< Ézéchiel 45 >

1 "''De plus, lorsque vous diviserez par le sort le pays pour l'héritage, vous présenterez une offrande à Yahvé, une portion sainte du pays. Sa longueur sera celle de vingt-cinq mille roseaux, et sa largeur de dix mille. Elle sera sainte dans toute son étendue, tout autour.
“‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
2 De cette mesure, il y aura un carré de cinq cents sur cinq cents pour le lieu saint, et cinquante coudées pour ses pâturages tout autour.
Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
3 Tu mesureras de cette mesure une longueur de vingt-cinq mille et une largeur de dix mille. C'est là que se trouvera le sanctuaire, qui est très saint.
Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
4 C'est une portion sainte du pays; elle sera pour les prêtres, les ministres du sanctuaire, qui s'approchent pour servir l'Éternel. Ce sera un lieu pour leurs maisons et un lieu saint pour le sanctuaire.
Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
5 Vingt-cinq mille coudées en longueur et dix mille en largeur seront pour les Lévites, les ministres de la maison, comme une possession pour eux-mêmes, pour vingt pièces.
Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
6 "''Tu établiras la propriété de la ville sur cinq mille coudées de largeur et vingt-cinq mille coudées de longueur, à côté de l'offrande de la portion sainte. Ce sera pour toute la maison d'Israël.
“‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
7 "''Ce qui sera pour le prince sera d'un côté et de l'autre du lotissement sacré et de la possession de la ville, devant le lotissement sacré et devant la possession de la ville, du côté ouest vers l'ouest, et du côté est vers l'est, et d'une longueur correspondant à l'une des portions, de la limite ouest à la limite est.
“‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
8 Dans le pays, il sera pour lui une possession en Israël. Mes princes n'opprimeront plus mon peuple, mais ils donneront le pays à la maison d'Israël selon ses tribus. »
Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
9 "'Le Seigneur Yahvé dit: « Assez, princes d'Israël! Supprimez la violence et le pillage, faites régner la justice et la droiture! Cessez de déposséder mon peuple! » dit le Seigneur Yahvé.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
10 « Vous aurez des balances justes, un épha juste et un bain juste.
Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
11 L'épha et le bain auront la même mesure: le bain contiendra un dixième de homer, et l'épha un dixième de homer. Sa mesure sera la même que celle du homer.
Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
12 Le sicle sera de vingt gérachs. Vingt shekels plus vingt-cinq shekels plus quinze shekels seront ton mina.
Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
13 "''Voici l'offrande que tu présenteras: la sixième partie d'un épha d'un homer de froment, et tu donneras la sixième partie d'un épha d'un homer d'orge,
“‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
14 et la part d'huile, du bain d'huile, un dixième de bain sur le cor, qui est de dix baths, un homer (car dix baths font un homer),
Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
15 et un agneau du troupeau sur deux cents, provenant des pâturages bien arrosés d'Israël, pour l'offrande, l'holocauste et le sacrifice de prospérité, afin de faire l'expiation pour eux, dit le Seigneur Yahvé.
Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
16 « Tout le peuple du pays donnera à cette offrande pour le prince en Israël.
Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
17 C'est au prince qu'il appartiendra de présenter les holocaustes, les offrandes de repas et les libations, aux fêtes, aux nouvelles lunes et aux sabbats, à toutes les fêtes fixées par la maison d'Israël. Il préparera le sacrifice pour le péché, l'offrande de repas, l'holocauste et les sacrifices de paix, afin de faire l'expiation pour la maison d'Israël. »
Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
18 "'Le Seigneur Yahvé dit: « Le premier mois, le premier jour du mois, tu prendras un jeune taureau sans défaut, et tu purifieras le sanctuaire.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
19 Le prêtre prendra du sang du sacrifice pour le péché et en mettra sur les montants de la porte de la maison, sur les quatre coins du rebord de l'autel et sur les montants de la porte du parvis intérieur.
Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
20 Tu feras ainsi, le septième jour du mois, pour celui qui a commis une erreur et pour celui qui est simple. Tu feras ainsi l'expiation pour la maison.
Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
21 "''Au premier mois, le quatorzième jour du mois, vous ferez la Pâque, une fête de sept jours; on mangera des pains sans levain.
“‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
22 Ce jour-là, le prince préparera pour lui et pour tout le peuple du pays un taureau en sacrifice pour le péché.
Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
23 Pendant les sept jours de la fête, il préparera un holocauste à l'Éternel: sept taureaux et sept béliers sans défaut par jour pendant sept jours, et un bouc par jour en sacrifice pour le péché.
Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
24 Il préparera une offrande de repas, un épha pour un taureau, un épha pour un bélier, et un hin d'huile pour un épha.
Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
25 "''Au septième mois, le quinzième jour du mois, pendant la fête, il fera comme cela pendant sept jours. Il fera les mêmes dispositions pour le sacrifice pour le péché, l'holocauste, l'offrande de repas et l'huile. »"
“‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.

< Ézéchiel 45 >