< Jérémie 22 >

1 Yahvé dit: « Descends à la maison du roi de Juda, et là, tu diras cette parole:
Bwana asema hivi, “Nenda kwenye nyumba ya mfalme wa Yuda, utangaze neno hili huko.
2 Écoute la parole de Yahvé, roi de Juda, qui es assis sur le trône de David, toi, tes serviteurs, et ton peuple qui entre par ces portes.
Ukaseme, 'Ewe Mfalme wa Yuda, wewe aliyeketi kiti cha Daudi, usikilize neno la Bwana. Nisikilizeni, enyi watumishi wake, na ninyi, watu wake mnaokuja kwa malango haya.
3 Yahvé dit: « Fais régner la justice et l'équité, et délivre de la main de l'oppresseur celui qui est dépouillé. Ne faites pas de mal. Ne faites pas violence à l'étranger, à l'orphelin et à la veuve. Ne répandez pas de sang innocent dans ce lieu.
Bwana asema hivi, “Fanya haki na uadilifu, na mtu yeyote ambaye ameibiwa-muokoeni kutoka mkononi mwa mshindani. Usimtendee mabaya mgeni yeyote katika nchi yako, au yatima au mjane. Usifanye vurugu au kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa.
4 Car si vous faites cela, des rois assis sur le trône de David entreront par les portes de cette maison, montés sur des chars et sur des chevaux, eux, leurs serviteurs et leur peuple.
Kwa kuwa mkifanya mambo hayo, basi wafalme wanaoketi kiti cha Daudi wataingia milango ya nyumba hii wakiendesha gari na farasi, yeye, watumishi wake, na watu wake!
5 Mais si vous n'écoutez pas ces paroles, je jure par moi-même, dit Yahvé, que cette maison deviendra une désolation. »'"
Lakini ikiwa hamsikilizi maneno haya kutoka kwangu ambayo nimeyasema-hili ndilo tamko la Bwana-basi nyumba hii ya kifalme itaharibiwa.'”
6 Car Yahvé dit à propos de la maison du roi de Juda: « Tu es Gilead pour moi, le chef du Liban. Mais je ferai de toi un désert, des villes qui ne sont pas habitées.
Kwa maana Bwana asema hivi juu ya nyumba ya mfalme wa Yuda, “Wewe uko kama Gileadi, au kama kilele cha Lebanoni kwangu. Hata hivyo nitakugeuza kuwa jangwa, katika miji isiyo na wenyeji.
7 Je préparerai des destructeurs contre toi, tout le monde avec ses armes, et ils couperont vos cèdres de choix, et les jeter dans le feu.
Kwa kuwa nimewaagiza waharibifu kuja juu yenu! Watu wenye silaha zao watakata mierezi yako iliyo bora na kuiacha kuanguka kwenye moto.
8 « Des nations nombreuses passeront près de cette ville, et chacune demandera à son voisin: « Pourquoi Yahvé a-t-il fait cela à cette grande ville? »
Kisha mataifa mengi yatapita kwenye mji huu. Kila mtu atamwambia yule anayefuata, “Mbona Bwana amefanya hivi kwa jiji hili kuu?”
9 Et l'on répondra: « Parce qu'ils ont abandonné l'alliance de Yahvé leur Dieu, qu'ils ont adoré d'autres dieux et qu'ils les ont servis. »"
Na mwingine atajibu, “Kwa sababu waliiacha agano la Bwana, Mungu wao, wakainama kwa miungu mingine, wakaiabudu.”
10 Ne pleurez pas les morts. Ne le déplore pas; mais pleure amèrement sur celui qui s'en va, car il ne reviendra plus, et ne pas voir son pays natal.
Usilie kwa ajili ya aliyekufa. Usiomboleze kwa ajili yake. Lakini mlilie mtu yeyote anayeingia kifungoni, kwa maana hatarudi tena kuiona nchi aliyozaliwa.'
11 Car Yahvé dit à propos de Shallum, fils de Josias, roi de Juda, qui a régné à la place de Josias, son père, et qui est sorti de ce lieu: « Il n'y retournera plus.
Maana Bwana asema hivi juu ya Yehoahazi, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyekuwa mfalme badala ya Yosia babaye, 'ametoka mahali hapa, wala hatarudi.
12 Mais il mourra dans le lieu où on l'a conduit en captivité. Il ne verra plus ce pays. »
Atakufa huko mahali ambapo walimchukua mateka, na hataiona tena nchi hii.'
13 « Malheur à celui qui bâtit sa maison par l'injustice, et ses chambres par l'injustice; qui utilise le service de son voisin sans rémunération, et ne lui donne pas son embauche;
Ole mtu yeyote anayejenga nyumba yake kwa uovu na vyumba vyake vya juu katika udhalimu; ambao wengine hufanya kazi, lakini hawalipwi.
14 qui dit: « Je me construirai une grande maison et des chambres spacieuses ». et découpe des fenêtres pour lui-même, avec un plafond en cèdre, et peint en rouge.
Ole mtu yeyote atakayesema, 'Nitajenga nyumba ndefu na vyumba vya juu vipana, na hujenga madirisha mapana, na kuta zenye mwerezi, na huipaka rangi nyekundu.'
15 « Devrais-tu régner parce que tu t'efforces d'exceller dans le cèdre? Ton père n'a pas mangé et bu, et faire la justice et la droiture? Alors tout allait bien pour lui.
