< Exode 16 >

1 Ils partirent d'Elim, et toute l'assemblée des enfants d'Israël arriva au désert de Sin, qui est entre Elim et Sinaï, le quinzième jour du second mois après leur sortie du pays d'Égypte.
Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka Elimu, wakafika Jangwa la Sini, lililokuwa kati ya Elimu na Sinai, siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili baada ya kutoka Misri.
2 Toute l'assemblée des enfants d'Israël murmura contre Moïse et Aaron dans le désert;
Huko jangwani hiyo jumuiya yote wakawanungʼunikia Mose na Aroni.
3 et les enfants d'Israël leur dirent: « Nous aurions voulu mourir par la main de Yahvé dans le pays d'Égypte, quand nous étions assis près des marmites à viande, quand nous mangions du pain à satiété, car vous nous avez fait sortir dans ce désert pour tuer toute cette assemblée par la faim. »
Waisraeli wakawaambia, “Laiti tungelikufa kwa mkono wa Bwana huko Misri! Huko tuliketi tukizunguka masufuria ya nyama na tukala vyakula tulivyovitaka, lakini ninyi mmetuleta huku jangwani ili mpate kuua mkutano huu wote kwa njaa.”
4 Yahvé dit à Moïse: « Voici, je ferai pleuvoir pour vous du pain du ciel, et le peuple sortira et ramassera chaque jour une portion d'un jour, afin de l'éprouver pour savoir s'il marchera ou non dans ma loi.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nitanyesha mikate kutoka mbinguni kwa ajili yenu. Watu watatoka kila siku na kukusanya kitakachowatosha kwa siku ile, kwa njia hii, nitawajaribu nione kama watafuata maelekezo yangu.
5 Le sixième jour, ils prépareront ce qu'ils auront apporté, et ce sera le double de ce qu'ils auront ramassé chaque jour. »
Siku ya sita watatayarisha kile waletacho ndani, nacho kitakuwa mara mbili kuliko ya kile walichokusanya kila siku.”
6 Moïse et Aaron dirent à tous les enfants d'Israël: « Le soir, vous saurez que Yahvé vous a fait sortir du pays d'Égypte.
Kwa hiyo Mose na Aroni wakawaambia Waisraeli wote, “Jioni mtajua kwamba Bwana ndiye aliwatoa Misri,
7 Au matin, vous verrez la gloire de l'Éternel, car il a entendu vos murmures contre l'Éternel. Qui sommes-nous, pour que vous murmuriez contre nous? »
kisha asubuhi mtauona utukufu wa Bwana, kwa sababu amesikia manungʼuniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani hata mtunungʼunikie?”
8 Moïse dit: « Maintenant, Yahvé vous donnera de la viande à manger le soir, et le matin du pain pour vous rassasier, parce que Yahvé entend les murmures que vous murmurez contre lui. Et nous, qui sommes-nous? Vos murmures ne sont pas contre nous, mais contre Yahvé. »
Pia Mose akasema, “Mtajua kuwa alikuwa Bwana wakati atakapowapa nyama mle ifikapo jioni na mikate yote mtakayohitaji asubuhi kwa sababu amesikia manungʼuniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani? Hamnungʼuniki dhidi yetu, bali dhidi ya Bwana.”
9 Moïse dit à Aaron: « Dis à toute l'assemblée des enfants d'Israël: « Approchez-vous de l'Éternel, car il a entendu vos murmures ».
Kisha Mose akamwambia Aroni, “Iambie jumuiya yote ya Waisraeli kwamba, ‘Mje mbele zake Bwana, kwa maana amesikia manungʼuniko yenu.’”
10 Comme Aaron parlait à toute l'assemblée des enfants d'Israël, ils regardèrent vers le désert, et voici que la gloire de Yahvé apparut dans la nuée.
Aroni alipokuwa akizungumza na jumuiya yote ya Waisraeli, wakatazama kuelekea jangwani, na huko wakaona utukufu wa Bwana ukitokeza katika wingu.
