< Daniel 3 >

1 Le roi Nebucadnetsar fit une statue d'or, dont la hauteur était de soixante coudées et la largeur de six coudées. Il la dressa dans la plaine de Dura, dans la province de Babylone.
Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya dhahabu, yenye kimo cha dhiraa sitini, na upana wa dhiraa sita, akaisimamisha kwenye tambarare ya Dura katika jimbo la nchi ya Babeli.
2 Et le roi Nebucadnetsar envoya rassembler les gouverneurs locaux, les adjoints, les gouverneurs, les juges, les trésoriers, les conseillers, les shérifs, et tous les chefs des provinces, pour qu'ils viennent à la dédicace de la statue que le roi Nebucadnetsar avait dressée.
Kisha mfalme akaita wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wote wa jimbo kuja kuizindua sanamu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
3 Et les gouverneurs locaux, les adjoints, les gouverneurs, les juges, les trésoriers, les conseillers, les shérifs et tous les chefs des provinces se rassemblèrent pour la dédicace de la statue que le roi Nebucadnetsar avait dressée, et ils se tinrent devant la statue que Nebucadnetsar avait dressée.
Basi wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wa jimbo walikusanyika ili kuizindua sanamu ile Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha, nao wakasimama mbele ya hiyo sanamu.
4 Alors le héraut cria à haute voix: « A vous, peuples, nations et langues, il est ordonné
Ndipo mpiga mbiu akatangaza kwa sauti kubwa, “Enyi watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha, hili ndilo mnaloamriwa kulifanya:
5 que, chaque fois que vous entendrez le son du cor, de la flûte, de la cithare, de la lyre, de la harpe, du chalumeau, et de toutes sortes de musiques, vous vous prosterniez et vous adoriez la statue d'or que le roi Nebucadnetsar a dressée.
Mara mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za sauti za ala za uimbaji, lazima mwanguke chini na kuabudu sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza ameisimamisha.
6 Celui qui ne se prosternera pas et n'adorera pas sera jeté à l'heure même au milieu d'une fournaise ardente. »
Mtu yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu sanamu hiyo, atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.”
7 En ce temps-là, quand tous les peuples entendirent le son du cor, de la flûte, de la cithare, de la lyre, de la harpe, du chalumeau et de toutes sortes de musiques, tous les peuples, les nations et les langues se prosternèrent et adorèrent la statue d'or que le roi Nebucadnetsar avait dressée.
Kwa hiyo, mara waliposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda na aina zote za ala za uimbaji, watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha wakaanguka chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
8 En ce temps-là, des Chaldéens s'approchèrent et portèrent plainte contre les Juifs.
Wakati huo baadhi ya Wakaldayo walijitokeza na kuwashtaki Wayahudi.
9 Ils prirent la parole devant le roi Nebucadnetsar: « O roi, vis éternellement!
Wakamwambia Mfalme Nebukadneza, “Ee mfalme, uishi milele!
10 Toi, ô roi, tu as donné l'ordre que tout homme qui entendra le son du cor, de la flûte, de la cithare, de la lyre, de la harpe, du chalumeau, et de toutes sortes de musiques, se prosternera et adorera la statue d'or;
Ee mfalme, umetoa amri kwamba kila mmoja atakayesikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda, zumari na aina zote za ala za uimbaji lazima aanguke chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu,
11 et quiconque ne se prosternera pas et n'adorera pas sera jeté au milieu d'une fournaise ardente.
na kwamba yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.
12 Il y a quelques Juifs que tu as nommés responsables des affaires de la province de Babylone: Shadrach, Meshach et Abednego. Ces hommes, ô roi, ne t'ont pas respecté. Ils ne servent pas tes dieux et n'adorent pas la statue d'or que tu as dressée. »
Lakini wako baadhi ya Wayahudi ambao umewaweka juu ya mambo ya jimbo la Babeli: yaani, Shadraki, Meshaki na Abednego, ambao hawakujali wewe, ee mfalme. Hawaitumikii miungu yako wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
13 Alors Nebucadnetsar, dans sa rage et sa fureur, ordonna qu'on amène Shadrac, Méschac et Abed-Nego. Ces hommes furent donc amenés devant le roi.
