< Jérémie 4 >

1 « Si tu reviens, Israël, dit Yahvé, si tu reviens à moi, et si tu éloignes de moi tes abominations, alors tu ne seras pas déplacé,
“Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli, nirudie mimi,” asema Bwana. “Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu na usiendelee kutangatanga,
2 et tu jureras: « Yahvé est vivant », dans la vérité, la justice et l'équité. Les nations se béniront en lui, et elles se glorifieront en lui. »
ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa, ‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’ ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye na katika yeye watajitukuza.”
3 Car Yahvé dit aux hommes de Juda et à Jérusalem: « Brisez votre jachère, et ne semez pas parmi les épines.
Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu, wala msipande katikati ya miiba.
4 Circoncisez-vous à Yahvé, et ôtez les prépuces de votre cœur, hommes de Juda et habitants de Jérusalem, de peur que ma colère ne sorte comme un feu, et ne brûle sans que personne ne puisse l'éteindre, à cause de la méchanceté de vos actions.
Jitahirini katika Bwana, tahirini mioyo yenu, enyi wanaume wa Yuda na watu wa Yerusalemu, la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mliotenda, ikiwaka pasipo wa kuizima.
5 Annoncez en Juda, publiez à Jérusalem, et dites: « Sonnez de la trompette dans le pays ». Criez à haute voix et dites: « Assemblez-vous! Criez à haute voix et dites: Rassemblez-vous, entrons dans les villes fortes!
“Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema: ‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’ Piga kelele na kusema: ‘Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie katika miji yenye maboma!’
6 Dressez une bannière vers Sion. Fuyez en toute sécurité! N'attendez pas, car je vais faire venir du nord le malheur et une grande destruction. »
Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni! Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa! Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini, maangamizi ya kutisha.”
7 Un lion est sorti de son fourré, un destructeur de nations. Il est en marche. Il est sorti de son lieu, pour faire de votre pays un désert, pour que vos villes soient dévastées, sans habitants.
Simba ametoka nje ya pango lake, mharabu wa mataifa amejipanga. Ametoka mahali pake ili aangamize nchi yenu. Miji yenu itakuwa magofu pasipo mtu wa kuishi humo.
8 A cause de cela, revêtez-vous d'un sac, lamentez-vous et gémissez; car l'ardente colère de Yahvé ne s'est pas détournée de nous.
Hivyo vaeni nguo za magunia, ombolezeni na kulia kwa huzuni, kwa kuwa hasira kali ya Bwana haijaondolewa kwetu.
9 « En ce jour-là, dit l'Éternel, le cœur du roi périra, ainsi que le cœur des princes. Les prêtres seront stupéfaits, et les prophètes s'étonneront. »
“Katika siku ile,” asema Bwana “mfalme na maafisa watakata tamaa, makuhani watafadhaika, na manabii watashangazwa mno.”
10 Alors je dis: « Ah, Seigneur Yahvé! Tu as beaucoup trompé ce peuple et Jérusalem, en disant: 'Vous aurez la paix', mais l'épée atteint le cœur. »
Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”
11 En ce temps-là, il sera dit à ce peuple et à Jérusalem: « Un vent chaud souffle des hauteurs dénudées du désert vers la fille de mon peuple, non pour vanner, ni pour purifier.
Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa,
12 Un vent plein vient de ceux-ci vers moi. Maintenant, je prononcerai aussi des jugements contre eux. »
upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”
13 Voici, il monte comme les nuages, et ses chars sont comme le tourbillon. Ses chevaux sont plus rapides que les aigles. Malheur à nous! Car nous sommes ruinés.
Tazama! Anakuja kama mawingu, magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli, farasi wake wana mbio kuliko tai. Ole wetu! Tunaangamia!
14 Jérusalem, lave ton cœur de la méchanceté, afin que tu sois sauvée. Jusqu'à quand tes mauvaises pensées resteront-elles en toi?
Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe. Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?
15 Car, de Dan, une voix annonce le mal, Et des collines d'Éphraïm, elle publie le mal:
Sauti inatangaza kutoka Dani, ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.
16 Dites aux nations: Voici, publiez contre Jérusalem: Des veilleurs viennent d'un pays lointain, Et ils élèvent la voix contre les villes de Juda.
“Waambie mataifa jambo hili, piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu: ‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali, likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.
17 Comme les gardiens d'un champ, ils sont contre elle tout autour, parce qu'elle s'est rebellée contre moi », dit Yahvé.
Wamemzunguka kama watu walindao shamba, kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’” asema Bwana.
