< Josué 11 >
1 Lorsque Jabin, roi de Hatsor, en eut connaissance, il envoya vers Jobab, roi de Madon, vers le roi de Shimron, vers le roi d'Achshaph,
Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
2 vers les rois qui étaient au nord, dans la montagne, dans la plaine au sud de Chinneroth, dans la plaine et sur les hauteurs de Dor, à l'ouest,
na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
3 aux Cananéens, à l'est et à l'ouest, aux Amoréens, aux Hittites, aux Phéréziens, aux Jébusiens, dans la montagne, et aux Héviens, au pied de l'Hermon, dans le pays de Mitspa.
kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
4 Ils sortirent, eux et toutes leurs armées avec eux, un peuple nombreux, comme le sable qui est au bord de la mer, en multitude, avec un très grand nombre de chevaux et de chars.
Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
5 Tous ces rois se réunirent, et ils vinrent camper ensemble près des eaux de Mérom, pour combattre Israël.
Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
6 Yahvé dit à Josué: « N'aie pas peur à cause d'eux, car demain, à cette heure, je les livrerai tous tués devant Israël. Tu enchaîneras leurs chevaux et tu brûleras au feu leurs chars. »
Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
7 Josué arriva soudain contre eux, avec tous les guerriers, près des eaux de Mérom, et il les attaqua.
Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
8 L'Éternel les livra entre les mains d'Israël, qui les battit et les poursuivit jusqu'à la grande Sidon, jusqu'à Misrephoth Maïm, et jusqu'à la vallée de Mitspa, à l'orient. Ils les frappèrent jusqu'à ce qu'il ne restât plus personne.
naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
9 Josué leur fit ce que Yahvé lui avait dit. Il paralysa leurs chevaux et brûla leurs chars par le feu.
Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
10 En ce temps-là, Josué revint sur ses pas, prit Hatsor et frappa son roi par l'épée, car Hatsor était le chef de tous ces royaumes.
Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
11 Ils frappèrent du tranchant de l'épée tous ceux qui s'y trouvaient, et les dévorèrent par interdit. Il n'y avait plus personne qui respirait. Il brûla Hazor par le feu.
Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
12 Josué prit toutes les villes de ces rois, avec leurs rois, et il les frappa du tranchant de l'épée et les dévoua par interdit, comme l'avait ordonné Moïse, serviteur de l'Éternel.
Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
13 Mais Israël ne brûla aucune des villes situées sur leurs monticules, à l'exception de Hatsor seulement. Josué la brûla.
Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
14 Les enfants d'Israël prirent tout le butin de ces villes, avec le bétail, comme butin pour eux-mêmes; mais ils frappèrent tous les hommes du tranchant de l'épée, jusqu'à ce qu'ils les eussent détruits. Ils n'ont laissé aucun de ceux qui respiraient.
Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
15 Comme Yahvé l'avait ordonné à Moïse, son serviteur, Moïse l'ordonna à Josué. Josué fit ainsi. Il ne négligea rien de tout ce que Yahvé avait ordonné à Moïse.
Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
16 Josué s'empara de tout ce pays, de la montagne, de tout le midi, de tout le pays de Gosen, de la plaine, de la plaine d'Arabie, de la montagne d'Israël et de sa plaine,
Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
17 depuis la montagne de Halak, qui monte vers Séir, jusqu'à Baal Gad, dans la vallée du Liban, sous la montagne de l'Hermon. Il prit tous leurs rois, les frappa et les fit mourir.
kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
18 Josué fit longtemps la guerre à tous ces rois.
Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
19 Il n'y eut pas une seule ville qui fit la paix avec les enfants d'Israël, sauf les Hivvites, habitants de Gabaon. Ils les prirent tous dans la bataille.
Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
20 Car c'était la volonté de l'Éternel d'endurcir leur cœur, de venir contre Israël dans la bataille, pour les dévaster, pour qu'ils n'aient aucune faveur, mais pour les détruire, comme l'Éternel l'avait ordonné à Moïse.
Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
21 Josué arriva en ce temps-là, et il extermina les Anakim de la montagne, d'Hébron, de Debir, d'Anab, de toute la montagne de Juda et de toute la montagne d'Israël. Josué les dévoua par interdit, avec leurs villes.
Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
22 Il ne resta aucun des Anakim dans le pays des enfants d'Israël. Il en resta seulement à Gaza, à Gath et à Asdod.
Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
23 Josué prit tout le pays, selon tout ce que l'Éternel avait dit à Moïse, et il le donna en héritage à Israël, selon ses tribus. Et le pays fut en repos de la guerre.
Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.