< Deutéronome 16 >

1 Observe le mois d'Abib et célèbre la Pâque en l'honneur de Yahvé ton Dieu, car c'est au mois d'Abib que Yahvé ton Dieu t'a fait sortir d'Égypte de nuit.
Shikeni mwezi wa Abibu, na kuiadhimisha Pasaka ya Bwana Mungu wenu, kwa sababu katika mwezi wa Abibu, Mungu aliwatoa Misri usiku.
2 Tu sacrifieras la Pâque à l'Éternel, ton Dieu, du menu et du gros bétail, dans le lieu que l'Éternel choisira pour y faire résider son nom.
Mtatoa dhabihu ya Pasaka ya mnyama kwa Bwana Mungu wenu kutoka kundi lenu la mbuzi na kondoo au la ngʼombe, mahali pale ambapo Bwana atapachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake.
3 Tu ne mangeras pas de pain levé avec elle. Tu mangeras avec lui des pains sans levain pendant sept jours, des pains d'affliction (car tu es sorti du pays d'Égypte en hâte), afin de te souvenir du jour où tu es sorti du pays d'Égypte, tous les jours de ta vie.
Msile nyama hiyo pamoja na mikate iliyotiwa chachu, lakini kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, mikate ya kujitesa, kwa sababu mliondoka Misri kwa haraka, ili kwamba siku zote za maisha yenu mpate kukumbuka wakati wenu wa kuondoka Misri.
4 Il n'y aura pas de levure avec vous dans tout votre territoire pendant sept jours; et aucune des viandes que vous sacrifierez le premier jour, le soir, ne restera toute la nuit jusqu'au matin.
Chachu isionekane katika mali zenu katika nchi yenu yote kwa siku saba. Nyama yoyote ya dhabihu mtakayotoa jioni ya siku ya kwanza isibakizwe mpaka asubuhi.
5 Tu ne sacrifieras pas la Pâque dans l'une des portes que l'Éternel, ton Dieu, te donne;
Kamwe msitoe dhabihu ya Pasaka katika mji wowote ambao Bwana Mungu wenu amewapa,
6 mais au lieu que l'Éternel, ton Dieu, choisira pour y faire résider son nom, là tu sacrifieras la Pâque le soir, au coucher du soleil, à l'époque où tu es sorti d'Égypte.
isipokuwa mahali atakapopachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake. Hapo ndipo lazima mtoe dhabihu ya Pasaka jioni, jua litakapotua, iwe kumbukumbu yenu ya kutoka Misri.
7 Tu la feras rôtir et tu la mangeras dans le lieu que choisira Yahvé ton Dieu. Le matin, tu retourneras dans tes tentes.
Okeni na mle mahali pale ambapo Bwana Mungu wenu atakapopachagua, kisha asubuhi mrudi kwenye mahema yenu.
8 Pendant six jours, tu mangeras des pains sans levain. Le septième jour, il y aura une assemblée solennelle en l'honneur de Yahvé, ton Dieu. Tu ne feras aucun travail.
Kwa siku sita mtakula mikate isiyotiwa chachu na siku ya saba fanyeni kusanyiko kwa ajili ya Bwana Mungu wenu na msifanye kazi.
9 Vous compterez pour vous-mêmes sept semaines. A partir du moment où vous commencerez à mettre la faucille sur le grain sur pied, vous commencerez à compter sept semaines.
Mhesabu majuma saba tangu wakati mnapoanza kuchukua mundu kuvuna nafaka.
10 Vous célébrerez la fête des semaines devant l'Éternel, votre Dieu, avec le tribut d'une offrande volontaire de votre main, que vous donnerez selon la manière dont l'Éternel, votre Dieu, vous bénira.
Kisha msherehekee Sikukuu ya Majuma kwa Bwana Mungu wenu kwa kutoa sadaka ya hiari kwa kadiri ya baraka ambayo Bwana Mungu wenu amewapa.
