< Genèse 18 >

1 Yahvé lui apparut près des chênes de Mamré, comme il était assis à l'entrée de la tente, dans la chaleur du jour.
Yahwe alimtokea Abraham katika Mialoni ya Mamre, alipokua ameketi mlangoni pa hema wakati wa jua.
2 Il leva les yeux et regarda, et il vit que trois hommes se tenaient près de lui. Il courut à leur rencontre depuis l'entrée de la tente, se prosterna à terre
Akatazama juu na, tazama, akaona wanaume watatu wamesimama mbele yake. Alipo waona, alikimbia kupitia mlango wa hema kuwalaki na kuinama chini hadi ardhini.
3 etdit: « Seigneur, si j'ai trouvé grâce à tes yeux, ne te sépare pas de ton serviteur.
Akasema, “Bwana, kama nimepata upendelea machoni pako, nakuomba usinipite na kuniacha mtumishi wako.
4 Allez maintenant chercher un peu d'eau, lavez vos pieds, et reposez-vous sous l'arbre.
Naomba maji kidogo yaletwe, mnawe miguu yenu, na mjipumzishe chini ya mti.
5 Je vais chercher un morceau de pain pour que vous puissiez vous rafraîchir le cœur. Après cela, vous pourrez vous en aller, maintenant que vous êtes venus vers votre serviteur. » Ils ont dit: « Très bien, faites ce que vous avez dit. »
Nami acha nilete chakula kidogo, ili kwamba mjiburudishe wenyewe. Ndipo baadae mwaweza kwenda zenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakasema, “Fanya kama ulivyo sema.”
6 Abraham se précipita dans la tente vers Sara, et dit: « Prépare vite trois seahs de fleur de farine, pétris-la et fais des gâteaux. »
Kisha Abraham akaenda upesi hemani kwa Sara, na akasema, “Harakisha, chukua vipimo vitatu vya unga safi, uukande, na fanya mkate.”
7 Abraham courut au troupeau, prit un veau tendre et bon, et le donna au serviteur. Celui-ci s'empressa de le panser.
Kisha Abraham akakimbia kundini, akachukua ndama wa ng'ombe aliye laini na mzuri, na akampatia mtumishi na kwa haraka akamwandaa.
8 Il prit du beurre, du lait et le veau qu'il avait habillé, et il le mit devant eux. Il se tint près d'eux sous l'arbre, et ils mangèrent.
Akatwaa siagi na maziwa na ndama aliye kwisha andaliwa, na akaweka chakula mbele yao, naye akasimama karibu nao chini ya mti wakati wanakula.
9 Ils lui demandèrent: « Où est Sarah, ta femme? » Il a dit: « Là, dans la tente. »
Wakamwambia, “Mke wako Sara yuko wapi?” akajibu. “pale hemani.”
10 Il dit: « Je reviendrai certainement chez toi l'année prochaine à peu près à la même époque; et voici que Sarah, ta femme, aura un fils. » Sara entendit à la porte de la tente, qui était derrière lui.
akasema, “Hakika nitarejea kwako majira ya machipuko, na tazama Sara mkeo atakuwa na mtoto wa kiume.” Sara alikuwa akisikiliza mlangoni pa hema iliyokuwa nyuma yake.
11 Or Abraham et Sara étaient vieux, d'un âge avancé. Sara avait dépassé l'âge de procréer.
Abraham na Sara walikuwa wazee, umri wao ulikuwa umeendelea sana, na Sara alikuwa amepita umri ambao mwanamke anaweza kuzaa watoto.
12 Sara riait en elle-même, disant: « Quand je serai vieille, aurai-je du plaisir, mon seigneur étant vieux aussi? »
Kwa hiyo Sara akajicheka mwenyewe, akijisemesha mwenyewe, “baada ya kuwa nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je ni tapata furaha hii?”
13 Yahvé dit à Abraham: « Pourquoi Sarah a-t-elle ri en disant: « Aurai-je vraiment un enfant quand je serai vieille?
Yahwe akamwambia Abraham, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, Je ni kweli nitazaa mtoto, nikiwa mzee'?
14 Y a-t-il quelque chose de trop difficile pour Yahvé? Au temps fixé, je reviendrai vers toi, à la saison qui vient, et Sara aura un fils. »
Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe? Itakuwa katika wakati nilioweka mimi majira ya machipuko, nitarejea kwako. Majira haya mwakani Sara atakuwa na mtoto wa kiume.”
15 Alors Sarah le nia, disant: « Je n'ai pas ri », car elle avait peur. Il a dit: « Non, mais vous avez ri. »
Kisha Sara akakataa na kusema, “sikucheka,” kwa kuwa aliogopa. Yahwe akasema, “hapana ulicheka.”
16 Les hommes se levèrent de là et regardèrent vers Sodome. Abraham alla avec eux pour les voir en chemin.
Kisha wale wanaume walisimama kuondoka na wakatazama chini kuelekea Sodoma. Abraham akafuatana nao kuona njia yao.
17 Yahvé dit: « Est-ce que je cacherai à Abraham ce que je fais,
Lakini Yahwe akasema, Je ni mfiche Abraham kile ninacho kusudia kufanya,
18 puisque Abraham deviendra une nation grande et puissante, et que toutes les nations de la terre seront bénies en lui?
