< Jérémie 38 >

1 Shephatia, fils de Mattan, Guedalia, fils de Pashhur, Jucal, fils de Shelemia, et Pashhur, fils de Malkija, entendirent les paroles que Jérémie adressa à tout le peuple, en disant:
Shefatia mwana wa Matani, na Gedalia mwana wa Pashuri, na Yehukali mwana wa Shelemia, na Pashuri mwana wa Malkiya wakasikia kile Yeremia alichokuwa akiwaambia watu wote wakati aliposema,
2 « Yahvé dit: Celui qui restera dans cette ville mourra par l'épée, par la famine et par la peste, mais celui qui partira pour les Chaldéens vivra. Il échappera à la mort et il vivra.
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Yeyote akaaye ndani ya mji huu atakufa kwa upanga, njaa au tauni, lakini yeyote atakayejisalimisha kwa Wakaldayo ataishi. Atakayeyatoa maisha yake kama nyara, ataishi.’
3 Yahvé dit: « Cette ville sera livrée entre les mains de l'armée du roi de Babylone, qui s'en emparera ».
Tena hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mji huu kwa hakika utatiwa mikononi mwa jeshi la mfalme wa Babeli, ambaye atauteka.’”
4 Et les princes dirent au roi: « Je t'en prie, que cet homme soit mis à mort, car il affaiblit les mains des hommes de guerre qui restent dans cette ville, et les mains de tout le peuple, en leur tenant de tels propos; car cet homme ne cherche pas le bien-être de ce peuple, mais le mal. »
Ndipo maafisa wakamwambia mfalme, “Mtu huyu imempasa kuuawa. Anawakatisha tamaa askari waliobaki katika mji huu, vivyo hivyo na watu wote pia, kwa ajili ya mambo anayowaambia. Mtu huyu hawatakii mema watu hawa, bali maangamizi yao.”
5 Le roi Sédécias dit: « Voici qu'il est entre tes mains, car le roi ne peut rien faire pour s'opposer à toi. »
Mfalme Sedekia akajibu, “Yeye yuko mikononi mwenu! Mfalme hawezi kufanya lolote kuwapinga ninyi.”
6 Ils prirent Jérémie et le jetèrent dans le cachot de Malkija, fils du roi, qui se trouvait dans la cour des gardes. Ils firent descendre Jérémie avec des cordes. Dans le cachot, il n'y avait pas d'eau, mais de la boue, et Jérémie s'enfonça dans la boue.
Basi wakamchukua Yeremia na kumtia kwenye kisima cha Malkiya, mwana wa mfalme, kilichokuwa katika ua wa walinzi. Wakamteremsha Yeremia kwa kamba ndani ya kisima. Hakikuwa na maji ndani yake, ila tope tu, naye Yeremia akazama ndani ya matope.
7 Lorsque Ebedmélec, l'Éthiopien, un eunuque, qui se trouvait dans la maison du roi, apprit qu'on avait mis Jérémie dans le cachot (le roi était alors assis à la porte de Benjamin),
Lakini Ebed-Meleki Mkushi, aliyekuwa afisa katika jumba la kifalme, akasikia kuwa walikuwa wamemtia Yeremia ndani ya kisima. Wakati mfalme alipokuwa ameketi katika Lango la Benyamini,
8 Ebedmélec sortit de la maison du roi et parla au roi, en disant:
Ebed-Meleki akatoka nje ya jumba la kifalme na kumwambia,
9 « Mon seigneur le roi, ces hommes ont mal agi dans tout ce qu'ils ont fait au prophète Jérémie, qu'ils ont jeté dans le cachot. Il risque de mourir dans le lieu où il se trouve, à cause de la famine, car il n'y a plus de pain dans la ville. »
“Mfalme bwana wangu, watu hawa wamefanya uovu kwa yote waliomtendea nabii Yeremia. Wamemtupa ndani ya kisima, mahali ambapo atakufa kwa njaa wakati ambapo hakuna chakula popote katika mji.”
