< Jérémie 44 >

1 La parole fut adressée à Jérémie au sujet de tous les Juifs qui habitaient au pays d'Égypte, à Migdol, à Tahpanès, à Memphis et dans le pays de Pathros, en ces termes:
Hili lilikuwa neno ambalo lilikuja kwa Yeremia kuhusu Wayahudi wote walioishi katika nchi ya Misri, wale wanaoishi Migdoli, Tahpanhesi, Memphis, na katika nchi ya Patrosi.
2 « Yahvé des armées, le Dieu d'Israël, dit: Vous avez vu tous les malheurs que j'ai fait venir sur Jérusalem et sur toutes les villes de Juda. Voici, elles sont aujourd'hui une désolation, et personne n'y habite,
“Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi: Wewe mwenyewe umeyaona maafa yote niliyoleta juu ya Yerusalemu na miji yote ya Yuda. Ona, ni ukiwa leo. Hakuna yeyote anaishi mwao.
3 à cause de la méchanceté qu'ils ont commise pour m'irriter, en allant brûler de l'encens, pour servir d'autres dieux qu'ils ne connaissaient pas, ni eux, ni vous, ni vos pères.
Hii ni kwa sababu ya mambo maovu waliyofanya kunikosea mimi kwa kwenda kuchoma ubani na kuabudu miungu mengine. Hawa walikuwa miungu ambao wala wao wenyewe, wala ninyi, wala mababu zenu walijua.
4 Cependant, j'ai envoyé vers vous tous mes serviteurs les prophètes, en me levant de bonne heure et en les envoyant dire: « Oh, ne faites pas cette chose abominable que je déteste. »
Basi nirudie kuwatuma watumwa wangu wote manabii kwao. Niliwatuma wao kusema, 'Acha kufanya vitu hivi machukizo ambayo nachukia.
5 Mais ils n'ont pas écouté et n'ont pas incliné leur oreille. Ils ne se sont pas détournés de leur méchanceté, pour cesser de brûler des parfums à d'autres dieux.
Lakini hawakunisikiliza. Walikataa kuwa makini au kuyaacha maovu kwa kuchoma ubani kwa miungu mingine.
6 C'est pourquoi ma fureur et ma colère se sont répandues, elles se sont enflammées dans les villes de Juda et dans les rues de Jérusalem, et elles sont dévastées et désolées, comme c'est le cas aujourd'hui.''
Basi hasira yangu na gadhabu yangu zilimwanga na kuwasha moto kwenye miji ya Yuda na mitaa ya Yerusalemu. Basi waliharibiwa na kuteketezwa, kama katika siku ya leo.”
7 C'est pourquoi Yahvé, le Dieu des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Pourquoi commettez-vous un grand mal contre vos propres âmes, en retranchant du milieu de Juda l'homme et la femme, l'enfant et le nourrisson, et en ne laissant subsister personne,
Basi sasa Yahwe, Mungu wa majeshi na Mungu wa Israel, asema hivi, “Kwanini unafanya maovu makubwa dhidi yenu? Kwanini mnasababisha ninyi wenyewe kujitenga kutoka miongoni mwa Yuda - wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao? Hakuna mabaki yenu yatabaki.
8 en m'irritant par les œuvres de vos mains, en offrant de l'encens à d'autres dieux dans le pays d'Égypte où vous êtes allés habiter, afin que vous soyez exterminés et que vous soyez une malédiction et un opprobre parmi toutes les nations de la terre?
Kwa maovu yenu mmenikosea pamoja na matendo ya mikono yenu, kwa kuchoma ubani kwa miungu mingine kwenye nchi ya Misri, ambapo mmekwenda kuishi. Mmeenda huko ili kwamba mtaangamizwa, ili kwamba mtalaaniwa na mashutumu miongoni mwa mataifa yote ya duniani.
9 As-tu oublié la méchanceté de tes pères, la méchanceté des rois de Juda, la méchanceté de leurs femmes, ta propre méchanceté et la méchanceté de tes femmes, qu'ils ont commise dans le pays de Juda et dans les rues de Jérusalem?
Mmesahau maovu yaliyofanywa na mababu zenu na maouvu yaliyofanywa na wafalme wa Yuda na wake zao? Mmesahau uovu uliofanywa na ninyi na wake zenu katika nchi ya Yuda na mitaa ya Yerusalemu?
10 Ils ne se sont pas humiliés jusqu'à ce jour, ils n'ont pas craint, ils n'ont pas marché dans ma loi et dans mes statuts, que j'ai mis devant vous et devant vos pères.''
Kwa siku hii, hawajanyenyekea bado. Hawashimu sheria yangu au maagizo niliyoweka mbele yao na mababu zao, wala hawatembei nazo.”
11 C'est pourquoi l'Éternel des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Voici que je tourne ma face contre vous pour faire du mal, et pour exterminer tout Juda.
Kwa hiyo sasa Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi, “Ona, Nimekaribia kuweka uso wangu dhidi yenu kuleta maafa kwenu na kuiharibu Yuda yote.
