< Actes 8 >

1 Saul consentait à sa mort. Une grande persécution s'éleva contre l'assemblée qui était à Jérusalem en ce jour-là. Ils étaient tous dispersés dans les régions de la Judée et de la Samarie, à l'exception des apôtres.
Sauli alikuwa kwenye makubaliano ya kifo chake. siku hiyo ndipo alipoanza kuwatesa kinyume cha kanisa lililokuwa Yerusalemu; na waaminio wote waliotawanyika katika majimbo ya Yudea na Samaria, isipokuwa mitume.
2 Des hommes pieux enterrèrent Étienne et se lamentèrent sur son sort.
Watu wachamungu walimzika Stefano na kufanya maombolezo makubwa juu yake.
3 Mais Saul ravagea l'assemblée, entrant dans toutes les maisons et traînant hommes et femmes en prison.
Lakini Sauli alilidhuru sana kanisa. Alikwenda nyumba kwa nyumba na kuwaburuza nje wanawake na waume, na kuwatupia gerezani.
4 Ceux qui étaient dispersés allaient donc de lieu en lieu prêcher la parole.
waaminio ambao walikuwa wametawanyika bado walilihubiri neno.
5 Philippe descendit dans la ville de Samarie et leur annonça le Christ.
Filipo akashuka katika mji wa Samaria na akamtangaza Kristo huko.
6 La foule écoutait d'un commun accord les paroles de Philippe, lorsqu'elle entendait et voyait les miracles qu'il faisait.
Baada ya makutano kusikia na kuona ishara alizofanya Filipo; wakaweka umakini juu ya kile alichosema.
7 Car des esprits impurs sortirent de plusieurs de ceux qui en avaient. Ils sortaient en criant d'une voix forte. Beaucoup de paralysés et de boiteux furent guéris.
Kutoka hapo watu wengi waliosikia, pepo wachafu waliwatoka watu huku wakilia kwa sauti kubwa, na wengi waliopooza na viwete waliponywa.
8 Il y eut une grande joie dans cette ville.
Na kulikuwa na furaha kubwa katika mji.
9 Or, il y avait dans la ville un homme, nommé Simon, qui avait l'habitude de pratiquer la sorcellerie et d'étonner les habitants de Samarie, se faisant passer pour un grand,
Lakini palikuwa na mtu mmoja katika mji ule jina lake Simon, ambaye alikuwa akifanya uchawi; ambao aliutumia kuwashangaza watu wa taifa la Samaria, wakati akisema kuwa yeye ni mtu wa muhimu.
10 et que tous écoutaient, du plus petit au plus grand, en disant: « Cet homme est la grande puissance de Dieu. »
Wasamaria wote tangu mdogo hata mkubwa, wakamsikiliza; wakasema;”mtu huyu ni ile nguvu ya Mungu ambayo ni kuu.”
11 Ils l'écoutaient, parce que depuis longtemps il les avait étonnés par ses sortilèges.
Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mrefu kwa uchawi wake.
12 Mais lorsqu'ils crurent que Philippe annonçait la bonne nouvelle du royaume de Dieu et du nom de Jésus-Christ, ils furent baptisés, hommes et femmes.
Lakini wakati walipoamini kuwa Filipo alihubiri juu ya ufalme wa Mungu na juu ya jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanaume kwa wanawake.
13 Simon lui-même crut aussi. Après avoir été baptisé, il poursuivit sa route avec Philippe. Voyant des signes et de grands miracles se produire, il était stupéfait.
Na Simoni mwenyewe aliamini: baada ya kubatizwa, aliendelea kuwa na Filipo; alipoona ishara na miujiza iliyokuwa ikitendeka, alishangaa.
14 Les apôtres qui étaient à Jérusalem, ayant appris que la Samarie avait reçu la parole de Dieu, y envoyèrent Pierre et Jean.
Wakati mitume wa Yerusalemu waliposikia kuwa Samaria imepokea neno la Mungu, wakawatuma Petro na Yohana.
15 Ceux-ci, étant descendus, prièrent pour eux, afin qu'ils reçoivent le Saint-Esprit;
Wakati walipokuwa wakishuka wakawaombea; kwamba wampokee Roho Mtakatifu.
16 car il n'était encore tombé sur aucun d'eux. Ils avaient seulement été baptisés au nom de Jésus-Christ.
Mpaka muda huo, Roho Mtakatifu alikuwa hajawashukia hata mmoja wao; walikuwa tu wamebatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
17 Alors ils leur imposèrent les mains, et ils reçurent le Saint-Esprit.
Ndipo Petro na Yohana wakawawekea mikono, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
18 Simon, voyant que le Saint-Esprit était donné par l'imposition des mains des apôtres, leur offrit de l'argent,
Wakati Simoni alipoona kwamba Roho Mtakatifu ametolewa kupitia kuwekewa mikono na mitume; akataka kuwapa pesa,
19 en disant: « Donnez-moi aussi ce pouvoir, afin que quiconque m'impose les mains reçoive le Saint-Esprit. »
Akasema, “Nipeni hii nguvu, ili kila nitakayemwekea mikono apokee Roho Mtakatifu.”
20 Mais Pierre lui dit: « Que ton argent périsse avec toi, parce que tu as cru pouvoir obtenir le don de Dieu avec de l'argent!
Lakini Petro akamwambia; pesa yako pamoja na wewe ipotelee mbali, kwa sababu umedhani kuwa karama ya Mungu inapatikana kwa pesa.
21 Tu n'as ni part ni lot dans cette affaire, car ton cœur n'est pas droit devant Dieu.
Hauna sehemu katika jambo hili, kwa sababu moyo wako si mnyoofu mbele za Mungu.
