< Joël 2 >
1 Sonnez de la trompette en Sion, et de sonner l'alarme dans ma montagne sacrée! Que tous les habitants du pays tremblent, car le jour de Yahvé arrive, car elle est proche:
Piga tarumbeta katika Sayuni, na piga kelele juu ya mlima wangu mtakatifu! Wakazi wote wa nchi watetemeke kwa hofu; maana siku ya Bwana inakuja; Hakika iko karibu.
2 Un jour de ténèbres et d'obscurité, un jour de nuages et d'obscurité épaisse. Comme l'aube qui se répand sur les montagnes, un peuple grand et fort; il n'y a jamais eu de tel, et il n'y en aura pas d'autres après eux, même jusqu'aux années de plusieurs générations.
Ni siku ya giza na weusi, siku ya mawingu na giza nene. Kama asubuhi inayoenea kwenye milima, jeshi kubwa na la nguvu linakaribia. Hakujawahi kuwako jeshi kama hilo, na hakutakuwa tena, hata baada ya vizazi vingi.
3 Un feu dévore devant eux, et derrière eux, une flamme brûle. La terre est comme le jardin d'Eden devant eux, et derrière eux, une étendue sauvage et désolée. Oui, et personne ne leur a échappé.
Moto unatumia kila kitu mbele yake, na nyuma yake moto unawaka. Nchi hiyo ni kama bustani ya Edeni mbele yake, lakini nyuma yake kuna jangwa lililoharibika. Hakika hakuna chochote kitakayotoroka.
4 Leur apparence est comme celle de chevaux, et ils courent comme des cavaliers.
Muonekano wa jeshi ni kama farasi, na wanakimbia kama wapanda farasi.
5 Comme le bruit des chars sur les sommets des montagnes, ils bondissent, comme le bruit d'une flamme de feu qui dévore le chaume, comme un peuple fort en ordre de bataille.
Wanaruka kwa kelele kama ile ya magari juu ya vilele vya milima, kama kelele za muale wa moto ambao huangamiza majani, kama jeshi la nguvu lililo tayari kwa vita.
6 En leur présence, les peuples sont dans l'angoisse. Tous les visages sont devenus pâles.
Mbele yao watu wako katika maumivu na nyuso zao zote zinakuwa za rangi.
7 Ils courent comme des hommes puissants. Ils escaladent le mur comme des guerriers. Ils marchent chacun dans sa ligne, et ils ne dévient pas de leur trajectoire.
Wanakimbia kama wapiganaji wenye nguvu; wanapanda kuta kama askari; wanasonga, kila mmoja kwa hatua, na hawavunji safu zao.
8 L'un ne bouscule pas l'autre. Ils suivent chacun leur propre chemin. Ils ont percé les défenses et ne rompez pas les rangs.
Wala hakuna mmoja anayemsukuma mwingine kando; wanasonga, kila mmoja katika njia yake; wao huvunja kwa njia ya ulinzi na si kuanguka nje ya mstari.
9 Ils se précipitent sur la ville. Ils courent sur le mur. Ils montent dans les maisons. Ils entrent par les fenêtres comme des voleurs.
Wanakimbilia jiji, wanakimbia kwenye ukuta, wanapanda ndani ya nyumba, na hupita kupitia madirisha kama wezi.
10 La terre tremble devant eux. Les cieux tremblent. Le soleil et la lune sont obscurcis, et les étoiles retirent leur éclat.
Nchi hutikisika mbele yao, mbingu hutetemeka, jua na mwezi ni giza, na nyota zinaacha kuangaza.
11 Yahvé fait tonner sa voix devant son armée, car ses forces sont très importantes; car celui qui obéit à ses ordres est fort; car le jour de Yahvé est grand et très impressionnant, et qui peut l'endurer?
Bwana huinua sauti yake mbele ya jeshi lake; maana wapiganaji wake ni wengi sana; kwa maana wao ni wenye nguvu, wale wanaofanya amri zake. Kwa maana siku ya Bwana ni kubwa na ya kutisha sana. Nani anayeweza kuishi?
