< 2 Samuel 14 >

1 Joab, fils de Tseruja, s'aperçut que le cœur du roi était tourné vers Absalom.
Yoabu mwana wa Seruya akatambua kwamba moyo wa mfalme ulitamani kumwona Absalomu.
2 Joab envoya à Tekoa et y fit venir une femme sage, à qui il dit: « Je t'en prie, agis comme une personne en deuil, mets des vêtements de deuil, je t'en prie, et ne t'oins pas d'huile, mais sois comme une femme qui a pleuré longtemps un mort.
Hivyo Yoabu akatuma neno huko Tekoa kumleta kwake mwanamke mwelevu. Akamwambia, “Tafadhari, vaa mavazi ya uombolezaji ujifanye kuwa mwombolezaji. Usijipake mafuta, lakini uwe kama mwanamke ambaye ameomboleza kwa muda mrefu kwa ajili yake aliyekufa.
3 Va vers le roi et parle-lui ainsi. » Joab mit les mots dans sa bouche.
Kisha ingia kwa mfalme na umwambiye maneno nitakayokueleza.” Hivyo Yoabu akamwambia maneno ambayo angeyasema kwa mfalme.
4 Lorsque la femme de Tekoa a parlé au roi, elle s'est prosternée à terre, s'est montrée respectueuse et a dit: « Au secours, ô roi! »
Wakati mwanamke kutoka Tekoa alipoongea na mfalme, aliinamisha uso wake chini na kusema,
5 Le roi lui dit: « Qu'est-ce qui te prend? » Elle répondit: « En vérité, je suis veuve, et mon mari est mort.
“Mfalme, anisaidie.” Mfalme akamwambia, “Shida yako ni nini?” Akajibu, Ukweli ni kwamba mimi ni mjane, mme wangu alikufa.
6 Ton serviteur avait deux fils; ils se sont battus ensemble dans les champs, et il n'y avait personne pour les séparer; mais l'un a frappé l'autre et l'a tué.
Mimi, mtumishi wako, nilikuwa na wana wawili, wakagombana shambani, na hakukuwa na wa kuwaachanisha. Mmoja wao akampiga mwenziwe na kumwua.
7 Voici que toute la famille s'est soulevée contre ton serviteur, et ils disent: « Délivrez celui qui a frappé son frère, afin que nous le tuions pour la vie de son frère qu'il a tué, et que nous fassions aussi périr l'héritier ». Ainsi, ils éteindraient mon charbon qui reste, et ne laisseraient à mon mari ni nom ni reste sur la surface de la terre. »
Na sasa ukoo wote umeinuka juu ya mtumishi wako, wanasema, 'Mtoe aliyempiga nduguye, ili tumwue kulipe uhai wa nduguye aliyeuawa.' Na hivyo watamwangamiza mrithi. Hivyo watalizima kaa liwakalo nililobakiwa, hata kumwondolea mme wangu jina na mzao juu ya uso wa nchi.”
8 Le roi dit à la femme: « Va dans ta maison, et je donnerai un ordre à ton sujet. »
Hivyo mfalme akamwambia mwanamke, “Nenda nyumbani kwako, nami nitaagiza jambo la kukufanyia.”
9 La femme de Tekoa dit au roi: « Mon seigneur, ô roi, que l'iniquité retombe sur moi et sur la maison de mon père, et que le roi et son trône soient sans reproche. »
Mwanamke kutoka Tekoa akamjibu mfalme, “Bwana wangu mfalme, hatia na iwe juu yangu na juu ya familia ya baba yangu. Mfalme na kiti chake cha enzi hawana hatia.”
10 Le roi dit: « Si quelqu'un te dit quelque chose, amène-le moi, et il ne t'ennuiera plus. »
Mfalme akasema, “Yeyote atakayekwambia neno umlete kwangu, naye hatakugusa tena.”
11 Et elle dit: « Je te prie, que le roi se souvienne de Yahvé, ton Dieu, afin que le vengeur du sang ne détruise plus, de peur qu'on ne fasse périr mon fils. » Il a dit: « Yahvé est vivant, aucun cheveu de ton fils ne tombera sur la terre. »
Kisha mwanamke akasema, “Tafadhari mfalme amkumbuke Yahwe Mungu wake, ili kwamba mlipa kisasi cha damu asiaribu zaidi, ili kwamba wasimwangamize mwanangu.” Mfalme akajibu, “Kama Mungu aishivyo, hakuna hata unywele mmoja wa mwanao utaanguka chini.”
12 Alors la femme dit: « Je te prie de laisser ton serviteur dire un mot à mon seigneur le roi. » Il a dit: « Dis-le. »
Kisha mwanamke akasema, “Tafadhari acha mtumishi wako anene neno moja zaidi kwa bwana wangu mfalme.” Akasema, “Sema.”