22 Repens-toi donc de cela, de ta méchanceté, et demande à Dieu si peut-être la pensée de ton cœur peut t'être pardonnée.
Hivyo basi tubu maovu yako na kumwomba Mungu labda utasamehewe fikra za moyo wako.
23 Car je vois que tu es dans le poison de l'amertume et dans la servitude de l'iniquité. »
Kwa maana naona uko katika sumu ya uchungu na kifungo cha dhambi.”
24 Simon répondit: « Priez pour moi le Seigneur, afin qu'il ne m'arrive rien de ce que vous avez dit. »
Simoni akajibu na kusema, “Mwombeni Bwana kwa ajili yangu, kwa kuwa mambo yote mliyozungumza yaweza kunitokea.
25 Après avoir témoigné et prononcé la parole du Seigneur, ils retournèrent donc à Jérusalem, et prêchèrent la Bonne Nouvelle dans plusieurs villages des Samaritains.
Wakati Petro na Yohana walipokuwa wameshuhudia na kuhubiri neno la Bwana, walirudi Yerusalemu kwa njia hiyo; walihubiri injili katika vijiji vingi vya Wasamaria.
26 Alors un ange du Seigneur parla à Philippe, en disant: « Lève-toi, et va du côté du midi, sur le chemin qui descend de Jérusalem à Gaza. C'est un désert. »
Basi malaika wa Bwana akanena na Filipo na kusema, “Angaza na uende kusini katika njia iendayo chini ya Yerusalemu kuelekea Gaza.” ( Njia hii iko katika jangwa).
27 Il se leva et partit. Et voici qu'un homme d'Éthiopie, eunuque de grande autorité sous Candace, reine des Éthiopiens, qui était à la tête de tout son trésor, était venu à Jérusalem pour se prosterner.
Akaangaza na kwenda. Tazama, kulikuwa na mtu wa Ethiopia, towashi mwenye mamlaka kuu chini ya kandase; malkia wa Ethiopia. Aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu.
28 Il s'en retournait, assis dans son char, et lisait le prophète Ésaïe.
Alikuwa akirejea ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.
29 L'Esprit dit à Philippe: « Approche-toi, et attache-toi à ce char. »
Roho akasema na Filipo, “Sogea karibu na gari hili ukashikamane nalo.
30 Philippe courut vers lui, l'entendit lire le prophète Ésaïe, et dit: « Comprends-tu ce que tu lis? »
“Hivyo Filipo akaenda mbio, akamsikia akisoma katika chuo cha nabii Isaya; akasema, Je unafahamu unachosoma?”
31 Il dit: « Comment le pourrais-je, si personne ne me l'explique? » Il pria Philippe de monter et de s'asseoir avec lui.
Muethiopia akasema, “nitawezaje mtu asiponiongoza?” Akamsihi Filipo apande garini na kuketi pamoja naye.
32 Or, le passage de l'Écriture qu'il lisait était celui-ci, « Il a été conduit comme un mouton à l'abattoir. Comme un agneau qui se tait devant son tondeur, pour qu'il n'ouvre pas sa bouche.
Sasa fungu la maandiko alilokuwa akisoma Muethiopia ni hili; Aliongozwa kama kondoo kwenda machinjioni kuchinjwa; na kama kondoo alinyamaza kimya, hakufungua kinywa chake:
33 Dans son humiliation, son jugement a été enlevé. Qui déclarera sa génération? Car sa vie est enlevée de la terre. »
Kwa kuhuzunishwa kwake hukumu yake iliondolewa: Nani ataeleza kizazi chake? maisha yake yameondolewa katika nchi.”
34 L'eunuque répondit à Philippe: « De qui le prophète parle-t-il? De lui-même, ou de quelqu'un d'autre? »
Hivyo towashi akamwuliza Filipo, na kusema, “nakuomba, ni nabii yupi ambaye anaongelewa habari zake, ni kuhusu yeye, au za mtu mwingine”?
35 Philippe ouvrit la bouche, et, commençant par cette Écriture, il lui annonça Jésus.
Filipo alianza kuongea, alianza kwa andiko hili la Isaya kumhubiria habari za Yesu.
36 Comme ils continuaient leur chemin, ils arrivèrent à de l'eau, et l'eunuque dit: « Voici de l'eau. Qu'est-ce qui m'empêche d'être baptisé? »
Wakiwa njiani, wakafika penye maji,' towashi akasema, “Tazama, pana maji hapa nini kinazuia nisibatizwe?,
maneno haya, “Hivyo Muethiopia akajibu “naamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu,” hayamo kwenyemaandiko ya kale). Ndipo Muethiopia akaamuru gari lisimame.
38 Il ordonna au char de s'arrêter, et ils descendirent tous deux dans l'eau, Philippe et l'eunuque, et il le baptisa.
Walikwenda ndani ya maji, pamoja Filipo na towashi, Filipo akambatiza.
39 Lorsqu'ils sortirent de l'eau, l'Esprit du Seigneur emporta Philippe, et l'eunuque ne le vit plus, car il s'en alla tout joyeux.
Wakati walipotoka kwenye maji, Roho wa Bwana ikampeleka Filipo mbali; towashi hakumwona, akaenda njia yake akishangilia.
40 Mais Philippe fut trouvé à Azot. En passant, il prêcha la bonne nouvelle dans toutes les villes, jusqu'à ce qu'il arrive à Césarée.
Lakini Philipo akatokea Azoto. Alipita katika mkoa ule na kuhubiri injili katika miji yote mpaka alipofika Kaisaria.

< Actes 8 >