12 Je prendrai les restes de Juda qui ont pris le parti d'aller habiter au pays d'Égypte, et ils seront tous consumés. Ils tomberont dans le pays d'Égypte. Ils seront consumés par l'épée et par la famine. Ils mourront, du plus petit au plus grand, par l'épée et par la famine. Ils seront un objet d'horreur, d'étonnement, de malédiction et d'opprobre.
Kwa kuwa nitachukua mabaki wa Yuda ambaye ameanza safari kwenda nchi ya Misri kuishi huko. Nitafanya hivi ili kwamba wataangamia wote katika nchi ya Misri. Wataanguka kwa upanga na njaa. Kutoka wadogo kwa wakubwa wataangamia kwa upanga na njaa. Watakufa na watakuwa sababu ya kuaapa, kulaani, mashutumu, na kitu kibaya.
13 Car je punirai les habitants du pays d'Égypte, comme j'ai puni Jérusalem, par l'épée, par la famine et par la peste;
Kwa kuwa nitawaadhibu watu wakazi wa nchi ya Misri kama nilivyoadhibu Yerusalem kwa upanga, njaa, na pigo.
14 de sorte qu'aucun des restes de Juda, qui sont allés vivre au pays d'Égypte, n'échappera ou ne sera laissé pour retourner dans le pays de Juda, où ils ont le désir de retourner pour y habiter; car personne ne retournera, sauf ceux qui échapperont.'"
Hakuna mkimbizi au mwathirika wa mabaki ya Yuda ambaye wataenda kuishi huko kwenye nchi ya Misri watarudi kwenye nchi ya Yuda, hata kama wanataka kurudi na kuishi huko. Hakuna kati yao atarudi, ijapokuwa wachache ambayo watatoroka kutoka huko.”
15 Alors tous les hommes qui savaient que leurs femmes offraient de l'encens à d'autres dieux, et toutes les femmes qui étaient là, une grande assemblée, tout le peuple qui habitait au pays d'Égypte, à Pathros, prirent la parole et dirent à Jérémie:
Kisha watu wote ambao walijua kwamba wake zao walikuwa wakichoma ubani kwa miungu mingine, na wanawake wote waliokuwa katika kusanyiko kuu, na watu wote ambao walikuwa wakiishi kwenye nchi ya Misri katika Pathrosi walimjibu Yeremia.
16 « Nous n'écouterons pas la parole que tu nous as adressée au nom de Yahvé.
Walisema, “Kuhusu neno ambalo mmetuambia sisi kwa jina la Yahwe: Hatutakusikiliza.
17 Mais nous exécuterons toutes les paroles qui sont sorties de notre bouche, pour offrir de l'encens à la reine du ciel et lui verser des libations, comme nous l'avons fait, nous et nos pères, nos rois et nos princes, dans les villes de Juda et dans les rues de Jérusalem; car alors nous avions de la nourriture en abondance, nous étions bien portants et nous ne voyions aucun mal.
Kwa hakika tutafanya mambo yote ambayo tulisema tungefanya: kuchoma ubani kwa malkia wa Mbingu na kumwaga kinywaji cha sadaka kwake kama sisi, mababu zetu, wafalme wetu, na viongozi wetu walivyofanya kwenye miji ya Yuda na mitaa ya Yerusalemu. Kisha tutajazwa pamoja na chakula na tutafanikiwa, pasipo kupata maafa yoyote.
18 Mais depuis que nous avons cessé d'offrir des parfums à la reine du ciel et de lui verser des libations, nous avons manqué de tout, et nous avons été consumés par l'épée et par la famine. »
Wakati tunajiepusha kutofanya mambo haya, si kutoa sadaka ya ubani kwa Malkia wa Mbinguni na si kumwanga kinywaji cha sadaka kwake, tulikuwa wote tunaumwa umaskini na tulikuwa tunakufa kwa upanga na njaa.”
19 Les femmes dirent: « Lorsque nous avons offert de l'encens à la reine du ciel et que nous lui avons versé des libations, avons-nous préparé des gâteaux pour l'adorer et versé des libations pour elle, sans nos maris? ».
Wanawake walisema, “Wakati tulipokuwa tunatengeneza ubani wa sadaka mbele ya Malkia wa Mbinguni na kumwaga kinywaji cha sadaka kwake, tulifanya hivi vitu pasipo waume wetu kujua.”
20 Jérémie dit alors à tout le peuple, aux hommes et aux femmes, à tous ceux qui lui avaient répondu:
Kisha Yeremia alisema kwa watu wote - kwa wanaume na wanawake, na watu wote waliomjibu yeye - alihubiri na kusema,
21 « L'encens que vous avez brûlé dans les villes de Juda et dans les rues de Jérusalem, vous et vos pères, vos rois et vos chefs, et le peuple du pays, Yahvé ne s'en est-il pas souvenu et n'y a-t-il pas pensé?
“Je Yahwe hakukumbuka ubani ambao mliuchoma kwenye miji ya Yuda na mitaa ya Yerusalem - wewe na mababu zenu, wafalme wenu na viongozi, na watu wa nchi? Kwa kuwa Yahwe anakumbuka hili kwenye akili; inakuja kwenye mawazo yake.
