< Ézéchiel 32 >

1 La douzième année, au douzième mois, le premier jour du mois, la parole de Yahvé me fut adressée, en ces termes:
Kisha ikawa katika mwezi wa kumi na mbili wa mwaka wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 « Fils d'homme, élève une complainte sur Pharaon, roi d'Égypte, et dis-lui, « Tu as été comparé à un jeune lion des nations; mais vous êtes comme un monstre dans les mers. Tu t'es échappé avec tes rivières, et tu as agité les eaux avec tes pieds, et ont souillé leurs rivières. »
“Mwanadamu, inua maombolezo kuhusu Farao mfalme wa Misri; mwambie, 'Wewe ni kama simba mdogo juu ya mataifa, lakini kama jitu la kutisha, unatoka kwenye maji, unayachafua maji kwa miguu yako na kuyachafua maji yao.
3 Le Seigneur Yahvé dit: « J'étendrai mon filet sur toi avec une compagnie de peuples nombreux. Ils vous feront monter dans mon filet.
Bwana Yahwe asema hivi: Basi nitautandaza wavu wangu juu yako katika kusanyiko la watu wengi, na watawainua juu katika wavu wangu.
4 Je vous laisserai sur la terre. Je vous jetterai en plein champ, et fera en sorte que tous les oiseaux du ciel se posent sur toi. Je rassasierai de toi les animaux de toute la terre.
Nitakuacha katika nchi. Nitakutupa kwenye shamba na kufanya ndege wote wa angani watue juu yako; njaa ya wanyama wote waishio juu ya nchi watashibishwa na wewe.
5 Je déposerai ta chair sur les montagnes, et remplissez les vallées de votre hauteur.
Kwa kuwa nitaiweka nyama yako juu ya milima, na nitayajaza mabonde kwa funza wako waliokufa.
6 J'arroserai aussi de votre sang le pays dans lequel vous vous baignez, même dans les montagnes. Les cours d'eau seront pleins de vous.
Kisha nitamwaga damu yako juu ya milima, na vitanda vya kijito vitajazwa kwa damu yako.
7 Quand je t'éteindrai, je couvrirai les cieux. et rend ses étoiles sombres. Je couvrirai le soleil d'un nuage, et la lune ne donnera pas sa lumière.
Kisha wakati nitakapokuzimisha, nitazifunika mbingu na kuzitia giza nyota zake; nitalifunika jua kwa mawingu, na mwezi hautatoa nuru yake usiku.
8 Je ferai s'obscurcir sur toi tous les luminaires du ciel, et mettre les ténèbres sur ton pays, dit le Seigneur Yahvé.
Mianga ya mbinguni nitaiweka giza juu yako, na nitaweka giza juu ya nchi-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
9 « Je vais aussi troubler le cœur de nombreux peuples, quand je vous détruirai parmi les nations, dans les pays que vous n'avez pas connus.
Hivyo nitaitisha mioyo ya watu wengi katika nchi ambao huwajui, wakati nitakapoleta kuhusu uvunjifu miongoni mwa mataifa, miongoni mwa nchi ambazo hukuzijua.
10 Oui, je ferai en sorte que beaucoup de peuples s'étonnent de toi, et leurs rois auront une peur bleue de toi, quand je brandirai mon épée devant eux. Ils trembleront à chaque instant, chaque homme pour sa propre vie, au jour de ta chute. »
Nitawashangaza watu wengi kuhusiana na wewe; wafalme wao watatetemeka kwa hofu kuhusiana na wewe nitakapoutikisa upanga wangu mbele yao. Kila wakati kila mmoja atatetemeka kwa sababu yako, katika siku ya kuanguka kwako.
11 Car le Seigneur Yahvé dit: « L'épée du roi de Babylone viendra sur toi.
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja juu yako.
12 Je ferai tomber ta multitude par les épées des puissants. Ce sont tous les impitoyables des nations. Ils réduiront à néant l'orgueil de l'Égypte, et toute sa multitude sera détruite.
Nitawafanya watu wako kuanguka kwa panga za mashujaa-kila shujaa ni tishio la mataifa. Hawa mashujaa watateketeza kiburi cha Misri na kuangamiza watu wake wote.