10 Alors le roi donna cet ordre à Ebedmelech, l'Éthiopien: « Prends avec toi trente hommes d'ici, et fais sortir Jérémie le prophète du cachot, avant qu'il ne meure. »
Basi mfalme akamwamuru Ebed-Meleki Mkushi, akisema, “Chukua watu thelathini kutoka hapa pamoja nawe, mkamtoe nabii Yeremia huko kwenye kisima kabla hajafa.”
11 Ebedmélec prit donc les hommes avec lui, et entra dans la maison du roi, sous le trésor; il prit là des chiffons et des vêtements usés, et les fit descendre par des cordes dans le cachot de Jérémie.
Basi Ebed-Meleki akawachukua watu pamoja naye, wakaenda mpaka kwenye chumba kilichoko chini ya hazina ndani ya jumba la kifalme. Akachukua matambaa makuukuu pamoja na nguo zilizochakaa kutoka huko, na kumshushia Yeremia kwa kamba ndani ya kisima.
12 Ebedmelech, l'Éthiopien, dit à Jérémie: « Mets maintenant ces chiffons et ces vêtements usés sous tes aisselles, sous les cordes. » Jérémie fit ainsi.
Ebed-Meleki Mkushi akamwambia Yeremia, “Weka haya matambaa makuukuu na hizo nguo zilizochakaa makwapani ili kuzuia kamba.” Yeremia akafanya hivyo,
13 Et ils soulevèrent Jérémie avec les cordes, et le firent monter hors du cachot; et Jérémie resta dans la cour des gardes.
nao wakamvuta juu kwa kamba na kumtoa katika kisima. Yeremia akakaa katika ua wa walinzi.
14 Alors le roi Sédécias envoya chercher Jérémie, le prophète, et le fit entrer dans la troisième entrée, celle de la maison de l'Éternel. Le roi dit alors à Jérémie: « Je vais te demander quelque chose. Ne me cache rien. »
Ndipo Mfalme Sedekia akatuma watu wamwitie nabii Yeremia wamlete kwake kwenye ingilio la tatu la Hekalu la Bwana. Mfalme akamwambia Yeremia, “Ninataka kukuuliza jambo fulani, usinifiche kitu chochote.”
15 Jérémie dit alors à Sédécias: « Si je te le déclare, ne me feras-tu pas mourir? Si je te donne un conseil, tu ne m'écouteras pas. »
Yeremia akamwambia Sedekia, “Nikikupa jibu, je, hutaniua? Hata kama nikikupa shauri, wewe hutanisikiliza.”
16 Et le roi Sédécias jura secrètement à Jérémie, en disant: « L'Éternel est vivant, lui qui a fait nos âmes, je ne te ferai pas mourir, et je ne te livrerai pas entre les mains de ces hommes qui en veulent à ta vie. »
Lakini Mfalme Sedekia akamwapia Yeremia kiapo hiki kwa siri, akisema, “Hakika kama aishivyo Bwana, ambaye ametupa pumzi, sitakuua wala sitakutia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wako.”
17 Jérémie dit alors à Sédécias: « Yahvé, le Dieu des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Si tu vas vers les princes du roi de Babylone, ton âme vivra, et cette ville ne sera pas brûlée par le feu. Tu vivras, ainsi que ta maison.
Kisha Yeremia akamwambia Sedekia, “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Ikiwa utajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, maisha yako yatasalimika, na mji huu hautateketezwa kwa moto. Pia wewe na jamaa yako mtaishi.
18 Mais si tu ne sors pas vers les chefs du roi de Babylone, cette ville sera livrée entre les mains des Chaldéens, qui la brûleront par le feu, et tu n'échapperas pas à leurs mains.'"
Lakini ikiwa hutajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, mji huu utatiwa mikononi mwa Wakaldayo na watauteketeza kwa moto, nawe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao.’”
