< Jérémie 48 >
1 De Moab. Yahvé des Armées, le Dieu d'Israël, dit: « Malheur à Nebo! Car elle est dévastée. Kiriathaim est déçu. Il est pris. Misgab est mis à mal et en panne.
Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.
2 Les louanges de Moab n'existent plus. A Heshbon, ils ont conçu le mal contre elle: « Venez! Coupons-lui la possibilité d'être une nation. Vous aussi, les fous, vous serez réduits au silence. L'épée vous poursuivra.
Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
3 Le son d'un cri venant de Horonaim, désolation et grande destruction!
Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.
4 Moab est détruit. Ses petits ont fait entendre un cri.
Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.
5 Car ils monteront par la montée de Luhith en pleurant continuellement. Car à la descente des Horonaïm, ils ont entendu la détresse du cri de destruction.
Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.
6 Fuyez! Sauvez vos vies! Soyez comme le buisson de genévrier dans le désert.
Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.
7 Car, parce que tu t'es confié dans tes œuvres et dans tes trésors, vous serez également pris. Chemosh partira en captivité, ses prêtres et ses princes ensemble.
Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.
8 Le destructeur s'abattra sur toutes les villes, et aucune ville n'y échappera; la vallée aussi périra, et la plaine sera détruite, comme Yahvé l'a dit.
Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.
9 Donnez des ailes à Moab, pour qu'elle puisse voler et s'enfuir: et ses villes deviendront une désolation, sans personne pour les habiter.
Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.
10 « Maudit soit celui qui accomplit l'œuvre de Yahvé avec négligence; et maudit soit celui qui retient son épée du sang.
“Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!
11 « Moab a été à l'aise dès sa jeunesse, et il s'est installé sur sa lie, et n'a pas été vidée d'un navire à l'autre, et il n'est pas allé en captivité; son goût reste donc en lui, et son odeur n'est pas modifiée.
“Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.
12 C'est pourquoi voici, les jours viennent, dit Yahvé, « que j'enverrai vers lui ceux qui versent, et ils vont le verser; et ils videront ses vaisseaux, et briser leurs récipients en morceaux.
Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.
13 Moab aura honte de Kemosch, comme la maison d'Israël a eu honte de Béthel, sa confiance.
Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.
14 « Comment pouvez-vous dire: « Nous sommes des hommes puissants »? et des hommes vaillants pour la guerre »?
“Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?
15 Moab est dévasté, et ils sont montés dans ses villes, et ses jeunes hommes choisis sont allés à l'abattoir, » dit le Roi, dont le nom est Yahvé des Armées.
Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
16 « La calamité de Moab est proche, et son malheur se précipite.
“Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.
17 Vous tous qui êtes autour de lui, plaignez-vous de lui; et vous tous qui connaissez son nom, dites, « Comment le personnel fort est brisé, la belle tige!
Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’
18 « Fille qui habite à Dibon, descends de ta gloire, et s'asseoir dans la soif; car le destructeur de Moab est monté contre toi. Il a détruit vos forteresses.
“Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.
19 Habitant d'Arœr, tenez-vous sur le chemin et veillez. Demandez à celui qui fuit, et à celle qui s'échappe; dire: « Qu'est-ce qui a été fait?
Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’
20 Moab est déçu; car il est en panne. Gémissez et pleurez! Dites par l'Arnon que Moab est dévasté.
Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.
21 Le jugement est venu sur le pays de la plaine - sur Holon, sur Jahzah, sur Mephaath,
Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,
22 sur Dibon, sur Nebo, sur Beth Diblathaim,
katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,
23 sur Kiriathaim, sur Beth Gamul, sur Beth Meon,
katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,
24 sur Kerioth, sur Bozrah, et sur toutes les villes du pays de Moab, de loin ou de près.
katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.
25 La corne de Moab est coupée, et son bras est cassé », dit Yahvé.
Pembe ya Moabu imekatwa, mkono wake umevunjwa,” asema Bwana.
26 « Fais-le boire, car il s'est élevé contre Yahvé. Moab se vautrera dans son vomi, et lui aussi sera tourné en dérision.
“Mlevye, kwa kuwa amemdharau Bwana. Moabu na agaegae katika matapishi yake, yeye na awe kitu cha dhihaka.
27 Car Israël n'était-il pas pour vous une dérision? Il a été trouvé parmi des voleurs? Car aussi souvent que vous parlez de lui, vous secouez la tête.
Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa? Je, alikamatwa miongoni mwa wezi, kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau kila mara unapozungumza juu yake?
28 Vous, habitants de Moab, quittez les villes, et habitez le rocher. Soyez comme la colombe qui fait son nid au-dessus de la bouche de l'abîme.
Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba, enyi mnaoishi Moabu. Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake kwenye mdomo wa pango.
29 « Nous avons entendu parler de l'orgueil de Moab. Il est très fier de sa hauteur, de son orgueil, son arrogance, et l'arrogance de son cœur.
“Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno, kiburi chake na ufidhuli wake, na kujivuna kwa moyo wake.
30 Je connais sa colère, dit Yahvé, et je sais qu'elle n'est rien; ses fanfaronnades n'ont rien donné.
Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,” asema Bwana, “nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.
