< Job 5 >
1 « Appelle maintenant; y a-t-il quelqu'un qui te réponde? Vers lequel des saints vous tournerez-vous?
Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
2 Car la rancune tue l'homme insensé, et la jalousie tue les simples.
Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
3 J'ai vu l'insensé prendre racine, mais j'ai soudainement maudit son habitation.
Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
4 Ses enfants sont loin de la sécurité. Ils sont écrasés dans la porte. Il n'y en a pas non plus pour les délivrer,
Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
5 dont la récolte est dévorée par les affamés, et le sortir même des épines. Le piège s'ouvre pour leur substance.
Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
6 Car l'affliction ne sort pas de la poussière, Les problèmes ne sortent pas non plus du sol;
Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
7 mais l'homme est né pour les problèmes, alors que les étincelles volent vers le haut.
Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
8 « Quant à moi, je chercherais Dieu. Je confierais ma cause à Dieu,
Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
9 qui fait de grandes choses qui ne peuvent pas être sondées, des choses merveilleuses sans nombre;
yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
10 qui donne la pluie sur la terre, et envoie des eaux sur les champs;
Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
11 afin qu'il élève en haut ceux qui sont bas, ceux qui pleurent sont élevés en sécurité.
Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
12 Il fait échouer les plans des rusés, de sorte que leurs mains ne peuvent pas accomplir leur entreprise.
Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
13 Il prend les sages dans leur propre ruse; le conseil des rusés est porté à bout de bras.
Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
14 Ils rencontrent les ténèbres pendant le jour, et tâtonnent à midi comme dans la nuit.
Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
15 Mais il sauve de l'épée de leur bouche, même le nécessiteux de la main des puissants.
Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
16 Le pauvre a donc de l'espoir, et l'injustice lui fait fermer la bouche.
Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
17 « Voici, heureux l'homme que Dieu corrige. Ne méprisez donc pas le châtiment du Tout-Puissant.
Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
18 Car il blesse et panse. Il blesse et ses mains réparent.
Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
19 Il te délivrera dans six épreuves; Oui, en sept, aucun mal ne vous touchera.
Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
20 Dans la famine, il te rachètera de la mort; dans la guerre, de la puissance de l'épée.
Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
21 Tu seras à l'abri du fléau de la langue, vous n'aurez pas non plus peur de la destruction quand elle viendra.
Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
22 Vous rirez de la destruction et de la famine, vous n'aurez pas non plus peur des animaux de la terre.
Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
23 Car vous serez alliés aux pierres des champs. Les animaux des champs seront en paix avec vous.
Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
24 Tu sauras que ta tente est en paix. Vous visiterez votre pli, et ne manquerez rien.
Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
25 Tu sauras aussi que ta descendance sera grande, ta progéniture comme l'herbe de la terre.
Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
26 Tu viendras au tombeau dans un âge avancé, comme un choc de grain vient en sa saison.
Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
27 Voici, nous avons fait des recherches. Il en est ainsi. Entendez-le, et sachez que c'est pour votre bien. »
Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”