19 Le roi Sédécias dit à Jérémie: « J'ai peur des Juifs qui sont passés aux Chaldéens, de peur qu'ils ne me livrent entre leurs mains et qu'ils ne se moquent de moi. »
Mfalme Sedekia akamwambia Yeremia, “Ninawaogopa Wayahudi ambao wamekimbilia kwa Wakaldayo, kwa kuwa Wakaldayo wanaweza kunitia mikononi mwao, nao wakanitenda vibaya.”
20 Mais Jérémie dit: « Ils ne te délivreront pas. Obéis, je t'en prie, à la voix de Yahvé, dans ce que je te dis; ainsi tu seras heureux, et ton âme vivra.
Yeremia akajibu, “Hawatakutia mikononi mwao. Mtii Bwana kwa kufanya kile ninachokuambia. Kisha utafanikiwa na maisha yako yatakuwa salama.
21 Mais si tu refuses de sortir, voici la parole que Yahvé m'a montrée:
Lakini ukikataa kujisalimisha, hili ndilo Bwana alilonifunulia:
22 Voici que toutes les femmes qui resteront dans la maison du roi de Juda seront amenées devant les princes du roi de Babylone, et ces femmes diront, « Vos amis familiers se sont retournés contre vous, et l'ont emporté sur vous. Vos pieds sont enfoncés dans la boue, ils se sont détournés de toi. »
Wanawake wote walioachwa katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda wataletwa mbele ya maafisa wa mfalme wa Babeli. Wanawake hao watakuambia: “‘Walikupotosha na kukushinda, wale rafiki zako uliowaamini. Miguu yako imezama matopeni; rafiki zako wamekuacha.’
23 Ils emmèneront toutes vos femmes et vos enfants chez les Chaldéens. Tu n'échapperas pas à leur main, mais tu seras pris par la main du roi de Babylone. Tu feras en sorte que cette ville soit brûlée par le feu.'"
“Wake zako wote na watoto wataletwa na kutiwa mikononi mwa Wakaldayo. Wewe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao. Lakini utatekwa na mfalme wa Babeli, na mji huu utateketezwa kwa moto.”
24 Sédécias dit alors à Jérémie: « Que personne ne sache rien de ces paroles, et tu ne mourras pas.
Kisha Sedekia akamwambia Yeremia, “Usiruhusu mtu yeyote ajue kuhusu haya mazungumzo, la sivyo utakufa.
25 Mais si les chefs apprennent que je t'ai parlé, qu'ils viennent te voir et te disent: « Déclare-nous maintenant ce que tu as dit au roi; ne nous le cache pas, et nous ne te ferons pas mourir; dis-nous aussi ce que le roi t'a dit »,
Maafisa wakisikia kwamba nimezungumza nawe, nao wakakujia na kusema, ‘Tuambie kile ulichozungumza na mfalme na kile mfalme alichokuambia, usitufiche au sivyo tutakuua,’
26 tu leur diras: « J'ai présenté ma supplique au roi, pour qu'il ne me fasse pas retourner dans la maison de Jonathan, afin d'y mourir ».
basi waambie, ‘Nilikuwa ninamsihi mfalme asinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani nisije nikafia humo.’”
27 Alors tous les princes vinrent auprès de Jérémie et l'interrogèrent; et il leur répondit selon toutes ces paroles que le roi avait ordonnées. Ils cessèrent donc de parler avec lui, car l'affaire n'était pas perçue.
Maafisa wote wakamjia Yeremia na kumuuliza, naye Yeremia akawaambia kila kitu mfalme alichomwagiza kusema. Kisha hawakusema lolote zaidi na Yeremia kwa sababu hakuna yeyote aliyesikia mazungumzo yake na mfalme.
28 Jérémie resta donc dans la cour des gardes jusqu'au jour de la prise de Jérusalem.
Naye Yeremia akabaki katika ua wa walinzi hadi siku Yerusalemu ilipotekwa.

< Jérémie 38 >