< Jérémie 24 >
1 L'Éternel me fit voir que deux corbeilles de figues étaient placées devant le temple de l'Éternel, après que Nebucadnetsar, roi de Babylone, eut emmené captifs de Jérusalem Jeconia, fils de Jojakim, roi de Juda, et les princes de Juda, avec les artisans et les forgerons, et les eut emmenés à Babylone.
Bwana alinionyeshea kitu. Tazama, vikapu viwili vya tini viliwekwa mbele ya hekalu la Bwana. (Maono haya yalitokea baada ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, kumchukua mateka Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, maofisa wa Yuda, mafundi na wafua vyuma kutoka Yerusalemu na kuwapeleka Babeli.)
2 L'un des paniers contenait de très bonnes figues, comme les figues de première maturité, et l'autre panier contenait de très mauvaises figues, qui ne pouvaient pas être mangées tant elles étaient mauvaises.
Kikapu kimoja cha tini kilikuwa nzuri sana, kama tini za kwanza zilizoiva, lakini kikapu kingine cha tini zilizokuwa mbaya sana zisizoweza kuliwa.
3 Alors Yahvé me demanda: « Que vois-tu, Jérémie? » J'ai dit: « Des figues. Les bonnes figues sont très bonnes, et les mauvaises sont très mauvaises, si mauvaises qu'on ne peut pas les manger. »
Bwana akaniambia, “Unaona nini Yeremia?” Nikasema, “Tini. Tini ambazo ni nzuri sana na tini ambazo ni mbaya sana haziwezi kuliwa.”
4 La parole de l'Éternel me fut adressée, en ces termes:
Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
5 L'Éternel, le Dieu d'Israël, dit: « Comme ces bonnes figues, je considère comme bons les captifs de Juda que j'ai envoyés de ce lieu au pays des Chaldéens.
“Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: nitawaangalia mateka wa Yuda kwa manufaa yao, kama vile tini hizi nzuri, nilipowatoa mateka kutoka hapa mpaka nchi ya Wakaldayo.
6 Car je les regarderai comme un bien, et je les ramènerai dans ce pays. Je les bâtirai, et je ne les abattrai pas. Je les planterai, et je ne les arracherai pas.
Nitaweka macho yangu kwao wapate mema na kuwarejeshea nchi hii. Nitawajenga, wala sitawaangamiza.
7 Je leur donnerai le cœur de me connaître, de savoir que je suis Yahvé. Ils seront mon peuple, et je serai leur Dieu, car ils reviendront à moi de tout leur cœur.
Nitawapanda, wala sitawang'oa. Ndipo nitawapa moyo wa kunijua; kwa kuwa mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu na mimi nitakuwa Mungu wao, hivyo watanirudia kwa moyo wao yote.
8 "'Comme les figues mauvaises qui ne se mangent pas, tant elles sont mauvaises, dit Yahvé, je livrerai Sédécias, roi de Juda, et ses princes, et le reste de Jérusalem qui demeure dans ce pays, et ceux qui habitent au pays d'Égypte.
Lakini kama vile tini mbaya ambazo ni hazifai kuliwa - asema Bwana - nitatenda hivi kwa Sedekia, mfalme wa Yuda, pamoja na viongozi wake, na pamoja na wengine wa Yerusalemu ambao wanabaki katika nchi hii au kwenda kukaa katika nchi ya Misri.
9 Je les livrerai même pour qu'ils soient ballottés parmi tous les royaumes de la terre, pour qu'ils soient un opprobre et un proverbe, une raillerie et une malédiction, dans tous les lieux où je les chasserai.
Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha, wapate maafa, mbele ya falme zote duniani, aibu na somo kwa mithali, matusi, na laana mahali pote nitakapowafukuza.
10 J'enverrai parmi eux l'épée, la famine et la peste, jusqu'à ce qu'ils soient exterminés du pays que j'ai donné à eux et à leurs pères.'"
Nitatuma upanga, njaa, na tauni dhidi yao watapotelea mbali kutoka kwenye nchi niliyowapa wao na baba zao.”