22 Ainsi Yahvé n'a pu le supporter plus longtemps, à cause de la méchanceté de vos actions et à cause des abominations que vous avez commises. C'est pourquoi votre pays est devenu une désolation, un objet d'étonnement et de malédiction, sans habitant, comme il l'est aujourd'hui.
Basi hawakuweza tena kuvumilia kwa sababu ya matendo yenu maovu, kwa sababu machukizo ambayo mlifanya. Basi nchi yenu imekuwa ukiwa, kutisha, na laana basi hapakuwa na mkazi tena kwa siku hii.
23 Parce que vous avez brûlé de l'encens et que vous avez péché contre l'Éternel, parce que vous n'avez pas écouté la voix de l'Éternel, parce que vous n'avez pas suivi sa loi, ses statuts et ses témoignages, ce malheur vous est arrivé, comme il arrive aujourd'hui. »
Kwa sababu mlichoma ubani na kufanya dhambi dhidi ya Yahwe, na kwa sababu msingesikiliza sauti yake, sheria yake, amri zake, au maagizo ya agano lake, maafa haya dhidi yenu yemetokea kama kwa siku hii. “
24 Jérémie dit à tout le peuple, y compris à toutes les femmes: « Écoutez la parole de l'Éternel, vous tous, Judéens, qui êtes au pays d'Égypte!
Kisha Yeremia alisema kwa watu wote na wanawake wote, “Sikia neno la Yahwe, Yuda yote ambao wamo katika nchi ya Misri.
25 Yahvé des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Vous et vos femmes, vous avez parlé de vos bouches, et de vos mains vous l'avez accompli, en disant: « Nous accomplirons les vœux que nous avons faits, pour offrir de l'encens à la reine du ciel et pour lui verser des libations. » "'Établissez donc vos vœux, et accomplissez vos vœux'.
Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi, Wewe na wake zako wote mmesema kwa vinywa vyenu na kubeba kwa mikono yenu kile mlichosema, “Hakika tutabeba viapo ambavyo tulifanya kumwabudu Malkia wa Mbinguni, kwanga kinywaji cha sadaka kwake.” Sasa timiza viapo vyenu, vibebe.”
26 C'est pourquoi, écoutez la parole de l'Éternel, vous tous, Judéens, qui habitez le pays d'Égypte: Voici, je le jure par mon grand nom, dit l'Éternel, on ne citera plus mon nom dans la bouche d'aucun homme de Juda, dans tout le pays d'Égypte, en disant: « Le Seigneur Yahvé est vivant. »
Basi, sikiliza neno la Yahwe, Yuda yote ambao mnaishi katika nchi ya Misri, 'Ona, Nimeapa kwa jina langu kuu-asema Yahwe. Jina langu halitaitwa kwa vinywa vya wanaume wowote wa Yuda kwenye nchi ya Misri, wewe ambaye sasa unasema, “Kama Bwana Yahwe aishivyo.”
27 Voici, je veille sur eux en mal et non en bien, et tous les hommes de Juda qui sont au pays d'Égypte seront consumés par l'épée et par la famine, jusqu'à ce qu'ils aient tous disparu.
Ona, Ninakutazama juu yako kwa ajili ya maafa na si kwa uzuri. Kila mtu wa Yuda katika nchi ya Misri ataangamia kwa upanga na njaa mpaka wote wameishia.
28 Ceux qui échapperont à l'épée reviendront du pays d'Égypte dans le pays de Juda, peu nombreux. Tous les restes de Juda, qui sont allés vivre au pays d'Égypte, sauront quelle parole tiendra, la mienne ou la leur.
Kisha waathirika wa upanga watarudi kutoka nchi ya Misri kwa nchi ya Yuda, peke idadi ndogo yao. Basi mabaki yote ya Yuda walioenda kwenye nchi ya Misri kuishi huko watajua ambao neno litakuwa kweli: yangu au yao.
29 "'Ce sera pour vous le signe, dit Yahvé, que je vous punirai en ce lieu, afin que vous sachiez que mes paroles vous seront opposées pour le mal.''
Hii itakuwa ishara kwa ajili yako - hili ni tamko la Yahwe - kwamba ninaweka dhidi yenu katika eneo hili, ili kwamba mtajua kwamba maneno yangu hakika yatawavamia pamoja na maafa.
30 Yahvé dit: « Voici que je livre Pharaon Hophra, roi d'Égypte, entre les mains de ses ennemis et de ceux qui en veulent à sa vie, comme j'ai livré Sédécias, roi de Juda, entre les mains de Nabuchodonosor, roi de Babylone, qui était son ennemi et qui en voulait à sa vie. »"
Yahwe asema hivi, 'Tazama, ninakaribia kumtoa Farao Hofra mfalme wa Misri kwenye mkono wa adui zake na kwenye mkono wa wale wanaotafuta kumuua. Itakuwa sawa kama wakati nilimpa Sedekia mfalme wa Yuda kwenye mkono wa Nebukadreza mfalme wa Babeli, adui wake aliyetafuta maisha yake.

< Jérémie 44 >