< Actes 11 >
1 Les apôtres et les frères qui étaient en Judée apprirent que les païens aussi avaient reçu la parole de Dieu.
Mitume na ndugu walioamini waliokuwa huko Uyahudi wakasikia kuwa watu wa Mataifa nao wamepokea neno la Mungu.
2 Lorsque Pierre fut monté à Jérusalem, ceux de la circoncision le contestèrent,
Hivyo Petro alipopanda Yerusalemu, wale wa tohara waliokuwa wameamini wakamshutumu,
3 en disant: « Tu es allé vers des incirconcis et tu as mangé avec eux. »
wakisema, “Ulikwenda kwa watu wasiotahiriwa na kula pamoja nao.”
4 Pierre commença, et leur expliqua dans l'ordre, en disant:
Ndipo Petro akaanza kuwaeleza kuhusu mambo yote yalivyotokea hatua kwa hatua akisema,
5 « J'étais dans la ville de Joppé, en train de prier, et j'ai eu une vision: un récipient qui descendait, comme une grande toile tendue du ciel par quatre coins. Il arriva jusqu'à moi.
“Nilikuwa katika mji wa Yafa nikiomba, nami nikapitiwa na usingizi wa ghafula, nikaona maono. Kulikuwa na kitu kama nguo kubwa ikishuka kutoka mbinguni, ikishushwa kwa ncha zake nne, nayo ikanikaribia.
6 Après l'avoir regardé attentivement, j'ai considéré et j'ai vu les quadrupèdes de la terre, les animaux sauvages, les reptiles et les oiseaux du ciel.
Nilipoangalia ndani yake kwa karibu niliona wanyama wenye miguu minne wa nchini, wanyama wa mwitu, watambaao na ndege wa angani.
7 J'entendis aussi une voix qui me disait: « Lève-toi, Pierre, tue et mange! »
Ndipo nikasikia sauti ikiniambia, ‘Petro, ondoka uchinje na ule.’
8 Mais je disais: « Non, Seigneur, car il n'est jamais entré dans ma bouche rien de souillé ni d'impur ».
“Nikajibu, ‘La hasha Bwana! Kitu chochote kilicho najisi hakijaingia kinywani mwangu.’
9 Mais, pour la seconde fois, une voix me répondit du ciel: « Ce que Dieu a purifié, ne l'appelle pas impur.
“Sauti ikasema kutoka mbinguni mara ya pili, ‘Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.’
10 Cela se passa trois fois, et tous remontèrent au ciel.
Jambo hili lilitokea mara tatu, ndipo kile kitu kikavutwa tena mbinguni.
11 Aussitôt, trois hommes se présentèrent devant la maison où j'étais, envoyés de Césarée vers moi.
“Wakati ule ule watu watatu, waliokuwa wametumwa kutoka Kaisaria waliwasili katika nyumba niliyokuwa nikikaa.
12 L'Esprit me dit d'aller avec eux sans distinction. Ces six frères m'accompagnèrent aussi, et nous entrâmes dans la maison de cet homme.
Roho Mtakatifu akaniambia niende nao bila kuwa na ubaguzi kati yao na sisi. Hawa ndugu sita pia walifuatana nami, nasi tukaingia nyumbani mwa huyo Kornelio.
13 Il nous raconta qu'il avait vu l'ange se tenir dans sa maison et lui dire: « Envoie à Joppé chercher Simon, surnommé Pierre,
Akatuambia jinsi alivyoona malaika aliyekuwa amesimama katika nyumba yake na kusema, ‘Tuma watu waende Yafa wakamlete Simoni aitwaye Petro.
14 qui te dira les paroles par lesquelles tu seras sauvé, toi et toute ta maison ».
Yeye atakupa ujumbe ambao kwa huo wewe na wa nyumbani mwako wote mtaokoka.’
15 Comme je commençais à parler, le Saint-Esprit tomba sur eux, comme sur nous au commencement.
“Nami nilipoanza kusema, Roho Mtakatifu akashuka juu yao kama vile alivyotushukia sisi hapo mwanzo.
16 Et je me suis souvenu de la parole du Seigneur, qui a dit: « Jean a baptisé dans l'eau, mais vous, vous serez baptisés dans l'Esprit Saint ».
Nami nikakumbuka neno la Bwana alivyosema, ‘Yohana alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu.’