13 Je détruirai aussi tous ses animaux à côté des grandes eaux. Le pied de l'homme ne les troublera plus, et les sabots des animaux ne les dérangeront pas.
Kwa kuwa nitaiharibu mifugo yote kutoka karibu na maji mengi; na mguu wa mtu hautayatibua tena, wala kwato za wanyama hazitayatibua.
14 Alors je rendrai leurs eaux limpides, et faire couler leurs rivières comme de l'huile, » dit le Seigneur Yahvé.
Kisha nitayafanya maji yao kuwa matulivu na kufanya mito yao kukimbia kama mafuta-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
15 « Quand je rendrai le pays d'Égypte désert et dévasté, une terre dépourvue de ce dont elle était pleine, quand je frapperai tous ceux qui y habitent, alors ils sauront que je suis Yahvé.
Wakati nitakapoifanya nchi ya Misri sehemu iliyojitenga, wakati nchi iliyopungukiwa na vitu viijazavyo, wakati nitakapo washambulia wakaao ndani yake, watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
16 "''C'est la complainte avec laquelle ils se lamenteront. C'est avec elle que les filles des nations se lamenteront. Elles se lamenteront avec elle sur l'Égypte et sur toute sa multitude, dit le Seigneur Yahvé.''"
Kutakuwa na maombolezo; binti za mataifa wataomboleza juu yake; wataomboleza juu ya Misri, juu ya watu wake wote wataomboleza-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
17 La douzième année, le quinzième jour du mois, la parole de l'Éternel me fut adressée, en ces mots:
Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya kumi na tano ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
18 Fils d'homme, pleure sur la multitude de l'Égypte, et précipite-la, elle et les filles des nations célèbres, dans les profondeurs de la terre, avec ceux qui descendent dans la fosse.
“Mwanadamu, omboleza kwa ajili watu wa misri na walete chini-yeye na binti za mataifa mashuhuri-hata chini ya dunia pamoja na wale walioshuka chini kwenye shimo.
19 Devant qui passes-tu en beauté? Descends, et sois couchée avec les incirconcis.
'Je! wewe ni mzuri zaidi kuliko mtu mwingine yeyote? Nenda chini na lala chini pamoja na wasiotahiriwa.'
20 Ils tomberont parmi ceux qui sont tués par l'épée. Elle est livrée au glaive. Emporte-la avec toute sa multitude.
Wataanguka miongoni mwao waliokuwa wameuawa kwa upanga. Upanga ulikuwa umewekwa! Alikuwa amepatiwa upanga; watamkamata na watu wake.
21 Le fort parmi les puissants lui parlera du milieu du séjour des morts, avec ceux qui le secourent. Ils sont descendus. Les incirconcis reposent, tués par l'épée. (Sheol h7585)
Hodari wa wapiganaji katika Sheoli atasema kuhusu Misri na rafiki zake, 'Wameshuka chini hapa! Watalala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale waliokuwa wameuawa kwa upanga.' (Sheol h7585)
22 « Asshur est là avec toute sa troupe. Ses tombeaux sont tout autour d'elle. Ils sont tous morts, tombés par l'épée,
Ashuru yupo huko pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yamemzunguka; wote waliuawa kwa upanga.
23 leurs tombes sont placées dans les profondeurs de la fosse, et sa troupe est autour de sa tombe, tous morts, tombés par l'épée, qui semaient la terreur dans le pays des vivants.
Wale ambao makaburi yao yamewekwa katika maficho ya mashimo yaliyo huko, pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yakiwazunguka wote waliokuwa wameuawa, walioanguka kwa upanga, wale walioleta hofu juu ya nchi ya walio hai.
24 « Voici Élam et toute sa multitude autour de son tombeau; tous ont été tués, sont tombés par l'épée, sont descendus incirconcis dans les profondeurs de la terre, ont semé la terreur dans le pays des vivants, et ont porté leur honte avec ceux qui descendent dans la fosse.
Elamu yupo huko pamoja na watu wake wote. Makaburi yake yamemzunguka; wote walikuwa wameuawa. Wale walioawa kwa upanga, walioshuka chini wasiotahiriwa hata sehemu ya chini kabisa ya dunia, waliowatia hofu juu ya nchi ya walio hai na wale waliobeba aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao chini kwenye shimo.