Ikiwa kwa hakika Abraham atakuwa mkuu na taifa lenye nguvu, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa?
19 Car je l'ai connu, afin qu'il commande à ses enfants et à sa famille après lui, pour qu'ils gardent la voie de l'Éternel, en pratiquant la justice et l'équité, afin que l'Éternel fasse venir sur Abraham ce qu'il a dit de lui. »
Kwa kuwa nimemchagua ili awaelekeze wanawe na nyumba yake baada yake waishike njia ya Yahwe, watende utakatifu na haki, ili kwamba Yahwe ampatie Abraham yale aliyo yasema kwake.”
20 Yahvé dit: « Puisque le cri de Sodome et de Gomorrhe est grand, et que leur péché est très grave,
Kisha Yahwe akasema, “Kwa sababu kilio cha Sodoma na Gomora ni kikuu, na kwa kuwa dhambi yao ni kubwa,
21 je descendrai maintenant, et je verrai si leurs actes sont aussi mauvais que les rapports qui me sont parvenus. Si ce n'est pas le cas, je le saurai. »
sasa nitashuka pale na kuona kilio kilicho nifikia dhidi yake, ikiwa kweli wamefanya au hawakufanya, nitajua.”
22 Les hommes se détournèrent de là et allèrent vers Sodome, mais Abraham se tenait encore devant Yahvé.
Kwa hiyo wale wanaume wakageuka toka pale, na kuelekea Sodoma, lakini Abraham akabaki amesimama mbele ya Yahwe.
23 Abraham s'approcha, et dit: Veux-tu consumer les justes avec les méchants?
Kisha Abraham alikaribia na kusema, “Je utawafutilia mbali watakatifu pamoja na waovu?
24 Et s'il y a cinquante justes dans la ville? Vas-tu consumer et ne pas épargner la place pour les cinquante justes qui s'y trouvent?
Huenda wakawepo wenye haki hamsini katika mji. Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?
25 Qu'il soit loin de toi de faire de telles choses, de tuer les justes avec les méchants, afin que les justes soient comme les méchants. Que cela soit loin de vous. Le Juge de toute la terre ne devrait-il pas faire ce qui est juste? »
Hasha usifanye hivyo, kuwauwa watakatifu pamoja na waovu, ili kwamba watakatifu watendewe sawa na waovu. Hasha! Je muhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?”
26 Yahvé dit: « Si je trouve à Sodome cinquante justes dans la ville, j'épargnerai tout le lieu à cause d'eux. »
Yahwe akasema, “Katika Sodoma nikipata watakatifu hamsini kwenye mji, nita uacha mji wote kwa ajili ya hao.”
27 Abraham répondit: « Voici, j'ai pris sur moi de parler au Seigneur, bien que je sois poussière et cendre.
Abraham akajibu na kusema, “Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu, hata kama mimi ni mavumbi na majivu!
28 Et s'il manque cinq des cinquante justes? Détruiras-tu toute la ville par manque de cinq? » Il a dit: « Je ne la détruirai pas si j'y trouve quarante-cinq personnes. »
Itakuwaje ikiwa kuna watano pungufu katika idadi ya hao watakatifu hamsini? Je utaangamiza mji wote kwa upungufu wa hao watano?” Akasema, “Sitaangamiza, ikiwa nitapata watu arobaini na watano pale.”
29 Il lui parla encore, et dit: « Et s'il y en a quarante qui se trouvent là? » Il a dit: « Je ne le ferai pas pour l'amour des quarante. »
Akaongea naye tena, na kusema, “Itakuwaje ikiwa arobaini watapatikana pale?” Akajibu, “Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.”
30 Il dit: « Oh, ne laissez pas le Seigneur se mettre en colère, et je parlerai. Et s'il y en a trente trouvés là? » Il a dit: « Je ne le ferai pas si j'en trouve trente là-bas. »
Akasema, Tafadhali usikasirike, Bwana, nikiongea. Pengine thelathini watapatikana pale.” Akajibu, 'Sitafanya, ikiwa nitapata thelathini pale.”
31 Il dit: « Voici, j'ai pris sur moi de parler au Seigneur. Et s'il y en a vingt qui se trouvent là? » Il a dit: « Je ne la détruirai pas à cause des vingt. »
Akasema, Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu! Pengine ishirini watapatikana pale.” Akajibu, “Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini.”
32 Il dit: « Oh, que le Seigneur ne se mette pas en colère, et je ne parlerai qu'une fois de plus. Et si l'on en trouve dix là-bas? » Il a dit: « Je ne la détruirai pas à cause des dix. »
Akasema, “Tafadhali usikasirike, Bwana, na nitasema jambo hili kwa mara ya mwisho. Huenda kumi wakaonekana kule.” Na akasema, sitaangamiza kwa ajili ya hao kumi.”
33 Yahvé s'en alla dès qu'il eut fini de s'entretenir avec Abraham, et Abraham retourna à sa place.
Yahwe akaendelea na njia yake mara tu baada ya kumaliza kuongea na Abraham, na Abraham akarudi nyumbani.

< Genèse 18 >