< Job 13 >

1 « Voici, mon œil a vu tout cela. Mon oreille l'a entendu et compris.
Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
2 Ce que vous savez, je le sais aussi. Je ne suis pas inférieur à vous.
Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
3 « Certes, je parlerais au Tout-Puissant. Je désire raisonner avec Dieu.
Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
4 Mais vous êtes des falsificateurs de mensonges. Vous êtes tous des médecins sans valeur.
Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
5 Oh, que vous soyez complètement silencieux! Alors vous seriez sage.
Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
6 Écoutez maintenant mon raisonnement. Écoutez les supplications de mes lèvres.
Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
7 Parleras-tu injustement pour Dieu, et parler mensongèrement pour lui?
Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
8 Allez-vous faire preuve de partialité à son égard? Allez-vous lutter pour Dieu?
Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
9 Est-il bon qu'il te cherche? Ou comme on trompe un homme, le tromperez-vous?
Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
10 Il vous réprimandera sûrement si vous faites secrètement preuve de partialité.
Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
11 Sa majesté ne vous fera-t-elle pas peur? et que son effroi s'abatte sur vous?
Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
12 Vos paroles mémorables sont des proverbes de cendre. Vos défenses sont des défenses d'argile.
Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
13 « Taisez-vous! Laissez-moi seul, que je puisse parler. Laisse venir sur moi ce qui va.
Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
14 Pourquoi devrais-je prendre ma chair dans mes dents, et mettre ma vie dans ma main?
Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
15 Voici, il va me tuer. Je n'ai pas d'espoir. Néanmoins, je maintiendrai mes voies devant lui.
Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
16 C'est là aussi que sera mon salut, qu'un homme impie ne viendra pas devant lui.
Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
17 Écoutez attentivement mon discours. Que ma déclaration soit dans vos oreilles.
Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
18 Voyez maintenant, j'ai mis ma cause en ordre. Je sais que je suis juste.
Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
19 Qui est celui qui contestera avec moi? Car alors je me tairais et abandonnerais l'esprit.
Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
20 « Seulement, ne me fais pas deux choses, alors je ne me cacherai pas de ta face:
Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
21 retire ta main loin de moi, et ne laisse pas ta terreur me faire peur.
Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
22 Alors appelez, et je répondrai, ou laissez-moi parler, et vous me répondez.
Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
23 Combien sont mes iniquités et mes péchés? Fais-moi connaître ma désobéissance et mon péché.
Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
24 Pourquoi cachez-vous votre visage, et me considérer comme votre ennemi?
Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
25 Harcèlerez-vous une feuille morte? Allez-vous poursuivre le chaume sec?
Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
26 Car vous écrivez des choses amères contre moi, et me faire hériter des iniquités de ma jeunesse.
Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
27 Tu as aussi mis mes pieds dans les ceps, et marque tous mes chemins. Tu as mis un lien à la plante de mes pieds,
Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
28 bien que je me décompose comme une chose pourrie, comme un vêtement usé par les mites.
japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.

< Job 13 >