< Ézéchiel 36 >
1 Toi, fils de l'homme, prophétise aux montagnes d'Israël, et dis: « Montagnes d'Israël, écoutez la parole de Yahvé.
“Na wewe, mwanadamu, itabirie milima ya Israeli na useme, 'Milima ya Israeli, lisikilizeni neno la Yahwe.
2 Le Seigneur Yahvé dit: Parce que l'ennemi a dit contre vous: « Ah! » et « Les anciens hauts lieux sont à nous ».
Bwana Yahwe asema hivi: Adui amesema kuhusu ninyi, “Aha!” na “Mahala pa juu pa zamani pamekuwa milki yetu.”'
3 prophétise donc, et dis: « Le Seigneur Yahvé dit: « Parce que, parce qu'on t'a dévasté, parce qu'on t'a englouti de toutes parts, afin que tu sois un bien pour le reste des nations, parce que tu es sur les lèvres des bavards, sur les mauvaises langues des peuples »
Kwa hiyo tabiri na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu ya ukiwa wenu na kwa sababu mashambulizi yaliyokuja juu yenu kutoka pande zote, mmekuwa milki ya mataifa mengine; mmeambiwa kwa midomo yao waongeao, na kwa masingizio ya watu.
4 c'est pourquoi, montagnes d'Israël, écoutez la parole du Seigneur Yahvé: Le Seigneur Yahvé dit aux montagnes et aux collines, aux cours d'eau et aux vallées, aux déserts et aux villes abandonnées, qui sont devenues la proie et la risée du reste des nations d'alentour;
Kwa hiyo, milima ya Israeli, sikilizeni neno la Bwana Yahwe: Bwana Yahwe asema hivi kwa milima na vilima, mifereji ya maji na mabonde, mahali palipoharibika kuwa ukiwa na miji iliyoachwa ambayo imetekwa nyara na kutokuwa huru kwa kutaniwa na mataifa yaliyowazunguka-
5 c'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: « Certes, dans le feu de ma jalousie, j'ai parlé contre le reste des nations et contre tout Édom, qui se sont attribué mon pays pour en faire une possession, avec la joie de tout leur cœur, avec le dépit de l'âme, pour le jeter en proie. »'
kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Hakika nimeongea katika moto wa hasira yangu juu ya mataifa meningine, juu ya Edemu na wote waliochukua nchi yangu kwa ajili yao wenyewe kama milki, dhidi ya wale walikuwa na furaha yote katika mioyo yao na dharau katika roho zao, kama walivyoitwaa nchi yangu kwamba wangeweza kudai nchi za malisho kwa ajili yao.
6 C'est pourquoi prophétise sur le pays d'Israël, et dis aux montagnes, aux collines, aux cours d'eau et aux vallées: « Le Seigneur Yahvé dit: « Voici que je parle dans ma jalousie et dans ma colère, parce que vous avez porté l'opprobre des nations. »
Kwa hiyo, tabiri kwa nchi ya Israeli na sema kwa milima na vilima, hata kwenye mifereji na mabonde, Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Katika ghadhabu yangu na hasira yangu nasema hivi kwa sababu mmechukua fedheha za mataifa.
7 C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: « J'ai juré: « Les nations qui sont autour de toi porteront leur honte.
Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Mimi mwenyewe nitainua mkono wangu kuapa kwamba mataifa yanayowazunguka yamkini yatawabebea aibu yao wenyewe.
8 "''Mais vous, montagnes d'Israël, vous pousserez vos rameaux et vous donnerez votre fruit à mon peuple d'Israël, car il est tout près de venir.
Lakini ninyi, milima ya Israeli, mtachipuza matawi na kuzaa matunda kwa ajili ya watu wangu Israeli, kwa kuwa watarudi kwenu.
9 Car voici, je suis pour vous, je viendrai chez vous, et vous serez cultivés et ensemencés.
Maana tazama, nipo kwa ajili yenu, na kuwachukulia kwa fadhili; mtalimwa na kupandwa mbegu.
10 Je multiplierai les hommes sur vous, toute la maison d'Israël, toute la maison d'Israël. Les villes seront habitées et les ruines seront bâties.
Hivyo nitawaongeza juu ya milima yenu watu katika nyumba ya Israeli, yote. Miji itakaa na palipoharibiwa kujengwa.
11 Je multiplierai sur toi les hommes et les animaux. Ils se multiplieront et seront féconds. Je te ferai habiter comme avant, et tu feras mieux qu'à tes débuts. Alors vous saurez que je suis Yahvé.
