< Job 6 >

1 Alors Job répondit,
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 « Oh! si mon angoisse était pesée, et que toutes mes calamités soient mises dans la balance!
“Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
3 Car maintenant, il serait plus lourd que le sable des mers, c'est pourquoi mes paroles ont été irréfléchies.
Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 Car les flèches du Tout-Puissant sont en moi. Mon esprit boit leur poison. Les terreurs de Dieu se sont dressées contre moi.
Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
5 L'âne sauvage braille-t-il quand il a de l'herbe? Ou le bœuf se penche-t-il sur son fourrage?
Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
6 Peut-on manger sans sel ce qui n'a pas de saveur? Ou y a-t-il un goût dans le blanc d'un œuf?
Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
7 Mon âme refuse de les toucher. Ils sont comme de la nourriture répugnante pour moi.
Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
8 « Oh, que je puisse avoir ma demande, que Dieu m'accorde la chose que je désire,
Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
9 même qu'il plairait à Dieu de m'écraser; qu'il lâche sa main, et me coupe!
kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
10 Qu'elle soit encore ma consolation, oui, laissez-moi exulter dans la douleur qui n'épargne pas, que je n'ai pas renié les paroles du Saint.
Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
11 Quelle est ma force, pour que j'attende? Quelle est ma fin, pour que je sois patient?
Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
12 Ma force est-elle la force des pierres? Ou ma chair est-elle de bronze?
Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
13 N'est-ce pas que je n'ai pas de secours en moi, que la sagesse est éloignée de moi?
Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
14 « A celui qui est prêt à s'évanouir, il faut que son ami fasse preuve de bonté; même à celui qui abandonne la crainte du Tout-Puissant.
Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
15 Mes frères ont agi de façon trompeuse comme un ruisseau, comme le canal des ruisseaux qui passent;
Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
16 qui sont noirs à cause de la glace, dans laquelle la neige se cache.
ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
17 Pendant la saison sèche, ils disparaissent. Quand il fait chaud, ils sont consommés hors de leur place.
Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
18 Les caravanes qui voyagent à côté d'eux se détournent. Ils montent dans le désert, et périssent.
Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
19 Les caravanes de Tema regardaient. Les compagnies de Saba les attendaient.
Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
20 Ils ont été affligés parce qu'ils étaient confiants. Ils sont arrivés là, et ont été confondus.
Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
21 Car maintenant vous n'êtes rien. Vous voyez une terreur, et vous avez peur.
Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
22 Ai-je jamais dit: « Donne-moi »? ou « Offrez-moi un cadeau de votre substance »?
Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
23 ou « Délivre-moi de la main de l'adversaire »? ou: « Délivre-moi de la main de l'oppresseur »?
Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
24 « Apprends-moi, et je me tairai. Fais-moi comprendre mon erreur.
Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
25 Quelle force ont les paroles de la droiture! Mais votre réprobation, que réprouve-t-elle?
Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
26 Avez-vous l'intention de réprouver les mots, puisque les discours de celui qui est désespéré sont comme du vent?
Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
27 Oui, vous tireriez même au sort pour l'orphelin, et faire de votre ami une marchandise.
Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
28 Maintenant, regardez-moi avec plaisir, car je ne te mentirai pas en face.
Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
29 Veuillez retourner. Qu'il n'y ait pas d'injustice. Oui, revenez encore. Ma cause est juste.
Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
30 Y a-t-il de l'injustice sur ma langue? Mon goût ne peut-il pas discerner des choses malicieuses?
Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?

< Job 6 >