moïse donna un héritage à la demi-tribu de Manassé. C'était pour la demi-tribu des fils de Manassé, selon leurs familles.
Musa aliwapa urithi nusu ya kabila la Manase. Urithi uligawiwa kwa nusu ya kabila la watu wa Manase kutokana na kabila zao.
30 Leur territoire s'étendait depuis Mahanaïm, tout Basan, tout le royaume d'Og, roi de Basan, et tous les villages de Jaïr, qui sont en Basan, soit soixante villes.
Miliki yao ilikuwa kutoka Mahanaimu, Bashani yote, ufalme wote wa mfalme Ogu wa Bashani, na miji yote ya Yairi, iliyo katika Bashani, miji sitini;
31 La moitié de Galaad, Aschtaroth et Édréi, villes du royaume d'Og en Basan, étaient pour les fils de Makir, fils de Manassé, pour la moitié des fils de Makir, selon leurs familles.
nusu ya Gileadi, na Ashitarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Miji hii iligawanywa kwa ukoo wa Makiri mwana wa Manase -nusu ya watu wa Makiri, walipewa kwa kila familia zao.
32 Tels sont les héritages que Moïse distribua dans les plaines de Moab, au-delà du Jourdain, à Jéricho, vers l'est.
Huu ndio urithi ambao Musa aliowagawia katika nyanda za Moabu, ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
33 Mais Moïse n'a pas donné d'héritage à la tribu de Lévi. Yahvé, le Dieu d'Israël, est leur héritage, comme il le leur a dit.
Musa hakulipa urithi kabila la Lawi. kwa kuwa Yahweh, Mungu wa israeli, ni urithi wao, kama vile alivyowaambia.