12 « Maintenant encore, dit Yahvé, tourne-toi vers moi de tout ton cœur, et avec le jeûne, et avec les pleurs, et avec le deuil. »
“Lakini hata sasa,” asema Bwana, “Nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote. Haraka, lia na omboleza.”
13 Déchire ton cœur et non tes vêtements, et tournez-vous vers Yahvé, votre Dieu; car il est gracieux et miséricordieux, lent à la colère, et abondant en bonté, et cesse d'envoyer des calamités.
Rarueni miyoyo yenu, si mavazi yenu tu, na kurudi kwa Bwana Mungu wenu. Kwa maana ni mwenye neema na mwenye huruma, si mwepesi wa hasira na wingi katika uaminifu wa agano, na angependa kugeuka kutokana na adhabu.
14 Qui sait? Il pourrait se retourner et céder, et laisser une bénédiction derrière lui, une offrande de repas et une offrande de boisson à Yahvé, ton Dieu.
Nani anajua? Labda angegeuka na kuwa na huruma, na kuacha baraka nyuma yake, sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji kwa Bwana, Mungu wenu?
15 Sonnez de la trompette en Sion! Sanctifier un jeûne. Convoquez une assemblée solennelle.
Piga tarumbeta huko Sayuni, itisha kwa ajili ya funga takatifu, na itisheni kusanyiko takatifu.
16 Rassemblez le peuple. Sanctifier l'assemblée. Rassemblez les anciens. Rassemblez les enfants, et ceux qui allaitent au sein. Que le marié sorte de sa chambre, et la mariée hors de sa chambre.
Kusanyeni watu, wito kwa kusanyiko takatifu. Kusanya wazee, kukusanya watoto na watoto wachanga. Bwana arusi waweze kutoka nje ya vyumba vyao, na bibi arusi kutoka kwenye vyumba vyao.
17 Que les prêtres, les ministres de Yahvé, pleurent entre le portique et l'autel, et qu'ils disent: « Épargne ton peuple, Yahvé, et ne donnez pas votre héritage à la réprobation, pour que les nations dominent sur eux. Pourquoi diraient-ils parmi les peuples, « Où est leur Dieu? »
Basi makuhani, watumishi wa Bwana, waliao kati ya patakatifu na madhabahu. Wawaambie, Waitie watu wako, Ee Bwana, wala usitoe urithi wako kwa aibu, ili mataifa watawawale juu yao. Kwa nini wanapaswa kusema kati ya mataifa, “Yuko wapi Mungu wao?”
18 Alors Yahvé fut jaloux de son pays, et a eu pitié de son peuple.
Ndipo Bwana alikuwa mwenye bidii kwa nchi yake na kuwahurumia watu wake.
19 Yahvé répondit à son peuple, « Voici que je vais vous envoyer du blé, du vin nouveau et de l'huile, et vous en serez satisfait; et je ne ferai plus de toi un objet d'opprobre parmi les nations.
Bwana akawajibu watu wake, Tazama, nitawaletea nafaka, divai mpya, na mafuta. Utaridhishwa nao, wala sitawafanya kuwa aibu kati ya mataifa.
20 Mais j'éloignerai l'armée du nord loin de vous, et le conduira dans une terre stérile et désolée, son front dans la mer orientale, et son retour dans la mer occidentale; et sa puanteur remontera, et sa mauvaise odeur s'élèvera. » Il a certainement fait de grandes choses.
Nitawaondoa washambuliaji wa kaskazini mbali nanyi, na nitawapitisha katika nchi kavu na iliyoachwa. Sehemu ya mbele ya jeshi lao itaingia bahari ya mashariki, na sehemuya nyuma itaingia bahari ya magharibi. Uvundo wake utainuka juu, na harufu yake mbaya itainuka juu. Hakika, amefanya mambo makuu.
21 Terre, n'aie pas peur. Soyez heureux et réjouissez-vous, car Yahvé a fait de grandes choses.
Msiogope, nchi, shangilieni na kufurahi, kwa kuwa Bwana atafanya mambo makuu.
