< Job 13 >

1 « Voici, mon œil a vu tout cela. Mon oreille l'a entendu et compris.
“Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
2 Ce que vous savez, je le sais aussi. Je ne suis pas inférieur à vous.
Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
3 « Certes, je parlerais au Tout-Puissant. Je désire raisonner avec Dieu.
Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
4 Mais vous êtes des falsificateurs de mensonges. Vous êtes tous des médecins sans valeur.
Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
5 Oh, que vous soyez complètement silencieux! Alors vous seriez sage.
Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
6 Écoutez maintenant mon raisonnement. Écoutez les supplications de mes lèvres.
Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
7 Parleras-tu injustement pour Dieu, et parler mensongèrement pour lui?
Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
8 Allez-vous faire preuve de partialité à son égard? Allez-vous lutter pour Dieu?
Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
9 Est-il bon qu'il te cherche? Ou comme on trompe un homme, le tromperez-vous?
Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
10 Il vous réprimandera sûrement si vous faites secrètement preuve de partialité.
Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
11 Sa majesté ne vous fera-t-elle pas peur? et que son effroi s'abatte sur vous?
Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
12 Vos paroles mémorables sont des proverbes de cendre. Vos défenses sont des défenses d'argile.
Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
13 « Taisez-vous! Laissez-moi seul, que je puisse parler. Laisse venir sur moi ce qui va.
“Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
14 Pourquoi devrais-je prendre ma chair dans mes dents, et mettre ma vie dans ma main?
Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
15 Voici, il va me tuer. Je n'ai pas d'espoir. Néanmoins, je maintiendrai mes voies devant lui.
Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
16 C'est là aussi que sera mon salut, qu'un homme impie ne viendra pas devant lui.
Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
17 Écoutez attentivement mon discours. Que ma déclaration soit dans vos oreilles.
Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
18 Voyez maintenant, j'ai mis ma cause en ordre. Je sais que je suis juste.
Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
19 Qui est celui qui contestera avec moi? Car alors je me tairais et abandonnerais l'esprit.
Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
20 « Seulement, ne me fais pas deux choses, alors je ne me cacherai pas de ta face:
“Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
21 retire ta main loin de moi, et ne laisse pas ta terreur me faire peur.
Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
22 Alors appelez, et je répondrai, ou laissez-moi parler, et vous me répondez.
Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
23 Combien sont mes iniquités et mes péchés? Fais-moi connaître ma désobéissance et mon péché.
Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
24 Pourquoi cachez-vous votre visage, et me considérer comme votre ennemi?
Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
25 Harcèlerez-vous une feuille morte? Allez-vous poursuivre le chaume sec?
Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
26 Car vous écrivez des choses amères contre moi, et me faire hériter des iniquités de ma jeunesse.
Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
27 Tu as aussi mis mes pieds dans les ceps, et marque tous mes chemins. Tu as mis un lien à la plante de mes pieds,
Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
28 bien que je me décompose comme une chose pourrie, comme un vêtement usé par les mites.
“Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.

< Job 13 >