25 Ils ont fait d'Élam un lit parmi les morts, avec toute sa multitude. Ses sépulcres sont autour d'elle, tous incirconcis, tués par l'épée; car leur terreur a été causée dans le pays des vivants, et ils ont porté leur honte avec ceux qui descendent dans la fosse. Il est mis au nombre de ceux qui sont tués.
Wamemuwekea kitanda kwa ajili ya Elamu na watu wake wote kati ya wachinjaji; kaburi lake limemzunguka. Wote hawajatahiriwa, kukatwa vipande kwa upanga, kwa sababu waliwaleta mashujaa wao juu ya nchi ya walio hai. Hivyo wamechukua aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao kwenye shimo miongoni mwa wote waliouawa, wale washukao kwenda shimoni. Elamu yu miongoni mwa wale waliokuwa wameuawa.
26 « Voilà Meshech, Tubal, et toute leur multitude. Leurs tombes les entourent, tous les incirconcis, tués par l'épée, car ils ont semé la terreur dans le pays des vivants.
Mesheki, Tubali, na watu wake wote wako huko! Makaburi yao yamewazunguka. Wote hawajatahiriwa, wameuawa kwa upanga, kwa sababu walileta utiisho wao juu ya nchi ya walio hai.
27 Ils ne coucheront pas avec les puissants tombés parmi les incirconcis, qui sont descendus au séjour des morts avec leurs armes de guerre et qui ont mis leurs épées sous leurs têtes. Leurs iniquités sont sur leurs os, car ils étaient la terreur des puissants au pays des vivants. (Sheol h7585)
Wasilale pamoja mashujaa walioanguka wa wasiotahiriwa walioshuka chini kwa Sheoli pamoja na silaha zao zote za vita, na pamoja na panga zao zote walizoziweka chini ya vichwa vyao na maovu yao juu ya mifupa yao. Kwa kuwa walikuwa tishio kwa mashujaa katika nchi ya walio hai. (Sheol h7585)
28 « Mais tu seras brisé parmi les incirconcis, et tu coucheras avec ceux qui sont tués par l'épée.
Basi wewe, Misri, utavunjika kati yao wasiotahiriwa! Utalala karibu nao waliokuwa wamekatwa vipande vipande kwa upanga.
29 « Voici Édom, ses rois et tous ses princes, qui, dans leur puissance, sont couchés avec ceux qui sont tués par l'épée. Ils seront couchés avec les incirconcis, et avec ceux qui descendent dans la fosse.
Edomu yuko huko na wafalme na viongozi wake wote. Walikuwa wamehifadhiwa katika uwezo wao pamoja na wale walioawa kwa upanga. Pamoja na wasiotahiriwa wamelala, pamoja na wale walioshuka kwenye shimo.
30 « Voilà les princes du nord, tous, et tous les Sidoniens, qui sont descendus avec les morts. Ils sont honteux de la terreur qu'ils ont causée par leur puissance. Ils gisent incirconcis avec ceux qui sont tués par l'épée, et ils portent leur honte avec ceux qui descendent dans la fosse.
Wakuu wa kaskazini wako huko-wote na Wasidoni wote walioshuka chini pamoja na hao waliokuwa wamekatwa vipande vipande. Walikuwa na nguvu na kuwafanya wengine kuogopa, lakini sasa wako huko kwa aibu, wasiotahiriwa pamoja na wale waliokatwa vipande vipande kwa upanga. Wamebeba aibu yao wenyewe, pamoja nao waendao kwenye shimo.
31 « Pharaon les verra et sera consolé de toute sa multitude, Pharaon et toute son armée, tués par l'épée », dit le Seigneur Yahvé.
Farao ataona na kupata faraja kuhusu kundi lake waliokatwa vipande vipande kwa upanga -Farao na jeshi lake lote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
32 « Car j'ai mis sa terreur dans le pays des vivants. Il sera couché parmi les incirconcis, avec ceux qui sont tués par l'épée, Pharaon et toute sa multitude », dit le Seigneur Yahvé.
Natamuweka kama utiisho wangu katika nchi ya walio hai, lakini atakuwa amelazwa chini katikati yao wasiotahiriwa, miongoni mwa wale walio katwa vipande kwa upanga, Farao na makundi yake yote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.

< Ézéchiel 32 >