22 N'ayez pas peur, bêtes des champs; car les pâturages du désert surgissent, car l'arbre porte ses fruits. Le figuier et la vigne donnent leur force.
Usiogope, wanyama wa kondeni, kwa kuwa malisho ya jangwa yatakua, miti itazaa matunda yake, na miti ya mizabibu na mizabibu itazaa mavuno yao yote.
23 « Réjouissez-vous donc, enfants de Sion, et réjouissez-vous en Yahvé, votre Dieu; car il vous donne la pluie du matin en juste mesure, et il fait tomber la pluie pour vous, la pluie précoce et la pluie tardive, comme auparavant.
Furahini, enyi watu wa Sayuni, na kufurahi katika Bwana, Mungu wenu. Kwa maana atakupa mvua ya vuli kwa kiasi na kuleta mvua kwa ajili yenu, mvua ya vuli na mvua ya masika kama hapo awali.
24 Les aires de battage seront pleines de blé, et les cuves déborderont de vin nouveau et d'huile.
Sakafu ya kupepetea zitajaa ngano, na vyombo vitafurika kwa divai mpya na mafuta.
25 Je vous rendrai les années que le criquet pèlerin a dévorées, le grand criquet, la sauterelle, et la chenille, ma grande armée, que j'ai envoyée parmi vous.
“Nitawawezesha miaka ya mazao ambayo nzige walikula, Palale, nzige, na nzige wakuteketeza - jeshi langu lenye nguvu ambalo nimelituma kati yenu.
26 Vous aurez beaucoup à manger et serez rassasiés, et vous louerez le nom de Yahvé, votre Dieu, qui a fait des merveilles avec vous; et mon peuple ne sera plus jamais déçu.
Mutakula chakula tele na kushiba, na kulitukuza jina la Bwana, Mungu wenu, aliyefanya miujiza kati yenu, wala sitawaletea tena watu wangu.
27 Vous saurez que je suis au milieu d'Israël, et que je suis Yahvé, ton Dieu, et qu'il n'y en a pas d'autre; et mon peuple ne sera plus jamais déçu.
Utajua ya kwamba mimi niko kati ya Israeli, na kwamba mimi ni Bwana, Mungu wako, wala hakuna mwingine, wala sitawaletea aibu watu wangu.
28 « Ensuite, il arrivera que je répandrai mon Esprit sur toute chair; et vos fils et vos filles prophétiseront. Vos vieux hommes feront des rêves. Vos jeunes hommes auront des visions.
Itakuwa baada ya hayo nitamimina Roho yangu juu ya wenye mwili yote, na wana wenu na binti zenu watatabiri. Wazee wenu wataota ndoto, vijana wenu wataona maono.
29 Et aussi sur les serviteurs et sur les servantes en ces jours-là, Je déverserai mon Esprit.
Pia juu ya watumishi na watumishi wa kike, siku hizo nitaimimina Roho wangu.
30 Je ferai des prodiges dans les cieux et sur la terre: du sang, du feu, et des colonnes de fumée.
Nitaonyesha maajabu mbinguni na duniani, damu, moto na nguzo za moshi.
31 Le soleil se changera en ténèbres, et la lune en sang, avant que n'arrive le jour grand et terrible de Yahvé.
Jua litakuwa giza na mwezi kuwa damu, kabla ya siku kuu na ya kutisha ya Bwana itakapokuja.
32 Il arrivera que quiconque invoquera le nom de Yahvé sera sauvé; car sur la montagne de Sion et à Jérusalem, il y aura ceux qui s'échapperont, comme Yahvé l'a dit, et parmi les restants, ceux que Yahvé appelle.
Itakuwa kwamba kila mtu anayeita jina la Yahweh ataokolewa. Kwa maana juu ya Mlima Sayuni na Yerusalemu watakuwa na wale waliokoka, kama Bwana alivyosema, na kati ya wale walisalia, wale ambao Bwana anawaita.