< Isaïe 10 >

1 Malheur à ceux qui décrètent des ordonnances injustes, Et aux rédacteurs qui écrivent des ordonnances oppressives
Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
2 pour priver de justice les indigents, Et pour dépouiller de leurs droits les pauvres de mon peuple, Afin que les veuves soient leur butin, Et qu'ils fassent de l'orphelin leur proie!
kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
3 Que ferez-vous au jour du châtiment, au jour de la désolation qui viendra de loin? Vers qui fuiras-tu pour demander du secours? Où laisserez-vous vos richesses?
Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
4 Ils ne se prosterneront que sous les prisonniers, et tomberont sous les morts. Pour autant, sa colère n'est pas détournée, mais sa main est encore tendue.
Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
5 Hélas Assyrien, la verge de ma colère, le bâton dans la main duquel est ma fureur!
“Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
6 Je l'envoie contre une nation profane, et contre le peuple qui m'irrite, je lui donne l'ordre de prendre le pillage et le butin, et de les fouler comme la boue des rues.
Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
7 Mais ce n'est pas ce qu'il veut, et ce n'est pas ce que son cœur pense; mais il a dans le cœur de détruire, et d'exterminer non pas quelques nations.
Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
8 Car il dit: « Tous mes princes ne sont-ils pas des rois?
Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
9 Calno n'est-elle pas comme Carménich? Hamath n`est-elle pas comme Arpad? Samarie n'est-elle pas comme Damas? »
Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
10 Comme ma main a trouvé les royaumes des idoles, dont les images gravées dépassaient celles de Jérusalem et de Samarie,
Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
11 ne ferai-je pas, comme j'ai fait à Samarie et à ses idoles, à Jérusalem et à ses idoles?
je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
12 C'est pourquoi, lorsque l'Éternel aura accompli toute son œuvre sur la montagne de Sion et sur Jérusalem, je punirai le fruit du cœur orgueilleux et volontaire du roi d'Assyrie, et l'insolence de ses regards arrogants.
Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
13 Car il a dit: « C'est par la force de ma main que j'ai agi, et par ma sagesse, car j'ai de l'intelligence. J'ai fait disparaître les limites des peuples, et j'ai dérobé leurs trésors. Comme un vaillant homme, j'ai abattu leurs chefs.
Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
14 Ma main a trouvé les richesses des peuples comme un nid, et comme on recueille des œufs abandonnés, j'ai recueilli toute la terre. Il n'y en a pas un qui ait remué l'aile, qui ait ouvert la bouche, ou qui ait gazouillé. »
Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
15 La hache se vante-t-elle de celui qui coupe? La scie doit-elle s'élever au-dessus de celui qui la scie? Comme si une verge devait élever ceux qui la soulèvent, ou comme si un bâton devait élever quelqu'un qui n'est pas du bois.
Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
16 C'est pourquoi l'Éternel, l'Éternel des armées, enverra parmi ses gros la maigreur, et sous sa gloire s'allumera une ardeur comme celle d'un feu.
Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
17 La lumière d'Israël sera comme un feu, et son Saint comme une flamme; et il brûlera et dévorera ses épines et ses ronces en un seul jour.
Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
18 Il consumera la gloire de sa forêt et de son champ fertile, l'âme et le corps. Ce sera comme lorsqu'un porte-étendard s'évanouit.
Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
19 Le reste des arbres de sa forêt sera peu nombreux, au point qu'un enfant pourrait écrire leur nombre.
Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
20 En ce jour-là, le reste d'Israël et les réchappés de la maison de Jacob ne s'appuieront plus sur celui qui les frappait, mais ils s'appuieront sur Yahvé, le Saint d'Israël, dans la vérité.
Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
21 Un reste reviendra, le reste de Jacob, vers le Dieu puissant.
Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
22 Car si ton peuple, Israël, est comme le sable de la mer, un reste seulement reviendra. Une destruction est prévue, débordante de justice.
Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
23 Car l'Éternel, le Yahvé des armées, fera une destruction complète, et déterminée, sur toute la terre.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
24 C'est pourquoi l'Éternel, le Yahvé des armées, dit: « Mon peuple qui habite Sion, ne craignez pas l'Assyrien, même s'il vous frappe de sa verge et qu'il lève son bâton contre vous, comme l'Égypte.
Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
25 Car encore un tout petit moment, et l'indignation contre vous s'accomplira, et ma colère se portera sur sa destruction. »
Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
26 Yahvé des armées suscitera contre lui un fléau, comme lors du massacre de Madian au rocher d'Oreb. Sa verge sera au-dessus de la mer, et il la lèvera comme il l'a fait contre l'Égypte.
Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
27 En ce jour-là, son fardeau disparaîtra de ton épaule, et son joug de ton cou, et le joug sera détruit à cause de l'huile d'onction.
Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
28 Il est arrivé à Aiath. Il passe par Migron. A Michmash, il range ses bagages.
Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
29 Ils ont franchi le col. Ils se logent à Guéba. Rama tremble. Gibéa de Saül s'est enfuie.
Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
30 Crie de ta voix, fille de Gallim! Écoute, Laisha! Pauvre Anathoth!
Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
31 Madmena est une fugitive. Les habitants de Guébim fuient pour se mettre en sûreté.
Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
32 Aujourd'hui même, il s'arrête à Nob. Il serre la main à la montagne de la fille de Sion, à la colline de Jérusalem.
Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
33 Voici que le Seigneur, l'Éternel des armées, fauche les rameaux avec terreur. Les grands seront abattus, et les grands seront abaissés.
Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
34 Ilabattra avec le fer les fourrés de la forêt, et le Liban tombera sous les coups du Puissant.
Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.

< Isaïe 10 >