< Jonas 2 >
1 Alors Jonas pria Yahvé, son Dieu, du fond du ventre du poisson.
Kisha Yona akamwomba Bwana Mungu wake kutoka katika tumbo la samaki.
2 Il dit, « J'ai appelé Yahvé à cause de mon affliction. Il m'a répondu. J'ai crié du ventre de Sheol. Tu as entendu ma voix. (Sheol )
Akasema, Nimemwita Bwana juu ya shida yangu naye akanijibu; kutoka tumbo la Kuzimu nililia kwa msaada! Uliisikia sauti yangu. (Sheol )
3 Car tu m'as jeté dans les profondeurs, au cœur des mers. Le déluge était tout autour de moi. Toutes tes vagues et tes tourbillons sont passés sur moi.
Ulikuwa umenitupa ndani ya kina, ndani ya moyo wa bahari, na maji yaliyonizunguka; mawimbi yako yote na gharika yalipita juu yangu.
4 J'ai dit: « J'ai été banni de ta vue »; mais je regarderai de nouveau vers ton temple saint.
Nikasema, 'Nimefukuzwa mbele ya macho yako; lakini nitaangalia tena juu ya hekalu lako takatifu. '
5 Les eaux m'ont entouré, jusqu'à l'âme. La profondeur était autour de moi. Les mauvaises herbes s'enroulaient autour de ma tête.
Maji yalifunika kunizunguka karibu na shingo yangu; kina kilinizunguka; mwani ukakizinga kichwa changu.
6 Je suis descendu au pied des montagnes. La terre m'a barré la route pour toujours; mais tu as fait sortir ma vie de la fosse, Yahvé mon Dieu.
Nilikwenda chini ya milima; nchi na baa zake zimefungwa juu yangu milele. Lakini wewe umeinua uhai wangu shimoni, Bwana, Mungu wangu!
7 « Quand mon âme s'est évanouie au-dedans de moi, je me suis souvenu de Yahvé. Ma prière est entrée chez toi, dans ton temple sacré.
Wakati nafsi yangu ilipozimia ndani yangu, nikamwita Bwana; basi sala yangu ilikujia, katika hekalu lako takatifu.
8 Ceux qui regardent de vaines idoles abandonnent leur propre miséricorde.
Wote ambao huzingatia miungu isiyofaa hukataa uaminifu wako wao wenyewe.
9 Mais je t'offrirai des sacrifices avec la voix de l'action de grâces. Je paierai ce que j'ai promis. Le salut appartient à Yahvé. »
Lakini mimi, nitakuchinjia kwa sauti ya shukrani; Nitayatimiza yale niliyoapa. Wokovu hutoka kwa Bwana!
10 Yahvé parla au poisson, et celui-ci vomit Jonas sur la terre ferme.
Kisha Bwana akanena na samaki, akamtapika Yona juu ya nchi kavu.