31 C'est pourquoi je me lamenterai sur Moab. Oui, je vais crier pour tout Moab. Ils pleureront les hommes de Kir Heres.
Kwa hiyo namlilia Moabu, kwa ajili ya Moabu yote ninalia, ninaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
32 Avec plus que les pleurs de Jazer Je pleurerai pour toi, vigne de Sibma. Vos branches sont passées au-dessus de la mer. Ils ont atteint jusqu'à la mer de Jazer. Le destructeur s'est abattu sur vos fruits d'été. et sur votre millésime.
Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo, enyi mizabibu ya Sibma. Matawi yako yameenea hadi baharini; yamefika hadi bahari ya Yazeri. Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva na mizabibu yako iliyoiva.
33 L'allégresse et la joie sont enlevées du champ fructueux. et du pays de Moab. J'ai fait cesser le vin dans les pressoirs. Personne ne marchera en criant. Les cris ne seront pas des cris.
Shangwe na furaha vimetoweka kutoka bustani na mashamba ya Moabu. Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo; hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe. Ingawa kuna kelele, sio kelele za shangwe.
34 Depuis le cri de Heshbon jusqu'à Elealeh, jusqu'à Jahaz, ils ont fait entendre leur voix, depuis Zoar jusqu'à Horonaïm, jusqu'à Eglath Shelishiyah; car les eaux de Nimrim deviendront aussi désolées.
“Sauti ya kilio chao inapanda kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi, kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya, kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.
35 Je ferai cesser les activités de Moab, dit l'Éternel, « celui qui offre dans le haut lieu, et celui qui brûle de l'encens à ses dieux.
Nitakomesha wale wote katika Moabu watoao sadaka mahali pa juu, na kufukiza uvumba kwa miungu yao,” asema Bwana.
36 C'est pourquoi mon cœur résonne pour Moab comme des flûtes, et mon cœur sonne comme des flûtes pour les hommes de Kir Heres. C'est pourquoi l'abondance qu'il a obtenue a péri.
“Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi; unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi. Utajiri waliojipatia umetoweka.
37 Car toutes les têtes sont chauves, et chaque barbe coupée. Il y a des boutures sur toutes les mains, et le sac sur la taille.
Kila kichwa kimenyolewa na kila mwenye ndevu zimekatwa; kila mkono umekatwa na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.
38 Sur tous les toits de Moab, et dans ses rues, on se lamente partout; car j'ai brisé Moab comme un vase qui ne plaît à personne, dit Yahvé.
Juu ya mapaa yote katika Moabu na katika viwanja hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo, kwa kuwa nimemvunja Moabu kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,” asema Bwana.
39 « Comme elle est brisée! Comme ils gémissent! Comme Moab a tourné le dos avec honte! Ainsi Moab deviendra-t-il une dérision et une terreur pour tous ceux qui l'entourent. »
“Tazama jinsi alivyovunjikavunjika! Jinsi wanavyolia kwa huzuni! Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa, kitu cha kutisha kwa wale wote wanaomzunguka.”
40 Car Yahvé dit: « Voici, il volera comme un aigle, et il déploiera ses ailes contre Moab.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama! Tai anashuka chini, akitanda mabawa yake juu ya Moabu.
41 Kerioth est pris, et les forteresses sont saisies. Le cœur des puissants hommes de Moab en ce jour-là sera comme le cœur d'une femme dans ses douleurs.
Miji itatekwa na ngome zake zitatwaliwa. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
42 Moab sera détruit et ne constituera plus un peuple, parce qu'il s'est élevé contre Yahvé.
Moabu ataangamizwa kama taifa kwa sababu amemdharau Bwana.
43 La terreur, la fosse et le piège sont sur toi, habitant de Moab », dit Yahvé.
Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea, enyi watu wa Moabu,” asema Bwana.
44 « Celui qui fuit la terreur tombera dans la fosse; et celui qui sortira de la fosse sera pris au piège, car je vais faire tomber sur lui, même sur Moab, l'année de leur visite », dit Yahvé.
“Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu ataanguka ndani ya shimo, yeyote atakayepanda kutoka shimoni, atanaswa katika mtego, kwa sababu nitaletea Moabu mwaka wa adhabu yake,” asema Bwana.
45 « Ceux qui ont fui se tiennent sans force sous l'ombre de Heshbon; car un feu est sorti de Heshbon, et une flamme du milieu de Sihon, et a dévoré le coin de Moab, et la couronne de la tête des tumultueux.
“Katika kivuli cha Heshboni, wakimbizi wamesimama pasipo msaada, kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni, mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni; unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu, mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.
46 Malheur à toi, ô Moab! Le peuple de Chemosh est défait; car tes fils sont emmenés en captivité, et tes filles en captivité.
Ole wako, ee Moabu! Watu wa Kemoshi wameangamizwa; wana wako wamepelekwa uhamishoni na binti zako wamechukuliwa mateka.
47 « Mais, dans la suite des temps, je ramènerai les captifs de Moab, » dit Yahvé. Ainsi va le jugement de Moab.
“Lakini nitarudisha mateka wa Moabu, katika siku zijazo,” asema Bwana. Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.