< Job 32 >
1 Ces trois hommes cessèrent donc de répondre à Job, car il était juste à ses propres yeux.
Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
2 Alors la colère d'Élihu, fils de Barachel, le Buzite, de la famille de Ram, s'enflamma contre Job. Sa colère s'enflamma parce qu'il se justifiait lui-même plutôt que Dieu.
Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
3 Sa colère s'enflamma aussi contre ses trois amis, parce qu'ils n'avaient pas trouvé de réponse, et qu'ils avaient pourtant condamné Job.
Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
4 Or Élihu avait attendu pour parler à Job, car ils étaient plus âgés que lui.
Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
5 Quand Élihu vit qu'il n'y avait pas de réponse dans la bouche de ces trois hommes, sa colère s'enflamma.
Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
6 Elihu, fils de Barachel, le Buzite, répondit, « Je suis jeune, et vous êtes très vieux. C'est pourquoi je me suis retenu, et je n'ai pas osé te montrer mon opinion.
Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
7 J'ai dit: « Les jours doivent parler, et la multitude d'années devrait enseigner la sagesse.
Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
8 Mais il y a un esprit dans l'homme, et l'Esprit du Tout-Puissant leur donne l'intelligence.
Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
9 Ce ne sont pas les grands qui sont sages, ni les personnes âgées qui comprennent la justice.
Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
10 C'est pourquoi j'ai dit: « Écoutez-moi; Je vais aussi montrer mon opinion.
Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
11 « Voici, j'attendais tes paroles, et j'ai écouté votre raisonnement, pendant que tu cherchais quoi dire.
Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
12 Oui, je vous ai accordé toute mon attention, mais personne n'a convaincu Job, ou qui ont répondu à ses paroles, parmi vous.
Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
13 Prenez garde de ne pas dire: « Nous avons trouvé la sagesse ». Dieu peut le réfuter, pas l'homme;
Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
14 car il n'a pas dirigé ses paroles contre moi; je ne lui répondrai pas non plus par vos discours.
Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
15 « Ils sont stupéfaits. Ils ne répondent plus. Ils n'ont pas un mot à dire.
Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
16 Dois-je attendre, car ils ne parlent pas? parce qu'ils restent immobiles, et ne répondent plus?
Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
17 Je vais aussi répondre à ma part, et je vais aussi montrer mon opinion.
La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
18 Car je suis plein de paroles. L'esprit qui est en moi me contraint.
Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
19 Voici, ma poitrine est comme un vin qui n'a pas d'issue; comme des outres neuves, il est prêt à éclater.
Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
20 Je vais parler, pour me rafraîchir. Je vais ouvrir mes lèvres et répondre.
Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
21 S'il vous plaît, ne me laissez pas respecter la personne d'un homme, Je ne donnerai pas non plus de titres flatteurs à un homme.
Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
22 Car je ne sais pas donner des titres flatteurs, ou bien mon Créateur m'emporterait bientôt.
Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.