< Josué 13 >

1 Or Josué était vieux et avancé en âge. Yahvé lui dit: « Tu es vieux et avancé en âge, et il te reste encore beaucoup de terres à posséder.
Yoshua alipokuwa mzee na umri wake ukiwa umesogea sana, Bwana akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado kumesalia sehemu kubwa sana za nchi ambazo ni za kutwaliwa.
2 « Voici le pays qui subsiste encore: toutes les régions des Philistins et tous les Gueschuriens,
“Nchi iliyosalia ni hii: maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:
3 depuis le Schichhor, qui est en face de l'Égypte, jusqu'à la frontière d'Ékron au nord, qui est comptée comme Cananéenne, les cinq seigneurs des Philistins, les Gazites, les Asdodites, les Ashkelonites, les Gittites et les Ékronites, et aussi les Avvim,
kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani (maeneo yale matano ya watawala wa Kifilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni: ndiyo nchi ya Waavi);
4 au sud; tout le pays des Cananéens, et Meara qui appartient aux Sidoniens, jusqu'à Aphek, jusqu'à la frontière des Amorrhéens;
kuanzia kusini, nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,
5 le pays des Gébalites, et tout le Liban, vers le soleil levant, depuis Baal Gad au pied de la montagne de l'Hermon jusqu'à l'entrée de Hamath;
eneo la Wagebali; Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
6 tous les habitants de la montagne, depuis le Liban jusqu'à Misrephoth Maïm, tous les Sidoniens. Je les chasserai de devant les enfants d'Israël. Tu le donneras en héritage à Israël, comme je te l'ai ordonné.
“Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza watoke mbele ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,
7 Maintenant, partagez donc ce pays en héritage entre les neuf tribus et la demi-tribu de Manassé. »
sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”
8 Les Rubénites et les Gadites reçurent avec lui l'héritage que Moïse leur avait donné, au-delà du Jourdain, à l'orient, comme Moïse, serviteur de Yahvé, le leur avait donné:
Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Mose aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Bwana alivyowagawia.
9 depuis Aroër, qui est sur le bord du torrent de l'Arnon, et la ville qui est au milieu du torrent, et toute la plaine de Medeba jusqu'à Dibon;
Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyoko ukingoni mwa Bonde la Arnoni kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba mpaka Diboni,
10 et toutes les villes de Sihon, roi des Amoréens, qui régnait à Hesbon, jusqu'à la frontière des enfants d'Ammon;
nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.
11 Galaad, le territoire des Gueschuriens et des Maacathiens, toute la montagne de l'Hermon, tout Basan jusqu'à Salca,
Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:
12 tout le royaume d'Og en Basan, qui régnait à Aschtaroth et à Édréi, le reste des Rephaïm, car Moïse les attaqua et les chassa.
yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Mose alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.
13 Cependant, les enfants d'Israël ne chassèrent pas les Gueshuriens et les Maacathiens; mais Gueshur et Maacath vivent en Israël jusqu'à ce jour.
Lakini Waisraeli hawakuwafukuza watu wa Geshuri na wa Maaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo hii.
14 Seulement, il ne donna aucun héritage à la tribu de Lévi. Les offrandes de Yahvé, le Dieu d'Israël, faites par le feu, sont son héritage, comme il le lui a dit.
Lakini kwa kabila la Lawi, Mose hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Bwana, Mungu wa Israeli, ndizo zilizokuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.
15 Moïse donna à la tribu des fils de Ruben, selon leurs familles.
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Reubeni ukoo kwa ukoo:
16 Leur territoire s'étendait depuis Aroër, qui est sur le bord du torrent de l'Arnon, et la ville qui est au milieu du torrent, et toute la plaine près de Medeba;
Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba
17 Hesbon et toutes ses villes qui sont dans la plaine; Dibon, Bamoth Baal, Beth Baal Meon,
hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,
18 Jahaz, Kedemoth, Mephaath,
Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,
19 Kiriathaïm, Sibma, Zereth Schahar sur la montagne de la vallée,
Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,
20 Beth Peor, les pentes du Pisga, Beth Jeshimoth,
Beth-Peori, materemko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:
21 toutes les villes de la plaine, et tout le royaume de Sihon, roi des Amoréens, qui régnait à Hesbon, et que Moïse frappa avec les chefs de Madian, Evi, Rékem, Tsur, Hur et Réba, princes de Sihon, qui habitaient le pays.
miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Mose alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.