11 Yahvé parla à Moïse et dit:
Bwana akamwambia Mose,
12 « J'ai entendu les murmures des enfants d'Israël. Parle-leur en disant: « Le soir, vous mangerez de la viande, et le matin, vous serez rassasiés de pain. Alors vous saurez que je suis Yahvé votre Dieu ».
“Nimesikia manungʼuniko ya Waisraeli. Waambie, ‘Jioni mtakula nyama, na asubuhi mtashiba mikate. Ndipo mtajua ya kwamba Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.’”
13 Le soir, les cailles montèrent et couvrirent le camp; et le matin, la rosée s'étendit autour du camp.
Jioni ile kware wakaja wakaifunika kambi na asubuhi kulikuwa na tabaka la umande kuzunguka kambi.
14 Lorsque la rosée qui s'était déposée eut disparu, voici qu'il y avait à la surface du désert une petite chose ronde, aussi petite que le givre sur le sol.
Wakati umande ulipoondoka, vipande vidogo vidogo kama theluji vilionekana juu ya uso wa jangwa.
15 Lorsque les enfants d'Israël la virent, ils se dirent les uns aux autres: « Qu'est-ce que c'est? » Car ils ne savaient pas ce que c'était. Moïse leur dit: « C'est le pain que l'Éternel vous donne à manger.
Waisraeli walipoona, wakaambiana, “Hiki ni nini?” Kwa kuwa hawakujua kilikuwa kitu gani. Mose akawaambia, “Huu ndio mkate ambao Bwana amewapa mle.
16 Voici ce que l'Éternel a ordonné: « Recueillez-en chacun selon ce qu'il mange: un omer par tête, selon le nombre de vos personnes, vous en prendrez chacun pour ceux qui sont dans sa tente. »
Hivi ndivyo Bwana alivyoamuru: ‘Kila mmoja akusanye kiasi anachohitaji. Chukueni pishi moja kwa kila mtu mliye naye katika hema yenu.’”
17 Les enfants d'Israël firent ainsi; les uns en recueillirent davantage, les autres moins.
Waisraeli wakafanya kama walivyoambiwa, baadhi yao wakakusanya zaidi, wengine pungufu.
18 Quand ils mesurèrent avec un omer, celui qui avait beaucoup ramassé ne manqua de rien, et celui qui avait peu ramassé ne manqua de rien. Chacun ramassait selon ce qu'il mangeait.
Nao walipopima katika pishi, yule aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, wala aliyekusanya kidogo hakupungukiwa. Kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji.
19 Moïse leur dit: « Que personne n'en laisse jusqu'au matin. »
Kisha Mose akawaambia, “Mtu yeyote asibakize chochote mpaka asubuhi.”
20 Mais ils n'écoutèrent pas Moïse, et quelques-uns d'entre eux en laissèrent jusqu'au matin, de sorte qu'il y eut des vers et que le produit devint fétide; Moïse fut irrité contre eux.
Hata hivyo, wengine hawakuzingatia aliyosema Mose, wakahifadhi kiasi fulani mpaka asubuhi, lakini kile alichohifadhi kikajaa mabuu na kuanza kunuka. Kwa hiyo Mose akawakasirikia.
21 Ils le ramassèrent matin par matin, chacun selon sa consommation. Lorsque le soleil se mit à chauffer, elle fondit.
Kila asubuhi, kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji na jua lilipokuwa kali, iliyeyuka.
22 Le sixième jour, ils ramassèrent deux fois plus de pain, deux omers pour chacun. Tous les chefs de l'assemblée vinrent en parler à Moïse.
Siku ya sita, wakakusanya mara mbili, kiasi cha pishi mbili kwa kila mtu, nao viongozi wa jumuiya wakaja kumwarifu Mose.
23 Celui-ci leur dit: « Voici ce qu'a dit l'Éternel: Demain est un repos solennel, un sabbat consacré à l'Éternel. Faites cuire ce que vous voulez faire cuire, faites bouillir ce que vous voulez faire bouillir, et tout ce qui restera vous sera réservé pour être gardé jusqu'au matin.
Mose akawaambia, “Hivi ndivyo alivyoagiza Bwana: ‘Kesho itakuwa siku ya mapumziko, Sabato takatifu kwa Bwana. Kwa hiyo okeni kile mnachotaka kuoka na mchemshe kile mnachotaka kuchemsha. Hifadhini chochote kinachobaki na mkiweke mpaka asubuhi.’”
