< Colossiens 1 >

1 Paul, apôtre de Jésus-Christ par la volonté de Dieu, et Timothée, notre frère,
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo,
2 aux saints et fidèles frères en Christ qui sont à Colosses: Grâce et paix à vous de la part de Dieu notre Père et du Seigneur Jésus-Christ.
tunawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Kolosai, ndugu zetu waaminifu katika kuungana na Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
3 Nous rendons grâces à Dieu, le Père de notre Seigneur Jésus-Christ, en priant toujours pour vous,
Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.
4 ayant entendu parler de votre foi en Jésus-Christ et de l'amour que vous avez pour tous les saints,
Maana tumesikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na juu ya upendo wenu kwa watu wote wa Mungu.
5 à cause de l'espérance qui vous est réservée dans les cieux, et dont vous avez entendu parler auparavant dans la parole de vérité de la Bonne Nouvelle
Wakati ujumbe ule wa kweli, yaani Habari Njema, ilipowafikieni kwa mara ya kwanza, mlipata kusikia juu ya lile tumaini linalopatikana kwake. Kwa sababu hiyo imani na upendo wenu vinategemea jambo lile mnalotumainia ambalo mmewekewa salama mbinguni.
6 qui vous est parvenue, comme elle est dans le monde entier, et qu'elle porte du fruit et croît, comme elle croît aussi en vous, depuis le jour où vous avez entendu et connu la grâce de Dieu dans la vérité,
Habari Njema inazidi kuzaa matunda na kuenea ulimwenguni kote kama vile ilivyofanya kwenu ninyi tangu siku ile mliposikia juu ya neema ya Mungu na kuitambua ilivyo kweli.
7 ainsi que vous l'avez appris d'Épaphras, notre bien-aimé compagnon de service, fidèle serviteur de Christ en votre faveur,
Mlijifunza juu ya neema ya Mungu kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu, ambaye ni mfanyakazi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
8 qui nous a aussi déclaré votre amour dans l'Esprit.
Yeye alitupa habari za upendo wenu mliojaliwa na Roho.
9 C'est pourquoi, nous aussi, depuis le jour où nous l'avons appris, nous ne cessons de prier et de demander pour vous, afin que vous soyez remplis de la connaissance de sa volonté en toute sagesse et intelligence spirituelles,
Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa mapenzi yake, awajazeni hekima yote na elimu iletwayo na Roho wake.
10 afin que vous marchiez d'une manière digne du Seigneur, pour lui plaire à tous égards, portant du fruit en toute bonne œuvre et croissant dans la connaissance de Dieu,
Hapo mtaweza kuishi kama anavyotaka Bwana na kutenda daima yanayompendeza. Maisha yenu yatakuwa yenye matunda ya kila namna ya matendo mema na mtazidi kukua katika kumjua Mungu.
11 fortifiés de toute puissance, selon la puissance de sa gloire, pour toute endurance et persévérance dans la joie,
Mungu awajalieni nguvu kwa uwezo wake mtukufu ili mweze kustahimili kila kitu kwa uvumilivu.
12 en rendant grâces au Père, qui nous a rendus aptes à participer à l'héritage des saints dans la lumière,
Na kwa furaha, mshukuruni Baba aliyewawezesha ninyi kuwa na sehemu yenu katika mambo yale Mungu aliyowawekea watu wake katika utawala wa mwanga.
13 qui nous a délivrés de la puissance des ténèbres et nous a transportés dans le royaume du Fils de son amour,
Yeye alituokoa katika nguvu ya giza, akatuleta salama katika ufalme wa Mwanae mpenzi,
14 en qui nous avons notre rédemption, le pardon de nos péchés.
ambaye kwa njia yake tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa.
15 Il est l'image du Dieu invisible, le premier-né de toute la création.
Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 Car par lui tout a été créé dans les cieux et sur la terre, les choses visibles et les choses invisibles, qu'il s'agisse de trônes, de dominations, de principautés ou de pouvoirs. Toutes choses ont été créées par lui et pour lui.
Maana kwa njia yake vitu vyote viliumbwa duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala, wakuu na wenye mamlaka. Vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
17 Il est avant toutes choses, et toutes choses subsistent en lui.
Kristo alikuwako kabla ya vitu vyote; kwa kuungana naye, vyote vyadumu mahali pake.
18 Il est la tête du corps, de l'assemblée, lui qui est le commencement, le premier-né d'entre les morts, afin d'avoir en toutes choses la prééminence.
Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.
19 Car il a plu à toute la plénitude d'habiter en lui,
Maana Mungu alipenda utimilifu wote uwe ndani yake.
20 et de réconcilier par lui toutes choses avec lui-même, tant celles qui sont sur la terre que celles qui sont dans les cieux, ayant établi la paix par le sang de sa croix.
Kwa njia yake Mungu alivipatanisha naye vitu vyote naam, viumbe vyote mbinguni na duniania; alileta amani kwa damu ya Kristo msalabani.
21 Vous qui, autrefois, étiez aliénés et ennemis dans votre esprit par vos mauvaises actions,
Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.
22 il vous a maintenant réconciliés par la mort dans le corps de sa chair, afin de vous présenter saints, irréprochables et sans défaut devant lui,
Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.
23 si du moins vous persévérez dans la foi, fondés et inébranlables, sans vous détourner de l'espérance de la Bonne Nouvelle que vous avez entendue et qui est proclamée dans toute la création sous le ciel, dont moi, Paul, j'ai été fait serviteur.
Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.
24 Or, je me réjouis de mes souffrances à cause de vous, et je comble de mon côté ce qui manque aux souffrances de Christ dans ma chair, pour l'amour de son corps, qui est l'assemblée,
Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani, nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa.
25 dont j'ai été fait serviteur selon l'office de Dieu qui m'a été confié envers vous pour l'accomplissement de la parole de Dieu,
Nami nimefanywa kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na mpango wake Mungu ambao alinikabidhi kwa faida yenu. Mpango wenyewe ni kuutangaza kwa ukamilifu ujumbe wake,
26 mystère caché depuis des siècles et des générations. Mais maintenant il a été révélé à ses saints, (aiōn g165)
ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake. (aiōn g165)
27 à qui Dieu a voulu faire connaître quelle est la richesse de la gloire de ce mystère parmi les païens, qui est le Christ en vous, l'espérance de la gloire.
Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
28 Nous l'annonçons, en exhortant tout homme et en l'instruisant en toute sagesse, afin de rendre tout homme parfait en Jésus-Christ.
Kwa sababu hiyo tunamhubiri Kristo kwa watu wote; tunawaonya na kuwafundisha wote kwa hekima yote, ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekomaa katika kuungana na Kristo.
29 C'est à quoi je m'efforce, moi aussi, selon son opération qui agit puissamment en moi.
Kwa madhumuni hayo mimi nafanya kazi na kujitahidi nikiitumia nguvu kuu ya Kristo ifanyayo kazi ndani yangu.

< Colossiens 1 >