22 Les enfants d'Israël tuèrent aussi par l'épée Balaam, fils de Beor, le devin, parmi le reste de leurs morts.
Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mchawi.
23 La limite des fils de Ruben était la rive du Jourdain. Tel fut l'héritage des fils de Ruben, selon leurs familles, les villes et leurs villages.
Mpaka wa Wareubeni ulikuwa ni ukingo wa Mto Yordani. Miji hii na vijiji vyake ndiyo iliyokuwa urithi wa Wareubeni ukoo kwa ukoo.
24 Moïse donna à la tribu de Gad, aux fils de Gad, selon leurs familles.
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
25 Leur limite était Jaezer, toutes les villes de Galaad et la moitié du pays des enfants d'Ammon, jusqu'à Arœr, près de Rabba;
Nchi ya Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Amoni iliyoenea hadi Aroeri, karibu na Raba;
26 depuis Hesbon, jusqu'à Ramath Mitspé, et Bétonim; depuis Mahanaïm, jusqu'à la frontière de Debir;
na kuanzia Heshboni mpaka Ramath-Mispa na Betonimu, na kutoka Mahanaimu hadi eneo la Debiri;
27 et dans la vallée, Beth Haram, Beth Nimrah, Succoth et Zaphon, le reste du royaume de Sihon, roi de Hesbon, la rive du Jourdain, jusqu'à l'extrémité de la mer de Chinnereth, au-delà du Jourdain, à l'est.
na katika bonde, Beth-Haramu, Beth-Nimra, Sukothi na Safoni na sehemu iliyobaki ya eneo la utawala wa Sihoni mfalme wa Heshboni (upande wa mashariki mwa Mto Yordani, eneo inayoishia kwenye Bahari ya Kinerethi).
28 Tel est l'héritage des fils de Gad, selon leurs familles, les villes et leurs villages.
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Gadi ukoo kwa ukoo.
29 Moïse donna un héritage à la demi-tribu de Manassé. C'était pour la demi-tribu des fils de Manassé, selon leurs familles.
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa hiyo nusu ya kabila la Manase, yaani kwa nusu ya jamaa ya uzao wa Manase, ukoo kwa ukoo:
30 Leur territoire s'étendait depuis Mahanaïm, tout Basan, tout le royaume d'Og, roi de Basan, et tous les villages de Jaïr, qui sont en Basan, soit soixante villes.
Eneo lililoenea kuanzia Mahanaimu, na kujumlisha Bashani yote, ufalme wote wa Ogu mfalme wa Bashani, makazi yote ya Yairi huko Bashani, miji sitini,
31 La moitié de Galaad, Aschtaroth et Édréi, villes du royaume d'Og en Basan, étaient pour les fils de Makir, fils de Manassé, pour la moitié des fils de Makir, selon leurs familles.
nusu ya Gileadi, na Ashtarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Hii ilikuwa kwa ajili ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, kwa ajili ya nusu ya wana wa Makiri, ukoo kwa ukoo.
32 Tels sont les héritages que Moïse distribua dans les plaines de Moab, au-delà du Jourdain, à Jéricho, vers l'est.
Huu ndio urithi alioupeana Mose wakati alipokuwa katika tambarare za Moabu, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
33 Mais Moïse n'a pas donné d'héritage à la tribu de Lévi. Yahvé, le Dieu d'Israël, est leur héritage, comme il le leur a dit.
Lakini kwa kabila la Walawi, Mose hakuwapa urithi; Bwana Mungu, Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.

< Josué 13 >