Nitaongeza mtu na wanyama juu yenu milima ili kwamba itaongezeka na kuzaa. Kisha nitawafanya kuishi kama mlivyokuwa, na nitawafanya kustawi zaidi kuliko mlivyokuwa zamani, kwa kuwa mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
12 Oui, je ferai en sorte que des hommes marchent sur toi, mon peuple Israël. Ils te posséderont, tu seras leur héritage, et tu ne les priveras plus jamais de leurs enfants. »
Nitawaleta watu, watu wangu Israeli, kutembea juu yenu. Watakumiliki, na utakuwa urithi wao, na hutasababisha tena watoto wao kufa.
13 "'Le Seigneur Yahvé dit: « Parce qu'on te dit: 'Tu es un dévoreur d'hommes, et tu as été un endeuillé de ta nation';
Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu wanakwambia, “Wewe unakula watu, na watoto wa nchi yako wamekufa,”
14 c'est pourquoi tu ne dévoreras plus d'hommes, et tu n'endeuilleras plus ta nation, dit le Seigneur Yahvé.
kwa hiyo hautawala watu wangu tena, na hutalifanya tena taifa lako kuomboleza vifo vyao. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
15 « Je ne te laisserai plus entendre la honte des nations. Tu ne porteras plus l'opprobre des peuples, et tu ne feras plus trébucher ta nation, dit le Seigneur Yahvé.'"
Wala sintokuruhusu kusikiliza fedhiha za mataifa tena; hautachukua tena aibu ya watu au kufanya taifa lako kuanguka-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
16 La parole de Yahvé me fut adressée, en ces termes:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
17 « Fils d'homme, lorsque la maison d'Israël habitait dans son pays, elle l'a souillé par ses voies et par ses actes. Leur conduite devant moi était comme la souillure d'une femme dans son impureté.
“Mwanadamu, wakati nyumba ya Israeli walipoikalia nchi yao, waliinajisi kwa njia zao na matendo yao. Njia zao zilikuwa kama uchafu wa hedhi ya mwanamke mbele yangu.
18 C'est pourquoi j'ai répandu ma colère sur eux, à cause du sang qu'ils ont versé sur le pays, et parce qu'ils l'ont souillé par leurs idoles.
Hivyo nilimwaga ghadhabu yangu juu yao kwa ajili ya damu ambayo waliyoimwaga juu ya nchi na kwa ajili ya uchafu wa hiyo kwa sanamu zao.
19 Je les ai dispersés parmi les nations, et ils se sont dispersés dans les pays. Je les ai jugés selon leur voie et selon leurs actes.
Nimewatawanya miongoni mwa mataifa; walitawanyika katika nchi nyingi. Nimewahukumu kulingana na njia zao na matendo yao.
20 Lorsqu'ils arrivèrent dans les nations où ils allèrent, ils profanèrent mon saint nom, car on disait d'eux: « C'est le peuple de l'Éternel, et ils ont quitté son pays ».
Kisha wakaenda kati ya mataifa, na popote walipoenda, walilitukana jina langu takatifu wakati watu waliwasema, 'Je! hawa kweli ni watu wa Yahwe? Kwa kuwa wamefukuzwa nje ya nchi yake.
21 Mais moi, j'ai eu égard à mon saint nom, que la maison d'Israël avait profané parmi les nations où elle était allée.
Lakini nilikuwa na huruma kwa ajili ya jina langu takatifu ambalo nyumba ya Israeli walilinajisi miongoni mwa mataifa, walipoenda huko.
22 « C'est pourquoi tu diras à la maison d'Israël: Le Seigneur Yahvé dit: « Je ne fais pas cela à cause de toi, maison d'Israël, mais à cause de mon saint nom, que tu as profané parmi les nations où tu es allé.
Kwa hiyo waambie nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Sifanyi haya kwa ajili yenu, nyumba ya Israeli, lakini jina langu, mlilolitukana miongoni mwa mataifa kila sehemu mlipoenda.
23 Je sanctifierai mon grand nom, qui a été profané parmi les nations, que vous avez profané parmi elles. Alors les nations sauront que je suis Yahvé, dit le Seigneur Yahvé, quand je serai sanctifié en vous sous leurs yeux.
Kwa kuwa nitalifanya jina langu kuu kuwa takatifu, mlilolitukana miongoni mwa mataifa-katikati ya mataifa, mmelitukana. Kisha mataifa watajua kwamba mimi ni Yahwe-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe-asemavyo-wakati mtakapoona kwamba mimi ni mtakatifu.
24 "''Car je vous prendrai d'entre les nations, je vous rassemblerai de tous les pays, et je vous amènerai dans votre pays.
Nitawachukua kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka kila nchi, na nitawaleta hata nchi yenu.
25 Je ferai sur vous une aspersion d'eau pure, et vous serez purs. Je vous purifierai de toutes vos souillures et de toutes vos idoles.
