< Genèse 14 >
1 Du temps d'Amraphel, roi de Schinear, d'Arioch, roi d'Ellasar, de Chedorlaomer, roi d'Élam, et de Tidal, roi de Gojim,
Ikiwa katika siku za Amrafeli, mfalme wa shinari, Arioko, mfalme wa Elasari, Kedorlaoma, mfalme wa Elam na Tidali, mfalme wa Goimu,
2 ils firent la guerre à Béra, roi de Sodome, à Birsha, roi de Gomorrhe, à Shinab, roi d'Adma, à Shemeber, roi de Zéboïm, et au roi de Béla (appelé aussi Zoar).
walifanya vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha, mfalme wa Gomora, Shinabu, mfalme wa Adma, Shemeberi, mfalme wa Seboim, na mfalme wa Bela(pia ikiitwa Soari).
3 Tous se rejoignaient dans la vallée de Siddim (appelée aussi la mer Salée).
Hawa wafalme watano wa mwisho waliungana pamoja katika bonde la Sidim (pia likiitwa bahari ya chumvi).
4 Ils servirent Chedorlaomer pendant douze ans, et la treizième année, ils se révoltèrent.
Kwa miaka kumi na mbili walimtumikia Kedorlaoma, lakini katika mwaka wa kumi na tatu waliasi.
5 La quatorzième année, Kedorlaomer et les rois qui étaient avec lui vinrent frapper les Rephaïm à Ashteroth Karnaïm, les Zuzim à Ham, les Emim à Shaveh Kiriathaïm,
Kisha katika mwaka wa kumi na nne, Kedorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja nae walikuja na kuwashambulia Warefai katika Ashteroth Karnaimu, na Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe Kiriathaimu,
6 et les Horites dans leur montagne de Séir, jusqu'à El Paran, qui est au bord du désert.
na Wahori katika mlima wao wa Seiri, mpaka El Parani iliyo karibu na jangwa.
7 Ils revinrent et arrivèrent à En Mischpat (appelée aussi Kadès), et ils battirent tout le pays des Amalécites et des Amorites, qui habitaient à Hatsatson-Tamar.
Kisha wakarudi wakaja En Misifati (Pia ikiitwa Kadeshi), na kuishinda nchi yote ya Waamaleki, na pia Waamori ambao waliishi Hasasoni Tamari.
8 Le roi de Sodome et le roi de Gomorrhe, le roi d'Adma, le roi de Zéboïm et le roi de Béla (appelé aussi Zoar) sortirent, et ils se rangèrent en bataille contre eux dans la vallée de Siddim
Kisha mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboim, na mfalme wa Bela (pia ikiitwa Soari) walikwenda na kuandaa vita
9 contre Kedorlaomer, roi d'Élam, Tidal, roi de Goïim, Amraphel, roi de Shinar, et Arioch, roi d'Ellasar; quatre rois contre les cinq.
dhidi ya Kadorlaoma, mfalme wa Elam, Tidali mfalme wa Goim, Amrafeli, mfalme wa Shinari, Arioki, mfalme wa Elasari; wafme wanne dhidi ya wale watano.
10 Or, la vallée de Siddim était pleine de puits de goudron; les rois de Sodome et de Gomorrhe s'enfuirent, et quelques-uns y tombèrent. Ceux qui restèrent s'enfuirent sur les collines.
Na sasa bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, na wafalme wa Sodoma na Gomora walipokimbia, wakaanguka pale. Wale waliosalia wakakimbilia milimani.
11 Ils prirent tous les biens de Sodome et de Gomorrhe, ainsi que toute leur nourriture, et s'en allèrent.
Kwa hiyo adui akachukua mali zote za Sodoma na Gomora na vyakula vyao vyote, na wakaenda zao,
12 Ils prirent Lot, fils du frère d'Abram, qui habitait à Sodome, et ses biens, et s'en allèrent.
walipoondoka, wakamchukua pia Lutu, mtoto wa ndugu yake na Abram ambaye aliishi Sodoma, pamoja na mali zake zote.