11 Tu te réjouiras devant l'Éternel, ton Dieu, toi, ton fils, ta fille, ton serviteur, ta servante, le Lévite qui est dans tes portes, l'étranger, l'orphelin et la veuve qui sont parmi toi, dans le lieu que l'Éternel, ton Dieu, choisira pour y faire résider son nom.
Shangilieni mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua kama makao ya Jina lake, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi walio katika miji yenu, na wageni, yatima na wajane waishio miongoni mwenu.
12 Tu te souviendras que tu as été esclave en Égypte. Tu observeras et tu mettras en pratique ces lois.
Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa kule Misri na mfuate amri hizi kwa uangalifu.
13 Tu célébreras la fête des cabanes pendant sept jours, après avoir ramassé ce qui vient de ton aire et de ta cuve.
Adhimisheni sikukuu ya vibanda kwa siku saba baada ya kukusanya mazao yenu ya nafaka na kukamua zabibu.
14 Tu te réjouiras de ta fête, toi, ton fils, ta fille, ton serviteur, ta servante, le lévite, l'étranger, l'orphelin et la veuve qui sont dans tes portes.
Mfurahie sikukuu yenu, ninyi, wana wenu, binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi, wageni, yatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.
15 Tu feras une fête à l'Éternel, ton Dieu, pendant sept jours, dans le lieu que l'Éternel choisira, car l'Éternel, ton Dieu, te bénira dans tout ton produit et dans tout le travail de tes mains, et tu seras tout entier dans la joie.
Kwa siku saba mtaiadhimisha sikukuu ya Bwana Mungu wenu katika mahali atakapopachagua Bwana. Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki katika mavuno yenu na katika kazi zote za mikono yenu na furaha yenu itakamilika.
16 Trois fois par an, tous tes mâles se présenteront devant l'Éternel, ton Dieu, dans le lieu qu'il choisira: à la fête des pains sans levain, à la fête des semaines et à la fête des kiosques. Ils ne se présenteront pas devant l'Éternel à vide.
Wanaume wenu wote lazima wajitokeze mara tatu kwa mwaka mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua: kwa ajili ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma, na Sikukuu ya Vibanda. Hakuna mtu atakayejitokeza mbele za Bwana mikono mitupu:
17 Chacun donnera selon ses moyens, en fonction de la bénédiction que l'Éternel, ton Dieu, t'a accordée.
Kila mmoja wenu ni lazima alete zawadi kulingana na jinsi ambavyo Bwana Mungu wenu alivyowabariki.
18 Tu établiras des juges et des officiers dans toutes tes portes, celles que l'Éternel, ton Dieu, te donne, selon tes tribus, et ils jugeront le peuple avec droiture.
Wateue waamuzi na maafisa kwa kila kabila lenu katika kila mji ambao Bwana Mungu wenu anawapa, nao watawaamua watu kwa usawa.
19 Tu ne pervertiras pas la justice. Tu ne feras pas preuve de partialité. Tu ne prendras pas de pot-de-vin, car le pot-de-vin aveugle les yeux des sages et pervertit les paroles des justes.
Msipotoshe haki wala msifanye upendeleo. Msikubali rushwa kwa sababu rushwa hupofusha macho ya wenye busara na kugeuza maneno ya wenye haki.
20 Tu suivras ce qui est tout à fait juste, afin de vivre et d'hériter du pays que l'Éternel, ton Dieu, te donne.
Mfuate haki na haki peke yake, ili mweze kuishi na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa.
21 Tu ne planteras pas d'ashère d'un arbre quelconque à côté de l'autel de Yahvé ton Dieu, que tu te feras toi-même.
Msisimamishe nguzo yoyote ya Ashera kando ya madhabahu mliyomjengea Bwana Mungu wenu,
22 Tu ne te dresseras pas non plus une pierre sacrée que Yahvé ton Dieu déteste.
wala msisimamishe jiwe la kuabudu, kwa maana Bwana Mungu wenu anavichukia vitu hivi.

< Deutéronome 16 >