17 Si donc Dieu leur a accordé le même don qu'à nous, lorsque nous avons cru au Seigneur Jésus-Christ, qui étais-je, pour résister à Dieu? »
Basi ikiwa Mungu aliwapa hawa watu kipawa kile kile alichotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani hata nifikirie kuwa ningeweza kumpinga Mungu?”
18 Quand ils entendirent ces choses, ils gardèrent le silence et glorifièrent Dieu, en disant: « Alors Dieu a aussi accordé aux païens la repentance à la vie! »
Waliposikia haya hawakuwa na la kupinga zaidi. Nao wakamwadhimisha Mungu wakisema, “Basi, Mungu amewapa hata watu wa Mataifa toba iletayo uzima wa milele.”
19 Ceux donc qui avaient été dispersés par l'oppression qui s'était élevée au sujet d'Étienne, allèrent jusqu'en Phénicie, à Chypre et à Antioche, ne parlant à personne, sinon aux Juifs seulement.
Basi wale waliotawanyika kwa ajili ya mateso yaliyotokana na kifo cha Stefano, wakasafiri hadi Foinike na Kipro na Antiokia. Nao hawakuhubiri lile Neno kwa mtu yeyote isipokuwa Wayahudi.
20 Mais quelques-uns d'entre eux, hommes de Chypre et de Cyrène, arrivèrent à Antioche et s'adressèrent aux Hellènes, prêchant le Seigneur Jésus.
Lakini baadhi yao walikuwepo watu wa Kipro na Kirene, ambao walipokuja Antiokia walinena na Wayunani pia wakiwahubiria habari njema za Bwana Yesu.
21 La main du Seigneur était avec eux, et un grand nombre crurent et se tournèrent vers le Seigneur.
Mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao, nayo idadi kubwa ya watu wakaamini na kumgeukia Bwana.
22 Le bruit qui courut à leur sujet parvint aux oreilles de l'assemblée qui était à Jérusalem. Ils envoyèrent Barnabas jusqu'à Antioche,
Habari hizi zilipofika masikioni mwa kanisa huko Yerusalemu, wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23 lequel, après être arrivé et avoir vu la grâce de Dieu, se réjouit. Il les exhorta tous à s'attacher de tout leur cœur au Seigneur.
Alipofika na kuona madhihirisho ya neema ya Mungu, akafurahi na kuwatia moyo waendelee kuwa waaminifu kwa Bwana kwa mioyo yao yote.
24 Car c'était un homme de bien, plein de l'Esprit Saint et de foi, et beaucoup de gens furent ajoutés au Seigneur.
Barnaba alikuwa mtu mwema, aliyejaa Roho Mtakatifu, mwenye imani, nayo idadi kubwa ya watu wakaongezeka kwa Bwana.
25 Barnabas partit pour Tarse, à la recherche de Saul.
Kisha Barnaba akaenda Tarso kumtafuta Sauli,
26 L'ayant trouvé, il l'emmena à Antioche. Pendant toute une année, ils furent réunis avec l'assemblée, et ils enseignèrent beaucoup de gens. C'est à Antioche que les disciples ont été appelés chrétiens pour la première fois.
naye alipompata akamleta Antiokia. Hivyo kwa mwaka mzima Barnaba na Sauli wakakutana na kanisa na kufundisha idadi kubwa ya watu. Ilikuwa ni katika kanisa la Antiokia kwa mara ya kwanza wanafunzi waliitwa Wakristo.
27 En ces jours-là, des prophètes descendirent de Jérusalem à Antioche.
Wakati huo manabii walishuka toka Yerusalemu hadi Antiokia.
28 L'un d'eux, nommé Agabus, se leva et annonça par l'Esprit qu'il devait y avoir une grande famine dans le monde entier, ce qui arriva aussi du temps de Claude.
Mmoja wao, jina lake Agabo, akasimama akatabiri kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itaenea ulimwengu mzima. Njaa hiyo ilitokea wakati wa utawala wa Klaudio.
29 Tous les disciples, qui étaient dans l'abondance, résolurent d'envoyer des secours aux frères qui habitaient la Judée,
Mitume wakaamua kwamba kila mtu, kulingana na uwezo alio nao, atoe msaada kwa ajili ya ndugu wanaoishi Uyahudi.
30 ce qu'ils firent aussi, en les envoyant aux anciens par les mains de Barnabas et de Saul.
Wakafanya hivyo, misaada yao ikapelekwa kwa wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.