< Isaïe 13 >

1 Le fardeau de Babylone, que vit Ésaïe, fils d'Amoz.
Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:
2 Dressez une bannière sur la montagne nue! Élève ta voix vers eux! Agite ta main, afin qu'ils entrent dans les portes des nobles.
Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu, wapazieni sauti, wapungieni mkono waingie katika malango ya wenye heshima.
3 J'ai donné des ordres à mes consacrés, J'ai appelé mes vaillants hommes pour ma colère, Même mes fiers exaltés.
Nimewaamuru watakatifu wangu; nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu: wale wanaoshangilia ushindi wangu.
4 Le bruit d'une multitude est dans les montagnes, comme celui d'un grand peuple; le bruit d'un tumulte des royaumes des nations rassemblées! L'Éternel des armées rassemble l'armée pour la bataille.
Sikilizeni kelele juu ya milima, kama ile ya umati mkubwa wa watu! Sikilizeni, makelele katikati ya falme, kama mataifa yanayokusanyika pamoja! Bwana Mwenye Nguvu Zote anakusanya jeshi kwa ajili ya vita.
5 Ils viennent d'un pays lointain, de l'extrémité des cieux, Yahvé, avec les armes de sa colère, pour détruire tout le pays.
Wanakuja kutoka nchi za mbali sana, kutoka miisho ya mbingu, Bwana na silaha za ghadhabu yake, kuangamiza nchi yote.
6 Gémissez, car le jour de l'Éternel est proche! Il viendra comme une destruction de la part du Tout-Puissant.
Ombolezeni, kwa maana siku ya Bwana i karibu, itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.
7 C'est pourquoi toutes les mains seront affaiblies, et le cœur de chacun se fondra.
Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea, moyo wa kila mtu utayeyuka.
8 Ils seront consternés. Des angoisses et des douleurs les saisiront. Ils souffriront comme une femme en travail. Ils se regarderont avec étonnement les uns les autres. Leurs visages seront des visages de flamme.
Hofu itawakamata, uchungu na maumivu makali yatawashika, watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa. Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake, nyuso zao zikiwaka kama moto.
9 Voici, le jour de l'Éternel arrive, jour cruel, jour de colère et de fureur, pour réduire le pays en désert, et en exterminer les pécheurs.
Tazameni, siku ya Bwana inakuja, siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali, kuifanya nchi kuwa ukiwa na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.
10 Car les étoiles du ciel et ses constellations ne donneront plus leur lumière. Le soleil s'obscurcira en s'éteignant, et la lune ne fera pas briller sa lumière.
Nyota za mbinguni na makundi ya nyota havitatoa mwanga wake. Jua linalochomoza litatiwa giza na mwezi hautatoa nuru yake.
11 Je punirai le monde pour sa méchanceté, et les méchants pour leur iniquité. Je ferai cesser l'arrogance des orgueilleux, et j'humilierai l'arrogance des terribles.
Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake, waovu kwa ajili ya dhambi zao. Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi, na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.
12 Je rendrai les hommes plus rares que l'or fin, les hommes plus rares que l'or pur d'Ophir.
Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi, watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.
13 C'est pourquoi je ferai trembler les cieux, et la terre sera secouée de sa place, dans la colère de l'Éternel des armées et au jour de son ardente fureur.
Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke, nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake katika ghadhabu ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika siku ya hasira yake iwakayo.
14 Il arrivera que, comme une gazelle en chasse et comme des brebis que personne ne rassemble, ils se tourneront chacun vers son propre peuple, et fuiront chacun dans son pays.
Kama swala awindwaye, kama kondoo wasio na mchungaji, kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.
15 Tous ceux qui seront trouvés seront transpercés. Tous ceux qui seront capturés tomberont par l'épée.
Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo, wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.
16 Leurs enfants aussi seront mis en pièces sous leurs yeux. Leurs maisons seront saccagées, et leurs femmes violées.
Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande mbele ya macho yao; nyumba zao zitatekwa na wake zao watatendwa jeuri.
17 Voici, je vais exciter contre eux les Mèdes, qui n'apprécieront pas l'argent, et quant à l'or, ils n'y prendront pas plaisir.
Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao, ambao hawajali fedha wala hawafurahii dhahabu.
18 Leurs arcs mettront en pièces les jeunes gens, et ils n'auront pas pitié du fruit des entrailles. Leurs yeux n'épargneront pas les enfants.
Mishale yao itawaangusha vijana, hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga wala hawataangalia watoto kwa huruma.
19 Babylone, la gloire des royaumes, la beauté de l'orgueil des Chaldéens, sera comme lorsque Dieu renversa Sodome et Gomorrhe.
Babeli, johari ya falme, utukufu wa kiburi cha Wababeli, itaangushwa na Mungu kama Sodoma na Gomora.
20 Elle ne sera jamais habitée, et on ne l'habitera pas de génération en génération. L'Arabe n'y dressera pas sa tente, et les bergers n'y feront pas reposer leurs troupeaux.
Hautakaliwa na watu kamwe wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko, hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.
21 Mais les bêtes sauvages du désert y coucheront, et leurs maisons seront remplies de chacals. Les autruches y habiteront, et les chèvres sauvages s'y ébattront.
Lakini viumbe wa jangwani watalala huko, mbweha watajaza nyumba zake, bundi wataishi humo nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.
22 Les hyènes crieront dans leurs forteresses, et les chacals dans les palais agréables. Son temps est proche, et ses jours ne se prolongeront pas.
Fisi watalia ndani ya ngome zake, mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari. Wakati wake umewadia, na siku zake hazitaongezwa.

< Isaïe 13 >