< Exode 8 >

1 Yahvé dit à Moïse: « Va trouver Pharaon et dis-lui: « Voici ce que dit Yahvé: Laisse aller mon peuple, afin qu'il me serve.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
2 Si tu refuses de le laisser partir, voici que je vais frapper de grenouilles tout ton territoire.
Kama ukikataa kuwaruhusu kuondoka, basi nitaipiga nchi yako yote kwa kuwaletea vyura.
3 Le fleuve grouillera de grenouilles, qui monteront et entreront dans ta maison, dans ta chambre, sur ton lit, dans la maison de tes serviteurs, sur tes gens, dans tes fours et dans tes pétrins.
Mto Naili utafurika vyura. Watakuja kwenye jumba lako la kifalme na katika chumba chako cha kulala na kitandani mwako, katika nyumba za maafisa wako na kwa watu wako, vyura hao wataingia katika meko yenu na kwenye vyombo vya kukandia unga.
4 Les grenouilles monteront sur toi, sur ton peuple et sur tous tes serviteurs. »'"
Vyura watapanda juu yako, juu ya watu wako na maafisa wako wote.’”
5 Yahvé dit à Moïse: « Dis à Aaron: « Étends la main de ta verge sur les rivières, sur les ruisseaux et sur les étangs, et fais monter les grenouilles sur le pays d'Égypte. »"
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha mkono wako ukiwa na ile fimbo yako juu ya vijito, mifereji na madimbwi, fanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.’”
6 Aaron étendit sa main sur les eaux d'Égypte; les grenouilles montèrent et couvrirent le pays d'Égypte.
Ndipo Aroni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, nao vyura wakatokea na kuifunika nchi.
7 Les magiciens firent de même avec leurs enchantements et firent monter les grenouilles sur le pays d'Égypte.
Lakini waganga wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao, nao pia wakafanya vyura kuja juu ya nchi ya Misri.
8 Alors Pharaon appela Moïse et Aaron, et dit: « Prie Yahvé qu'il éloigne les grenouilles de moi et de mon peuple; et je laisserai aller le peuple pour qu'il sacrifie à Yahvé. »
Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kusema, “Mwombeni Bwana awaondoe vyura kutoka kwangu na kwa watu wangu, nami nitawaachia watu wenu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
9 Moïse dit à Pharaon: « Je te fais l'honneur de fixer le moment où je prierai pour toi, pour tes serviteurs et pour ton peuple, afin que les grenouilles soient détruites chez toi et dans tes maisons, et qu'elles ne restent que dans le fleuve. »
Mose akamwambia Farao, “Ninakupa heshima ya kuamua ni wakati gani wa kukuombea wewe, maafisa wako na watu wako ili kwamba vyura watoke kwenu na kwenye nyumba zenu. Isipokuwa wale walio katika Mto Naili.”
10 Pharaon a dit: « Demain. » Moïse dit: « Qu'il en soit ainsi, afin que vous sachiez qu'il n'y a personne comme Yahvé notre Dieu.
Farao akasema, “Kesho.” Mose akamjibu, “Itakuwa kama unavyosema, ili upate kujua kwamba hakuna yeyote kama Bwana Mungu wetu.
11 Les grenouilles s'éloigneront de vous, de vos maisons, de vos serviteurs et de votre peuple. Elles ne resteront que dans le fleuve. »
Vyura wataondoka kwako na katika nyumba zako, kwa maafisa wako na kwa watu wako, ila watabakia katika Mto Naili tu.”
12 Moïse et Aaron sortirent de chez Pharaon, et Moïse cria à Yahvé au sujet des grenouilles qu'il avait fait venir sur Pharaon.
Baada ya Mose na Aroni kuondoka kwa Farao, Mose akamlilia Bwana kuhusu vyura aliokuwa amewaleta kwa Farao.
13 Yahvé fit selon la parole de Moïse, et les grenouilles moururent dans les maisons, dans les cours et dans les champs.
Naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Vyura wakafia ndani ya nyumba, viwanjani na mashambani.
14 On les rassembla en tas, et le pays se mit à puer.
Wakayakusanya malundo, nchi nzima ikanuka.
15 Mais lorsque Pharaon vit qu'il y avait un répit, il endurcit son cœur et ne les écouta pas, comme l'avait dit l'Éternel.
Lakini Farao alipoona pametokea nafuu, akaushupaza moyo wake na hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
16 Yahvé dit à Moïse: « Dis à Aaron: « Étends ta verge, et frappe la poussière de la terre, afin qu'elle devienne des poux dans tout le pays d'Égypte. »
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha fimbo yako uyapige mavumbi ya ardhi,’ nayo nchi yote ya Misri mavumbi yatakuwa viroboto.”
17 Ils firent ainsi. Aaron étendit sa main avec sa verge et frappa la poussière de la terre, et il y eut des poux sur l'homme et sur l'animal; toute la poussière de la terre devint des poux dans tout le pays d'Égypte.
Wakafanya hivyo, Aroni aliponyoosha mkono wake wenye fimbo na kuyapiga mavumbi ya nchi, viroboto wakawajia watu na wanyama. Mavumbi yote katika nchi ya Misri yakawa viroboto.
18 Les magiciens essayèrent avec leurs enchantements de produire des poux, mais ils ne purent pas. Il y avait des poux sur l'homme et sur l'animal.