Mfalme Nebukadneza, akiwa amekasirika na mwenye ghadhabu kali, akawaita Shadraki, Meshaki na Abednego. Hivyo watu hawa wakaletwa mbele ya mfalme,
14 Nebucadnetsar leur répondit: « Est-il vrai, Schadrac, Méschac et Abed-Nego, que vous ne servez pas mes dieux et que vous n'adorez pas la statue d'or que j'ai dressée?
naye Nebukadneza akawauliza, “Je, ni kweli kwamba ninyi Shadraki, Meshaki na Abednego hamuitumikii miungu yangu wala kuiabudu sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
15 Maintenant, si vous êtes prêts, dès que vous entendez le son du cor, de la flûte, de la cithare, de la lyre, de la harpe, du chalumeau et de toutes sortes de musiques, à vous prosterner et à adorer la statue que j'ai faite, tant mieux; mais si vous n'adorez pas, vous serez jetés à l'heure même au milieu d'une fournaise ardente. Quel est ce dieu qui vous délivrera de mes mains? »
Basi wakati mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za ala za uimbaji, kama mtakuwa tayari kusujudu na kuiabudu hiyo sanamu niliyoitengeneza, vyema sana. Lakini kama hamtaiabudu, mtatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto. Naye ni mungu yupi atakayeweza kuwaokoa ninyi, kutoka mkono wangu?”
16 Schadrac, Méschac et Abed-Nego répondirent au roi: « Nebucadnetsar, nous n'avons pas à te répondre dans cette affaire.
Shadraki, Meshaki na Abednego wakamjibu mfalme, “Ee Nebukadneza, hatuhitaji kujitetea mbele zako kuhusu jambo hili.
17 S'il arrive quelque chose, notre Dieu que nous servons peut nous délivrer de la fournaise ardente, et il nous délivrera de ta main, ô roi.
Ikiwa tutatupwa ndani ya tanuru iwakayo moto, Mungu tunayemtumikia anaweza kutuokoa na moto, naye atatuokoa kutoka mkononi mwako, ee mfalme.
18 Mais si cela n'arrive pas, que l'on sache, ô roi, que nous ne servirons pas tes dieux et que nous n'adorerons pas la statue d'or que tu as dressée. »
Lakini hata ikiwa hatatuokoa, ee mfalme, tunataka ufahamu kwamba, hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
19 Alors Nebucadnetsar fut plein de fureur, et sa physionomie se modifia contre Schadrac, Méschac et Abed-Nego. Il prit la parole et ordonna qu'on chauffe la fournaise sept fois plus qu'elle ne l'était habituellement.
Ndipo Nebukadneza akawa na ghadhabu kali sana kwa Shadraki, Meshaki na Abednego, nayo nia yake ikabadilika kwao. Akaagiza tanuru ichochewe moto mara saba kuliko kawaida yake
20 Il donna l'ordre à des hommes puissants qui faisaient partie de son armée de lier Schadrac, Méschac et Abed-Nego, et de les jeter dans la fournaise ardente.
na kuwaamuru baadhi ya askari wake wenye nguvu zaidi katika jeshi lake kuwafunga Shadraki, Meshaki na Abednego na kuwatupa ndani ya tanuru iwakayo moto.
21 Ces hommes furent liés par leurs pantalons, leurs tuniques, leurs manteaux et leurs autres vêtements, et ils furent jetés au milieu de la fournaise ardente.
Hivyo watu hawa, walifungwa na kutupwa ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamevaa majoho yao, suruali, vilemba na nguo zao nyingine.
22 Comme l'ordre du roi était pressant et que la fournaise était extrêmement chaude, la flamme du feu tua les hommes qui portaient Shadrac, Méschac et Abed-Nego.