24 Ils le conservèrent jusqu'au matin, comme Moïse l'avait ordonné, et il ne devint pas infecte, et il n'y avait pas de vers dedans.
Kwa hiyo wakavihifadhi mpaka asubuhi, kama Mose alivyoagiza, na havikunuka wala kuwa na mabuu.
25 Moïse dit: « Mangez-en aujourd'hui, car aujourd'hui est un jour de sabbat pour l'Éternel. Aujourd'hui, vous ne la trouverez pas dans les champs.
Mose akawaambia, “Kuleni leo, kwa sababu leo ni Sabato kwa Bwana. Hamtapata chochote juu ya nchi leo.
26 Pendant six jours, vous le ramasserez, mais le septième jour est le sabbat. Il n'y en aura point. »
Kwa siku sita mtakusanya, lakini siku ya saba, yaani Sabato, hakutakuwepo chochote.”
27 Le septième jour, une partie du peuple sortit pour ramasser, mais ils ne trouvèrent rien.
Hata hivyo, baadhi ya watu wakatoka kwenda kukusanya siku ya saba, lakini hawakupata chochote.
28 Yahvé dit à Moïse: « Jusques à quand refuserez-vous d'observer mes commandements et mes lois?
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Je, mtaacha kushika maagizo na maelekezo yangu mpaka lini?
29 Voici, parce que Yahvé vous a donné le sabbat, il vous donne le sixième jour le pain de deux jours. Que chacun reste à sa place. Que personne ne sorte de sa place le septième jour. »
Fahamuni kuwa Bwana amewapa ninyi Sabato, ndiyo sababu katika siku ya sita amewapa mikate ya siku mbili. Kila mmoja inampasa kukaa pale alipo katika siku ya saba. Hata mmoja haruhusiwi kutoka.”
30 Le peuple se reposa donc le septième jour.
Kwa hiyo watu wakapumzika siku ya saba.
31 La maison d'Israël l'appela « Manne ». Elle était semblable à de la graine de coriandre, de couleur blanche, et son goût était semblable à celui des galettes au miel.
Watu wa Israeli wakaita ile mikate mana Ilikuwa myeupe kama mbegu za mtama na ladha yake ilikuwa kama mkate mwembamba uliotengenezwa kwa asali.
32 Moïse dit: « Voici ce que Yahvé a ordonné: qu'on en garde un omer plein pour vos descendants, afin qu'ils voient le pain dont je vous ai nourris dans le désert, quand je vous ai fait sortir du pays d'Égypte ».
Mose akasema, “Hivi ndivyo alivyoagiza Bwana: ‘Chukueni pishi ya mana na kuhifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo ili vione mikate niliyowapa mle jangwani nilipowatoa katika nchi ya Misri.’”
33 Moïse dit à Aaron: « Prends un pot, mets-y un omer plein de manne et dépose-le devant l'Éternel, pour qu'il soit conservé par vos générations. »
Kwa hiyo Mose akamwambia Aroni, “Chukua gudulia na uweke pishi moja ya mana ndani yake. Kisha uweke mbele za Bwana ili kihifadhiwe kwa ajili ya vizazi vijavyo.”
34 Comme l'Éternel l'avait ordonné à Moïse, Aaron la déposa devant le Témoignage, pour qu'elle soit conservée.
Kama Bwana alivyomwagiza Mose, hatimaye Aroni alikuja kuihifadhi ndani ya Sanduku la Ushuhuda.
35 Les enfants d'Israël mangèrent la manne pendant quarante ans, jusqu'à leur arrivée dans un pays habité. Ils mangèrent la manne jusqu'à ce qu'ils arrivent aux frontières du pays de Canaan.
Waisraeli wakala mana kwa miaka arobaini, mpaka walipofika katika nchi iliyokaliwa na watu; walikula mana hadi walipofika mpakani mwa Kanaani.
36 Or, un omer, c'est le dixième d'un épha.
(Pishi moja ni sehemu ya kumi ya kipimo cha efa.)

< Exode 16 >