Lakini waganga walipojaribu kutengeneza viroboto kwa siri ya uganga wao, hawakuweza. Nao viroboto walikuwa juu ya watu na wanyama.
19 Les magiciens dirent à Pharaon: « C'est le doigt de Dieu ». Mais le cœur de Pharaon s'endurcit et il ne les écouta pas, comme l'avait dit Yahvé.
Waganga wale wakamwambia Farao, “Hiki ni kidole cha Mungu.” Lakini moyo wa Farao ukawa mgumu naye hakuwasikiliza, kama vile Bwana alivyosema.
20 Yahvé dit à Moïse: « Lève-toi de bon matin, et tiens-toi devant Pharaon; voici qu'il sort pour aller à l'eau; dis-lui: « Voici ce que dit Yahvé: laisse aller mon peuple, afin qu'il me serve ».
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi na usimame mbele ya Farao wakati anapokwenda mtoni nawe umwambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
21 Sinon, si tu ne laisses pas aller mon peuple, voici que j'enverrai des nuées de mouches sur toi, sur tes serviteurs, sur ton peuple, et dans tes maisons. Les maisons des Égyptiens seront pleines de mouches, et le sol sur lequel elles reposent sera aussi plein de mouches.
Kama hutawaachia watu wangu waondoke nitakupelekea makundi ya mainzi juu yako, kwa maafisa wako, kwa watu wako na kwenye nyumba zenu. Nyumba za Wamisri zitajazwa mainzi, hata na ardhi yote ya Misri.
22 En ce jour-là, je mettrai à part le pays de Gosen, où habite mon peuple, pour qu'il n'y ait pas d'essaims de mouches, afin que vous sachiez que je suis Yahvé sur la terre.
“‘Lakini siku ile nitafanya kitu tofauti katika nchi ya Gosheni, ambapo watu wangu wanaishi, hapatakuwepo na makundi ya mainzi, ili mpate kujua kwamba Mimi, Bwana, niko katika nchi hii.
23 Je mettrai une séparation entre mon peuple et ton peuple. Ce signe arrivera d'ici demain. »'"
Nitaweka tofauti kati ya watu wangu na watu wenu. Ishara hii ya ajabu itatokea kesho.’”
24 Yahvé fit ainsi. Il y eut des nuées de mouches dans la maison de Pharaon et dans les maisons de ses serviteurs. Dans tout le pays d'Égypte, la terre se corrompit à cause des nuées de mouches.
Naye Bwana akafanya hivyo. Makundi makubwa ya mainzi yalimiminika katika jumba la kifalme la Farao na katika nyumba za maafisa wake, pia nchi yote ya Misri ikaharibiwa na mainzi.
25 Pharaon appela Moïse et Aaron, et dit: « Allez, sacrifiez à votre Dieu dans le pays. »
Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kuwaambia, “Nendeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu katika nchi hii.”
26 Moïse répondit: « Il n'est pas convenable d'agir ainsi, car nous allons sacrifier l'abomination des Égyptiens à Yahvé notre Dieu. Si nous sacrifions l'abomination des Égyptiens sous leurs yeux, ne nous lapideront-ils pas?
Lakini Mose akamwambia, “Hilo halitakuwa sawa. Dhabihu tutakazomtolea Bwana Mungu wetu zitakuwa chukizo kwa Wamisri. Kama tukitoa dhabihu ambazo ni chukizo mbele yao, je, hawatatupiga mawe?
27 Nous ferons trois jours de marche dans le désert, et nous sacrifierons à Yahvé notre Dieu, comme il nous l'ordonnera. »
Ni lazima twende mwendo wa siku tatu mpaka tufike jangwani ili tumtolee Bwana Mungu wetu dhabihu, kama alivyotuagiza.”
28 Pharaon dit: « Je te laisserai partir pour que tu sacrifies à Yahvé ton Dieu dans le désert, mais tu n'iras pas très loin. Prie pour moi. »
Farao akamwambia, “Nitawaruhusu mwende kumtolea Bwana Mungu wenu dhabihu huko jangwani, lakini hamna ruhusa kwenda mbali sana. Sasa mniombee.”
29 Moïse dit: « Voici, je m'en vais loin de vous. Demain, je prierai Yahvé pour que les mouches s'éloignent de Pharaon, de ses serviteurs et de son peuple; seulement, que Pharaon ne trompe plus le peuple en l'empêchant d'aller sacrifier à Yahvé. »
Mose akajibu, “Mara tu nitakapoondoka, nitamwomba Bwana na kesho mainzi yataondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake. Hakikisha tu kwamba Farao hatatenda kwa udanganyifu tena kwa kutokuwaachia watu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
30 Moïse sortit de chez Pharaon et pria Yahvé.
Ndipo Mose akamwacha Farao na kumwomba Bwana,
31 Yahvé fit selon la parole de Moïse, et il fit disparaître les mouches de Pharaon, de ses serviteurs et de son peuple. Il n'en resta pas une seule.
naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Mainzi yakaondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake, wala hakuna hata inzi aliyebakia.
32 Cette fois encore, Pharaon endurcit son cœur et ne laissa pas partir le peuple.
Lakini wakati huu pia Farao akaushupaza moyo wake, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.

< Exode 8 >