Amri ya mfalme ilikuwa ya haraka sana na tanuru ilikuwa na moto mkali kiasi kwamba miali ya moto iliwaua wale askari waliowapeleka Shadraki, Meshaki na Abednego.
23 Ces trois hommes, Schadrac, Méschac et Abed-Nego, tombèrent liés au milieu de la fournaise ardente.
Watu hawa watatu walianguka ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamefungwa kwa uthabiti sana.
24 Alors le roi Nebucadnetsar fut étonné et se leva en hâte. Il prit la parole et dit à ses conseillers: « N'avons-nous pas jeté au milieu du feu trois hommes liés? » Ils ont répondu au roi: « C'est vrai, ô roi. »
Ndipo Mfalme Nebukadneza akashangaa, akainuka kwa haraka na kuwauliza washauri wake, “Je, hawakuwa watu watatu ambao tuliwafunga na kuwatupa ndani ya moto?” Washauri wakajibu, “Hakika, ee mfalme.”
25 Il répondit: « Regarde, je vois quatre hommes libres, marchant au milieu du feu, et ils sont indemnes. L'apparence du quatrième est comme un fils des dieux. "
Mfalme akasema, “Tazama! Naona watu wanne wakitembeatembea ndani ya moto, hawajafungwa wala kudhurika, naye mtu yule wa nne anaonekana kama mwana wa miungu.”
26 Alors Nebucadnetsar s'approcha de l'entrée de la fournaise ardente. Il prit la parole et dit: « Schadrac, Méschac et Abed-Nego, serviteurs du Dieu Très-Haut, sortez, et venez ici! » Alors Schadrac, Méschac et Abed-Nego sortirent du milieu du feu.
Ndipo Nebukadneza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iwakayo moto na kupaza sauti, “Shadraki, Meshaki na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, tokeni! Njooni hapa!” Ndipo Shadraki, Meshaki na Abednego wakatoka ndani ya moto.
27 Les gouverneurs locaux, les députés, les gouverneurs et les conseillers du roi, étant réunis, virent ces hommes, et le feu n'avait aucun pouvoir sur leurs corps. Les cheveux de leur tête n'étaient pas roussis. Leurs pantalons n'étaient pas changés. L'odeur du feu n'était même pas sur eux.
Nao maliwali, wasimamizi, watawala na washauri wa mfalme wakakusanyika kuwazunguka. Waliona kwamba moto haukudhuru miili yao, wala unywele wa vichwa vyao haukuungua, majoho yao hayakuungua, wala hapakuwepo na harufu ya moto kwenye miili yao.
28 Nebucadnetsar prit la parole et dit: Béni soit le Dieu de Schadrac, de Méschac et d'Abed-Nego, qui a envoyé son ange et délivré ses serviteurs qui se sont confiés en lui, qui ont changé la parole du roi et qui ont livré leur corps, afin qu'ils ne servent ni n'adorent aucun autre dieu que leur propre Dieu.
Ndipo Nebukadneza akasema, “Ahimidiwe Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego, ambaye amemtuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake. Walimtumaini na kukaidi amri ya mfalme, nao wakawa tayari kufa kuliko kutumikia au kuabudu mungu mwingine yeyote isipokuwa Mungu wao.
29 C'est pourquoi je décrète que tous les peuples, toutes les nations et toutes les langues qui diront du mal du Dieu de Schadrac, de Méschac et d'Abed-Nego seront taillés en pièces, et que leurs maisons seront réduites en tas de fumier, parce qu'il n'y a pas d'autre dieu qui soit capable de délivrer ainsi. »
Kwa hiyo ninaamuru kwamba watu wa taifa lolote au lugha yoyote watakaosema kitu chochote dhidi ya Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego wakatwe vipande vipande na nyumba zao zifanywe kuwa malundo ya kokoto, kwa maana hakuna mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.”
30 Alors le roi promut Shadrac, Méschac et Abed-Nego dans la province de Babylone.
Kisha mfalme akawapandisha vyeo Shadraki, Meshaki na Abednego katika jimbo la Babeli.

< Daniel 3 >