Kisha nitanyunyiza maji masafi juu yenu ili muwe wasafi kutoka kwenye uchafu wote, na nitawasafisha kutoka sanamu zenu zenu.
26 Je vous donnerai un cœur nouveau et je mettrai en vous un esprit nouveau. J'ôterai de votre chair le cœur de pierre, et je vous donnerai un cœur de chair.
Nitawapatia moyo mpya na roho mpya sehemu zenu za ndani, na nitautoa moyo wa jiwe kutoka kwenye nyama zenu. Kwa kuwa nitawapatia moyo wa nyama.
27 Je mettrai mon esprit en vous, et je ferai en sorte que vous marchiez selon mes lois. Tu observeras mes ordonnances et tu les mettras en pratique.
Nitaiweka Roho yangu ndani yenu na kuwawezesha kutembea katika sheria zangu na kuziweka hukumu zangu, hivyo mtazitenda.
28 Vous habiterez dans le pays que j'ai donné à vos pères. Vous serez mon peuple, et je serai votre Dieu.
Kisha mtakaa katika nchi niliyowapa babu zenu; mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
29 Je vous délivrerai de toutes vos impuretés. J'appellerai le blé et je le multiplierai, et je ne vous imposerai pas la famine.
Kwa kuwa nitawaokoa kutokana na uchafu wenu wote. Nitaita ngano kuiongeza. Sitaweka tena njaa juu yenu.
30 Je multiplierai les fruits des arbres et les produits des champs, afin que vous n'ayez plus à souffrir de la famine parmi les nations.
Nitaongeza tunda la mti na kuzalisha kwenye mashamba ili kwamba msichukue tena aibu ya njaa juu ya mataifa.
31 "''Alors vous vous souviendrez de vos mauvaises voies, de vos actions qui n'étaient pas bonnes, et vous vous dégoûterez à vos propres yeux de vos iniquités et de vos abominations.
Kisha mtazikumbuka njia zenu mbaya na matendo yenu ambayo hayakuwa mazuri, na mtaonyesha chuki kwenye nyuso zenu kwa sababu ya dhambi zenu na matendo yenu maovu.
32 Je ne fais pas cela à cause de vous, dit le Seigneur Yahvé. « Que cela vous soit connu. Soyez honteux et confus de vos voies, maison d'Israël. »
Sifanyi hili kwa ajili yenu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-ijulikane kwenu. Hivyo tahayarikeni na kufadhaika kwa sababu ya njia zenu, nyumba ya Israeli.
33 "'Le Seigneur Yahvé dit: « Le jour où je vous purifierai de toutes vos iniquités, je ferai en sorte que les villes soient habitées et que les ruines soient bâties.
Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku niliyowatakasa kutoka kwenye uovu wenu wote, nitawafanya miji ikaliwe na kuzijenga sehemu zilizoharibiwa.
34 Le pays qui était dévasté sera cultivé au lieu d'être une désolation aux yeux de tous ceux qui passaient par là.
Kwa kuwa mtailima nchi iliyoharibiwa hadi itakapoonekana haijaaharibika mbele za macho ya wote wapitao karibu.
35 Ils diront: « Cette terre désolée est devenue comme le jardin d'Eden ». Les villes désertes, désolées et en ruines sont fortifiées et habitées.'
Kisha watasema, “Hii nchi ilikuwa ukiwa, lakini imekuwa kama bustani ya Edeni; miji ya ukiwa na isiyo na wakaaji iliyo magofu ambayo ilibomolewa sasa inakaliwa.
36 Alors les nations qui resteront autour de toi sauront que moi, Yahvé, j'ai bâti les ruines et planté les ruines. Moi, Yahvé, je l'ai dit et je le ferai. »
Kisha mataifa mengine waliowazunguka watajua yakwamba mimi ni Yahwe, kwamba nimejenga palipokuwa pameharibiwa na kuipanda mbegu sehemu iliyokuwa ukiwa.
37 "'Le Seigneur Yahvé dit: « Pour cela, d'ailleurs, je serai sollicité par la maison d'Israël, pour le faire pour eux: Je les multiplierai en hommes comme un troupeau.
Bwana Yahwe asema hivi: Tena nitaulizwa na nyumba ya Israeli kufanya hivi kwa ajili yao, kuwaongeza kama kundi la watu.
38 Comme le troupeau pour les sacrifices, comme le troupeau de Jérusalem lors de ses fêtes, ainsi les villes désertes seront remplies de troupeaux d'hommes. Alors ils sauront que je suis Yahvé.'"
Kama kundi lililotengwa kwa ajili ya sadaka, kama kundi katika Yerusalimu katika sikukuu yake iliyoteuliwa, hivyo miji itaharibiwa kwa kujazwa na makundi ya watu na watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'