18 « Ta voie et tes actions t'ont amené ces choses. C'est ta méchanceté, car elle est amère, car elle atteint ton cœur. »
“Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe yameleta haya juu yako. Hii ndiyo adhabu yako. Tazama jinsi ilivyo chungu! Tazama jinsi inavyochoma moyo!”
19 Mon angoisse, mon angoisse! Je souffre au plus profond de mon cœur! Mon cœur tremble au-dedans de moi. Je ne puis me taire, car tu as entendu, ô mon âme, le son de la trompette, l'alarme de la guerre.
Ee mtima wangu, mtima wangu! Ninagaagaa kwa maumivu. Ee maumivu makuu ya moyo wangu! Moyo wangu umefadhaika ndani yangu, siwezi kunyamaza. Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta, nimesikia kelele ya vita.
20 Destruction sur destruction est décrétée, car tout le pays est dévasté. Soudain, mes tentes sont détruites, et mes rideaux disparaissent en un instant.
Maafa baada ya maafa, nchi yote imekuwa magofu. Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa, makazi yangu kwa muda mfupi.
21 Jusqu'à quand verrai-je l'étendard et entendrai-je le son de la trompette?
Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita na kusikia sauti za tarumbeta?
22 « Car mon peuple est insensé. Ils ne me connaissent pas. Ce sont des enfants insensés, et ils n'ont pas d'intelligence. Ils sont habiles à faire le mal, mais ils ne savent pas faire le bien. »
“Watu wangu ni wapumbavu, hawanijui mimi. Ni watoto wasio na akili, hawana ufahamu. Ni hodari kutenda mabaya, hawajui kutenda yaliyo mema.”
23 Je regardai la terre, et voici qu'elle était vide et déserte, et les cieux, et ils n'avaient pas de lumière.
Niliitazama dunia, nayo haikuwa na umbo tena ni tupu; niliziangalia mbingu, mianga ilikuwa imetoweka.
24 J'ai vu les montagnes, et voici qu'elles tremblaient, et toutes les collines bougeaient d'avant en arrière.
Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka, vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.
25 Je regardai, et voici, il n'y avait pas d'homme, et tous les oiseaux du ciel avaient pris la fuite.
Nilitazama, wala watu hawakuwepo; kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.
26 Je regardai, et voici, le champ fertile était un désert, et toutes ses villes étaient détruites devant l'Éternel, devant son ardente colère.
Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa, miji yake yote ilikuwa magofu mbele za Bwana, mbele ya hasira yake kali.
27 Car Yahvé dit: « Tout le pays sera dévasté, mais je ne le détruirai pas complètement.
Hivi ndivyo Bwana asemavyo: “Nchi yote itaharibiwa, ingawa sitaiangamiza kabisa.
28 A cause de cela, la terre sera dans le deuil, et les cieux en haut seront noirs, parce que je l'ai annoncé. Je l'ai projeté, je ne me suis pas repenti, et je ne reviendrai pas sur ma décision. »
Kwa hiyo dunia itaomboleza na mbingu zilizo juu zitakuwa giza, kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma, nimeamua na wala sitageuka.”
29 Chaque ville fuit au bruit des cavaliers et des archers. Ils s'enfoncent dans les fourrés et grimpent sur les rochers. Toute ville est abandonnée, et pas un homme n'y habite.
Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde kila mji unakimbia. Baadhi wanakimbilia vichakani, baadhi wanapanda juu ya miamba. Miji yote imeachwa, hakuna aishiye ndani yake.
30 Et toi, quand tu seras dévastée, que feras-tu? Tu as beau te vêtir d'écarlate, te parer d'ornements d'or, agrandir tes yeux avec du fard, c'est en vain que tu te fais belle. Tes amants te méprisent. Ils en veulent à ta vie.
Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa? Kwa nini unajivika vazi jekundu na kuvaa vito vya dhahabu? Kwa nini unapaka macho yako rangi? Unajipamba bure. Wapenzi wako wanakudharau, wanautafuta uhai wako.
31 Car j'ai entendu une voix comme celle d'une femme en travail, une angoisse comme celle qui accouche de son premier enfant, la voix de la fille de Sion, qui a le souffle coupé, qui étend ses mains en disant: « Malheur à moi! Car mon âme s'évanouit devant les meurtriers. »
Nasikia kilio kama cha mwanamke katika utungu wa kuzaa, kilio cha uchungu kama cha anayemzaa mtoto wake wa kwanza: kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua, akiinua mikono yake, akisema, “Ole wangu! Ninazimia; maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”

< Jérémie 4 >