< Isaïe 29 >
1 Malheur à Ariel! Ariel, la ville où David a campé! Ajoutez une année à l'autre, laissez les fêtes se succéder;
Ole wako, wewe Arieli, Arieli, mji alimokaa Daudi! Ongezeni mwaka kwa mwaka, na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.
2 Alors j'affligerai Ariel, et il y aura du deuil et des lamentations. Elle sera pour moi comme un foyer d'autel.
Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.
3 Je camperai contre toi tout autour de toi, et je t'assiégerai avec des troupes postées. J'élèverai contre toi des ouvrages de siège.
Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.
4 Tu seras abattu, et tu parleras du sol. Ta parole sortira de la poussière en marmonnant. Ta voix sera comme celle d'un esprit familier, sortant de la terre, et ton discours murmurera dans la poussière.
Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini, utamumunya maneno yako kutoka mavumbini. Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu, utanongʼona maneno yako toka mavumbini.
5 Mais la multitude de tes ennemis sera comme une fine poussière, et la multitude des impitoyables comme de la paille qui s'envole. Oui, ce sera en un instant, soudainement.
Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini, kundi la wakatili watakuwa kama makapi yapeperushwayo. Naam, ghafula, mara moja,
6 Elle sera visitée par l'Éternel des armées avec des tonnerres, des tremblements de terre, un grand bruit, des tourbillons et des tempêtes, et avec la flamme d'un feu dévorant.
Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu, atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.
7 La multitude de toutes les nations qui combattent Ariel, tous ceux qui s'attaquent à elle et à sa forteresse, et qui l'affligent, seront comme un songe, une vision de la nuit.
Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli, yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi, watakuwa kama ilivyo ndoto, kama maono wakati wa usiku:
8 Ce sera comme quand un homme affamé rêve, et voici qu'il mange; mais il se réveille, et sa faim n'est pas satisfaite; ou comme quand un homme assoiffé rêve, et voici qu'il boit; mais il se réveille, et voici qu'il est faible, et il a encore soif. La multitude de toutes les nations qui combattent contre la montagne de Sion sera comme cela.
kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula, lakini huamka, bado njaa yake ingalipo, kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji, lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.
9 Pause et émerveillement! Aveuglez-vous et soyez aveugle! Ils sont ivres, mais non de vin; ils chancellent, mais non de boisson forte.
Duwaeni na kushangaa, jifanyeni vipofu wenyewe na msione, leweni, lakini si kwa mvinyo, pepesukeni lakini si kwa kileo.
10 Car l'Éternel a répandu sur vous un esprit de profond sommeil; il a fermé vos yeux, prophètes, et il a couvert vos têtes, voyants.
Bwana amewaleteeni usingizi mzito: Ameziba macho yenu (ninyi manabii); amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).
11 Toute vision est devenue pour vous comme les mots d'un livre scellé, que l'on remet à un homme instruit en disant: « Lis ceci, je te prie », et qui répond: « Je ne peux pas, car c'est scellé »;
Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.”
12 et l'on remet le livre à un homme sans instruction en disant: « Lis ceci, je te prie », et qui répond: « Je ne peux pas lire ».
Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”
13 L'Éternel dit: « Parce que ce peuple s'approche de sa bouche et m'honore de ses lèvres, mais qu'il a éloigné de moi son cœur, et que sa crainte de moi est un commandement d'hommes qui a été enseigné;
Bwana anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao na kuniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Ibada yao kwangu inatokana na maagizo waliyofundishwa na wanadamu.
14 c'est pourquoi voici que je vais accomplir une œuvre merveilleuse au milieu de ce peuple, une œuvre merveilleuse et un prodige; et la sagesse de ses sages périra, et l'intelligence de ses hommes prudents sera cachée. »
Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa, kwa ajabu juu ya ajabu. Hekima ya wenye hekima itapotea, nayo akili ya wenye akili itatoweka.”
15 Malheur à ceux qui cachent profondément leurs conseils à Yahvé, et dont les actes sont dans l'obscurité, et qui disent: « Qui nous voit? » et « Qui nous connaît? ».
Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu kumficha Bwana mipango yao, wafanyao kazi zao gizani na kufikiri, “Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”
16 Vous mettez tout sens dessus dessous! Faut-il penser que le potier est semblable à l'argile, que la chose faite dise de celui qui l'a faite: « Il ne m'a pas fait », ou que la chose formée dise de celui qui l'a formée: « Il n'a pas d'intelligence? ».
Mnapindua mambo juu chini, kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi! Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga, “Wewe hukunifinyanga mimi?” Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi, “Wewe hujui chochote?”
17 N'est-ce pas encore un tout petit moment, et le Liban sera changé en un champ fertile, et le champ fertile sera considéré comme une forêt?
Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?
18 En ce jour-là, les sourds entendront les paroles du livre, et les yeux des aveugles verront de l'obscurité et des ténèbres.
Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu, na katika utusitusi na giza macho ya kipofu yataona.
19 Les humbles aussi accroîtront leur joie en Yahvé, et les pauvres parmi les hommes se réjouiront du Saint d'Israël.
Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana, wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
20 Car l'impitoyable est réduit à néant, le moqueur cesse d'exister, et tous ceux qui sont attentifs à faire le mal sont retranchés
Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea, nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,
21 qui font accuser quelqu'un par une parole, qui tendent un piège à celui qui réprimande à la porte, et qui privent l'innocent de justice par un faux témoignage.
wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia, wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama, na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki yeye asiye na hatia.
22 C'est pourquoi Yahvé, qui a racheté Abraham, dit à propos de la maison de Jacob: « Jacob ne sera plus confus, et son visage ne pâlira plus.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataaibishwa tena, wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.
23 Mais quand il verra au milieu de lui ses enfants, l'œuvre de mes mains, ils sanctifieront mon nom. Oui, ils sanctifieront le Saint de Jacob, et ils craindront le Dieu d'Israël.
Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao, kazi ya mikono yangu, watalitakasa Jina langu takatifu; wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli.
24 Ceuxqui ont l'esprit égaré parviendront à l'intelligence, et ceux qui se plaignent recevront une instruction. »
Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu, nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”