< 2 Rois 16 >

1 La dix-septième année de Pékach, fils de Remalia, Achaz, fils de Jotham, roi de Juda, commença à régner.
Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Achaz avait vingt ans lorsqu'il devint roi, et il régna seize ans à Jérusalem. Il ne fit pas ce qui est droit aux yeux de l'Éternel, son Dieu, comme David, son père.
Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
3 Mais il marcha dans la voie des rois d'Israël et fit même passer son fils par le feu, selon les abominations des nations que l'Éternel avait chassées devant les enfants d'Israël.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
4 Il offrait des sacrifices et brûlait des parfums sur les hauts lieux, sur les collines et sous tout arbre vert.
Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
5 Alors Retsin, roi de Syrie, et Pékah, fils de Remalia, roi d'Israël, montèrent à Jérusalem pour faire la guerre. Ils assiégèrent Achaz, mais ne purent le vaincre.
Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
6 En ce temps-là, Retsin, roi de Syrie, récupéra Élath au profit de la Syrie et chassa les Juifs d'Élath; les Syriens s'installèrent à Élath et y ont vécu jusqu'à ce jour.
Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
7 Achaz envoya des messagers à Tiglath Pileser, roi d'Assyrie, en disant: « Je suis ton serviteur et ton fils. Monte et sauve-moi de la main du roi de Syrie et de la main du roi d'Israël, qui s'élèvent contre moi. »
Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
8 Achaz prit l'argent et l'or qui se trouvaient dans la maison de l'Éternel et dans les trésors de la maison du roi, et il les envoya en cadeau au roi d'Assyrie.
Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
9 Le roi d'Assyrie l'écouta; et le roi d'Assyrie monta contre Damas et s'en empara, emmena son peuple captif à Kir, et fit mourir Rezin.
Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
10 Le roi Achaz alla à Damas pour rencontrer Tiglath Pileser, roi d'Assyrie, et il vit l'autel qui était à Damas. Le roi Achaz envoya au prêtre Urie un dessin de l'autel et les plans pour le construire.
Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
11 Le prêtre Urie construisit l'autel. Selon tout ce que le roi Achaz avait envoyé de Damas, le prêtre Urie le construisit pour l'arrivée du roi Achaz de Damas.
Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
12 Lorsque le roi arriva de Damas, il vit l'autel; il s'approcha de l'autel et y fit des offrandes.
Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
13 Il brûla son holocauste et son offrande, versa sa libation et fit aspersion sur l'autel du sang de ses sacrifices de prospérité.
Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
14 Il fit venir l'autel d'airain qui était devant l'Éternel, de l'avant de la maison, entre son autel et la maison de l'Éternel, et le plaça au nord de son autel.
Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
15 Le roi Achaz donna cet ordre au prêtre Urie: « Sur le grand autel, brûlez l'holocauste du matin, l'offrande du soir, l'holocauste du roi et son offrande, ainsi que l'holocauste de tous les habitants du pays, leur offrande et leurs libations, et répandez-y tout le sang de l'holocauste et tout le sang du sacrifice; mais l'autel d'airain sera pour moi un lieu de consultation. »
Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
16 Le prêtre Urie fit ainsi, selon tout ce que le roi Achaz avait ordonné.
Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
17 Le roi Achaz coupa les panneaux des socles, enleva la cuvette de dessus, enleva la mer de dessus les bœufs de bronze qui étaient dessous, et la posa sur un pavé de pierre.
Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
18 Il enleva le chemin couvert pour le sabbat qu'on avait construit dans la maison, et l'entrée extérieure du roi dans la maison de Yahvé, à cause du roi d'Assyrie.
Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
19 Le reste des actes d'Achaz, qu'il fit, n'est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois de Juda?
Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 Achaz se coucha avec ses pères et fut enterré avec ses pères dans la ville de David; et Ézéchias, son fils, régna à sa place.
Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Rois 16 >