< Job 14 >
1 « L'homme, qui est né d'une femme, est de peu de jours, et pleine d'ennuis.
Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
2 Il croît comme une fleur, et on le coupe. Il fuit aussi comme une ombre, et ne continue pas.
Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
3 Ouvrez-vous les yeux sur une telle personne, et m'amener en jugement avec vous?
Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
4 Qui peut faire sortir un objet pur d'un objet impur? Pas un seul.
Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
5 Voyant que ses jours sont déterminés, le nombre de ses mois est avec vous, et vous avez nommé ses limites qu'il ne peut pas dépasser.
Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
6 Détournez les yeux de lui, pour qu'il se repose, jusqu'à ce qu'il accomplisse, comme un mercenaire, sa journée.
Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
7 « Car il y a de l'espoir pour un arbre si on le coupe, qu'il germera à nouveau, que sa tendre branche ne cessera pas.
Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
8 Mais sa racine vieillit dans la terre, et son stock meurt dans le sol,
Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
9 pourtant, grâce à l'odeur de l'eau, il bourgeonnera, et faire pousser des rameaux comme une plante.
hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
10 Mais l'homme meurt, il est abattu. Oui, l'homme abandonne l'esprit, et où est-il?
Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
11 Comme les eaux s'éloignent de la mer, et la rivière se vide et s'assèche,
Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
12 Alors l'homme se couche et ne se relève pas. Jusqu'à ce que les cieux ne soient plus, ils ne se réveilleront pas, ni être tirés de leur sommeil.
vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
13 « Oh! si tu me cachais dans le séjour des morts, que tu me garderais secret jusqu'à ce que ta colère soit passée, que vous me désigniez un moment précis et que vous vous souveniez de moi! (Sheol )
Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol )
14 Si un homme meurt, vivra-t-il de nouveau? J'attendrais tous les jours de ma guerre, jusqu'à ce que je sois libéré.
Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
15 Vous appeliez, et je vous répondais. Vous auriez un désir pour le travail de vos mains.
Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
16 Mais maintenant, tu comptes mes pas. Ne veillez-vous pas sur mon péché?
Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
17 Ma désobéissance est enfermée dans un sac. Vous fixez mon iniquité.
Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
18 « Mais la montagne qui s'écroule n'aboutit à rien. La pierre est retirée de sa place.
Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
19 Les eaux usent les pierres. Ses torrents emportent la poussière de la terre. Donc vous détruisez l'espoir de l'homme.
maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
20 Vous l'emportez à jamais sur lui, et il s'en va. Vous changez son visage, et le renvoyez.
Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
21 Ses fils viennent à l'honneur, et il ne le sait pas. Ils sont rabaissés, mais il ne le perçoit pas d'eux.
Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
22 Mais sa chair, sur lui, souffre, et son âme en lui se lamente. »
Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.