13 La femme dit: « Pourquoi donc as-tu imaginé une telle chose contre le peuple de Dieu? Car en prononçant cette parole, le roi est comme un coupable, en ce que le roi ne ramène pas son banni.
Hivyo mwanamke akasema, “Kwa nini basi umetenda kwa hila dhidi ya watu Mungu? Maana kwa kusema hivi, mfalme ni kama mtu mwenye hatia, kwa kuwa mfalme hamjamrudisha tena mwanaye aliyeondoka.
14 Car nous devons mourir, et nous sommes comme de l'eau répandue sur le sol, qui ne peut être recueillie; et Dieu n'ôte pas la vie, mais il conçoit des moyens, afin que celui qui est banni ne soit pas exclu de lui.
Kwa maana sisi sote tutakufa, kwa kuwa tu kama maji yamwagwayo juu ya ardhi na kwamba hayawezi kukusanywa tena. Lakini Mungu hatachukua uhai; badala yake, utafuta njia kwa walio mbali kurejeshwa.
15 Maintenant, si je suis venu pour dire cette parole à mon seigneur le roi, c'est parce que le peuple m'a fait peur. Ton serviteur a dit: « Je vais maintenant parler au roi; il se peut que le roi exauce la demande de son serviteur ».
Sasa basi, nimesema jambo hili kwa bwana wangu mfalme, kwa sababu watu wamenitisha. Hivyo mtumishi wako akajinenea nafsini mwake, 'Sasa nitaongea na mfalme. Huenda mfalme akampa mtumishi wake haja yake.
16 Car le roi écoutera, pour délivrer son serviteur de la main de l'homme qui voulait nous faire périr, moi et mon fils, hors de l'héritage de Dieu.
Kwa maana mfalme atanisikiliza, ili kwamba kumtoa mtumishi wake katika mikono ya mtu ambaye angeniangamiza mimi na mwanangu pamoja, tutoke katika urithi wa Mungu.
17 Ton serviteur dit: « Que la parole de mon seigneur le roi apporte le repos, car comme un ange de Dieu, mon seigneur le roi sait discerner le bien et le mal. Que Yahvé, ton Dieu, soit avec toi. »
Kisha mtumishi wako akaomba, 'Yahwe, tafadhari ruhusu neno la bwana wangu mfalme linipe msaada, kwa maana bwana wangu mfalme ni kama malaika wa Mungu kwa kutofautisha wema na ubaya.' Yahwe, Mungu na awe pamoja nawe.”
18 Alors le roi répondit à la femme: « Je t'en prie, ne me cache rien de ce que je te demande. » La femme dit: « Que mon seigneur le roi parle maintenant. »
Ndipo mfalme akajibu na kumwambia yule mwanamke, Tafadhari usinifiche neno lolote nikuulizalo.” Mwanamke akajibu, “Basi bwana wangu mfalme na aseme sasa.
19 Le roi dit: « La main de Joab est-elle avec toi dans tout cela? » La femme répondit: « Aussi vrai que ton âme est vivante, mon seigneur le roi, personne ne peut se détourner à droite ou à gauche de ce que mon seigneur le roi a dit; car ton serviteur Joab m'a pressée, et il a mis toutes ces paroles dans la bouche de ta servante.
Mfalme akasema, Je siyo mkono wa Yoabu ulio pamoja nawe katika haya yote? Mwanamke akajibu na kusema, “Kama uishivyo bwana wangu mfalme, hakuna awezae kuelekea mkono wa kulia wala wa kushoto kwa yale bwana wangu mfalme aliyosema. Ni mtumishi wako Yoabu aliyeniambia na kuniagiza kusema kile mtumishi wako alichokisema.
20 Ton serviteur Joab a fait cela pour changer la face de l'affaire. Mon seigneur est sage, selon la sagesse d'un ange de Dieu, pour connaître toutes les choses qui sont sur la terre. »
Mtumishi wako Yoabu amefanya hivi ili kubadilisha hali ya kile kinachotendeka. Bwana wangu ni mwenye akili kama hekima ya malaika wa Mungu, ajuaye yote yatendekayo ndani ya nchi.”
21 Le roi dit à Joab: « Voici, j'ai accordé cette chose. Va donc, et ramène le jeune homme Absalom. »
Hivyo mfalme akamwambia Yoabu, “Tazama, nitatenda jambo hili. Nenda na umrudishe huyo kijana Absalomu.”