Je, hii ndiyo inakufanya uwe mfalme mzuri, kwamba unataka kuwa na mbao za mwerezi? Je baba yako hakula na kunywa, lakini lakini alifanya hukumu na haki? Kisha mambo yakawa mazuri kwa ajili yake.
16 Il a jugé la cause des pauvres et des nécessiteux; alors c'était bien. Ce n'était pas pour me connaître? » dit Yahvé.
Alihukumu maneno ya masikini na mhitaji. Ilikuwa vizuri. Je, huku siko kunijua mimi? - hili ni tamko la Bwana.
17 Mais tes yeux et ton cœur ne sont que pour ta convoitise, pour avoir versé du sang innocent, pour l'oppression, et pour faire de la violence ».
Lakini hakuna kitu machoni na moyoni mwako isipokuwa wasiwasi kwa faida yako isiyo ya haki na kwa kumwaga damu isiyo na hatia, kwa ukandamizaji kuwatendea jeuri wengine.
18 C'est pourquoi Yahvé dit au sujet de Jehoïakim, fils de Josias, roi de Juda: « Ils ne se lamenteront pas pour lui, en disant: « Ah mon frère! » ou « Ah ma sœur! ». Ils ne se lamenteront pas pour lui, en disant « Ah le seigneur » ou « Ah sa gloire ».
Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda. Hawatamwomboleza wakisema 'ole, ndugu yangu! au 'Ole, dada yangu!' Hawataomboleza kwa kusema 'Ole, bwana! ' au 'ole, utukufu!'
19 Il sera enterré avec la sépulture d'un âne, tirés et chassés au-delà des portes de Jérusalem. »
Atazikwa maziko ya punda, ataburuzwa mbali na kutupwa nje ya milango ya Yerusalemu.
20 « Monte au Liban, et crie. Élevez votre voix en Bashan, et crie depuis Abarim; car tous tes amants ont été détruits.
Panda milima ya Lebanoni piga kelele. Paza sauti yako Bashani. Piga kelele kutoka kwenye milima ya Abarimu, kwa maana marafiki zako wote wataharibiwa.
21 Je t'ai parlé dans ta prospérité, mais tu as dit: « Je n'écouterai pas ». C'est ce que tu fais depuis ta jeunesse, que tu n'as pas obéi à ma voix.
Nilinena nawe wakati ulioko salama, lakini ukasema, 'Sitasikia.' Hii ilikuwa desturi yako tangu ujana wako, kwani hukusikiliza sauti yangu.
22 Le vent nourrira tous vos bergers, et tes amants iront en captivité. Sûrement alors vous aurez honte et confondues pour toutes vos méchancetés.
Upepo utawalisha wachungaji wako wote, na marafiki zako watakwenda kufungwa. Hakika wewe utakuwa na aibu na kufadhaika kwa matendo yako yote mabaya.
23 Habitant du Liban, qui fait ton nid dans les cèdres, combien tu seras à plaindre lorsque les douleurs t'atteindront, la douleur comme celle d'une femme en travail!
Wewe mfalme, wewe ambaye huishi katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni, wewe aliyefanya kiota kati ya mierezi, utakuwa na hali ya kuhurumiwa utakapopata utungu kama wakati wa kuzaa.”
24 « Je suis vivant, dit Yahvé, quand Conias, fils de Jojakim, roi de Juda, serait le sceau de ma main droite, je t'en arracherais quand même.
“Kama mimi niishivyo-hili ndilo tamko la Bwana-hata kama wewe, Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, ulikuwa alama ya mkono wangu wa kulia, ningekuangusha.
25 Je te livrerais entre les mains de ceux qui en veulent à ta vie et entre les mains de ceux que tu crains, entre les mains de Nebucadnetsar, roi de Babylone, et entre les mains des Chaldéens.
Kwa kuwa nimewatia mikono ya wale wanaotaka uhai wenu na kwenye mkono wa wale ambao mnawaogopa, hata mkononi mwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli na Wakaldayo.
26 Je te chasserai avec ta mère qui t'a porté dans un autre pays, où tu n'es pas né, et là tu mourras.
Nitawatupa wewe na mama yako aliyekuzaa katika nchi nyingine, nchi ambayo hujazaliwa, na huko utakufa.
27 Mais dans le pays où leur âme aspire à retourner, là ils ne retourneront pas. »
Na kuhusu eneo hili ambalo watataka kurudi, hawatarudi hapa.
28 Cet homme, Conia, est-il un vase brisé méprisé? Est-il un récipient dans lequel personne ne se complaît? Pourquoi sont-ils chassés, lui et sa progéniture, et jetés dans un pays qu'ils ne connaissent pas?
Je! Hiki ni chombo kilichodharauliwa na kilichopasuka? Je, Konia ni chombo kilichodharauliwa? Kwa nini wamemtupa yeye na wazao wake, kumpeleka katika nchi wasiyoijua?
29 O terre, terre, terre, écoutez la parole de Yahvé!
Ee Ardhi, Ardhi, Ardhi! Sikieni neno la Bwana!
30 Yahvé dit, « Enregistrez cet homme comme étant sans enfant, un homme qui ne prospérera pas dans ses jours; car l'homme ne prospérera plus de sa descendance, assis sur le trône de David et à régner sur Juda. »
Bwana asema hivi, 'Andika juu ya mtu huyu Konia Yeye hatakuwa na mtoto. Hatafanikiwa wakati wa siku zake, wala hakuna hata mmoja kati ya uzao wake atakayefanikiwa au kuketi tena kwenye kiti cha Daudi na kutawala juu ya Yuda.'”

< Jérémie 22 >