13 Un rescapé vint le dire à Abram, l'Hébreu. En ce temps-là, il habitait près des chênes de Mamré, l'Amoréen, frère d'Eshcol et frère d'Aner. Ils étaient les alliés d'Abram.
Mmoja ambaye alitoroka alikuja na kumwambia Abram mwebrania. Alikuwa anaishi katika mialoni ya Mamre, mwamori ambaye alikuwa ni ndugu wa Eshkoli na Aneri ambao walikuwa washirika wa Abram.
14 Lorsqu'Abram apprit que son parent avait été emmené en captivité, il fit sortir ses trois cent dix-huit hommes entraînés, nés dans sa maison, et les poursuivit jusqu'à Dan.
Abram aliposikia kuwa maadui wamemteka ndugu yake, akawaongoza wanaume waliofunzwa na kuzaliwa nyumbani mwake 318 na akawaongoza hadi Dani.
15 Il se divisa contre eux pendant la nuit, lui et ses serviteurs, les battit, et les poursuivit jusqu'à Hoba, qui est à gauche de Damas.
Akawagawanya watu wake dhidi yao usiku na kuwavamia, na kuwafukuza mpaka Hoba, ambayo iko kaskazini mwa Dameski.
16 Il ramena tous les biens, et il ramena aussi son parent Lot et ses biens, les femmes aussi, et le reste du peuple.
Kisha akarudisha mali zote, pia akamrudisha ndugu yake Lutu na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
17 Le roi de Sodome sortit à sa rencontre, après son retour du massacre de Chedorlaomer et des rois qui étaient avec lui, dans la vallée de Shaveh (c'est-à-dire la vallée du roi).
Baada ya Abram kurudi kutoka kumpiga Kadorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja nae, mfalme wa Sodoma akatoka kuonana nae katika bonde la Shawe (pia iliitwa bonde la mfalme).
18 Melchisédek, roi de Salem, fit sortir du pain et du vin. Il était prêtre du Dieu Très-Haut.
Melkizedeki, mfalme wa Salem, akaleta mkate na divai. Alikuwa ni kuhani wa Mungu aliye juu sana.
19 Il le bénit et dit: « Béni soit Abram du Dieu Très-Haut, possesseur du ciel et de la terre.
Alimbariki akisema, “Abarikiwea Abram na Mungu aliye juu sana, muumba wa mbingu na nchi.
20 Béni soit le Dieu Très-Haut, qui a livré tes ennemis entre tes mains. » Abram lui a donné un dixième de tout.
Abarikiwe Mungu aliye juu sana, ambaye amekupatia adui zako katika mikono yako.” Kisha Abram akampatia sehemu ya kumi ya kila kitu.
21 Le roi de Sodome dit à Abram: « Donne-moi le peuple, et prends les biens pour toi. »
Mfalme wa Sodama akamwambia Abram, “Nipatie watu, na ujichukulie wewe mwenyewe mali.”
22 Abram dit au roi de Sodome: « J'ai levé la main vers Yahvé, Dieu Très-Haut, qui possède le ciel et la terre,
Abram akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua juu mkono wangu kwa Yahwe, Mungu aliye juu sana, muumbaji wa mbingu na nchi,
23 pour ne prendre ni fil, ni lanière de sandale, ni rien de ce qui t'appartient, de peur que tu ne dises: « J'ai enrichi Abram ».
kwamba sitachukua uzi wala gidamu ya kiatu, au kitu chochote ambacho ni chako, 'ili kwamba usiseme, nimemfanya Abram kuwa tajiri.'
24 Je n'accepterai rien de toi, si ce n'est ce que les jeunes gens ont mangé, et la part des hommes qui sont partis avec moi: Aner, Eshcol et Mamré. Qu'ils prennent leur part. »
Sitachukua chochote isipokuwa kile ambacho vijana wamekula na sehemu za watu waliokwenda nami. Aneri, Eskoli, na Mamre na wachukue sehemu zao.”