22 Joab tomba à terre sur sa face, fit preuve de respect et bénit le roi. Joab dit: « Ton serviteur sait aujourd'hui que j'ai trouvé grâce à tes yeux, mon seigneur, ô roi, puisque le roi a exécuté la demande de son serviteur. »
HivyoYoabu akainamisha uso wake chini juu ya ardhi katika heshima na shukurani kwa mfalme. Yoabu akasema, “Mtumishi wako amejua kwamba amepata neema mbele zako, bwana wangu, mfalme, kwa vile mfalme amempa mtumishi wake haja ya moyo wake.
23 Joab se leva, alla à Gueschur, et amena Absalom à Jérusalem.
Hivyo Yoabu akainuka na kwenda Geshuri, akamrejesha Absalomu Yerusalemu tena.
24 Le roi dit: « Qu'il retourne dans sa maison, mais qu'il ne voie pas mon visage. » Absalom retourna donc dans sa maison, et ne vit pas le visage du roi.
Mfalme akasema, “Na arudi nyumbani kwake, lakini hasinione uso wangu.” Hivyo Absalomu akarudi katika nyumba yake mwenyewe, na hakuweza kuuona uso wa mfalme.
25 Or, dans tout Israël, il n'y avait personne qui fût aussi loué qu'Absalom pour sa beauté. Depuis la plante de son pied jusqu'au sommet de sa tête, il n'y avait en lui aucun défaut.
Hakukuwa na mtu katika Israeli aliyesifiwa kwa uzuri kama Absalomu. Kutoka katika wayo wa mguu wake hadi katika utosi wake hakuwa na waa lolote.
26 Lorsqu'il se coupait les cheveux de sa tête (c'était à la fin de chaque année qu'il les coupait; comme ils étaient lourds pour lui, il les coupait), il pesait les cheveux de sa tête à deux cents sicles, selon le poids du roi.
Alipokata nywele za kichwa chake mwishoni mwa kila mwaka, kwa sababu zilikuwa nzito juu yake, alipima nywele zake zaidi ya shekeli mia mbili, kwa kiwango cha kipimo cha mfalme.
27 Trois fils naquirent à Absalom, et une fille, dont le nom était Tamar. C'était une femme qui avait un beau visage.
Kwake Absalomu walizaliwa wana watatu na binti mmoja, jina lake Tamari. Alikuwa mwanamke mzuri.
28 Absalom vécut deux années entières à Jérusalem, et il ne vit pas le visage du roi.
Absalomu akaishi Yerusalem miaka miwili pasipo kuona uso wa mfalme.
29 Absalom envoya alors chercher Joab, pour l'envoyer auprès du roi, mais celui-ci ne voulut pas venir à lui. Il envoya encore une seconde fois, mais il ne voulut pas venir.
Kisha Absalome akatuma neno kwa Yoabu ili ampeleke kwa mfalme, lakini Yoabu hakwenda kwake. Hivyo Absalomu akatuma neno mara ya pili, lakini Yoabu hakuja bado.
30 Il dit alors à ses serviteurs: « Voici, le champ de Joab est près du mien, et il y a de l'orge. Allez-y et mettez-y le feu. » Les serviteurs d'Absalom mirent donc le feu au champ.
Hivyo Absalomu akawambia watumishi wake, “Tazameni, shamba la Yoabu lipo karibu na langu, naye ana shayiri kule. Nendeni mkalichome moto” Hivyo watumishi wa Absalome wakalichoma moto lile shamba.
31 Alors Joab se leva et vint chez Absalom, dans sa maison, et lui dit: « Pourquoi tes serviteurs ont-ils mis le feu à mon champ? »
Kisha Yoabu akainuka na kwenda nyumbani kwa Absalomu akamwambia, “Kwa nini watumishi wako wamelichoma moto shamba langu?
32 Absalom répondit à Joab: « Voici, je t'ai envoyé dire: Viens ici, afin que je t'envoie dire au roi: « Pourquoi suis-je venu de Gueshur? Il vaudrait mieux que j'y sois encore. Maintenant, que je voie la face du roi, et s'il y a en moi de l'iniquité, qu'il me fasse mourir ».
Absalomu akamjibu Yoabu, “Tazama nilituma neno kwako kusema, 'Njoo ili nikutume kwa mfalme kusema, “Kwa nini nilikuja kutoka Geshuri? Ingekuwa heri kwangu kama ningesalia huko. Kwa hiyo sasa niache niuone uso wa mfalme na kama nina hatia basi na aniue.”
33 Joab se rendit auprès du roi et lui en fit part. Après avoir appelé Absalom, il vint auprès du roi et se prosterna à terre, face contre terre, devant le roi; et le roi embrassa Absalom.
Hivyo Yoabu akaenda kwa mfalme na kumwambia. Mfalme alipomwita, Absalomu alikuja kwa mfalme na akainama hadi juu ya uso nchi mbele ya mfalme na mfalme akambusu Absalomu.

< 2 Samuel 14 >