< 2 Rois 24 >
1 De son temps, Nebucadnetsar, roi de Babylone, monta et Jehoïakim devint son serviteur pendant trois ans. Puis il se retourna et se rebella contre lui.
Katika siku za Yehoyakimu, Nebukadreza mfalme wa Babeli akaiteka Yuda; Yehoyakimu akawa mtumishi kwa muda wa miaka mitatu. Kisha Yehoyakimu akarudi na kuasi dhidi ya Nebukadreza.
2 Yahvé envoya contre lui des troupes de Chaldéens, des troupes de Syriens, des troupes de Moabites et des troupes d'Ammonites, et il les envoya contre Juda pour le détruire, selon la parole de Yahvé, qu'il avait prononcée par ses serviteurs les prophètes.
Yahwe akatuma vikosi vya Wakaldayo dhidi ya Yehoyakimu, Washami, Wamoabu, na Waamoni; akawatuma dhidi ya Yuda kuiharibu. Hii ilikuwa ni kuthibitisha pamoja na neno la Yahwe ambalo aliloliongea kupitia watumishi wake manabii.
3 Mais, sur l'ordre de l'Éternel, cela arriva à Juda, pour le soustraire à sa vue, à cause des péchés de Manassé, selon tout ce qu'il a fait,
Ilikuwa baada ya mda mfupi kwenye kinywa cha Yahwe kwamba hili likaja juu ya Yuda, kuwaondoa usoni mwa uso wake, kwa sabau ya dhambi za Manase, yote aliyoyafanya,
4 et aussi à cause du sang innocent qu'il a répandu, car il a rempli Jérusalem de sang innocent, et l'Éternel n'a pas voulu pardonner.
na pia kwa sababu ya damu isiyokuwa na hatia aliyoimwaga, kwa kuijaza Yerusalemu kwa damu isiyokuwa na hatia. Yahwe hakuwa tayari kusamehe hilo.
5 Le reste des actes de Jojakim, et tout ce qu'il a fait, cela n'est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois de Juda?
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Yehoyakimu, na yote aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
6 Jehoïakim se coucha avec ses pères, et Jehoïakin, son fils, régna à sa place.
Yehoyakimu akalala pamoja na wazee wake, na Yekonia mtoto wake akawa mfalme katika sehemu yake.
7 Le roi d'Égypte ne sortit plus de son pays, car le roi de Babylone avait pris, depuis le ruisseau d'Égypte jusqu'au fleuve Euphrate, tout ce qui appartenait au roi d'Égypte.
Mfalme wa Misri hakushambulia tena nje ya nchi yake, kwa sababu mfalme wa Babeli alakuwa amezishinda nchi zote ambazo zilikuwa zikitawaliwa na mfalme wa Misri, kutoka kwenye kitabu cha Misri mpaka Mto wa Frati.
8 Jojakin avait dix-huit ans lorsqu'il devint roi, et il régna trois mois à Jérusalem. Le nom de sa mère était Nehushta, fille d'Elnathan, de Jérusalem.
Yekonia alikuwa na umri wa miaka kumi na nane alipoanza kutawala; alitawala Yerusalemu miezi mitatu. Mama yake alikuwa anaitwa Nehushta; alikuwa binti wa Elnathani wa Yerusalemu.
9 Il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, selon tout ce qu'avait fait son père.
Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe; alifanya yale yote ambayo baba yake aliyafanya.
10 En ce temps-là, les serviteurs de Nebucadnetsar, roi de Babylone, montèrent à Jérusalem, et la ville fut assiégée.
Katika kipindi hicho jeshi la Nebukadreza mfalme wa Babeli liliishambulia Yerusalemu na kuuzunguka mji.
11 Nebucadnetsar, roi de Babylone, arriva dans la ville pendant que ses serviteurs l'assiégeaient.
Nebukadreza mfalme wa Babeli akaja kwenye mji wakati maaskari wake walipokuwa wameuzunguka,
12 Jehoïachin, roi de Juda, sortit vers le roi de Babylone, lui, sa mère, ses serviteurs, ses chefs et ses officiers, et le roi de Babylone le captura la huitième année de son règne.
na Yekonia mfalme wa Yuda akatoka nje kwenda kwa mfalme wa Babeli, yeye, mama yake, watumishi wake, watoto wake, na maafisa wake. Mfalme wa Babeli akamteka katika mwaka wa nane wa utawala wake.
13 Il emporta de là tous les trésors de la maison de l'Éternel et les trésors de la maison du roi, et il mit en pièces tous les vases d'or que Salomon, roi d'Israël, avait faits dans le temple de l'Éternel, comme l'Éternel l'avait dit.
Nebukadreza akachukua kutoka pale vitu vyote vya thamani katika nyumba ya Yahwe, na walio katika nyumba ya kifalme. Akavikata vipande vipande vitu vyote vya dhahabu ambavyo Suleimani mfalme wa Israeli alivitengeneza katika hekalu la Yahwe, kama alivyokuwa amesema ingetokea.
14 Il emmena tout Jérusalem, tous les chefs et tous les vaillants hommes, dix mille captifs, et tous les artisans et les forgerons. Il ne resta plus que le peuple le plus pauvre du pays.
Akawachukua wote utumwani Yerusalemu, viongozi wote, na wapiganaji wote, mateka elfu kumi, na mafundi wote, na wafua vyuma. hakuna aliyekuwa amesalia isipokuwa watu maskini katika nchi.
15 Il emmena Jehoïachin à Babylone, avec la mère du roi, les femmes du roi, ses officiers et les chefs du pays. Il les emmena en captivité de Jérusalem à Babylone.
Nebukadreza akamchukua Yekonia utumwani Babeli, pia na mama yake na mfalme, wake, maafisa, na wakuu wa nchi. Akawachukua kwenda utumwani kutoka Yerusalemu mpaka Babeli.
16 Le roi de Babylone emmena en captivité à Babylone tous les vaillants hommes, au nombre de sept mille, et les artisans et les forgerons, au nombre de mille, tous forts et aptes à la guerre.
Wapiganaji wote, elfu saba kwa hesabu, na mafundi elfu moja na wafua vyuma, wote wanaostahili kumpiga- mfalme wa Babeli aliwaleta hawa watu kwenye utumwa Babeli.
17 Le roi de Babylone fit régner à sa place Matthania, frère du père de Jojakin, et changea son nom en Sédécias.
Mfalme wa Babeli akamfanya Matania, kaka yake na baba yake na Yehokimu, mfalme katika sehemu yake, na kubadilisha jina lake kuwa Sedekia.
18 Sédécias avait vingt et un ans lorsqu'il devint roi, et il régna onze ans à Jérusalem. Le nom de sa mère était Hamutal, fille de Jérémie, de Libna.
Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na moja wakati alipoanza kutawala; alitawala miaka kumi na moja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Hamutali; alikuwa binti wa Yeremia kutoka Libna.
19 Il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, selon tout ce qu'avait fait Jehoïakim.
Alifanya yaliyo maovu machoni mwa Yahwe; aliyafanya yale yote ambayo Yehokimu aliyoyafanya.
20 Car, par la colère de l'Éternel, cela arriva à Jérusalem et en Juda, jusqu'à ce qu'il les eût chassés de sa présence. Sédécias s'est alors rebellé contre le roi de Babylone.
Kupitia hasira ya Yahwe, haya matukio yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, hadi alipowaondoa kwenye uso wake. Kisha Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.