< 2 Chroniques 1 >

1 Salomon, fils de David, était fermement établi dans son royaume. Yahvé, son Dieu, était avec lui et l'a rendu extrêmement grand.
Selemani mwana wa Daudi, aliimariswa katika utawala wake, na Yahwe Mungu wake alikuwa pamoja naye na alimpa nguvu nyingi sana.
2 Salomon parla à tout Israël, aux chefs de milliers et de centaines, aux juges, à tous les princes de tout Israël, aux chefs de famille.
Sulemani akasema kwa Israleli wote, na maakida wa maelfu na wa mamia, na kwa waamuzi, na kwa kila mfalme kiongozi katika Israeli yote, wakuu wa kaya.
3 Puis Salomon, et toute l'assemblée avec lui, se rendit sur le haut lieu qui était à Gabaon, car c'était là que se trouvait la tente de la Rencontre de Dieu, que Moïse, serviteur de Yahvé, avait construite dans le désert.
Hivyo Sulemani na kusanyiko lote wakaenda pamoja naye sehemu ya juu iliyokuwa Gibeoni, maana ndipo palikuwepo hema ya kukutania ya Mungu, ambayo Musa mtumishi wa Yahwe, alikuwa ameitengeneza jangwani.
4 Et David avait fait monter l'arche de Dieu de Kiriath Jearim au lieu que David avait préparé pour elle, car il avait dressé une tente pour elle à Jérusalem.
Lakini Daudi alikuwa ameleta pale sanduku la Mungu kutoka Kiriath yeriam hadi sehemu ambayo alikuwa ametayarisha, maana alikuwa ameliandalia hema huko katika Yerusalemu.
5 L'autel d'airain que Betsaleel, fils d'Uri, fils de Hur, avait fait, était là, devant la tente de Yahvé; et Salomon et l'assemblée y consultaient.
Zaidi ya hayo, madhabahu ya shaba iliyotengenezwa na Bezaleli mwana wa uri mwana wa Huri ilikuwepo huko kabla ya mbele ya madhabahu ya Yahwe; Sulemani na kusanyiko wakaenda ilikokuwa. (Maandiko ya zamani yanasema
6 Salomon monta là à l'autel d'airain devant Yahvé, qui était à la tente d'assignation, et il y offrit mille holocaustes.
Selemani akaenda huko kwenye kwenye madhabahu ya shaba mbele za Yahwe, ambayo ilikuwepo mahali pa hema ya kukutamia, na akatoa sadaka elfu za kuteketezwa juu yake.
7 Cette nuit-là, Dieu apparut à Salomon et lui dit: « Demande ce que tu veux que je te donne. »
Mungu akamtokea Selemani usiku huo na akasema kwake, “Omba! Nikupe nini?”
8 Salomon dit à Dieu: « Tu as fait preuve d'une grande bonté envers David, mon père, et tu m'as fait roi à sa place.
Selemani akasema kwa Mungu, “Umeonesha agano la uaminifu mkuu kwa Daudi baba yangu, na umenifanya mfalme katika nafasi yaye.
9 Maintenant, Yahvé Dieu, que ta promesse à David, mon père, s'accomplisse, car tu m'as établi roi sur un peuple nombreux comme la poussière de la terre.
Sasa, Yahwe Mungu, ahadi yako kwa Daudi baba yangu itimie, maana umenifanya mfalme juu ya watu wengi kama mavumbi ya dunia.
10 Maintenant, donne-moi la sagesse et la connaissance, afin que je puisse sortir et entrer devant ce peuple; car qui peut juger ton grand peuple? »
Sasa nipe hekima na maarifa, ili niweze kuwaongoza watu hawa, maana ni nani anayeweza kuwaamua watu wako, ambao ni wengi sana kwa idadi?”
11 Dieu dit à Salomon: « Parce que cela était dans ton cœur, et que tu n'as pas demandé des richesses, des biens, des honneurs, ni la vie de ceux qui te haïssent, ni même une longue vie, mais que tu as demandé la sagesse et la connaissance pour toi-même, afin de pouvoir juger mon peuple, sur lequel je t'ai établi roi,
Mungu akasema kwa Selemani, “Kwa kuwa hili lilikuwa kwenye moyo wako, na kwa kuwa hujaomba mali, utajiri, au heshima, wala maisha ya wale wanaokuchukia, wala maish marefu kwa jili yako binafsi, lakini umeomba hekima na maarifa kwa ajili yako, ili uwatawale watu wangu, ambao juu yao nimekufanya mfame, na hivi ndivyo nitafanya.
12 la sagesse et la connaissance te sont accordées. Je te donnerai des richesses, des biens et des honneurs, tels qu'aucun des rois qui ont été avant toi n'en a eu, et qu'aucun n'en aura après toi. »
Sasa nitakupa hekima na maarifa, pia nitakupa mali na utajiri, na heshima, kuliko wafalme wote waliokuwepo kabla yako walivyokuwa, na baada yako hakuna yeyote atakayekuwa navyo.”
13 Et Salomon quitta le haut lieu qui était à Gabaon, devant la tente de la Rencontre, pour venir à Jérusalem, et il régna sur Israël.
Kwa hiyo Selemani akaenda Yerusalemu kutoka sehemu ya juu iliyokuwepo Gibeoni, kutoka mbele ya hema ya kukutania; akatawala juu ya Israeli.
14 Salomon rassembla des chars et des cavaliers. Il avait mille quatre cents chars et douze mille cavaliers qu'il plaça dans les villes de chars et auprès du roi à Jérusalem.
Selemani akakusanya magari na wanaume waendesha farasi, naye alikuwa na magari 1, 400 na waendesha farasi kumi na mbili elfu ambao aliwaweka katika miji ya magari, pamoja naye, mfalme katika Yerusalemu.
15 Le roi rendit l'argent et l'or aussi communs que les pierres à Jérusalem, et il rendit les cèdres aussi communs que les sycomores qui sont dans la plaine.
Mfalme akatengeneza fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe katika Yerusalemu, na mbao za mierezi kuwa kama miti ya mikuyu iliyomo katika nyanda za chini.
16 Les chevaux que possédait Salomon avaient été amenés d'Égypte et de Kué. Les marchands du roi les achetaient à Kué.
Selemani katika uagizaji wa farasi kutoka Misiri, wafanya biashara wake walinunua farasi kutoka Misiri kwa bei stahiki.
17 Ils importèrent d'Égypte puis exportèrent un char pour six cents pièces d'argent et un cheval pour cent cinquante. Ils les exportèrent aussi aux rois hittites et aux rois syriens.
Waliagiza gari kutoka Misiri kwa shekeli mia sita za fedha, na farasi mmoja kwa shekeli 150. Pia walinunua kutoka kwa wafalme wa Wahiti na wafalme wa Washamu.

< 2 Chroniques 1 >