< Genèse 11 >

1 Toute la terre avait une seule langue et un seul langage.
Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
2 Comme ils voyageaient vers l'est, ils trouvèrent une plaine dans le pays de Shinar, et ils y habitèrent.
Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
3 Ils se dirent les uns aux autres: « Venez, faisons des briques, et brûlons-les bien. » Ils avaient la brique pour pierre, et le goudron pour mortier.
Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
4 Ils dirent: « Venez, bâtissons-nous une ville et une tour dont le sommet atteint le ciel, et faisons-nous un nom, de peur que nous ne soyons dispersés sur la surface de toute la terre. »
Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
5 Yahvé descendit pour voir la ville et la tour que les enfants des hommes avaient bâties.
Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
6 L'Éternel dit: « Voici, ils forment un seul peuple, et ils ont tous une seule langue, et voici ce qu'ils commencent à faire. Maintenant, rien ne leur sera refusé de ce qu'ils ont l'intention de faire.
Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
7 Venez, descendons, et là nous confondrons leur langue, afin qu'ils ne comprennent pas le langage les uns des autres. »
Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
8 Yahvé les dispersa donc à partir de là sur la surface de toute la terre. Ils cessèrent de construire la ville.
Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
9 C'est pourquoi on l'appela Babel, parce que Yahvé y confondit le langage de toute la terre. De là, Yahvé les dispersa sur la surface de toute la terre.
Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
10 Voici l'histoire des générations de Sem: Sem était âgé de cent ans lorsqu'il engendra Arpachshad, deux ans après le déluge.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
11 Sem vécut cinq cents ans après avoir engendré Arpacshad, et il engendra d'autres fils et d'autres filles.
Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
12 Arpacshad vécut trente-cinq ans, et il engendra Shéla.
Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
13 Arpacshad vécut quatre cent trois ans après avoir engendré Shéla, et il engendra d'autres fils et d'autres filles.
Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
14 Shéla vécut trente ans, et il engendra Eber.
Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 Shéla vécut quatre cent trois ans après avoir engendré Eber, et il engendra d'autres fils et d'autres filles.
Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
16 Eber vécut trente-quatre ans, et devint le père de Péleg.
Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 Eber vécut quatre cent trente ans après avoir engendré Peleg, et il engendra d'autres fils et d'autres filles.
Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
18 Péleg vécut trente ans et devint le père de Reu.
Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 Péleg vécut deux cent neuf ans après avoir engendré Reu, et il engendra d'autres fils et d'autres filles.
Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
20 Reu vécut trente-deux ans, et devint le père de Serug.
Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
21 Reu vécut deux cent sept ans après avoir engendré Serug, et il engendra d'autres fils et d'autres filles.
Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
22 Serug vécut trente ans, et devint le père de Nachor.
Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 Serug vécut deux cents ans après avoir engendré Nachor, et il engendra d'autres fils et d'autres filles.
Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
24 Nachor vécut vingt-neuf ans, et devint le père de Térah.
Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 Nachor vécut cent dix-neuf ans après avoir engendré Térah, et il engendra d'autres fils et d'autres filles.
Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
26 Térah vécut soixante-dix ans et devint le père d'Abram, de Nahor et de Haran.
Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
27 Voici l'histoire des générations de Térah. Térah est le père d'Abram, de Nahor et de Haran. Haran est le père de Lot.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
28 Haran mourut dans le pays où il était né, à Ur des Chaldéens, alors que son père Térah vivait encore.
Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
29 Abram et Nachor épousèrent des femmes. Le nom de la femme d'Abram était Saraï, et le nom de la femme de Nachor était Milca, fille de Haran, qui était aussi le père d'Isca.
Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
30 Saraï était stérile. Elle n'avait pas d'enfant.
Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
31 Térah prit Abram, son fils, Lot, fils de Haran, fils de son fils, et Saraï, sa belle-fille, femme de son fils Abram. Ils partirent d'Ur des Chaldéens, pour aller au pays de Canaan. Ils arrivèrent à Haran et y habitèrent.
Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
32 Les jours de Térah furent de deux cent cinq ans. Térah mourut à Haran.
Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.

< Genèse 11 >